Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Yote hayo anayasema Pengo leo ni kwa sababu anayetawala sasa ni Mkatoliki ambaye inadaiwa kwa makusudi anaipa Favor ya juu taasisi ya Ukatoliki hapa Tanzania.

Kama mtawala angekuwa ni Muislamu (kama kipindi kile cha Kikwete) Askofu Pengo ungemwona yuko busy kila Jumapili kuikosoa serikali na kudai uwepo wa katiba mpya yenye kutoa haki kwa Watanzania.
 
Kiongozi wa Kanisa katoliki Tanzania !
 
Mwamini ninayejitabua sipangiwi. Katiba mpya ni lazima.
 
Nimesikitishwa sana na kauli ya Kardinali Pengo juu ya Katiba Mpya.Nilitegemea Kardinali Pengo angeungana na Watanzania kutaka Katiba Mpya badala yake anasema eti IJE BAADAE.
 
Na yeye sio msemaji wa sisi waumini.
 
Nimesikitishwa sana na kauli ya Kardinali Pengo juu ya Katiba Mpya. Nilitegemea Kardinali Pengo angeungana na Watanzania kutaka Katiba Mpya badala yake anasema eti IJE BAADAE.
Walianza wapinzani, wakaja media, wakaja.........
Bado kidogo dini nayo itaanza kuisoma namba na akili zao ndo zitakaa mguu pande mguu sawa.
 
Pengo anaposema Kipaumbele chake ni kuona wananchi wanapata huduma kwanza na sio katiba mpya, inaashiria Akili yake imeanza kuzeeka vibaya.

Mimi nilitaka kumuuliza tu, kwanini Kanisa katoliki miaka yoyote limekuwa likitenga bajeti kubwa sana kwa ajili ya kuhubiri injili, kuwatunza vizuri Mapadri na Masista, kujenga makanisa makubwa na mazuri kuliko kutenga bajeti kubwa kwa ajili ya kuwanunulia chakula wahanga wote wanaokufa kwa njaa duniani?

Kipaumbele chao ni nini?
 
Nimesikitishwa sana na kauli ya Kardinali Pengo juu ya Katiba Mpya.Nilitegemea Kardinali Pengo angeungana na Watanzania kutaka Katiba Mpya badala yake anasema eti IJE BAADAE.
Uingereza haijawahi kuwa na katiba na haina mpango wa kuwa na katiba lakini ni nchi iliyoendelea. Katiba sio kipaumbele cha maendeleo.
 
Wataalam wa mambo ya Akili huwa wanasema ukiwa na umri mkubwa unavyozidi kukua kiumri ndiyo uwezo wa kufikiri hupungua.
 
Mtu asiejulikana
 

Hii ni aibu kubwa kwa Kanisa Katoliki...kuwa na kiongozi wa dini wa aina hii.
Mbona amekuwa mnafiki kiasi hiki?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…