Pendekezo: Francis Mutungi na Sisty Nyahyoza waondolewe Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, wametumika kupandikiza migogoro kwenye vyama vya siasa

Pendekezo: Francis Mutungi na Sisty Nyahyoza waondolewe Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, wametumika kupandikiza migogoro kwenye vyama vya siasa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Maadam sasa tumeamua kufanya mabadiliko basi ni vema Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ikaletewa watu wapya ili kuondoa manung'uniko.

Mutungi ametumika mara kadhaa kupandikiza migogoro kwenye vyama vya siasa kwa kuyalinda makundi ya wahalifu , huku akisimamia kugawa ruzuku halali ya Cuf kwa rafiki yake Lipumba kwa kutumia akaunti binafsi ya raia , kuna uvumi kwamba Mutungi alipewa 10% ( hajawahi kukanusha ), sasa mtu kama huyu ama Msaidizi wake Sisty Nyahyoza, ambaye hajawahi kuficha mapenzi yake kwa ccm hawafai kuendelea kukalia ofisi hii nyeti ya Umma.

Iko wazi kwamba vyama vya siasa kwa kipindi cha miaka 6 chini ya Utawala wa Magufuli vilipigwa marufuku kufanya shughuli zote za kisiasa kinyume kabisa cha Katiba ya nchi na kinyume cha Sheria za vyama vya siasa , lakini Mutungi akiwa mlezi wa vyama hivyo na huku akijua kwamba sheria za nchi zinavunjwa hakuwahi kukemea , aliamua kuufyata na kunyamaza , kiongozi kama huyu muoga anasubiri nini kwenye ofisi hii?
 
Mwaka jana ilisemwa kuwa, Mutungi anaumwa na hata barua nyingi za ofisi ya Msajili zimekuwa zikisainiwa na wasaidizi wake. Na toka kampeni za uchaguzi 2020 zianze huyu bwana hajaonekana kwa umma hata kwenye chaguzi na mikutano ya CCM; Sheria ya Utumishi wa Umma Kupitia kanuni zake za mwaka 2003 inasema ukiwa mgonjwa kwa zaidi ya miezi 6 unapewa likizo ya ugonjwa na miezi 6 inayofuata unalipwa nusu mshahara na ikiwa bado unaendelea kuumwa unastaafishwa. (kanuni ya 100 (2) ya Kanuni za Utumishi wa Umma, 2003).

Kama Mutungi bado ni mgonjwa au la, Watanzania tujulishwe hali yake na kama ni mgonjwa astaafishwe kwa mujibu wa sheria.

Screen Shot 2021-05-12 at 2.31.20 PM.png
 
Mbali na CUF, chama gani kingine kilisababishiwa mgogoro na hao watendaji?
 
Mwaka jana ilisemwa kuwa, Mutungi anaumwa na hata barua nyingi za ofisi ya Msajili zimekuwa zikisainiwa na wasaidizi wake. Na toka kampeni za uchaguzi 2020 zianze huyu bwana hajaonekana kwa umma hata kwenye chaguzi na mikutano ya CCM; Sheria ya Utumishi wa Umma Kupitia kanuni zake za mwaka 2003 inasema ukiwa mgonjwa kwa zaidi ya miezi 6 unapewa likizo ya ugonjwa na miezi 6 inayofuata unalipwa nusu mshahara na ikiwa bado unaendelea kuumwa unastaafishwa. (kanuni ya 100 (2) ya Kanuni za Utumishi wa Umma, 2003).

Kama Mutungi bado ni mgonjwa au la, Watanzania tujulishwe hali yake na kama ni mgonjwa astaafishwe kwa mujibu wa sheria.

View attachment 1781995
ATAKUWA ANA MGAO WAKE KULE CUF
 
Back
Top Bottom