Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Soma uzi wa mkuu barafu kuhusu kanisa na Utawala utaelewa, Tangu zamani kanisa Katoliki limetumika kufanya dhuluma sana, Mpaka leo kanisa limejaa unafiki na uchafu, Wakatoliki wamegeuzwa watu wa ndio tu, Hata askofu akibaka husema ndio tuzidi kumuheshimu, Wakatoliki wamekuwa watu wa kuwayawaya tu, Kanisa limegeuzwa miliki ya askofu na mapandri, Waumini kazi yao ni kutii amri na miongozo ya kanisa, Unaweza cheka sana ukiuliza unaambiwa mapokeo wapi imeandikwa utasikia Papa gani sijui au mtaguso gani sijui, Biblia wameweka kapuni
 
Chadema upepo umebadilika...2020 mtalia zaidi
 


Wewe unalijua Kanisa Katoliki kuliko Kardinali Pengo ambaye anakaa meza moja na Papa? Pengo ana kiti chake Roma kwenye Meza moja na Papa, Pengo anaweza kuongea na Papa kwa Simu, wewe takataka unaweza kumpigia nani Simu hata akapokea?
 
Pengo sidhani Kama alimshitaki gwajima. Andika unachotaka kumpinga bila kutia chumvi.
 

Kwa hiyo mtu yoyote akiwa na mtazamo tofauti na wewe basi anatumika? Itakuwa makosa mtu akisema na wewe unatumika?
 
Pengo nimtu mkubwa asiye na vision tumsamehe tu.....

kanisa catholic najua ugumu walionao na hawana cha kufanya. maana mzee kashika fungu huwezi ingia wala toka kama hajaruhusu.

atalipa fadhira mpaka mwisho wa pumzi yake

sidhani kama mungu anaona

angekuwa mungu asumani ningeomba ampe ulemavu mjalabu
 
Wewe unalijua Kanisa Katoliki kuliko Kardinali Pengo ambaye anakaa meza moja na Papa? Pengo ana kiti chake Roma kwenye Meza moja na Papa, Pengo anaweza kuongea na Papa kwa Simu, wewe takataka unaweza kumpigia nani Simu hata akapokea?
Mkuu umepanic....hiyo post ni kwa Pengo as a person,sio kwa Institution ya RC
 
Huwa hampendi kuambiwa ukweli.....
Mbna hamkumkosoa GWAJIMA kipindi kile yupo upande wenu....
Askofu PENGO yupo sahihi maana kaona mtu sahihi
Kama ambavyo Mbowe anavyosifia mazuri ya MAGUFULI....mbna hausemi ana kiharibu chadema?
Ukikuta kiongozi anasema katiba kwa sasa siyo kipaumbele basi huyo ni mchumia tumbo tuu.
 
Baadhi ya viongozi wa dini ni wakala au wafanyakazi wa taasisi za kijasusi za Serikali.
Kama ilivyo ada majasusi wapo katika fani zote, wakulima, wavuvi, wafugaji, wanamichezo, waalimu, madaktari, wachungaji (Mapadre, Maaskofu, Mashehe, Masista, mabraza, wainjilisti) Waandisi, Wachuuzi,Wafanyabiashara wakubwa kwawadogo, waandishi wa habari nk.

Mtawatambua kwa mienendo yao.
 
Papa si Mungu
Roma si mbinguni.

GET WELL SOON LISSU

Hapo uko sawa, lkn kumbuka tunaongelea Kanisa Katoliki ambalo Mkuu wake ni Papa, ukitoka nje ya Kanisa Katoliki unaweza kumkwepa Papa lkn siyo ndani, na pia Kanisa Roma lina wafuasi 1.23 billion Duniani kati Binadamu Billioi 7, na hawa wote 1.24 billion Mkuu wao ni Papa!
 
Wewe unalijua Kanisa Katoliki kuliko Kardinali Pengo ambaye anakaa meza moja na Papa? Pengo ana kiti chake Roma kwenye Meza moja na Papa, Pengo anaweza kuongea na Papa kwa Simu, wewe takataka unaweza kumpigia nani Simu hata akapokea?
Umechemka, papa, pengo na mleta mada ni sawa mbele ya mungu na kanisa ni mapokeo kwa hiyo mleta mada anao uwezo wa kulielewa kanisa katoliki kuliko pengo, kama wewe unavyo ijua katiba ya CCM kuliko viongozi wengi wa CCm wakati wewe sio kiongozi.
 
Kwani uliambiwa kuwa msimamo aliotoa ni wa dini yako?Padri anapotoa ibada na akatoa mifano mbalimbali kwa kizazi cha sasa je unakuwa umemtuma?Kwanini unajibia kitu ambacho kipo wazi tu na nitofauti na unachojibia?pengo vipi?
 
Hiyo shule ya Upadri uliyosoma ipo mkoa gani? Acha mambo yako ya ajabu kumuhusisha Askofu na siasa zenu chafu, unatafuta huruma kwa kanisa.
 
Hapo kuhusu Gwajima ni uwongo mkubwa. Pengo hajawahi mshitaki Gwajima.

Pia kumbuka maelezo ya Pengo yalikuwa kwamba anafafanua kuwa kauli ya Niwemugizi siyo ya kanisa kwani tayari ulikuwa na hiyo argument iliyohitaji ufafanuzi
 
Pia Pengo sio msemaji wa kanisa katoliki Tanzania bali baraza la maaskofu ndio lenye kuweza kusema kupitia kaatibu wake au Rais wa baraza.

Pili kila askofu anayo mamlaka ya kutoa msimamo wa jimbo analosimamia bila kuingiliwa na Pengo.
Je hiyo mamlaka ya kumkosoa huyo askofu ameipata wapi.

Lakini pia hoja ya askofu Niwemugizi sioni kama inakinzana na kanisa na unaweza kuwa msimammo wa waumini wa jimbo lake na pia unaweza kuwa msimaamo wake binafsi. Na wala hakusema ndio msimamo wa kanisa kardinali Pengo ametoka wapi kumjibu?

Mojawapo ya sifa ya kanisa katoliki ni kusema kweli pasipo kificho ama unafiki.

Mhashamu Kardinali Pengo umekengeuka kwa hili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…