Peniela (Story ya kijasusi)

Peniela (Story ya kijasusi)

LEGE ukipata nafasi so mbaya ukashusha hata vi4 uache tunahangaika navyo mkuu.
 
Mkuu Mwandishi Hayuko Fair kbs hata kama Eli alimkosea Paniela lakini anachotaka kukifanya Paniela ni kibaya zaidi binafs nimefura hasira toka nimeanza kusoma hii kitu Hakuna sehem iloniudhi kama hii
Mkuu LEGE hizo hata usipo zileta binafs Sijafurahishwa kbs
mkuu hii story ni nzuri sana na haya mambo na visa kama hivi ndio vinanogesha sana na kuifanya iwe ya tofauti kwa mpangilio wa visa .
 
Mkuu LEGE Kama una uhakika Mathew hato mkula Paniela Basi Idondoshe Story
Ila kama watakulana Tafadhali sana Mkuu Usiniharibie Siku
Ombi kwako LEGE
hahaha mkuu mbona sasa mm napenda amtafune,asuuze rungu ili apate munkari wa kupiga kazi.ngale zimemzidia sana
 
Kuna wenzangu na mie tuliokuwa tunahangaika kuchungukia CAS na NOAS kila mara. Lege umetusaidia sana maana ukiendelea yaani tarehe 23 itafika faster.
 
peniela weeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
PENIELA SEASON 3

SEHEMU YA 26


MTUNZI : PATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ Elibariki amenifanyia kitendo cha aibu sana na ameniumiza mno.Nilimpenda sana lakini kwa kitendo alichokifanya sitaki tena kuendelea naye.Nimeanza kuvutiwa na Mathew.Ni kijana mzuri anajitambua na kujiheshimu tofauti na Elibariki ambaye anaonekana kuwa na tamaa.Mathew anaonekana ni mtu mwenye msimamo kwani toka mke wake alipofariki hajawahi kujiingiza tena katika mapenzi na mwanamke mwingine .Sina hakika kama ananipenda lakini nina hakika na kitu kimoja kwamba ana hisa Fulani juu yangu.Nina uhakika huo kutokana na namna alivyokuwa ananiangalia .Hii ni sehemu nzuri kwa kuanzia .” akawaza Peniela.
Aliandaa chakula chepesi haraka haraka kisha akarejea chumbani .Bado Mathew alikuwa amekaa katika jaccuzi akioga.Kichwa chake kilijaa mawazomengi sana.Mara mlango wa bafu ukafunguliwa akaingia peniela akiwa amejifunga taulo.Mathew macho yakamtoka pima.Peniela akamtazama akatabasamu na kusema
“ Mbona umestuka Mathew? Umestuka kuniona hivi? Akauliza Peniela huku akitoa kichekokidogo

“ Usiogope Mathew kwani hakuna kitu ambacho hujakiona.”akasema Peniela na kuliangusha taulo akabaki mtupu.



ENDELEA……………………………


“ Ouh my God !!..Huyu Peniela anataka kufanya nini ? Mbona ananiingiza katika jaribu kubwa ? Akawaza Mathew huku mwili ukimsisimka kwa kuushuhudia wazi wazi mwili ule mwororo wa Peniela uliokuwa uking’aa kama malaika.
Huku akitabasamu,Peniela akaingia ndani ya jaccuzi ,Mathew akabaki anamtazama.Ghafla Picha ya moto mkubwa ukiiteketeza nyumba yake ambayo ndani yake walikuwemo mke wake na wanae wawili ikamjia tena kichwani , akainuka na kutoka ndani ya jaccuzi akaelekea chumbani na kuvaa nguo zake.Peniela akashangaa sana naye akatoka ndani ya jaccuzi akamfuata Mathew chumbani.Alikuwa mtupu.Mathew akachukua taulo na kumvalisha

“ Mathew what’s wrong? Unaogopa nini? Akauliza Peniela huku akionyesha kushangaa

“ C’mon Mathew.Usiogope tafadhali “ akasema Peniela.

“ I cant do that Peniela .Tafadhali nenda kaoge kisha tuondoke “ akasema Mathew

“ Mathew usiwe muoga namna hiyo.No body is watching us.Its just me and you.Tafadhali Mathew naomba unisaidie kuniondolea machungu ya kuumizwa na Elibariki.I need you just for few minutes”
“ Peniela naomba unielewe kwamba siwezi kufanya kitu hicho unachotaka tufanye” Mathew akaendelea kusisitiza.Peniela akamfuata na kusimama karibu yake akamtazama kwa macho yake malegevu na kusema

“ Mathew its been years since your wife passed away so you need this.Najua unahitaji sana kufanya mapenzi na mimi na ndiyo maana hata sasa nyeti zako zimefura.Tafadhali usiendele kujitesa Mathew.Let us do it”

“ Peniela nimekwisha kwambia kwamba siwezi kufanya hicho kitu.Ni kweli mke wangu amefariki muda mrefu sasa na toka alipofariki sijajihusisha tena katika mahusiano na sitaki kufanya hivyo.”
“ Kwa nini Mathew unajitesa hivyo? Akauliza Peniela

“ Because I still love her !! akajibu Mathew

“ Hahahaha Mathew ,your wife is gone and she will never come back so you have to move on.Mathew naomba nikuweke wazi kwamba ninakutamani sana na mwili wangu uko tayari kwa ajili ya kukufurahisha .Please Mathew…” akasema Peniela.Mathew akaitazama saa yake na kusema
“ Peniela muda unakwenda sana.Kesho ni siku ndefu na tuna kazi nyingi kwa hiyo jiandae tuondoke.Utanikuta ninakusubiri sebuleni” akasema Mathew na kuanza kupiga hatua kuondoka mle chumbani.Peniela akamuita
“ Mathew !!..
Mathew akageuka na kumtazama

“ Mathew are you sure that you don’t want to make love with me? Akauliza Peniela.Mathew akamtazama na kusema

“ Yes ! I’m sure”
Peniela akamsogelea na kusema

“ Ninajifahamu mimi ni mzuri na uzuri wangu ni kama ua lenye harufu nzuri ambalo huwavutia nyuki kutua na kuling’ang’ania .Sifahamu ni kitu gani ninacho ambacho huwafanya wanaume wachanganyikiwe na mimi na hiyo imenifanya niamini kwamba hakuna mwanaume ambaye nitamtaka katika hii dunia ataniambia hapana na haijawahi kunitokea kwa mwanaume kuniambia hapana lakini kwa usiku wa leo kwa mara ya kwanza nimekutana na mwanaume ambaye amenitazama nikiwa mtupu akanitazama machoni na kuniambia Hapana.Si kunitamkia tu neno hilo bali ameokota taulo na kunivisha ili asiendelee kunitazama nikiwa mtupu.Wanaume wengine wote hufurahi na kuchanganyikiwa wakiniona nikiwa mtupu lakini kwako imekuwa tofauti.Mathew thank you so much.Kitendo cha kunikatalia kufanya mapenzi usiku huu kimeonyesha ni namna gani unavyonithamini.Uliokota taulo na kunivisha kunionyesha kwamba mwili wangu una thamani kubwa na hautakiwi kuachwa utupu bila sababu.Mathew wewe ni wa kipekee kabisa na kitendo hiki cha leo kimenifanya nizidi kutamani kukufahamu zaidi kwani nahisi bado sijakufahamu vizuri wewe ni mtu wa aina gani.You are different from all men I know ” akasema Peniela.Mathew akamtazama na kusema
“ Tukiwa nyumbani uliniuliza swali ni mwanamke wa aina gani ninayemuona ndani yako na nikakujibu kwamba ninapokuona ninamuona mwanamke jasiri,mwenye ndoto na ambaye yuko tayari kwenda hadi ncha ya mwisho wa dunia ili azitimize ndoto zake,mwanamke asiye kata tamaa ,mwanamke mwenye nguvu kubwa ndani yake licha ya mwili wake kuwa mdogo, mwanamke mwenye sauti laini lakini inayoweza kupenya hadi ndani ya mioyo ya watu wenye nguvu na wakavifunga vinywa vyao kumsikia.Mwanamke wa aina hii ni mwanamke ambaye binafsi ninamuheshimu sana zaidi ya ninavyoweza kueleza na sistahili hata kuugusa mwili wake.Peniela hata mimi ni binadamu na nina matamanio kama wengine na ninakiri kwamba hili ni jaribu langu kubwa sana kuwahi kunitokea lakini siwezi kuuchezea mwili wako kwa sababu ninakuheshimu sana ,na ninaomba nikuweke wazi kwamba moyo wangu unaniuma sana pale ambapo mwili wako hutumika kufanikisha baadhi ya mambo kama ilivyotokea leo kwa Deus.Ili kupata taarifa tulizohitaji ulilazimika kuutoa sadaka mwili wako na ndipo akakueleza kile tunachokitaka.Mwili wako umegeuzwa bidhaa and no body cares..jambo hili linaniumiza sana na ndiyo maana ninasema kwamba muda sio mrefu jambo hili litafikia mwisho na utaishi maisha yako kwa uhuru na amani na wala hutalazimika tena kuutumia mwili wako huu wa thamani kubwa kwa ajili ya kupata taarifa mbali mbali kama ufanyavyo sasa kwani katika wakati huo hakutakuwa tena na team SC 41. “ akasema Mathew . Peniela akashindwa kujizuia akamfuata na kumkumbatia kwa nguvu huku machozi yakimtoka.
“ Mathew ulikuwa wapi? Wewe nI mwanaume ambaye nilikuwa ninakuhitaji sana katika maisha yangu.Ee Mungu Ahsante sana kwa kuniletea kijana huyu ambaye ndiye haswa niliyekuwa ninamtafuta katika maisha yangu.Ananijali na kunithamini huyu ndiye atakayenifaa . Huyu ndiye mwanaume wa maisah yangu. “ akawaza Peniela
“ Thank you Mathew.Thank you so much.Sina neno la kusema kwa hayo maneno mazito uliyoyatamka” akasema Peniela huku machozi yakimdondoka.Mathew akamfuta machozi na kusema
“ Peniela muda unakwenda kwa kasi kwa hiyo jiandae ili tuweze kuondoka” akasema Mathew na kuitoa mikono ya Peniela iliyokuwa imeng’ang’ania halafu akafungua mlango wa chumbani na kutoka akaelekea sebuleni
“ Ee Mungu ahsante kwa kunipa nguvu ya kulishinda jaribu hili kubwa.Haikuwa rahisi ,Ilihitaji nguvu ya ziada kuweza kulishinda .Hata Peniela mwenyewe ameshangaa sana na kushindwa kuamini kwamba nimekataa kufanya naye mapenzi licha ya ushawishi wote alioufanya.kwa maelezo yake mwenyewe ni kwamba hajawahi kukutana na mtu ambaye ameuona mwili wake na akakataa kufanya naye mapenzi.” Akawaza Mathew wakati akielekea sebuleni

“ Team SC41 wamemfanya Peniela aondoe kabisa thamani ya utu wake na ndyo maana yuko tayari kuutoa mwili wake kwa mwanaume yeyote Yule ili mradi kuna kitu anakkitaka kwake.Peniela ni mwanamke mzuri na anayestahili heshima kubwa na hapaswi kuuchezea mwili wake kama afanyavyo sasa.Nitahakikisha anakuwa na maisha yake ya kawaida ambayo hayatamlazimu kuutumia mwili wake kama chambo” akawaza Mathew.Akaketi sofani na kujimiminia mvinyo kidogo katika glasi akanywa
Baada ya dakika kumi Peniela akatokea .Alikuwa amependeza sana.
“ Dah ! mwanamke huyu ana uzuri wa ajabu sana. Kila ninapomuona mwili wote unanisisimka.Nina wasiwasi kwamba nisipokuwa makini yawezekana na mimi nikajikuta nimeanguka na kuzama katika penzi zito na malaika huyu..” akawaza Mathew

“ Mathew samahani sana kwa jambo lililotokea chumbani.” Akasema Peniela
“ Usijali Peniela.Ni jambo la kawaida.”
“ Mathew kuna jambo ninataka kuliomba toka kwako.”
“ Jambo gani?

“ Ninaomba baada ya mambo haya kumalizika ,mimi na wewe tupate nafasi ya kwenda mahala na kupumzika hata kama ni nje ya nchi .I want to spend much time with you.I want to know you better” akasema Peniela,.Mathew akatabasamu na kusema

“ Tutaangalia kama itawezekana .”
“ Thank you Mathew “ akasema Peniala na kuchuua simu ambayo huitumia kuwasiliana na Dr Joshua akabonyeza namba Fulani na kuiweka sikioni.
“ namba yako ya utambulisho tafadhali ” ikasema sauti ya upande wa pili iliyopokea simu.
“ pkp46 “ akasema Peniela
“ Ok subiri kidogo” akasema yule mwanadada aliyepokea simu.Baada ya kama dakika moja hivi sauti nzito ya kiume ikasikika katika simu
“ Hallow Peniela” ilikuwa ni sauti ya Dr Joshua

“ Dr Joshua “ akasema Peniela

“ Hallo my queen..Unaendeleaje? Nimestuka kidogo ulipoamua kutumia njia hii ya dharura.” Akasema Dr Jshua
“ Dr Joshua najua si matumizi sahihi ya simu hii ya dharura lakini sikuwa na namna nyingine ya kuweza kuwasiliana nawe .Lengo langu ni kutaka kukujulia hali na kukupa pole sana kwa kifo cha Flaviana.Nimesikitishwa mno na kifo hiki.Pole sana my love” akasema Peniela
“ Peniela ahsante sana.Madaktari walijitahidi kwa kila namna walivyoweza lakini ikashindikana haikuwezekana kupona.”
“ Pole sana Dr Joshua.”

“ Ahsante sana Peniela”

“ kwa hiyo lini mwili wa Flaviana utarejeshwa nchini kwa mazishi? Akauliza Peniela

“ Kesho saa tano asubuhi mwili wa Flaviana utarejeshwa nyumbani kwa ajili ya maandalizi mazishi.”

“ Ahsante kwa taarifa Dr Joshua.Tutashirikiana pamoja katika kuupokea mwili na hadi tutakapohitimisha safari ya mwisho ya Flaviana.”
“ Ahsante sana Peniela"

“ Pamoja na hayo Dr Joshua nina ombi moja kwako”
“ Peniela nimekwisha kupa ruhusa ya kuomba chochote kile unachokitaka bila hata ya kuniuliza kwanza”
“ Ahsante Dr Joshua.Nnajua kesho utakuwa na shughuli nyingi lakini ninataka utafute nafasi tuonane hata kwa dakika ishirini tu.Nina maongezi nawe na ninataka nitumie dakika hizo chache kukufariji mpenzi wangu.Nataka tukutane katika ile nyumba yetu kule ufukweni” akasema Peniela

“ Uliponiambia kuna kitu unataka kuniomba nilidhani kuna jambo kubwa na zito kumbe ni hilo tu,basi usijali Peniela kesho mara tu baada ya kutua na kuelekea nyumbani nitatafuta muda na tutaonana.Saa saba za mchana tutaonana.Hata mimi nina hamu sana ya kukuona malaika wangu.Ninahitaji sana faraja yako na vile vile kuna jambo ninataka tuongee mimi na wewe linalohusu maisha yetu” akasema Dr Joshua
“ Ahsante sana kwa kunikubalia ombi langu mpenzi wangu.Basi naomba nikutakie usiku mwema na safari njema hiyo kesho.Tutaonana hiyo kesho.I love you so much” akasema Peniela na kukata simu kisha akaitupa pembeni na kumtazama Mathew

“ Samahani Mathew kwa kusikia maongezi yangu na huyu mzee lakini hivi ndivyo huongea naye.Anachotaka kukisikia Dr Joshua toka kwangu ni kwamba ninampenda sana nami siku zote huwa ninajaribu kumuhakikishia kwamba ninampenda lakini laiti angeweza kuusoma moyo wangu na namna ninavyomchukia angeniogopa kama kifo.Ninamchukia sana Yule mzee lakini sina namna nyingine ya kuweza kumuepuka lazima nikubali kumpenda ili mipango yetu ifanikiwe.” Akasema Peniela
“ Usijali Peniela.Mambo haya yatakwisha muda si mrefu.” Akasema Mathew.
“ Huyu mwanamke ana kitu gani anachokitumia kuwachanganya wanaume akili kiasi hiki? KIla mwanaume anayetembea naye anachanganyikiwa kabisa kama alivyomchaganya rais wa nchi.Peniela ni mwanamke mwenye uwezo wa kipekee na ni hatari zaidi ya watu wanavyomchukulia.Kama ameweza kupenya hadi kujenga mahusiano na rais wa nchi basi anaweza kuingia sehemu yoyote ile na akafanya chochote .Kuna nyakati hata mimi mwenyewe ninamuogopa kutokana na uwezo alionao wa kushawishi mtu yeyote Yule.Wasiwasi wangu ni kwamba hata mimi najihisi kwamba muda si mrefu ninaweza nikajikuta nimeshindwa kuendelea na msimamo wangu na kujikuta nikizama mapenzini na kimwana huyu kwani kadiri ninavyozidi kukaa naye karibu ndivyo ninavyojikuta nikizidi kuvutiwa naye na kutamani kuwa naye karibu zaidi na zaidi…………..” akawaza Mathew kisha akasema.

“ Peniela jambo kubwa lililotuleta hapa kwako ni kuzungumza na Dr Joshua na tayari umekwisha ongea naye.Nadhani sasa tunaweza kuondoka.” Akasema Mathew

“ Mathew are you sure you don’t want to spend time here at my house? Usihofu hapa ni sehemu salama sana “ akasema Peniela
“ Hapana Peniela tunatakiwa turejee nyumbani kwangu .Ninaamini sana usalama ulioko pale kuliko sehemu nyingine yoyote ile.” akasema Mathew.Peniela akaenda kufunga chumba chake halafu wakaingia garini na kuondoka
“ Peniela kuna mambo uliniambia unataka tuyajadili,mbona hukunikumbusha tena ili tujadili? Akauliza Mathew wakiwa garini

“ Ah ! usijali Mathew tutajadili siku nyngine tena kama tukifanikiwa kupata nafasi nzuri kama tuliyoipata leo.” Akasema Peniela na Mathew akatabsamu
“ Tutapata nafasi Peniela usijali.Bado tuna muda mwingi wa kuweza kukaa na kujadili mambo mengi tu “ akasema Mathew na mara simu ya Mathew ikaita.Alikuwa ni Anitha

“ Hallow anitha.Bado hujalala mpaka mida hii? Akaulzia Mathew

“ Nitalala vipi bil akuhakikisha umerejea salama? Akasema Anitha

“ Ahsante sana Anitha kwa kunijali.Kuna jambo jipya?
“ Mathew unakumbuka kuna wanati Peniela alitumia simu ya hapa ndani kumipigia mtu wake na kumfahamisha kwamba hatarejea leo?
“ Ndiyo ninakumbuka ,alimpigia Josh” akasema Mathew
“ Basi kijana Yule yuko katika laini ya simu anataka kuongea na Peniela” akasema Anitha.Mathew akampa simu Peniela
“ Josh wants to talk to you” akasema Mathew
“ Hallow” akasema Peniela.

“ Peniela ngoja nikuunganishe na Josh anataka kuongea nawe” akasema Anitha na kumuunganisha josh na Peniela
“ hallow Peniela” akasema Josh
“ Josh,is everything ok? Akauliza Peniela

“ Peniela you are being followed “ akasema Josh
“ Followed by whom? Peniela akashangaa
“ Ulionekana kupitia kamera zilizofungwa nyumbani kwako ukiingia kwako usiku huu ukiwa umeongozana na Mathew na hivyo wakatuma watu kuja kukuchunguza ulikuwa wapi na unafanya nini.Wako nyuma yako wanakufuatilia.Kuwa makini sana” akasema Josh

“ Ouh my gosh !! akasema Peniela
“ Peniela kuna nini?

“ Team SC41 wanatufuatilia” akasema Peniela.Nikweli kupitia kioo cha pembeni Mathew akagundua kwamba kuna gari lilikuwa linawafuatilia .
“ Hata mimi nilihisi kuna gari linatufuatilia toka tulipoondoka nyumbani kwako.Get ready.We must do something…” akasema Mathew na kuongeza mwendo wa gari.



TUKUTANE SEHEMU IJAYO
 
Penny yuko kikazi zaidi nadhani hata rijali Mathew akawa ktk target pia...wacha tusubiri kwani hatachomoka bila ya kudownload stock material.
 
jaji elibariki na metw watazinguana,coz peni na metw watarudi kule asubuhi kitu ambacho kitamuuma eli
 
PENIELA SEASON 3

SEHEMU YA 27


MTUNZI 😛ATRICK.CK

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ hallow Peniela” akasema Josh

“ Josh,is everything ok? Akauliza Peniela

“ Peniela you are being followed “ akasema Josh
“ Followed by whom? Peniela akashangaa

“ Ulionekana kupitia kamera zilizofungwa nyumbani kwako ukiingia kwako usiku huu ukiwa umeongozana na Mathew na hivyo wakatuma watu kuja kukuchunguza ulikuwa wapi na unafanya nini.Wako nyuma yako wanakufuatilia.Kuwa makini sana” akasema Josh
“ Ouh my gosh !! akasema Peniela

“ Peniela kuna nini?

“ Team SC41 wanatufuatilia” akasema Peniela.Nikweli kupitia kioo cha pembeni Mathew akagundua kwamba kuna gari lilikuwa linawafuatilia .
“ Hata mimi nilihisi kuna gari linatufuatilia toka tulipoondoka nyumbani kwako.Get ready.We must do something…” akasema Mathew na kuongeza mwendo wa gari.



ENDELEA…………………………….



“ Wewe na Amos mlikuwa ni watu muhimu na mnaotegemewa sana na Team Sc41 katika zoezio zima la kuipata package na baada ya Amos kuuawa ,umebaki peke yako .Uliondoka bila kuwaaga na hawajui umeelekea wapi .Tayari team SC41 wamekwisha anza kuwa na wasiwasi na wewe na ndiyo maana wanakufuatilia ili wazifahamu nyendo zako.Tayari wamehisi kuna kitu hakiko sawa ” Akasema Mathew
“ kwa hiyo tutafanya nini Mathew? Hata mimi nina wasiwasi kwamba tayari wamekwisha gundua kwamba nina shirikianananyi kwani Dr Martin aliwaambia wale madaktari waliotoka Marekani kwamba haliya John ilibadilika baada ya wewe kumtolea vitisho.Walitaka sana kukufahamu na wakamuhoji Josh maswalimengi kama anakufahamu lakini alikana kukujua na akasema kwamba mimi ndiye ninayekufahamu kwa hiyowalikuwa wanatafuta nafasi ya kunihoji.Nilipoondoka kule hospitali bila kuaga kumewapa maswali mengi na kuwafanya waamini kwamba ni kweli kuna watu ninashirikiana nao.Mathew watu hawa ni hataisana na tusipojitahidi wanaweza wakatuua.” Akasema Peniela kwa wasi wasi huku akilitazama gari lile lililokuwa linawafuata nyuma yao.
“ Siku zote usihofu unapokuwa karibu na mimi” akasema Mathew na kufungua droo ya gari kulikuwa na bastora nne.Peniela akachukua mbili na kumpatia Mathew mbili.
“ Utafuata kile nitakachokuelekeza sawa? Akasema Mathew
“ Sawa Mathew.” Akajibu Peniela lakini kabla hawajafanya lolote zikatokea gari mbili mbele yao ambazo zilikuwa zinakuja kwa kasi huku zikiwasha taa zote kubwa na kumfanya Mathew apate ugumu kuona mbele

“ Damn it !!..akasema Mathew na kufunga breki za ghafla ,akageuza shingo ili aweze kulitazama gari lile lililokuwa linawafuatilia nyuma,lilikuwa karibu sana.Pembeni ya bara bara kulikuwa na vibanda vitatu ambavyo vilionekana ni kama vya wafanya biashara ndogo ndogo.
“ Peniela nahisi hizi gari mbili zinazokuja mbele yetu ni za kwao pia.Hatuwezi kuendelea mbele wametudhibiti kila kona.Shuka garini nenda kajifiche katika kibanda kimoja wapo kuna kitu ninataka kufanya.” Akasema Mathew na bila kupoteza hata sekunde Peniela akafungua mlango na kukimbia hadi katika kibanda kimoja wapo akajificha.Mathew akaliona tofali pale karibu yake akafungua mlango na kulichukua tofali kisha akaiganzamiza pedeli ya mafuta kwa kutulia tofali lile na yeye akaruka nje.Gari ilifyatuka kwa mwendo mkali sana nazile gari mbilizilizokuwa zinakuja mbele yao zikasimama na haraka haraka milango ikafunguliwa watu wakashuka na mara ikaanza kusikika milio ya risasi ,wale jamaa walianza kulimiminia risasi gari la Mathew wakiamini kuna mtu ndani na ghafla kikasikika kishindo cha magari kugongana.Garila Mathew liligonga mojawapo ya zile gari mbili.
.Mathew alitoka mtaroni alikoangukia mara aliporuka garini na kuelekea nyuma ya kibanda alichokuwa amejibanza Peniela.Baada ya kishindo kile wale jamaa wakalizunguka gari la Mathew an kuchungulia ndani lakini hakukuwa na mtu yeyote.Lile gari lililokuwa likiwafuata nyuma akinamathew likasimamana wakashuka watu wanne na kuanza kukimbia kuelekea mahala walipokuwa wenzao.walijadiliana kwa sekunde kadhaa kisha wakaanza kuwatafuta akina Mathew.
“ Hawako mbali na hapa.lazima watakuwa maeneo ya karibu i”akasema mmoja wao

“Wanatutafuta.Tunatakiwa tuwastukize “akasema Mathew na kisha akainuakichwa na kuchungulia nakwa kasi ya ajabu wote wawili wakasimama na kuanza kuwachafua wale jamaa kwa risasi.lilikuwa ni shambulio ambalo hawakulitarajia ,watu wanne wakaanguka chini .
“ Tayari wamekwisha tuona tulipokaa,let us get out of here”akasema Mathew na kabla
na hawajaondoka akapigwa risasi akaanguka chini
“ Aaaaaghhhhh !!!..akatoa mguno na kuanguka chini,

“ Mathew ! Mathew !..akaita Peniela huku akimtingisha Mathew aliyekuwa akigala gala kwa maumivu .

“ Nyuma yako Penny!!!.” Mathew akapaaza sauti.Penny akageuka na kumuona mtu mmoja akiwa amesimama nyuma yao akiwa amewaelekezea bastora.
Kwa kasi ya aina yake ambayo Mathew hakuitarajia Peniela akanyakua bastora yake na kumchakaza Yule jamaa kwa risasi akaanguka chini.Mivumo ya risasi ikaanza kusikika kuelekea kule mahala waliko.Mathew akainuka na kuegemea kibanda ,Peniela akamsaidia kuinuka wakaenda kujificha nyuma ya kizimbacha kuusanyia taka taka.
“ Mathew are you hurt? Akauliza Peniela
“ I’m ok Peniela.Risasi haijagusa mfupa imepita kwenye nyama” akasema Mathew na mara gari tatu nyingine zikawasili

"wanaongezeka.Bastora yangu imebakiza riasi chache sana” akasema Mathew

“ Me too.. I’m empty” akasema Peniela
“ we have to get out of here.Tusipo harakisha kutoka eneo hili wanaweza wakatuua hawa jamaa.Risasi tulizo nazo hazitoshi kupambana nao.Tuitumie nafasi hii ambayo wanajipanga tuondoke eneo hili” akasema Mathew kisha akachungulia na kwa msaada wa taa ya gari akaweza kuwaona watu zaidi ya sita wakiwa wamesimama wakijadiliana jambo
“ Mathew jereha lako linatoa damu nyingi,kutoka hapa hadi nyumbani kwangu hakuna umbali mrefu.Turejee nyumbani tukatibu jeraha hilo na kuchukua silaha .Ninazo silaha pale ndani”akashauri Peniela.Mathew akamtazama na kusema
“ Tutambae chini ya mtaro tutokee upande wa pili hahafu tupotee kabisa eneo hili.Tangulia.I’ll cover you” akasema Peniela akaanza kutambaa taratibu na kuingia mtaroni Mathew naye akafuata.Bado wale jamaa walikuwa wamesimama wakijadiliana jambo yawezekana hawakuwa wametegemea kupata upinzani mkali kiasi kile.
Mathew na Peniela wakatambaa katika mtaro ule wa maji machafu yaliyokuwa na harufu kali na kutokea upande wa pili wa bara bara kisha wakaambaa ambaa na mtaro hadi usawa wa nyumba moja kubwa nyeupe .Wakatoka mtaroni na kupita katika uchochoro uliokuwa pembeni ya nyumba ile kisha wakaanza kukimbia na kutokea katika mtaa wa pili .

“ Mathew unavuja damu sana.” Akasema Peniela.
“UsijaliPeniela.” akasema Mathew wakaendelea kutembea kwa kasi kubwa.Ni sauti za mbwa ndizo zilisikika.Ghafla Peniela akasimama baada ya kuona miale mikubwa ya moto katika mtaa unaofuata iliko nyumba yake.
“ Mathew kuna moto mkubwa unaonekana mtaa wa pili”akasema peniela.

“ Yawezekana kuna nyumba inaungua”akasema Mathew kisha wakapita katika nyumba moja yenye maduka manne na kutokea katika mtaa iliko nyumbaya Peniela.Taratibu Peniela akaishiwa nguvu na kuanguka chini.Nyumba ya Peniela ilikuwa inawaka moto

“ Peniela ! peniela ! akaita Mathew…



******


Jaji Elibariki alikaa kitandani na kuinamisha kichwa halafu akasimama akaenda dirishani akachungulia nje.Kulikuwa kimya kabisa.Akarudi kukaa kitandani
“ Lazima nikubaliane na ukweli kwamba maisha yangu tayari yame haribika .Sifahamu ni lini nitatoka humu ndani na hata kama nikitoka sijui hatima yangu ni nini kwani tayari jina langu limekwisha chafuka na ninasakwa kila kona ya nchi hii kwakosa la kusababisha mauaji .Mathew anajitahidi sana kuhakikisha suala hili linafika mwisho lakini kila anapopiga hatua fulani jambo lingine linaibuka.”akawaza na akainuka tena na kusimama dirishani.

“ maisha yangu yameharibika .Nimempoteza mke wangu,nimepoteza kazi,nimepoteza kila kitu.Sina tena muelekeo katika maisha yangu .Kinachoniumiza zaidi ni kitendo cha kukutwa na Naomi .Sijui ni shetani gani alinipitia na nikajisahau kabisa hadinikakutwa na akinaMathew.Heshima yangu imeshuka mbele ya Peniela kwa sababu ya huyu kahaba Naomi.Ninampenda sana penela na tayari nilikuwa na mipango naye mingi tu baada ya mambo haya kumalizika lakini sina hakika tena kama kuna kitu kitakachoendelea tena kati yetu baada ya tukio la leo.Nimejidhalilisha sana kwa watu walioniheshimu na kunithamini ,walioyatoa maisha yao kunisaidia.Hakuna namna ninayoweza kuwaeleza na wakanielewa kwamba haikuwa ridhaa yangu mimi kufanya vile na kujishushai heshima kiasi hiki. “akaendelea kuwaza jaji Elibariki.
“ Mathew alisema kwamba Deus Mkozumi alikuwa na mpango mkubwa juu yangu na hakunieleza kwa kina ni mpango gani huo ila alisema kwamba ni mpango wa kutufanya mimi na Peniela wenye nguvu.Mpango huu utawezekanaje wakati ninaishi kama mfungwa.Natamani sana kuufahamu mpango huo , anaMathew ameonekana kama vile hataki kunieleza na kwa kuw ampangohuo unatuhusu mimi na peniela sidhani kama mpangohuo utawezekana tena kwani Peniela amekwisha vunja rasmi mahusiano yangu na yeye.Natakiwa kuonana na Deus mkozumi mimi mwenyewe ili aniambie ana mpango gani kuhusu mimi.Natakiwa kutafuta namna ya kutokahumu ndani ili ili niweze kunana na Deus nijue ana mipango gani juu yangu. “ akawaza Elibariki

“ Ninahitaji kumpata mtu ambaye atanisaidia kutoka hapa nilipo ,niweze kusafisha jna langu na mwisho maisha yangu yaweze kurejea kama awali.Ni nani ambaye anaweza akanisaidia katika jambo hili? Akaendelea kujiuliza na kushindwa kupata jibu akaenda kukaa kitandani
“ Nisipofanya bidii nitakwama hapa nilipo na maisha yangu yatahamia ndani ya nyumba hii.Dr Joshua na wenzake wamenitengenezea kesi mbaya sana ya kusababisha kifo cha Flaviana na kwa vyovyote vile endapo nitakamatwa hata kama sina hatia nilazima nitasota gerezani kwa kipindi kirefu kwani watu wanaonitafuta niwatu wenye nguvu sana na watatengeneza kila aina ya ushahidi mpaka wahakikshe nimekutw ana hatia na kufungwa.. Lazima nikiri kwamba hapa sina ujanja tena kwani siwezi kuepuka kukaa gerezani .Jaji wa mahakama kuu na mwenye heshima kubwa sana nchini,nitatuhumiwa na kesi ya kumuua mke wangu tena mtotowa rais.Dah ! balaa gani hili” akaendelea kuwazua jaji Elibariki

“ Naona akili yangu imefikia mwisho wake wa kufanya kazi na sioni msaada wowote tena ambao unaweza ukanitoa hapa nilipo na kunirudisha katika maisha yangu ya kawaida.Najuta ni kwa nini nilijiingiza katika mambo haya.Awali nilikuwa na maisha mazuri tu na kama nisingejingiza katika masuala haya basi nisingefika hapa nilipofika sasa hivi.Lakini haya yote yamesababishwa na Peniela.Nilitaka nimtafute muuaji wa Edson ili nimuonyesha peniela ni namna gani ninamjali na ili niweze kulisafisha jina lake katika jamii.Nilimpenda Peniela na ndiyo maana nikajitolea kufanya haya yote kwa ajili yake lakini mambo yamebadilika.Peniela nimemkosa na jina langu limechafuka na sijui nitumie njia gani kulisafisha tena.Najuta sana kujiingiza katika mapaambanohaya na watu wenye nguvu..” akatoka mle chumbani na kuelekea jikoni katika kabati ambalo huhifadhiwa chupa za pombe akafungua na kuchukua moja.wakati anatoka mle chumbani akakutana na Anitha

“ Elibariki hujalaa bado? Akauliza Anitha

” Hapana Anitha ,nimekosa usingizi kabisa .Nataka nipate mvino kidogo labda ninaweza kupata usingizi” akasema jaji Elibariki na kuelekea chumbani kwake akaanza kunywa pombe ile kali

“ Kuna wazo limenijia ,kwa nini nisitafute muafaka na rais? Akasimama na kutabasamu

“ Hili ni wazo zuri sana.Hakuna ubaya wowote kama nikijishusha na kuomba msamaha kwa rais na mambo haya yakaisha.Bila ya kufanya hivyo katu hakutakuwa na muafaka wowote ule.kwa kuwa yeye ndiye aliyeviagiza vyombo vya usalama vinisake kila kona ya nchi anaweza akaviamuru viachane na msako huo ,kesiyangu ikafutwa na jinalangu likasafishwa.Nitarejea kazini na maisha yangu yataendelea kuwa ya kawaida kama zaman japokuwa nitakuwa na maumivu ya kumpoteza mke wangu Flaviana na peniela pia.” Uso wa jaji Elibariki ukapambwa na tabasamu baada ya kupata wazo lile.Akachukua chupa ya mvinyo akanywa kidogo

“ hakuna ujanja mwingine , lazima nionane na Dr Joshua nimuombe msamaha ili mambo haya yamalizike.Natumai endapo nikimuangukia na kumuomba msamaha atanielewa na anaweza akanisamehe na mambo haya yatakwisha.Lakini endapo nikionana na Dr Joshua ina maana lazima niwasaliti wenzangu kwa kuianika mipango yao yote wanayoipanga kwa Dr Joshua ili aweze kuniamini . Huu ni usaliti mkubwa sana lakini nitafanya nini? Sina namna nyingine ya kufanya.” Akaendelea kuwaza.
“ Elibariki na wenzake wamenifanyia mambo mengi makubwa hadi hapa tulipofika na kuwasaliti itakuwa ni dhambi mbaya sana.lakini nitaendelea kukaa humu ndani hadi lini? Nitaendelea kujificha hadi lini wakati sina kosa? Nitakubali maisha yangu yaharibike na niendelee kuwa mkimbizi hadi lini? Elibariki akachukua mvinyo akanywa na kuendelea kutafakari
“ Hapana siwezi kukubali maisha yangu yaharibike kiasi hiki.I must do something to save myself.Hakuna ambaye atanisaidia kunikwamua ..Mathew ana mambo mengi sana ya kushughulikia na nisipo jihangaikia mwenywe nitaozea humu ndani.Ni lazima nifanye maamuzi magumu kwa ajili ya mustakabali mzima wa maisha yangu ya sasa na yajayo.”akaenda dirishani akatazama nje

“ Moyo unaniuma sana lakini nitafanya nini wakati sina ujanja tena .Nililianzisha jambo hili na mimi ndiye nitakayelimaliza na ili kulimaliza hakuna namna nyingine ya kufanya zaidi ya kutafuta muafaka na Dr Joshua.Tayari amekwishanizidi nguvu na sina namna ya kupambana naye tena.Ninafahamu maovu yake ,ninafahamu kamuua mke wake,na amesababisha kifo cha mkewangu Flaviana lakini sina namna zaidi ya kumuangukia kwani nikiendelea kupambana naye ni sawa na kupambana na ukuta nitajiumiza mwenyewe.Potelea mbali litakalokuwa na liwe tu lakini sitaki tena kuendelea kuishi maisha haya.Acha tu niibebe dhambi hii ya usaliti lakini lazima nirejee katika maisha yangu ya kawaida.” Akawaza Elibariki
“ Lakini nitaonana vipi na Dr Joshua? Si rahisi kuonana naye hivi hivi lazimaawepo mtu wa kuniunganisha naye .Ni nani basi ambaye anaweza kunisaidia kwa hili? Akajiuliza na kutafakari kwa sekunde kadhaa halafu akapata wazo

“ Rosemary Mkozumi.Huyu anaweza akanisaidia sana kuniunganisha na Dr johua.Huyu mwanamke ana mtandao mkubwa wa watu na anaweza kuwa na msaada mkubwa kwangu.lakini ili anisaidie lazima nimfungue kule chini alikofungwa.Nafahamu Rosemary ni mtu hatari sana na anashirikiana na magaidi lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya kumuachia huru ili aweze kunisaidia.Ninakumbuka kila kitu alichokifanya Mathew wakati tunamuingiza Rosemary kule chini.Ninazikumbuka namba alizobonyeza na mlango ukafunguka.Ninachotakiwa kufanya ni kumdhibiti kwanza Anitha “
Jaji Elibariki akaufungua mlango akachungulia nje.Nyumba yote ilikuwa kimya kabisa akatoka akaelekea katika chumba cha ofisi akachungulia na kumuona Anitha amekaa akiendelea na kazi akaufungu amlango na kuingia mle ofisini.Anitha akastuka

“ Jaji hulali leo? Akauliza
“ Nimekosa usingizi kabisa.Mathew na Peniela hawajarejea?

“ Hapana bado hawajarejea.Kuna tatizo limetokea”

“ Pole sana Anitha.let me make you a coffee”akasema Mathew

“ No thankyou Elibariki.situmii kahawa tafadhali” akasema Anitha na mara simu ikaita..
“halow Mathew.What happened? akasema Anitha kwa wasi wasi
“Hii ni nafasi ambayo natakiwa kuitumia vizuri”akawaza Elibariki na kwa kasi ya aina yake akakinyakua chungu cha maua kilichokuwa karibu yake na kumpiga nacho Anitha Kichwani akaanguka na kupoteza fahamu.Akaikanyaga kanyaga simu ile akakimbia hadi katika mlango wa chumba cha Mathew na kujaribu kuufungua.Ulikuwa umefungwa.Akarudi nyuma hatua kadhaa na kuurukia teke mlango ule ukafunguka akaingia ndani na moja kwa moja akaeleka katika kile kisanduku chenye namba.Akabonyeza namba alizozikumbuka lakini mlango haukufunguka.

“ C’mon nimekosea wapi? Mbona namba alizobonyeza Mathew ni hizi hizi? Akajaribu tena lakini bado mlango haukufunguka
“Nimekumbuka kulikuwa na namba mbili mwisho nasi namba tano.”
Akarudia tena kubonyeza na safari hii kabati kubwa la ukutani likasogea pembeni na mlango ukafunguka kwa akaanza kushuka kuelekea chini
 
Back
Top Bottom