PENDEKEZO: Rais Samia atangaze rasmi tarehe 17 Machi iwe Sikukuu ya kitaifa kumuenzi Hayati Magufuli

Ukiendekeza huo ujinga itafika kipindi mwaka mzima tutakua tunaomboleza, jumatatu nyerere jumanne mkapa,jumatano sokoine, alhamis magufuli, ijumaa Samuel sitta
 
Yaani unataka siku hiyo unataka tupumzike na kunywa bia kwa furaha kumshukuru Mungu kwa wema aliotutendea?

Yaani tuitolee Corona sadaka ya shukrani?
 
Basi iwe siku ya mapumziko kwa kutambua mchango wa marais wote waliopita na wajao, na badala ya kuitwa Magufuli Day iitwe Presidents Day. Au unaonaje hapo bwashee?
 
Pendekezo mwenda chato, jina lake liondolewe katika orodha ya Marais waliowahi kutawala nchi hii, Kwan mzimu wake ni hatari kwa Taifa, na itachukua miaka mingi nchi hii Kutengamaa, matatzo mengi tuliyonayo Sasa hayapati suluhu, sababu ya mzimu wa mwenda chato.
 
Mufti Mkuu
Mbona Kama Nawe Una Matatizo Mno, Sasa Ikitangazwa Hiyo Tarehe Na Watu Tutakufa Kila Siku Atatangaza Mwaka Mzima
 
Watu wengi wameporwa mali, wameumizwa na hata kuuwawa wakati wa utawala wa Magufuli. Fedha nyingi zimepotea, ubadhirifu, madeni makubwa, matumizi mabaya ya madaraka, ubaguzi wa kikabila, …, n.k. Aenziwe?! Kwa lipi?!!!
 
Watu wengi wameporwa mali,wameumizwa na hata kuuwawa wakati wa utawala wa Magufuli. Fedha nyingi zimepotea, ubadhirifu, madeni makubwa, matumizi mabaya ya madaraka, ubaguzi wa kikabila, …, n.k. Aenziwe?! Kwa lipi?!!!
 
What about BW Mkapa? Unadhani yeye hastahili kuenziwa?

Wakuwaenzi wabaki kuwa NYERERE na KARUME[emoji41] wanatosha.
Kumbukumbu za viongozi wote wakitaifa zingewekwa katika siku moja tu, yaani Sikukuu ya Mashujaa. Hakuna haja ya kuwa na utitiri wa sikukuu nyingi katika nchi maskini kama yetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…