Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Chadema wanataka kila mtu aseme wanachotaka wao, wanashindwa kuelewa kuwa kila kitu kina taratibu zake, kwa staili hii ikulu wataisikia tu.
 
Kama huna cha maana cha kuandika ni bora kukaa kimya badala ya kujidharaulisha kiasi hiki. Chadema si chama cha kanisa au wakristo au wachagga na ndiyo sababu kimeweza kushamiri Tanzania nzima hata kule Zenj kinakubaliwa na ndiyo sababu CUF hawakuona matatizo ya kushirikiana na Chadema.

Uwe unafikiri kwa kina kabla ya kukurupuka na kuandika pumba kiasi hiki.

Uchaguzi wa 2010 Kanisa lilishiriki kikamilifu kuwashawishi waumini wake, kutoa waraka wa aina ya viongozi wanaohitajika, kutoa elimu ya uraia na haki zao kwa waumini wao.

Ni wakati huo Chadema ilikuwa inaungwa mkono na jamii kubwa hasa wasomi na vijana.

Ni wakati huo Watanzania wengi walijitolea kuitetea Chadema kwa jasho na Damu....

Ilifika wakati ikawa ni aibu kwa Mtanzania hasa wa mjini kujitambulisha yeye ni ccm.

Iwe kwenye mkusanyiko au vyombo vya usafiri ukitetea ccm jamii yote inageuka kukuangalia wewe ni mtu wa aina gani...

Hii yote ilichangia na ushawishi wa Kanisa....

Uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 uliweka rekodi kwenye siasa za upinzani Tanzania hasa Chadema, Chadema walichukua vijiji vingi sana hata kule ambako hakukutarajiwa walishinda.

Hii yote ilitokana na Mbegu iliyopandwa kwenye uchaguzi wa 2010.

Kosa kubwa mlilofanya ni kumkabidhi Lowasa chama, wenye akili walikaa pembeni na wengine kumuunga mkono Magufuli....wasomi wengi walikaa pembeni, watetezi walikata tamaa. chama kikabaki kutembelea kivuli cha 2010.

Kosa kubwa zaidi mnalolifanya ni kulishambulia Kanisa na viongozi wake, hili ndio kosa litakalowapoteza zaidi kwenye siasa za ushindani.

Dunia yote inatambua uwezo na nguvu ya ushawishi wa Kanisa, hivyo kujaribu kupambana na kanisa ni sawa na kunywa chai kwa mluzi....
 
Kwani Pengo ndiye kanisa?
Ungejua tu hata maaskofu wenzake wanamuona mzigo usingesema haya
Pengo sio kanisa katoliki.na kiufupi amechokwa .tena sio kuchokwa kidogo.sana tu
Baraza la Maaskofu ndilo lenye mamlaka na Kanisa katoliki Tanzania

Natumaini ulisoma hili Tamko la TEC

Baraza la Maaskofu Katoliki watoa tamko kulaani wauaji na shambulio kwa Tundu Lissu
Ndio Mkuu Pengo sio Kanisa, lakini huwezi kupuuza ushawishi wa Kardinali pengo ndani kanisa...

Japo Kardinali pengo sio kiongozi mkuu wa kanisa Katoliki Tanzania, lakini watanzania wengi hasa wakatoliki wanamfahamu na kumheshimu Kardinali Pengo kuliko kiongozi yoyote yule wa kanisa nchini unaemfahamu wewe.
 
Chadema wanataka kila mtu aseme wanachotaka wao, wanashindwa kuelewa kuwa kila kitu kina taratibu zake, kwa staili hii ikulu wataisikia tu.
endapo tu wewe hukuwa mmoja wa wale milioni sita tulioichagua CHADEMA...So huwezi kuwa na chochote Positive.
Watanzania wanaendelea kutuamini na wamewachoka CCM isivyo kifani
 
Hivi uchaguzi wa mwaka 2015 Chadema iliungwa mkono na Catholic? Hatutarudi nyuma, Pengo ni adui wa ustawi wa demokrasia! Aondoke kanisani!
Kanisa Katoliki sio kama Bavicha.!
 
Kwa hili baba askofu naye angetoa tu mawazo yake badala ya kusema ule sio msimo wa kanisa?manake hata wake si msimamo wa kanisa.na wakati mwingine mie naona ni vizuri kuwa neutral kwenye vitu km hivi.
 
Ndio Mkuu Pengo sio Kanisa, lakini huwezi kupuuza ushawishi wa Kardinali pengo ndani kanisa...

Japo Kardinali pengo sio kiongozi mkuu wa kanisa Katoliki Tanzania, lakini watanzania wengi hasa wakatoliki wanamfahamu na kumheshimu Kardinali Pengo kuliko kiongozi yoyote yule wa kanisa nchini unaemfahamu wewe.
Nani kakudanganya kuwa pengo ana ushawishi ndani ya kanisa?
Uliza uambiwe.
Pengo kwa sasa hata pale TEC wanamdharau kulikoni
Amepoteza credibility yake Big time
Ni vile tu bado ana voting power ya Pope
Fanya utafiti kidogo arif sio kuropoka.Ongea na wakatoliki tukuambie
 
Kupitia wizi wa kura na mtutu wa bunduki Chadema haiwezi kuingia Ikulu, lakini kupitia katiba mpya ya rasimu ya Warioba na Tume huru ya uchaguzi MACCM wanajua kipigo watakachokipata nchi nzima na hata ndani ya CCM wanajua hivyo maana wamechokwa kila kona ya nchi na sera zao MUFILISI.



Chadema wanataka kila mtu aseme wanachotaka wao, wanashindwa kuelewa kuwa kila kitu kina taratibu zake, kwa staili hii ikulu wataisikia tu.
 
Daa aisee we jamaa mbishi sana utuulize tuliosoma hizo shule.. ni za kanisa katolic.. kama unabisha tena nenda pale msimbazi centre ukawaulize st mary's visiga sminRy ni ya mama rwakatare or ya kanisa katoliki..
93d12ca2de52ba48d4fa41665bc85baa.jpg
Saint Mery's ni shule za madhebu ya kilokole na siyo shule za kanisa katoliki.
Zipo seminary nyingi za kikatoliki zinaitwa st Mary.. mf ile ya hapo mbalizi mbeya inaitwa st mary mbalizi... kuna moja iko hapo pwani inaitwa st. Mary's pia au maarufu kama Visiga seminary
Fatilia vizuri ujue mmiliki wa hiyo st.Mary ya Mbeya na hiyo ya pwani utajua kua hizo shule hazina muunganiko na kanisa Katoliki. Hizo mkurugenzi wake ni Mchungaji Mama Rwakatare.
 
Chadema wanataka kila mtu aseme wanachotaka wao, wanashindwa kuelewa kuwa kila kitu kina taratibu zake, kwa staili hii ikulu wataisikia tu.
Kinachowagharimu ni kukosa mikakati na kujua ya kesho.
 
endapo tu wewe hukuwa mmoja wa wale milioni sita tulioichagua CHADEMA...So huwezi kuwa na chochote Positive.
Watanzania wanaendelea kutuamini na wamewachoka CCM isivyo kifani
Pole sana kwa kuichoka ccm lakini kwa mbinu mnazotumia ikulu mtaisikia tu. Mimi sina chama by the way.
 
Askofu Pengo anatumika vibaya na mwisho wa siku ataumbuka tuu,kwani unafiki haijawahi kuacha mtu salama
 
Fatilia vizuri ujue mmiliki wa hiyo st.Mary ya Mbeya na hiyo ya pwani utajua kua hizo shule hazina muunganiko na kanisa Katoliki. Hizo mkurugenzi wake ni Mchungaji Mama Rwakatare.

Usiwe mjinga wa kiasi hicho Seminary ya St Mary's inamilikiwa na Pengo ipo Visiga, Kibaha.
 
Kama huna cha maana cha kuandika ni bora kukaa kimya badala ya kujidharaulisha kiasi hiki. Chadema si chama cha kanisa au wakristo au wachagga na ndiyo sababu kimeweza kushamiri Tanzania nzima hata kule Zenj kinakubaliwa na ndiyo sababu CUF hawakuona matatizo ya kushirikiana na Chadema.

Uwe unafikiri kwa kina kabla ya kukurupuka na kuandika pumba kiasi hiki.
Hakuna niliposema Chadema ni Chama cha kanisa....ila nimeongelea mchango wa kanisa kwenye ukuaji wa Chadema...
 
Back
Top Bottom