Pengo kwenye Muungano

Pengo kwenye Muungano

Critiquing Extracts from the book “Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru”

Mwandishi anasema hivi:

Masuala ya Kujiuliza
Wazee wengi wenye kusimuliya simulizi za Mapinduzi ya Zanzibar ni wazee ambao wamebobea kwenye historia ya Mapinduzi. Ni wazee waliyokaa kitako mara nyingi na kukongeshwa kwenye viti vyao kwa fikra na mawazo ya muda mrefu ambayo hawajawahi kuwakabidhi watoto na wajukuu zao. Kitabu kinauliza masuala matatu ya msingi. Jawabu za masuala hayo zilimezwa xxvi Utangulizi na nyangumi aliyeamuwa kuzamiya au aliyezamishwa kwa makusudi kwenye bahari ya historia kwa zaidi ya miaka 46. Masuala ambayo msomaji wa kitabu hichi anafaa kuyazingatiya kwa umakini mkubwa ni haya yafuatayo:


1) Ufunuo wa Mapinduzi ya Zanzibar ndani ya kipindi cha maridhiyano baina ya Wazanzibari utaweza kuisaidiya Tanganyika kuisitisha mivutano iliyojitokeza kwa kuukaribisha mfungamano ndani ya Zanzibar ambayo ni sehemu ya pili ya Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar?


My critique of this point of the book:

Mwandishi ameshindwa vibaya sana sana kuonyesha ni njia gani itumike kuondoa magugu na mbegu za utengano na chuki hizi za leo ambazo zilipandikizwa na U-hizbu tangu kabla ya muungano (muungano haujapandikiza hizi chuki) ambapo Nyerere na Karume wamekuja kufanya kazi kubwa ya kuwaunganisha Ma-Hizbu na Ma-ASPs kwamba leo wanaweza kusoma skuli moja, darasa moja, chuo kimoja, bweni moja, msikiti mmoja, Kanisa moja, Jamatini moja, Hekalu moja, gereza moja, misibani, kwenye maulidi, markiti, mwaloni kwenye uchuuzi wa bidhaa za baharini za uchumi wa bluu, kukaa boti moja kwenda Pemba-Unguja-Tanga-Dsm-Mombasa nk.


2) Umoja wa maridhiyano baina ya Wazanzibari wenyewe kwa wenyewe, baina ya Wazanzibari na Watanganyika, na baina ya Waafrika Weusi na Waarabu Waafrika, utakuwa na faida gani kubwa za kisiasa na za kiuchumi kwa wananchi walio wengi wa Afrika Mashariki na Kati?


My critique of this point of the book:

Mwandisi hajaonyesha ni namna gani ambayo wafuasi wa Hizbu (akiwamo Jagina) wameishapata uhuru anaoubeza na wanaoupigia kelele. Hizbu wanaamini kuwa walio huru leo ni wafuasi wa ASP tu lakini wao Hizbu wanaamini bado wako kwenye minyororo ya utumwa wa Mwarabu lakini watumwa wanaokula vinono na kunywa sharubati za uhuru wa Mapinduzi wanayoyakataa na kutamani kubaki kwenye enzi kongwe za utumwa na ukoloni wa Mwarabu. Mwandishi hajaonyesha jinsi hawa wana Hizbu walivyokuwa ni watumwa wa aina ya pekee duniani ambao wanapatikana tu kwenye visiwa hivyo vya mwani na vanilla. Mtumwa anayemiliki mitaji, mashamba, haki za binadamu, haki ya kuchagua na kuchaguliwa, haki ya kiuhamiaji (Immigrationh Rights, ambayo wameipata kwa Wapemba na Waunguja kujazana Tz-Bara, Ulaya, Uarabuni na US) nk.


3) Madola makubwa ya Magharibi yalishiriki katika upangaji na utekelezaji wa Mapinduzi au waliyasaidiya kwa kuzidharau kwa makusudi taarifa za kiusalama walizokuwa nazo kwa sababu Mapinduzi na Muungano ilikuwa ni mihimili miwili yenye maslahi na wao zaidi kuliko maslahi ya Wazanzibari, ya Wazanzibari na Watanganyika, na ya Waafrika na Waarabu?


My critique of this point of the book:

Mwandishi anapungua (haenei) kwenye mzani wa uanazuoni wa viwango na hasa waliotabahari kwenye siasa za muungano duniani pale aliposhindwa kuwahakikishia Ma-Hizbu wenzake kuwa kamwe wasiote ndoto za sungura kwamba wanatarajia Mapinduzi ya pili ya kuong’oa uhuru uliokwishapatikana ili kuleta uhuru bandia wa mkataba na mwovu Mwarabu. Marekani ijitathmini kwanza kwanini imeshindwa kuungana na Mexico ndipo ije mbele kuchagiza utengano wa Zanzibar na Tanganyika. Aidha, Waarabu wao wanaungana kama ilivyo Ulaya na kwingineko ilhali masalia ya Ma-Hizbu wa Zanzibar wanadai utengano kwa gharama wasiyoweza kulipa kwa vizazi.


Dosari ndogondogo za Kitabu:

1. Hakikuhaririwa kwa uweledi (Only glossing over).

2. Isimu ni tatizo kubwa kwa Mwandishi na kushusha hadhi ya kitabu kwa kuvuruga agenda nyeti, mantiki na maudhui.

3. Muundo (structure), lafudhi na lahaja za Kiswahili alichotumia zina mgogoro wenyewe kwa wenyewe.

4. Mwandishi ameegemea u-diaspora na kutegemea kwa kiwango kikubwa taarifa hasi na pandikizi kuliko hali halisi iliyopo kwenye ground (biasness).

5. Namba 2 – 4 hapo juu zinathibitisha kuwa ametumia uandishi wa aina ya “creative writing” wa kubuni badala ya “empirical writing” Kwenye creative writing ametegemea tu table research (rejea ya machapisho). Hii inafanya kitabu chake kisifanye vizuri sokoni kwasababu kimesheheni hoja za ubunifu (usanii) zaidi kuliko hoja halisia zinazoweza kupatikana kwa tafiti za kwenda kwenye field.


Angalizo:

1. Kitabu hiki siyo Alpha na Omega. Wengi wameandika juu ya muungano kama akina Godfrey Mwakikagile, Harisson Mwakyembe (thesis), Greg Cameron, Haroub Othman (papers), Julius K. Nyerere (speeches), Kabudi Palamagamba (speeches), Pius Msekwa (articles) nk.

2. Masimulizi ya kweli yanayoweka uwiano mzuri wa mitazamo kuhusu Zanzibar na Mapinduzi ya 1964 yanapatikana kwenye kitabu cha “Masimulizi ya Sheikh Thabit Kombo Jecha” kilichoandikwa na Minael Hosanna O. Mdundo, dibaji na Mwl. Nyerere na kuhaririwa na Paul Sozigwa.

3. Changamoto ya msingi ya muungano tangu mwanzo ilikuwa ni hofu ya dola za Magharibi hasa US kuwa Zanzibar ingekuwa Cuba ya Afrika dhidi ya Ubepari wao na hofu hii pia walikuwa nayo kuhusu jitihada za ujenzi wa Ujamaa Ethiopia. Hofu hii ilipata nguvu kwa kuwekeza kwenye mawazo potofu ya wafuasi wa iliyokuwa Hizbu (chama cha Jagina).


Mapendekezo kuhusu kuulea muungano:

1. Muungano usijadiliwe kwa hisia za kiitikadi za makundi maslahi, ufumbuzi hautapatikana asilani.

2. Umma uaminishwe juu ya manufaa ya dhana ya “Umoja ni Nguvu, Utengano ni Udhaifu”

3. Ikampeniwe kwa bidii kubwa mikakati ya kuuendeleza muungano na ikanwe mikakati ya kuuvunja muungano.

4. Historia isipotoshwe na propaganda zisizotafitiwa.

5. Maboresho ya mitaala ifanyike ili kuwe na somo la muungano na uzalendo.


Hitimisho:

Kitabu hiki cha “Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru” kiondolewe sokoni (recall the book).

Truth That Hurts.

Kajifundishe kuandika ,

Ndio umeandika kitu gani hapo ??

Huko Kivukoni ndio mnavyofundishwa kuandika ??

Elimu ameiua Laanatullahi Nyerere, yaani ndio unajisifu umeandika la maana hapo ?
 
As a leader it is also a mistake to think that you need to have all the right answers all the time. Trying to be right all the time is stressful, slows progress and causes procrastination Skip Prichard, (2016).


Hivi umefika darasa la ngapi wewe ??
 
Kwa mujib wa taarifa ya mamlaka ya tabia nchi duniani Zanzibar inazama baada ya miaka 50 ijayo kwann tusiwape uhuru wao wajitegemee baadae wapige mbizi kuja Tanga na Dar, Bagamoyo, Mtwara waje na passport.
Maneno hayo ya Mamlaka hayo ya hali ya hewa uliyapata kanisani ??
 
Kwa mujib wa taarifa ya mamlaka ya tabia nchi duniani Zanzibar inazama baada ya miaka 50 ijayo kwann tusiwape uhuru wao wajitegemee baadae wapige mbizi kuja Tanga na Dar, Bagamoyo, Mtwara waje na passport.
Mkuu,
I can't hold my laughter for this comic piece!
 
Maneno hayo ya Mamlaka hayo ya hali ya hewa uliyapata kanisani ??
We pimbi ngoja tuwafukuze woote uanzia posta, kariakoo, magomeni mkajazane mpakanjia, bububu na mchambawima ndo mtaelewa
 
We pimbi ngoja tuwafukuze woote uanzia posta, kariakoo, magomeni mkajazane mpakanjia, bububu na mchambawima ndo mtaelewa
Elimu ya baba yako wa pili Nyerere ndio hiyo ?? Hata kujibu swali unashindwa ??

Sasa jibu swali


Maneno hayo ya Mamlaka hayo ya hali ya hewa uliyapata kanisani ??
 
Elimu ya baba yako wa pili Nyerere ndio hiyo ?? Hata kujibu swali unashindwa ??

Sasa jibu swali


Maneno hayo ya Mamlaka hayo ya hali ya hewa uliyapata kanisani ??
Sikia nendeni kwenu kwanza huku mnatubana kajitegemeeni hivi mnafikiri tunakosa nn bila nyie? Now we have goo naval force mtakuwa kama Taiwan, na muondoke woote huku Tanganyika
 
Elimu ya baba yako wa pili Nyerere ndio hiyo ?? Hata kujibu swali unashindwa ??

Sasa jibu swali


Maneno hayo ya Mamlaka hayo ya hali ya hewa uliyapata kanisani ??
Kanisa linahusikaje hapo? Why mention Kanisa in lieu of Mosque or Synagogue? Keep the Holy Houses of God away from the discussion as not everybody trust in God that you trust; nor prescribe from your favourite religious doctrine. Learn to relax in a complex cum hot situation that drags you to a loss of defensive points and render you unable to convince any mind. Ni ushauri tu nakupa mkuu Jagina.
 
Kanisa linahusikaje hapo? Why mention Kanisa in lieu of Mosque or Synagogue? Keep the Holy Houses of God away from the discussion as not everybody trust in God that you trust; nor prescribe from your favourite religious doctrine. Learn to relax in a complex cum hot situation that drags you to a loss of defensive points and render you unable to convince any mind. Ni ushauri tu nakupa mkuu Jagina.
Unatumia Id mbili ? Sisi wengine hichi kiengereza cha Chato hatukiwezi
 
Kwa mujib wa taarifa ya mamlaka ya tabia nchi duniani Zanzibar inazama baada ya miaka 50 ijayo kwann tusiwape uhuru wao wajitegemee baadae wapige mbizi kuja Tanga na Dar, Bagamoyo, Mtwara waje na passport.
Maldives itazama chini ya bahari katika miaka 80 ijayo.
REVEALED: This holiday hotspot is SINKING and will have disappeared within 80 years


Kiribati, Fiji na Marshall kuzama katika miaka 50
These Five Islands Could Be Underwater in as Little as 50 Years
 
mi naona pengo kubwa ni kwanza watuonyeshe Tanganyika ipo wapi kwenye huu muungano?
JPM angeendelea kuwepo huenda siku moja angefanya maamuzi magumu ya kurudisha Tanganyika. Alikuwa hahudhurii maadhimisho ya Mapinduzi Zanzibar (uhuru). Alitaka kufungulia Wanauamsho mara mbili akawa anazuiliwa kwamba asubirie kidogo. Alikuwa anaisaka Tanganyika kwa udi na uvumba kimyakimya lakini mauti yakamuwahi. Aliamini kwenye muungano wa 50 kwa 50 kama siyo 40 kwa 60.
 
JPM angeendelea kuwepo huenda siku moja angefanya maamuzi magumu ya kurudisha Tanganyika. Alikuwa hahudhurii maadhimisho ya Mapinduzi Zanzibar (uhuru). Alitaka kufungulia Wanauamsho mara mbili akawa anazuiliwa kwamba asubirie kidogo. Alikuwa anaisaka Tanganyika kwa udi na uvumba kimyakimya lakini mauti yakamuwahi. Aliamini kwenye muungano wa 50 kwa 50 kama siyo 40 kwa 60.
Soma ulichokiandika huko nyuma Na hichi ulichokiandika hapa , umechanganyikiwa au unaongeza pages Za uzi wako
 
Soma ulichokiandika huko nyuma Na hichi ulichokiandika hapa , umechanganyikiwa au unaongeza pages Za uzi wako
Sina shida kwa Tanganyika kupatikana, sina shida kwa Muungano kuendelea kuishi. Ulipaswa uniulize ninapenda mfumo upi wa Muungano?
 
Biblia ipi hiyo imeandika?
Jaribu kuwa makini na masuala ya imani za watu nakushauri tena! Kuna jukwaa la masuala ya imani unawezapatembelea na kupost huko. Extremism and Fundamentalism are twins b/o idea dropout.
 
Back
Top Bottom