LEGE
JF-Expert Member
- Oct 14, 2011
- 5,122
- 9,209
- Thread starter
-
- #1,221
PENELA SEASON 3
SEHEMU YA 28
MTUNZI : PATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Hii ni nafasi ambayo natakiwa kuitumia vizuri”akawaza Elibariki na kwa kasi ya aina yake akakinyakua chungu cha maua kilichokuwa karibu yake na kumpiga nacho Anitha Kichwani akaanguka na kupoteza fahamu.Akaikanyaga kanyaga simu ile akakimbia hadi katika mlango wa chumba cha Mathew na kujaribu kuufungua.Ulikuwa umefungwa.Akarudi nyuma hatua kadhaa na kuurukia teke mlango ule ukafunguka akaingia ndani na moja kwa moja akaeleka katika kile kisanduku chenye namba.Akabonyeza namba alizozikumbuka lakini mlango haukufunguka.
“ C’mon nimekosea wapi? Mbona namba alizobonyeza Mathew ni hizi hizi? Akajaribu tena lakini bado mlango haukufunguka
“Nimekumbuka kulikuwa na namba mbili mwisho nasi namba tano.”
Akarudia tena kubonyeza na safari hii kabati kubwa la ukutani likasogea pembeni na mlango ukafunguka kwa akaanza kushuka kuelekea chini
ENDELEA………………………
Jaji Elibariki akaufunguua mlango wa chumba alimowekwa Rosemary akaingia.Tayari Rosemary alikwisha pitiwa na usingizi. Elibariki akamuamsha.Rose akafumbua macho na kupatwa na mshangao mkubwa kwa kumuona Elibariki mle chumbani
“ Jaji ?!! akashangaa Rose
“ Rosemary amka” akasema Elibariki
“ jaji unafanya nini huku?
“ Rose I’ve come to free you” akasema jaji Elibariki huku akiangaza angaza kama angeweza kupata kitu chochote cha kumuwezesha kufungulia pingu alizofungwa Rosemary
“ You want to free me?akauliza Rosemary kwa mshangao
“ Ndiyo.Nataka nikuondoe hapa.”akajibu jaji Elibariki
“ jaji mbona sikuelewi? Unataka kunifungua? Unataka kunipeleka wapi?
“ Sikiliza Rose,hatuna muda mrefu hapa.Elibariki anaweza akatokea muda wowote na akinikuta huku tumekwisha kwa hiyo acha kuuliza maswali na unisadie mawazo namna ya kufungua pingu hizi ulizofungwa” akasema Elibariki
“ Hebu subiri kwanza jaji .Bado sijakuelewa unataka kufanya nini.Umesema unataka kunifungua? Unataka kunipeleka wapi? Akauliza Rose
“ Mathew hajanituma nikufungue lakini nimeamua mimi mwenyewe nikusaidie uweze kutoka humu ndani.Mathew hafahamu chochote juu ya hiki ninachokifanya”
“ Mathew hayupo?akauliza Rose
“Mathew hayupo ndiyo maana nimepata nafasi ya kuja humu.Unadhani angekuwepo ungeniona humu? Akauliza jaji Elibariki
“ jaji natamani sana nikuamini lakini ninasita.Wewe ni mshirika mkubwa wa Mathew unanishangaza sana kwa kitu unachotaka kukifanya.Are you betraying your friends? Akauliza Rose.Jaji Elibariki akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Rose acha kuuliza maswali mengi .Ninataka nikutoe humu.Unahakika Mathew atakuachia? Nakuhakikishia kwamba hanampango wowote wa kukuachia huru kwa hiyo naomba tafadhali ukubali nikusaidie.”akasema Elibariki.
“ kwa nini unafany ahivi Elibariki? Kwa niniunawasaliti wenzako kwa sababu yangu? Akauliza Rosemary.
“ Rose nina tatizo kubwa na nimeona ni wewe pekee unayeweza kunisaidia ndiyo maana nimelazimika kufanya hivi ..Kabla sijakufungua ninataka unihakikishie kwamba utanisaidia tatizo langu.”
“Ni tatizo gani ulilonalo na unalotaka nikusaidie?akauliza Rose
“ hatuna muda wa kupoteza Rose.Mathew anaweza akatokea hapa muda wowote kwa hiyo nitakueleza baada ya kuwa tumetoka hapa.”akasema jaji Elibariki.
“ Ok jaji tafuta kitu kidogo kama waya au sindano nikuonyeshe namna ya kufungua” akasema Rose.jaji Elibariki akatoka kwa kasi mle chumbani hadi katika chumba cha Mathew akaanza kupekua sehemu mbali mbali akitafuta kitu cha kumuwezesha kufungua pingu zile alizofungwa Rose.Katika mojwapo ya droo akaziona funguo ambazo alihisi zinaweza kuwa ni zakufungulia pingu zile.Kwa kasi akarejea chini na kweli kama alivyokuwa amehisi funguo zile ziliweza kufungua pingu na Rosemary akabaki huru.Alikuwa amechubukana mwli wake wote umatapakaa damu.
“ I’m free now”akasema Rosemary.
“ Lets get out of here” akasema jaji Elibariki akamsaidia Rose kushka katika kitanda hlafu akamtegemeza wakatoka mle ndani.Rosemary alikuwa akihisimaumivu makali kutokanna kukatwa vidole na Mathew.Walielekea hadi katika chumba cha ofisi.Rosemary akastuka alipomuna Anitha amelala sakafuni hana fahamu
“ Na huyu naye vipi?akauliza
“ Huyu ndiye aliyekuwepo humu ndani na alikuwa ni kikwazo kikubwa kwangu hivyo nikampiga na mtungi wa maua kichwani akazimia.Tusipoteze muda wapigie watu wako waje watuchukue haraka kabla Mathew hajarejea.” Akasema Elibariki huku akichukua waya na kumfunga Anitha miguu na mikono
Juu ya meza Rose akaiona simu yake pamoja na kompyuta yake akaichukua simu akaiwasha na kuongeana mtufulani simuni akamuhakikshia kwamaba yuko salama na akamuomba waje haraak wamchukue.Rose hakuwa akipafahamu mahala walipo,hivyo akampa Elibariki simu ili amuelekeze Yule jamaa..
“Mathew kaenda wapi? Akauliza Rose
“ Aliondoka na Peniela na sijui wameelekea wapi.” Akajibu Elibariki.
“ watu wako watachukua muda gani kufika hapa?akauliza Elibariki
“ Sijui watatumia muda gani lakini watajitahidi sana kufika ndaniya muda mfupi.” Akasema Rose huku akiichukua kompyuta yake
“ washenzi sana hawa vijana.Sintawasamehe kabisa kwa jambo walilonifanyia. “ akasema Rose
“ jaji kwa kitendo hiki ulichokifanya ujue umewasaliti wenzako na watakutafuta kila kona ya nchi hadi wahakikishe wamekupata.Una hakika kwamba unataka kufanya jambo hili? Akauliza Rose
“ Najua nimefanya jambo baya la kuwasaliti wenzangu lakini sina namna nyingine ya kufanya kutokana na matatizo niliyonayo ndiyo manaa nikaamua kukusaida kuwa huru ili na wewe unisaidie.”akasema Elibariki
“ Jaji umenifanyia jambo kubwa sana na lazima na mimi nikusaidiae katika matatizo yako.Watu wangu wanaweza kufika hapa muda wowote kwa hiyo nenda getini ukawasubiri ili wasipotea” akasema Rose na Elbariki akatoka mle ndani akaenda getini.
“ Nimewasaliti rafiki zangu .Nimefanya jambo baya sana lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya hivi nilivyofanya.Siwezi kukubali maisha yangu yawe niya kujificha humu ndani.”akawaza jaji Elibariki.
“ Katika maisha yangu sijawahi kukutana na vijana washenzi kama hawa.Bado sielewi mpaka leo hii wamewezaje kufanikiwa kunitia mikononi mwao.Tayari wamekwisha fahamu mambo mengi kuhusu mimi na kila ninachokifanya.Wameipekua kompyuta yangu kila mahala na wamegundua mambo mengi sana.Wamefahamu mambo yangu mengi ninayoyafanya,wamewafahamu washirika wangu wote.Ninaapa sintawasamehe hata kdogo.lazima niwafanyie kitu kibaya sana.Wameuwasha moto wenyewe na hawatauzima tena.Ni nani yuko nyuma yao? Lazima kuna mtu ambaye anawapa nguvu ya kuweza kufanya haya yote.Nina wasi wasi na Deus.Mimi na yeye kwa sasa ni maadui wakubwa na ninahisi yeye ndiye atakayekuwa nyuma ya hawa vijana na anawapa habari zangu kisha wakanivamia na kunishikilia.”akawaza Rose huku uso wake ukiwa umejikunja kwa hasira.Akaitazama mikono yake namna ilivyoumizwa ,akaviangalia vidole vyake vya miguu akakumbuka namna Mathew alivyovikata bila huruma..
“ Yule kijana amenisababishia ulemavu kwa kunikata vidolevyangu viwili.Amenitesa sana na kwa hili ninaapa sintomsamehe.Nitamsaka kila kona ya nchi hadi nihakikishe nimempata naye nimtese kama alivyonitesa mimi.Hataweza kunikimhia nina hakika ndaniyamuda mfupi nitakuwa nimempata.Mtandao wangu ni mkubwa na umesambaa kila kona.Nitampata tu.”akaendelea kuwaza Rose na kuketi kitini kwani alianza kuhisi maumivu mguuni.Akachukua simu yake na kuwapigia tena vijana wake kujua wamefika wapi na wakamuhakikishia kwamba wako karibu sana kufika.
“ Leo ninaiteketeza nyumba hii na watakaporejea watakuta imebaki majivu matupu na kila kitu chao kimeteketea .Lazima niwaonyeshe nguvu zangu.Wao na huyo anayewatuma watanitambua mimi ni nani.Watajuta kwa hiliwalilolianzisha .”akawaza Rose.
Baada ya dakika ishirini jaji Elibariki akaingia ofisini alimokuwa amekaa Rose akiwa ameongozana na vijana sita wakiwa na silaha.Vijana wale walistuka sana kwa haliwaliyomkuta nayo Rose.
“Pole sana madam.Who did this to you? Akauliza kijana mmoja aliyekuwa ameshika bastora na aliyeonekana ni kiongozi wa vijana wale.Rose akamtazama Elibariki kisha akatoa maelekezo kwa wale vijana wake
“Mkamateni huyo jamaa mfungeni,tunaondoka naye.Nimtu muhimu sana kwetu.Mwagieni petrol nyumba nzima na kisha tuichome moto nyumba yote.”akasema Rose na kisha akamuaangalia Anitha aliyekuwa amelala pale chini.
“Mchukueni hata huyu pia.Tunaondoka naye” akasema
“ Rose what is the meaning of this? We had an agreements!!!..jaji Elibariki akashangaa.
Rose akainuka akajitahidi kutembea kwa shida halafu akamnasa kofi.
“ You’ve betrayed your friends do you think I can believe you? Take him away ”Rose akawaamuru vijana wake.jaji Elibariki akafungwa pingu na kuanza kutolewa mle ndani.
“ Rose hivi sivyo tulivyokubaliana” akasema jaji Elibariki kwa nguvu lakini vijana wale wenye miili iliyojengeka wakamchukua kwa nguvu na kumfunga na kamba wakamrushia ndani ya gari.Anitha naye akachukuliwa na kurushwa ndani ya gari pamoja na Elibariki
“ Rose anafanya nini tena? Mbona anafanya kinyume na tulivyokubaliana?.Nimemsaidia kumuokoa lakini amenigeuka.Sikupaswa kabisa kumuamini huyu mwanamke.Maskini nyumba ya Mathew inataka kuteketezwa kwa moto.Sikujua kama huyu mwanamke ni mnyama kiasi hiki.”Mathew akastuliwa mawazoni na mlango uliofunguliwa na Naomi akarushwa ndani.
“ jaji nini kinaendelea? hawa watu ni akina nani? Tumevamiwa? mathew yuko wapi? Akauliza Naomi.
Vijana wawili wakamtegemeza Rose kwani alikuwa akisikia maumivu makali ya miguu kwa sababu ya vidole alivyokatwa na Mathew,wakampeleka katika gari.
Mlango wa nyumba ambayo Mathew huhifadhia magari yake ukavunjwa mle ndani yakakutwa magaloni manne ya mafuta ya akiba wakayachukua na kuyamimina ndani ya nyumba halafu wakapanda katika magari yao .Mmoja wao akawasha kiberiti akakirushia ndani na nyumba ikaanza kuwaka moto kisha wakaondoka.
“This is just the beginning .Wamenichokoza wao wenyewe na sasa ni zamu yangu kuwaonyesha mimi ni nani.Vijana wadogo kama wale hawawezi wakanifanya mimi namna hii.Wamenivamia nyumbani kwangu,wakamuua mpenzi wangu kwa risasi,wakaniteka na kunificha humu katika nyumba yao,wamenitesa mno na katu siwezi kukubali kuteswa na vijana wadogo kama hawa wasiokuwa na adabu hata chembe.Nitawasaka kila mahala na kuhakikisha nimewapata na mimi niwakate vidole vyao kama walivyonikata vyangu.Nitamsaka pia na anayewatumia ili kupambana na mimi ambaye nina hakika lazima atakuwa ni Deus.”akawaza Rosemary Mkozumi
.
*******
“ Peniela!..Peniela !!!..”akaita Mathew lakini Peniela hakuwa na nguvu kabisa.Umati wa watu ulianza kuongezeka katika mtaa ule wakija kushuhudia tukio lile la nyumba ya Peniela kuwaka moto .
Mathew akautazama moto ule mkubwa akavuta pumzi ndefu.
“ Hili si eneo salama tena.Team SC41 wameamua kuichoma nyumba ya Peniela kwa makusudi.They did this to me also and killed my wife.I have to save Peniela”akawaza Mathew na kumuinua Peniela akamuweka begani na kuondoka naye akapita kichochoro kadhaa na kutokea sehemu moja iliyokuwa na nyumba inayoendelea kujengwa akaingia ndani na kumlaza Peniela katika mojawapo ya chumba.Jasho jingi lilikuwa linamtoka akavua shati. Na kuanza kumpepea Peniela
“ Nilifanya vizuri kukataa kukaa pale kwa Peniela kama alivyokuwa ameniomba.Kumbe Team SC41 walikuwa wanamfuatilia kwa karibu sana kutaka kufahamu yuko wapi ,yuko na nani na anafanya nini.Hawa jamaa watamtafuta Peniela kila kona hadi wahakikishe wamempata kwani tayari wamekwisha gundua kwamba amewasaliti.Masikini Peniela jumba lake lote limeteketea kwa moto.Namuonea huruma sana kwa namna anavyoteseka.Ninaapa lazima nihakikishe kwamba ninamlinda kwa kila namna ninavyoweza.”akawaza Mathew na kisha akamuinamia peniea
“ Peniela ! Peniela..”akamtikisa kidogo na Peniela akafumba macho.
“ Ahsante Mungu:”akasema Mathew na kumuegemeza Peniela ukutani..
“ Unajisikiaje Peniela?akauliza Mathew
“ Mwili wote hauna nguvu kabisa.”akajbu Peniela
“Peniela.Jikaze kidogo na tondoke eneo hili.Eneo hili si salama kabisa kwetu kwa sasa”akasema Mathew
“ Mathew wamechoma nyumba yangu.Wameunguza nyumba yangu !! Peniela akaangua kilio
“ Shhh !!Peniela usilie tafadhali.Huu si wakati wa kulia”akasema Mathew
“ Mathew kila kitu changu wamekiteketeza.kwa nini wanifanyie hivi? Nimewafanyia mambo mangapi mazuri hadi wanifanyie hivi? akauliza Peniela huku machozi yakimwagika
“ peniela nadhani sasa umeelewa kwamba Team SC 41 si watu wazuri hata kidogo.Hata uwafanyie nini hawatakuthamini .Tunachotakiwa kufanya kwa sasa ni kuelekeza nguvu katika kuhakikisha kwamba tunaipata package kutoka kwa Dr Joshua na baada ya hapo tutawageukia Team SC41.Ninakuhakikishia Peniela kwamba nitapambana hadi nihakikishe tumelifyeka kabisa kundi lote la Team Sc41 hapa nchini .Usijali kuhsu vitu vyako vilivyoungua.Utavipata vingine” akasema Mathew.
“ Mathew siwezi kukuficha nimeishiwa nguvu kabisa.Sikuwahi kuhisi kama team Sc41 wanaweza wakafikia hatua ya kunifanyia kitu kama hiki na kusahau mambo yote mazuri niliyowafanyia.Kama wameweza kunichomea nyumba yangu na kila kitu changu basi dakika yote wakinipata wataniua.Nitafanya nini Mathew?akauliza Peniela
“Peniela nitakulinda .Niamini nikwambiavyo kwamba nitakulinda” akasema Mathew
“ Mathew I don’t know if I can do this anymore”akasema Peniela.mathew akamuangalia
“Peniela anahitaji muda wa kutuliza akili yake.Tukio lile la kuishuhudia nyumba yake inateketekea limemuumiza sana” akawaza Mathew halafu akapapasa katika mifuko yake akachukua simu yake akaitazama kama iko salama
“ Thanks God simu yangu iko salama hata baada ya rabsha zile zote”akawaza Mathew na kuzitafuta namba za simu za Anitha akampigia.
“Hallow Mathew .What happened? Akauliza Anitha
“ Anitha tumepatwa na matatizo.Nahitaji msaada.Nataka uchukue gari utufuate sehemu nitakayokuelekeza ili uje utuchukue kwani Peniela hawezi kutembea.” Akasema Mathew lakini hakusikia Anitha akimjibu
“Anitha umenisikia? Akauliza lakini bado kulikuwa kimya na mara simu katika.Akapiga tena lakini simu ya Anitha haikuwa ikipatikana,akapiga namba nyingine za simu zilizomo mle ofisini lakini zote hazikupokelewa.
“ What happened? Kwa nini Anitha hataki kupokea simu? Akajiuliza
“ Nimeanza kuwa na hisia mbaya kwanini Anitha akatike ghafla simuni? Anyway ngoja nitafute msaada sehemu nyingine tena.Nani anayeweza kunisaidia muda huu? Akajiuliza Mathew
“ jason !..japokuwa mara ya mwisho tulikwaruzana lakini nina hakika akisikia kuhusu peniela lazima atakuwa tayari kumsaidia”akawaza Mathew na kuzitafuta namba za simu za Jason akampigia .Simu ikaita mara ya kwanza na kukatika.Ikaita mara ya pili ikapokelewa
“ Hallow Mathew” akasema jason
“ Jason samahani kwa kukupigia usiku huu.Nina shida nahitaji msaada wako.”
“Mathew I cant help you .Mara ya mwisho tulipoachana wakati tukitoka kwa John mwaulaya ulinitamkia maneno mabaya sana ya dharau . Siwezi kukusaidia Mathew hata iweje” akasema Jason
“ Josh its peniela.If you cant help me then help her” akasema Mathew
“ Peniela kafanya nini?
“Amepatwa na tatizo na anahitaji msaada”
Jason alipotajiwa jina la Peniela alishindwa kukataa,Mathew akamuelekeza sehemu ambayo atawakuta .
“ peniela nimempigia simu jason anatufuata .Jikaze tuondoke tuelekee sehemu ambayo tutakutana.” akasema Mathew akamuinua peniela wakatoka nje ya lile jumba.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………
SEHEMU YA 28
MTUNZI : PATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Hii ni nafasi ambayo natakiwa kuitumia vizuri”akawaza Elibariki na kwa kasi ya aina yake akakinyakua chungu cha maua kilichokuwa karibu yake na kumpiga nacho Anitha Kichwani akaanguka na kupoteza fahamu.Akaikanyaga kanyaga simu ile akakimbia hadi katika mlango wa chumba cha Mathew na kujaribu kuufungua.Ulikuwa umefungwa.Akarudi nyuma hatua kadhaa na kuurukia teke mlango ule ukafunguka akaingia ndani na moja kwa moja akaeleka katika kile kisanduku chenye namba.Akabonyeza namba alizozikumbuka lakini mlango haukufunguka.
“ C’mon nimekosea wapi? Mbona namba alizobonyeza Mathew ni hizi hizi? Akajaribu tena lakini bado mlango haukufunguka
“Nimekumbuka kulikuwa na namba mbili mwisho nasi namba tano.”
Akarudia tena kubonyeza na safari hii kabati kubwa la ukutani likasogea pembeni na mlango ukafunguka kwa akaanza kushuka kuelekea chini
ENDELEA………………………
Jaji Elibariki akaufunguua mlango wa chumba alimowekwa Rosemary akaingia.Tayari Rosemary alikwisha pitiwa na usingizi. Elibariki akamuamsha.Rose akafumbua macho na kupatwa na mshangao mkubwa kwa kumuona Elibariki mle chumbani
“ Jaji ?!! akashangaa Rose
“ Rosemary amka” akasema Elibariki
“ jaji unafanya nini huku?
“ Rose I’ve come to free you” akasema jaji Elibariki huku akiangaza angaza kama angeweza kupata kitu chochote cha kumuwezesha kufungulia pingu alizofungwa Rosemary
“ You want to free me?akauliza Rosemary kwa mshangao
“ Ndiyo.Nataka nikuondoe hapa.”akajibu jaji Elibariki
“ jaji mbona sikuelewi? Unataka kunifungua? Unataka kunipeleka wapi?
“ Sikiliza Rose,hatuna muda mrefu hapa.Elibariki anaweza akatokea muda wowote na akinikuta huku tumekwisha kwa hiyo acha kuuliza maswali na unisadie mawazo namna ya kufungua pingu hizi ulizofungwa” akasema Elibariki
“ Hebu subiri kwanza jaji .Bado sijakuelewa unataka kufanya nini.Umesema unataka kunifungua? Unataka kunipeleka wapi? Akauliza Rose
“ Mathew hajanituma nikufungue lakini nimeamua mimi mwenyewe nikusaidie uweze kutoka humu ndani.Mathew hafahamu chochote juu ya hiki ninachokifanya”
“ Mathew hayupo?akauliza Rose
“Mathew hayupo ndiyo maana nimepata nafasi ya kuja humu.Unadhani angekuwepo ungeniona humu? Akauliza jaji Elibariki
“ jaji natamani sana nikuamini lakini ninasita.Wewe ni mshirika mkubwa wa Mathew unanishangaza sana kwa kitu unachotaka kukifanya.Are you betraying your friends? Akauliza Rose.Jaji Elibariki akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Rose acha kuuliza maswali mengi .Ninataka nikutoe humu.Unahakika Mathew atakuachia? Nakuhakikishia kwamba hanampango wowote wa kukuachia huru kwa hiyo naomba tafadhali ukubali nikusaidie.”akasema Elibariki.
“ kwa nini unafany ahivi Elibariki? Kwa niniunawasaliti wenzako kwa sababu yangu? Akauliza Rosemary.
“ Rose nina tatizo kubwa na nimeona ni wewe pekee unayeweza kunisaidia ndiyo maana nimelazimika kufanya hivi ..Kabla sijakufungua ninataka unihakikishie kwamba utanisaidia tatizo langu.”
“Ni tatizo gani ulilonalo na unalotaka nikusaidie?akauliza Rose
“ hatuna muda wa kupoteza Rose.Mathew anaweza akatokea hapa muda wowote kwa hiyo nitakueleza baada ya kuwa tumetoka hapa.”akasema jaji Elibariki.
“ Ok jaji tafuta kitu kidogo kama waya au sindano nikuonyeshe namna ya kufungua” akasema Rose.jaji Elibariki akatoka kwa kasi mle chumbani hadi katika chumba cha Mathew akaanza kupekua sehemu mbali mbali akitafuta kitu cha kumuwezesha kufungua pingu zile alizofungwa Rose.Katika mojwapo ya droo akaziona funguo ambazo alihisi zinaweza kuwa ni zakufungulia pingu zile.Kwa kasi akarejea chini na kweli kama alivyokuwa amehisi funguo zile ziliweza kufungua pingu na Rosemary akabaki huru.Alikuwa amechubukana mwli wake wote umatapakaa damu.
“ I’m free now”akasema Rosemary.
“ Lets get out of here” akasema jaji Elibariki akamsaidia Rose kushka katika kitanda hlafu akamtegemeza wakatoka mle ndani.Rosemary alikuwa akihisimaumivu makali kutokanna kukatwa vidole na Mathew.Walielekea hadi katika chumba cha ofisi.Rosemary akastuka alipomuna Anitha amelala sakafuni hana fahamu
“ Na huyu naye vipi?akauliza
“ Huyu ndiye aliyekuwepo humu ndani na alikuwa ni kikwazo kikubwa kwangu hivyo nikampiga na mtungi wa maua kichwani akazimia.Tusipoteze muda wapigie watu wako waje watuchukue haraka kabla Mathew hajarejea.” Akasema Elibariki huku akichukua waya na kumfunga Anitha miguu na mikono
Juu ya meza Rose akaiona simu yake pamoja na kompyuta yake akaichukua simu akaiwasha na kuongeana mtufulani simuni akamuhakikshia kwamaba yuko salama na akamuomba waje haraak wamchukue.Rose hakuwa akipafahamu mahala walipo,hivyo akampa Elibariki simu ili amuelekeze Yule jamaa..
“Mathew kaenda wapi? Akauliza Rose
“ Aliondoka na Peniela na sijui wameelekea wapi.” Akajibu Elibariki.
“ watu wako watachukua muda gani kufika hapa?akauliza Elibariki
“ Sijui watatumia muda gani lakini watajitahidi sana kufika ndaniya muda mfupi.” Akasema Rose huku akiichukua kompyuta yake
“ washenzi sana hawa vijana.Sintawasamehe kabisa kwa jambo walilonifanyia. “ akasema Rose
“ jaji kwa kitendo hiki ulichokifanya ujue umewasaliti wenzako na watakutafuta kila kona ya nchi hadi wahakikishe wamekupata.Una hakika kwamba unataka kufanya jambo hili? Akauliza Rose
“ Najua nimefanya jambo baya la kuwasaliti wenzangu lakini sina namna nyingine ya kufanya kutokana na matatizo niliyonayo ndiyo manaa nikaamua kukusaida kuwa huru ili na wewe unisaidie.”akasema Elibariki
“ Jaji umenifanyia jambo kubwa sana na lazima na mimi nikusaidiae katika matatizo yako.Watu wangu wanaweza kufika hapa muda wowote kwa hiyo nenda getini ukawasubiri ili wasipotea” akasema Rose na Elbariki akatoka mle ndani akaenda getini.
“ Nimewasaliti rafiki zangu .Nimefanya jambo baya sana lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya hivi nilivyofanya.Siwezi kukubali maisha yangu yawe niya kujificha humu ndani.”akawaza jaji Elibariki.
“ Katika maisha yangu sijawahi kukutana na vijana washenzi kama hawa.Bado sielewi mpaka leo hii wamewezaje kufanikiwa kunitia mikononi mwao.Tayari wamekwisha fahamu mambo mengi kuhusu mimi na kila ninachokifanya.Wameipekua kompyuta yangu kila mahala na wamegundua mambo mengi sana.Wamefahamu mambo yangu mengi ninayoyafanya,wamewafahamu washirika wangu wote.Ninaapa sintawasamehe hata kdogo.lazima niwafanyie kitu kibaya sana.Wameuwasha moto wenyewe na hawatauzima tena.Ni nani yuko nyuma yao? Lazima kuna mtu ambaye anawapa nguvu ya kuweza kufanya haya yote.Nina wasi wasi na Deus.Mimi na yeye kwa sasa ni maadui wakubwa na ninahisi yeye ndiye atakayekuwa nyuma ya hawa vijana na anawapa habari zangu kisha wakanivamia na kunishikilia.”akawaza Rose huku uso wake ukiwa umejikunja kwa hasira.Akaitazama mikono yake namna ilivyoumizwa ,akaviangalia vidole vyake vya miguu akakumbuka namna Mathew alivyovikata bila huruma..
“ Yule kijana amenisababishia ulemavu kwa kunikata vidolevyangu viwili.Amenitesa sana na kwa hili ninaapa sintomsamehe.Nitamsaka kila kona ya nchi hadi nihakikishe nimempata naye nimtese kama alivyonitesa mimi.Hataweza kunikimhia nina hakika ndaniyamuda mfupi nitakuwa nimempata.Mtandao wangu ni mkubwa na umesambaa kila kona.Nitampata tu.”akaendelea kuwaza Rose na kuketi kitini kwani alianza kuhisi maumivu mguuni.Akachukua simu yake na kuwapigia tena vijana wake kujua wamefika wapi na wakamuhakikishia kwamba wako karibu sana kufika.
“ Leo ninaiteketeza nyumba hii na watakaporejea watakuta imebaki majivu matupu na kila kitu chao kimeteketea .Lazima niwaonyeshe nguvu zangu.Wao na huyo anayewatuma watanitambua mimi ni nani.Watajuta kwa hiliwalilolianzisha .”akawaza Rose.
Baada ya dakika ishirini jaji Elibariki akaingia ofisini alimokuwa amekaa Rose akiwa ameongozana na vijana sita wakiwa na silaha.Vijana wale walistuka sana kwa haliwaliyomkuta nayo Rose.
“Pole sana madam.Who did this to you? Akauliza kijana mmoja aliyekuwa ameshika bastora na aliyeonekana ni kiongozi wa vijana wale.Rose akamtazama Elibariki kisha akatoa maelekezo kwa wale vijana wake
“Mkamateni huyo jamaa mfungeni,tunaondoka naye.Nimtu muhimu sana kwetu.Mwagieni petrol nyumba nzima na kisha tuichome moto nyumba yote.”akasema Rose na kisha akamuaangalia Anitha aliyekuwa amelala pale chini.
“Mchukueni hata huyu pia.Tunaondoka naye” akasema
“ Rose what is the meaning of this? We had an agreements!!!..jaji Elibariki akashangaa.
Rose akainuka akajitahidi kutembea kwa shida halafu akamnasa kofi.
“ You’ve betrayed your friends do you think I can believe you? Take him away ”Rose akawaamuru vijana wake.jaji Elibariki akafungwa pingu na kuanza kutolewa mle ndani.
“ Rose hivi sivyo tulivyokubaliana” akasema jaji Elibariki kwa nguvu lakini vijana wale wenye miili iliyojengeka wakamchukua kwa nguvu na kumfunga na kamba wakamrushia ndani ya gari.Anitha naye akachukuliwa na kurushwa ndani ya gari pamoja na Elibariki
“ Rose anafanya nini tena? Mbona anafanya kinyume na tulivyokubaliana?.Nimemsaidia kumuokoa lakini amenigeuka.Sikupaswa kabisa kumuamini huyu mwanamke.Maskini nyumba ya Mathew inataka kuteketezwa kwa moto.Sikujua kama huyu mwanamke ni mnyama kiasi hiki.”Mathew akastuliwa mawazoni na mlango uliofunguliwa na Naomi akarushwa ndani.
“ jaji nini kinaendelea? hawa watu ni akina nani? Tumevamiwa? mathew yuko wapi? Akauliza Naomi.
Vijana wawili wakamtegemeza Rose kwani alikuwa akisikia maumivu makali ya miguu kwa sababu ya vidole alivyokatwa na Mathew,wakampeleka katika gari.
Mlango wa nyumba ambayo Mathew huhifadhia magari yake ukavunjwa mle ndani yakakutwa magaloni manne ya mafuta ya akiba wakayachukua na kuyamimina ndani ya nyumba halafu wakapanda katika magari yao .Mmoja wao akawasha kiberiti akakirushia ndani na nyumba ikaanza kuwaka moto kisha wakaondoka.
“This is just the beginning .Wamenichokoza wao wenyewe na sasa ni zamu yangu kuwaonyesha mimi ni nani.Vijana wadogo kama wale hawawezi wakanifanya mimi namna hii.Wamenivamia nyumbani kwangu,wakamuua mpenzi wangu kwa risasi,wakaniteka na kunificha humu katika nyumba yao,wamenitesa mno na katu siwezi kukubali kuteswa na vijana wadogo kama hawa wasiokuwa na adabu hata chembe.Nitawasaka kila mahala na kuhakikisha nimewapata na mimi niwakate vidole vyao kama walivyonikata vyangu.Nitamsaka pia na anayewatumia ili kupambana na mimi ambaye nina hakika lazima atakuwa ni Deus.”akawaza Rosemary Mkozumi
.
*******
“ Peniela!..Peniela !!!..”akaita Mathew lakini Peniela hakuwa na nguvu kabisa.Umati wa watu ulianza kuongezeka katika mtaa ule wakija kushuhudia tukio lile la nyumba ya Peniela kuwaka moto .
Mathew akautazama moto ule mkubwa akavuta pumzi ndefu.
“ Hili si eneo salama tena.Team SC41 wameamua kuichoma nyumba ya Peniela kwa makusudi.They did this to me also and killed my wife.I have to save Peniela”akawaza Mathew na kumuinua Peniela akamuweka begani na kuondoka naye akapita kichochoro kadhaa na kutokea sehemu moja iliyokuwa na nyumba inayoendelea kujengwa akaingia ndani na kumlaza Peniela katika mojawapo ya chumba.Jasho jingi lilikuwa linamtoka akavua shati. Na kuanza kumpepea Peniela
“ Nilifanya vizuri kukataa kukaa pale kwa Peniela kama alivyokuwa ameniomba.Kumbe Team SC41 walikuwa wanamfuatilia kwa karibu sana kutaka kufahamu yuko wapi ,yuko na nani na anafanya nini.Hawa jamaa watamtafuta Peniela kila kona hadi wahakikishe wamempata kwani tayari wamekwisha gundua kwamba amewasaliti.Masikini Peniela jumba lake lote limeteketea kwa moto.Namuonea huruma sana kwa namna anavyoteseka.Ninaapa lazima nihakikishe kwamba ninamlinda kwa kila namna ninavyoweza.”akawaza Mathew na kisha akamuinamia peniea
“ Peniela ! Peniela..”akamtikisa kidogo na Peniela akafumba macho.
“ Ahsante Mungu:”akasema Mathew na kumuegemeza Peniela ukutani..
“ Unajisikiaje Peniela?akauliza Mathew
“ Mwili wote hauna nguvu kabisa.”akajbu Peniela
“Peniela.Jikaze kidogo na tondoke eneo hili.Eneo hili si salama kabisa kwetu kwa sasa”akasema Mathew
“ Mathew wamechoma nyumba yangu.Wameunguza nyumba yangu !! Peniela akaangua kilio
“ Shhh !!Peniela usilie tafadhali.Huu si wakati wa kulia”akasema Mathew
“ Mathew kila kitu changu wamekiteketeza.kwa nini wanifanyie hivi? Nimewafanyia mambo mangapi mazuri hadi wanifanyie hivi? akauliza Peniela huku machozi yakimwagika
“ peniela nadhani sasa umeelewa kwamba Team SC 41 si watu wazuri hata kidogo.Hata uwafanyie nini hawatakuthamini .Tunachotakiwa kufanya kwa sasa ni kuelekeza nguvu katika kuhakikisha kwamba tunaipata package kutoka kwa Dr Joshua na baada ya hapo tutawageukia Team SC41.Ninakuhakikishia Peniela kwamba nitapambana hadi nihakikishe tumelifyeka kabisa kundi lote la Team Sc41 hapa nchini .Usijali kuhsu vitu vyako vilivyoungua.Utavipata vingine” akasema Mathew.
“ Mathew siwezi kukuficha nimeishiwa nguvu kabisa.Sikuwahi kuhisi kama team Sc41 wanaweza wakafikia hatua ya kunifanyia kitu kama hiki na kusahau mambo yote mazuri niliyowafanyia.Kama wameweza kunichomea nyumba yangu na kila kitu changu basi dakika yote wakinipata wataniua.Nitafanya nini Mathew?akauliza Peniela
“Peniela nitakulinda .Niamini nikwambiavyo kwamba nitakulinda” akasema Mathew
“ Mathew I don’t know if I can do this anymore”akasema Peniela.mathew akamuangalia
“Peniela anahitaji muda wa kutuliza akili yake.Tukio lile la kuishuhudia nyumba yake inateketekea limemuumiza sana” akawaza Mathew halafu akapapasa katika mifuko yake akachukua simu yake akaitazama kama iko salama
“ Thanks God simu yangu iko salama hata baada ya rabsha zile zote”akawaza Mathew na kuzitafuta namba za simu za Anitha akampigia.
“Hallow Mathew .What happened? Akauliza Anitha
“ Anitha tumepatwa na matatizo.Nahitaji msaada.Nataka uchukue gari utufuate sehemu nitakayokuelekeza ili uje utuchukue kwani Peniela hawezi kutembea.” Akasema Mathew lakini hakusikia Anitha akimjibu
“Anitha umenisikia? Akauliza lakini bado kulikuwa kimya na mara simu katika.Akapiga tena lakini simu ya Anitha haikuwa ikipatikana,akapiga namba nyingine za simu zilizomo mle ofisini lakini zote hazikupokelewa.
“ What happened? Kwa nini Anitha hataki kupokea simu? Akajiuliza
“ Nimeanza kuwa na hisia mbaya kwanini Anitha akatike ghafla simuni? Anyway ngoja nitafute msaada sehemu nyingine tena.Nani anayeweza kunisaidia muda huu? Akajiuliza Mathew
“ jason !..japokuwa mara ya mwisho tulikwaruzana lakini nina hakika akisikia kuhusu peniela lazima atakuwa tayari kumsaidia”akawaza Mathew na kuzitafuta namba za simu za Jason akampigia .Simu ikaita mara ya kwanza na kukatika.Ikaita mara ya pili ikapokelewa
“ Hallow Mathew” akasema jason
“ Jason samahani kwa kukupigia usiku huu.Nina shida nahitaji msaada wako.”
“Mathew I cant help you .Mara ya mwisho tulipoachana wakati tukitoka kwa John mwaulaya ulinitamkia maneno mabaya sana ya dharau . Siwezi kukusaidia Mathew hata iweje” akasema Jason
“ Josh its peniela.If you cant help me then help her” akasema Mathew
“ Peniela kafanya nini?
“Amepatwa na tatizo na anahitaji msaada”
Jason alipotajiwa jina la Peniela alishindwa kukataa,Mathew akamuelekeza sehemu ambayo atawakuta .
“ peniela nimempigia simu jason anatufuata .Jikaze tuondoke tuelekee sehemu ambayo tutakutana.” akasema Mathew akamuinua peniela wakatoka nje ya lile jumba.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………