Paul Makonda: Kuna makundi matano yanataka kuniua, likiwemo wanaotafuta kulipa kisasi kwa Wasaidizi wa Magufuli

Paul Makonda: Kuna makundi matano yanataka kuniua, likiwemo wanaotafuta kulipa kisasi kwa Wasaidizi wa Magufuli

Camilo Cienfuegos

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2015
Posts
18,960
Reaction score
67,654
Aliyekuwa RC wa Dar es salaam, Paul Makonda anasema kuna makundi matano yanamuwinda ili kumuua.

Ameandika hayo kupitua ukurasa wake wa Instagram na kusema Makundi hayo ni pamoja na Wauza Madawa ya kulevya, mashoga nk

Ameandika: Nafahamu kuna mkakati unaoratibiwa na Makundi 5 kuangamiza maisha yangu.

1) WAUZA MADAWA YA KULEVYA
2)WANUFAIKA NA MADAWA YA KULEVYA
3) MASHOGA
4)WANAOKESHA USIKU KUCHA KUTAFUTA KULIPA KISASI KWA WASAIDIZI WA DR MAGUFULI.
5) WALIOWAHI KUWA SEHEMU YA ……. Nafahamu pia juu ya mbinu zinazoandaliwa ili kuniuwa kwa faida ya familia zao pamoja na kutengeneza mashaidi wa uongo ili mnipe kesi ya uhujumu uchumi.

Mambo mawili najiuliza

1)PAMOJA NA KAZI ZOTE NZURI NILIZOZIFANYA KWA CHAMA CHANGU,SERIKALI YANGU NA WANANCHI WA DAR HAYA NDIYO MALIPO YAKE?

2)Hakika ukiwa mtumishi mwaminifu unaetetea haki za wanyonge tena ukitokea kwenye familia masikini haya ndiyo malipo yake ?

MTU aliejemga hospital , aliejenga ofc cha CCM, Magari ya police 👮‍♀️, ofc za Walimu, vituo vya police, shule za secondary mpaka na msingi, kutibu wagonjwa mpaka Meli kuja Tanzania,kuhudumia Makundi mbali mbali mpaka kuiunganisha Serikali na Viongozi wa Dini. leo hii naonekana eti natakiwa kunyongwa.

Pamoja na kwamba lipo kundi kwenye mitandao linalolipwa ili kuwaanda watanzania pale watakapo nikamata ionekane ni sawa. Hakika ipo siku Walemavu, yatima, wajane na waliotamani watoto WAO wasife kwa MADAWA ya KULEVYA SAUTI ZAO ZITASIKIKA.

#Ukiona maji yametulia jua kina nikilefu.”

ADF897B4-6329-46AA-B4D6-79C3132EA7DA.jpeg
 
Huyu dawa yake yake imechemka muda mrefu, mama Samia, tuma mtu akaiipue, kama alijaribu kumuwinda Lissu, arobaini yake imefika.

Anahofia kesi ya uhujumu uchumi wakati nyumbani kajaza magari ya kudhulumu? Kadhulumu viwanja? Alimpakaza Ruge na ma scjajajakaaaa mkononi siku anapatanishwa mbele ya JPM baada ya hapo Ruge akaanza kuugua?, bilionea asiye na biashara!, Alipata ubilionea baada ya kuwa Mkuu wa Mkoa mwenye mshahara wa milioni tano!. Alikuwa anafika katika maofisi ya mabilionea anachota Hela kwa nguvu!

Lemutuz naye kamkimbia, a lone wolf!
 
Makonda akili ndio hua hana.

Yeye angetulia tu watu wamsahau aendelee na maisha yake.

Kuendelea kutafta public sympathy na kuropoka ropoka asisahau kua watu wengi aliwafanyia ujinga bado wapo na wengine wana nafasi kubwa serikalini.

Angalai hapa anamtukana na kumkaripia Chogolo kama mtoto mdogo hadi jamaa anasema haya bana.

Ila kwa kua Makonda akili hana ataendelea kuropoka hadi wanaomkingia kifua watachoka watamuacha ashambiliwe na mbwa mwitu.

.
 
Pole sana Makonda.

Hii nchi watu washazoea kula vya kupiga. Sasa hivi watu wametulia wanakula tu milungula na wametulia tuli. Wanasiasa nao wanapata pesa nzuri toka huko serikalini ili kupunguza joto la ushindani. Siasa za Bongo haziendi bila unafiki.

Ila utafaulu huu mtihani.
 
Kwani Instagram ndio police post mpaka anaenda kuripoti huko?

Au nae leo hawaamini polisi? haya maisha siku hizi yanaenda kasi sana.

Anyway nikimsoma maandiko yake, psychologically Makonda is not ok, anaonekana ana msongo wa mawazo, anajua his days are numbered in whichever way.
 
Sasa shoga anawezaje kuua mtu atampiga na ndala au upande wa kanga?

Kikubwa PM aliishi maisha mabaya wakati akiwa kiongozi alisahau kesho huwenda ikawa si leo ndiyo maana vita imekuwa kubwa kwake kila aliyekwaruzana naye anamtaka, bora hata angetishiwa na wauza madawa tu ila si mashoga.
 
Back
Top Bottom