Paul Makonda: Wananchi walioikimbia Dar warudi, Mauti hauikimbii. Siku ya Jumapili, kila mtu afanye fujo awezavyo na kupiga kelele na vigeregere!

Huyu mtu ni wa kumpuuza, Corona ipo na inaua.
Huu ushauri wa kipumbavu atakaye ufuata basi atakuwa ni mpumbavu zaidi ya wapumbavu wote duniani.
Mzee JK alituasa, za kuambiwa changanya na za kwako. Tumsikie tu Makonda alichosema, lakini wananchi tuchukue hatua kujua kuwa kuumwa ni sisi na kufa tutakufa sisi.

Hakuna mahali tutakapoweza kwenda kudai uhai endapo utapotea. Tuwaache wao waseme yao. Jilinde wewe na mlinde mwenzio. Ya Makonda, mwachie yeye na hao wanaoungana nae.
 
Na wale wanaojiuza waende watupu kabisa haina shida amri isharuhusiwa
 
Corona itashindwa kwa chanjo au dawa au muujiza. Si kwa matamko. Inaonekana kama waaminio imekwisha wanazungumzia muujiza!! Ni saa ya kuthibitisha kuwa muujiza umetendeka.

Tupime na kuthibitishia hilo ulimwengu. Kama sio hivo, hizi sarakasi zinatuaibisha!!
 
Rais Magufuli ni nahodha bora ametuvusha salama kwenye corona.

Vibaraka wa mabeberu wanaenda kuaibika vibaya.
Viva rais, Viva Makonda. Sasa nimeamini kweli kiongozi wetu ameletwa na Mungu. Hivi kwanini hayo maombi ya siku 3 tusiombe na chakula kishushwe tu tuachane na kufanya kazi kwani ajira zenyewe hakuna.
 
Msisikilize wanasiasa wakuu wao wanaangalia matumbo yao,kwasasa uchumi umepiga mweleka sasa wanataka watu warudi makazini wafungue biashara bila kuweka wazi kwamba ugonjwa upo na unaua,kwa undani kuhusu taarifa za covid19 utazipata kwa KGG wa TWITA.
 
Tupige kazi huku tukiomba
Viva rais, Viva Makonda. Sasa nimeamini kweli kiongozi wetu ameletwa na Mungu. Hivi kwanini hayo maombi ya siku 3 tusiombe na chakula kishushwe tu tuachane na kufanya kazi kwani ajira zenyewe hakuna.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…