Pendekezo: Majina ya viongozi yaondolewe miradi ya umma

Pendekezo: Majina ya viongozi yaondolewe miradi ya umma

1. John Fitzgerald Kennedy (JFK) International Airport - USA
2. General Charles De Gaulle Airport - France
3. Hastings Kamuzu Banda Boulevard - Malawi
4.
Sijui niendelee?
Msiige , hawa wa Tanzania hawafai
 
1. John Fitzgerald Kennedy (JFK) International Airport - USA
2. General Charles De Gaulle Airport - France
3. Hastings Kamuzu Banda Boulevard - Malawi
4.
Sijui niendelee?
Hao ni watu waliozifanyia nchi zao mambo makubwa, sasa John Kijazi au Mfugale wamefanya nini kikubwa katika taifa hili
 
Viongozi wa Tanzania waliopo na waliopita wamepachika au wamepachikiwa majina yao kwenye mali na miradi ya nchi, hili jambo halina maana wala tija yoyote ile.

Kwa mfano, si sawa kwa stendi ya mabasi ya kimataifa ya Mbezi Luis, uwanja wa soka wa Taifa, viwanja vya ndege, madaraja, vivuko, shule, hospitali na mali nyingine za Taifa kupewa majina ya viongozi, wawe hai au wamekufa. Hii ni kwa sababu mali za umma zimegharamiwa na kodi za wananchi, hivyo si haki kuweka jina la kiongozi, eti kwa vile tu vitu hivyo vilijengwa wakati mhusika akiwa madarakani, wala hata hakutumia hela za mfukoni mwake. Huku ni kukengeuka, halafu ni nani anayependekeza majina hayo na kwa mchakato upi?

Kusimamia ujenzi wa kitu chochote katika nchi haimaanishi kwamba mhusika anayo hati miliki ya jina lake kupachikwa kwenye huo mradi. Hii ni kwa vile pesa zilizotumika kujenga miradi ya nchi si zake binafsi, ni hela za umma. Majina yanayopaswa kuitwa miradi hiyo yawe majina ya maeneo ulipo mradi huo, mfano uwanja wa ndege wa Dar es Salaam, daraja la Busisi, barabara ya Mwendokasi, mradi wa umeme Kinyerezi, nk.

Lakini mali za umma kama stendi ya Mbezi Luis kuiita jina la mtu mmoja ni sawa na ubaguzi uliojaa ubinafsi. Napendekeza stendi ya Mbezi iitwe "Stendi ya Mabasi ya Mikoa ya Mbezi Luis". Jambo hili linaweza kuondoa nuksi, laana, na mikosi itokanayo na kutumia jina la mtu mmoja tu tena ambaye hajawahi kuwa mkazi wa eneo hilo na wala hajawahi hata kupanda mabasi yenyewe. Uwanja wa Taifa wa soka urudishiwe jina lake la awali na jina la Nyerere liondolewe kwenye uwanja wa ndege, urudi kuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam.

Kama tunataka kuwaenzi marehemu wetu au hata viongozi waliopo, basi ni rahisi sana. Majina yao yawekwe kwenye ofisi za vyama vyao, kwa mfano, badala ya kuita ofisi ya chama Kisiwandui, basi iitwe "Ofisi ya Magufuli Kisiwandui".

Naomba kuwasilisha.
Uwanja wa ndege wa kimataifa Dar es Salaam haukutoa hela ya ujenzi, hela ametoa mama Samia mwenyekiti wa CCM hivyo hauwezi kumchagulia majina. Wewe tafuta hela zako uweke majina unayoyataka, hakuna atakaye kuuliza.
 
Kama huna hoja basi acha kutoa hoja. Ningependa kama ungesema kwamba kuwa na sheria,taratibu na kanuni za kuamua Naming rights zinakuwaje kwa public infrastructures kama barabara, majengo etc.Ila sio kusema kwamba ETI yasiwekwe.

SIONI Ubaya Magufuli Terminal Kuitwa Magufuli Terminal kwani UBUNGO, MBEZI, KIMARA yote ni Majina ya WATU tena ambao hata wengine historia yao hatufahamu. QUIT THIS SHIT muwe mnaleta mijadala ambayo ni maslahi kwa umma
Ubungo, Mbezi na Kimara inawezekana ni majina ya watu, lakini hakuna mtu mwenye hakimiliki wa majina hayo hivyo wenyewe ni wakusadikika.
 
Viongozi wa Tanzania waliopo na waliopita wamepachika au wamepachikiwa majina yao kwenye mali na miradi ya nchi, hili jambo halina maana wala tija yoyote ile.

Kwa mfano, si sawa kwa stendi ya mabasi ya kimataifa ya Mbezi Luis, uwanja wa soka wa Taifa, viwanja vya ndege, madaraja, vivuko, shule, hospitali na mali nyingine za Taifa kupewa majina ya viongozi, wawe hai au wamekufa. Hii ni kwa sababu mali za umma zimegharamiwa na kodi za wananchi, hivyo si haki kuweka jina la kiongozi, eti kwa vile tu vitu hivyo vilijengwa wakati mhusika akiwa madarakani, wala hata hakutumia hela za mfukoni mwake. Huku ni kukengeuka, halafu ni nani anayependekeza majina hayo na kwa mchakato upi?

Kusimamia ujenzi wa kitu chochote katika nchi haimaanishi kwamba mhusika anayo hati miliki ya jina lake kupachikwa kwenye huo mradi. Hii ni kwa vile pesa zilizotumika kujenga miradi ya nchi si zake binafsi, ni hela za umma. Majina yanayopaswa kuitwa miradi hiyo yawe majina ya maeneo ulipo mradi huo, mfano uwanja wa ndege wa Dar es Salaam, daraja la Busisi, barabara ya Mwendokasi, mradi wa umeme Kinyerezi, nk.

Lakini mali za umma kama stendi ya Mbezi Luis kuiita jina la mtu mmoja ni sawa na ubaguzi uliojaa ubinafsi. Napendekeza stendi ya Mbezi iitwe "Stendi ya Mabasi ya Mikoa ya Mbezi Luis". Jambo hili linaweza kuondoa nuksi, laana, na mikosi itokanayo na kutumia jina la mtu mmoja tu tena ambaye hajawahi kuwa mkazi wa eneo hilo na wala hajawahi hata kupanda mabasi yenyewe. Uwanja wa Taifa wa soka urudishiwe jina lake la awali na jina la Nyerere liondolewe kwenye uwanja wa ndege, urudi kuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam.

Kama tunataka kuwaenzi marehemu wetu au hata viongozi waliopo, basi ni rahisi sana. Majina yao yawekwe kwenye ofisi za vyama vyao, kwa mfano, badala ya kuita ofisi ya chama Kisiwandui, basi iitwe "Ofisi ya Magufuli Kisiwandui".

Naomba kuwasilisha.
Mamluki njooni mnitukane na huku
 
Viongozi wa Tanzania waliopo na waliopita wamepachika au wamepachikiwa majina yao kwenye mali na miradi ya nchi, hili jambo halina maana wala tija yoyote ile.

Kwa mfano, si sawa kwa stendi ya mabasi ya kimataifa ya Mbezi Luis, uwanja wa soka wa Taifa, viwanja vya ndege, madaraja, vivuko, shule, hospitali na mali nyingine za Taifa kupewa majina ya viongozi, wawe hai au wamekufa. Hii ni kwa sababu mali za umma zimegharamiwa na kodi za wananchi, hivyo si haki kuweka jina la kiongozi, eti kwa vile tu vitu hivyo vilijengwa wakati mhusika akiwa madarakani, wala hata hakutumia hela za mfukoni mwake. Huku ni kukengeuka, halafu ni nani anayependekeza majina hayo na kwa mchakato upi?

Kusimamia ujenzi wa kitu chochote katika nchi haimaanishi kwamba mhusika anayo hati miliki ya jina lake kupachikwa kwenye huo mradi. Hii ni kwa vile pesa zilizotumika kujenga miradi ya nchi si zake binafsi, ni hela za umma. Majina yanayopaswa kuitwa miradi hiyo yawe majina ya maeneo ulipo mradi huo, mfano uwanja wa ndege wa Dar es Salaam, daraja la Busisi, barabara ya Mwendokasi, mradi wa umeme Kinyerezi, nk.

Lakini mali za umma kama stendi ya Mbezi Luis kuiita jina la mtu mmoja ni sawa na ubaguzi uliojaa ubinafsi. Napendekeza stendi ya Mbezi iitwe "Stendi ya Mabasi ya Mikoa ya Mbezi Luis". Jambo hili linaweza kuondoa nuksi, laana, na mikosi itokanayo na kutumia jina la mtu mmoja tu tena ambaye hajawahi kuwa mkazi wa eneo hilo na wala hajawahi hata kupanda mabasi yenyewe. Uwanja wa Taifa wa soka urudishiwe jina lake la awali na jina la Nyerere liondolewe kwenye uwanja wa ndege, urudi kuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam.

Kama tunataka kuwaenzi marehemu wetu au hata viongozi waliopo, basi ni rahisi sana. Majina yao yawekwe kwenye ofisi za vyama vyao, kwa mfano, badala ya kuita ofisi ya chama Kisiwandui, basi iitwe "Ofisi ya Magufuli Kisiwandui".

Naomba kuwasilisha.
Umewapandisha hasira, sasa stesheni hazitakuwa za miji husika stesheni na treni zitaitwa majina ya yao viongozi wa CCM.
 
Hakika ni kujikweza kwa hali ya juu mali za umma kuitwa kwa majina ya watu. Kama kiongozi kasimamia mradi ilikuwa ni jukumu lake na alilipwa kwa kazi hiyo. Huu ni ugonjwa wa cancer kwa wanasiasa wanaopenda kujikweza kwa sababu wataalamu hawana kasumba hiyo.
 
Ni utamaduni tu na sizan km kuna ubaya
Ziwa victoria ni jina la mtu
Mtaa wa livingston ni jina la mtu
Bibi titi ni jina la mtu
Forodhani jina la mjukuu wa mfalme

Shida watanzania tumechanganyikiwa na huu ugumu wa maisha na mdororo wa uchumi ad unasababisha tunashindwa kuwaza mambo makubwa tunawaza mawazo ya kitoto sasa jina la raisi au kiongozi likitumika km utambulisho lina madhara gan au linapunguza nini ktk huo mradi na ata sku akitoka itabakia km kumbukumbu
 
Back
Top Bottom