Pendekezo: Majina ya viongozi yaondolewe miradi ya umma

Pendekezo: Majina ya viongozi yaondolewe miradi ya umma

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Viongozi wa Tanzania waliopo na waliopita wamepachika au wamepachikiwa majina yao kwenye mali na miradi ya nchi, hili jambo halina maana wala tija yoyote ile.

Kwa mfano, si sawa kwa stendi ya mabasi ya kimataifa ya Mbezi Luis, uwanja wa soka wa Taifa, viwanja vya ndege, madaraja, vivuko, shule, hospitali na mali nyingine za Taifa kupewa majina ya viongozi, wawe hai au wamekufa. Hii ni kwa sababu mali za umma zimegharamiwa na kodi za wananchi, hivyo si haki kuweka jina la kiongozi, eti kwa vile tu vitu hivyo vilijengwa wakati mhusika akiwa madarakani, wala hata hakutumia hela za mfukoni mwake. Huku ni kukengeuka, halafu ni nani anayependekeza majina hayo na kwa mchakato upi?

Kusimamia ujenzi wa kitu chochote katika nchi haimaanishi kwamba mhusika anayo hati miliki ya jina lake kupachikwa kwenye huo mradi. Hii ni kwa vile pesa zilizotumika kujenga miradi ya nchi si zake binafsi, ni hela za umma. Majina yanayopaswa kuitwa miradi hiyo yawe majina ya maeneo ulipo mradi huo, mfano uwanja wa ndege wa Dar es Salaam, daraja la Busisi, barabara ya Mwendokasi, mradi wa umeme Kinyerezi, nk.

Lakini mali za umma kama stendi ya Mbezi Luis kuiita jina la mtu mmoja ni sawa na ubaguzi uliojaa ubinafsi. Napendekeza stendi ya Mbezi iitwe "Stendi ya Mabasi ya Mikoa ya Mbezi Luis". Jambo hili linaweza kuondoa nuksi, laana, na mikosi itokanayo na kutumia jina la mtu mmoja tu tena ambaye hajawahi kuwa mkazi wa eneo hilo na wala hajawahi hata kupanda mabasi yenyewe. Uwanja wa Taifa wa soka urudishiwe jina lake la awali na jina la Nyerere liondolewe kwenye uwanja wa ndege, urudi kuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam.

Kama tunataka kuwaenzi marehemu wetu au hata viongozi waliopo, basi ni rahisi sana. Majina yao yawekwe kwenye ofisi za vyama vyao, kwa mfano, badala ya kuita ofisi ya chama Kisiwandui, basi iitwe "Ofisi ya Magufuli Kisiwandui".

Naomba kuwasilisha.
 
Wewe ni kiazi kweli hiyo mitaa iliyojaa majina ya watu wa akimiliki,kilaza sana wewe, nilimwambia leta jina la babako tuweke

USSR
Sheria ya Halmashauri ya kuweka jina la Mtaa lina mambo ya kuzingatia , yako wazi sana .
 
Napendekeza Stendi ya Mbezi iitwe STENDI YA MABASI YA MIKOANI YA MBEZI LUIS , Jambo hili linaweza kuondoa nuksi , laana na mikosi itokanayo na kutumia Jina la Mtu mmoja tu tena ambaye hajawahi kuwa mkazi wa eneo
Dk chache umeona comment ya mtu kwnye thread ya NCard uwanja wa magu ushakuja kufungulia Uzi Huku😂
 
Kama huna hoja basi acha kutoa hoja. Ningependa kama ungesema kwamba kuwa na sheria,taratibu na kanuni za kuamua Naming rights zinakuwaje kwa public infrastructures kama barabara, majengo etc.Ila sio kusema kwamba ETI yasiwekwe.

SIONI Ubaya Magufuli Terminal Kuitwa Magufuli Terminal kwani UBUNGO, MBEZI, KIMARA yote ni Majina ya WATU tena ambao hata wengine historia yao hatufahamu. QUIT THIS SHIT muwe mnaleta mijadala ambayo ni maslahi kwa umma
 
Kama huna hoja basi acha kutoa hoja.Ningependa kama ungesema kwamba kuwa na sheria,taratibu na kanuni za kuamua Naming rights zinakuwaje kwa public infrastrucures kama barabara,majengo etc.Ila sio kusema kwamba ETI yasiwekwe.SIONI Ubaya Magufuli Terminal Kuitwa Magufuli Terminal kwani UBUNGO,MBEZI,KIMARA yote ni Majina ya WATU tena ambao hata wengine historia yao hatufahamu.QUIT THIS SHIT muwe mnaleta mijadala ambayo ni maslahi kwa umma
Uko sahihi... Mtoa post amedhihirisha Ujinga wake....
Post yake imekosa akili kabisa
 
Back
Top Bottom