Peniela (Story ya kijasusi)

Peniela (Story ya kijasusi)

poleni sana wakuu nilikuwa nashida kidogo na halotel jana wakanikatili kwenye network basi ikawa kimyaa.tunaliendeleza week end hii hakuna kutoka home wala kuchepuka. ni mwendo wa peniele tuu

mwaga vitu mkuu usijisumbue kutujb mb zinapungua tumia zote kupost story
 
SEASON 2
SEHEMU YA 31
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ natamani sana kujua kama John anaendeleaje lakini kwa namna akivyoniudhi sitaki hata kumsikia.Ngoja kwanza nimalize suala hili la operesheni 26B halafu nitaangalia pengine ninaweza kumsaidia na pengin…………….” Peniela akastuliwa mawazoni na mlio wa simu yake.Alikuwa ni captain amos
“ Halow Amos” akasema Perniela baada ya kupokea simu
“ Peniela good Job.Kigomba amenipigia simu na kunieleza namna alivyochanganyikiwa kwako.Amekiri kwamba hata ile kazi aliyopewa na Dr Joshua ya kukuchunguza haitaki tena yeye anachotaka ni kuwa na wewe tu.Huu ni wakati wetu Peniela wa kuimaliza operesheni 26 B.Endelea kumchanganya Kigomba na nitakuwa nikikufahamisha kila kinachoendelea.” Akasema Captain Amos
“ Usijali Amos.Kigomba tayari nimemuweka mfukoni na ninachosubiri ni kuikamilisha tu operesheni yetu.” akasema Peniela
“ Nitakufahamisha pindi rais atakapomkabidhi Dr Kigomba ule mzigo” akasema Amos na kukata simu.Akaelekea moja kwa moja nyumbani kwake akaoga na kubadili mavazi halafu akaelekea nyumbani kwa Mathew

ENDELEA……………….
Captain Amos alipomaliza kuongea na Peniela simuni na kumueleza namna alivyomchanganya Dr Kigomba katika kipindi kifupi,akaiweka simu ile pembeni akachukua simu nyingine akaiwasha kisha akazitafuta namba Fulani na kupiga .Simu ikapokelewa na mwanamama mwenye sauti ya kukwaruza
“ namba yako tafadhali” akasema yule mwanamama
“ VP 8601/W” akasema Captain Amos na bada ya sekunde kama ishirini hivi Yule mwanamama akasema
“ 3600 North.Savana ” akasema yule mwanamama na mara moja Captain Amos akaelea maelekezo yale yalimanisha nini.Akawasha gari na kuendelea na safari yake
“ Jackson atakuwa amenisubiri sana.Sijui kwa nini leo ametaka nikakutane naye pale Savana hoteli.Alinisisitiza sana kwamba lazima leo nionane naye.” akawaza Captain Amos.
Aliwasili Savana Hoteli.Geti la kuingilia hotelini lilikuwa limefungwa mlinzi akafika kumsikiliza,Amos akatoa kijikadi Fulani chenye namba mlinzi yule akaondoka nacho hadi katika kijichumba chake kilichokuwa na kompyuta akakiingiza kikadi kile katika mashine Fulani ndogo halafu akakitoa na kumfungulia Amos geti.Mlango wakuingilia ndani ya hoteli ulikuwa umefungwa ,akakinyonga kitasa na kuingia ndani akaelekea mapokezi ambako alimkuta mwanadada mmoja mrembo.Haikuwa ni mara ya kwanza kwa Captain Amos kufika hapa Savana hoteli kuonana na Jackson kwani ndiye mmiliki wa hoteli hii kubwa na nzuri.Katika hoteli hii kikundi Fulani cha watu hukutana mara kwa mara hasa nyakati za usiku na kujadili mambo yao.Captain Amos naye alikuwa ni mmoja wao.
“ Namba yako tafadhali” akasema yule mwanadada na Amos akamtajia namba yake halafu akaiandika katika kompyuta yake na kuinuka kitini akamuomba Amos aongozane naye.Walielekea katika chumba kimoja ambacho kilikuwa kinafunguliwa kwa kutumia namba na ndani ya chumba kile kulikuwa na ngazi iliyokuwa ikishuka chini wakaifuata ngazi ile na kushuka chini wakakutana na varanda refu na kulifuata na hatimaye wakawasili katika mlango mmoja ambao nao ulikuwa ukifunguliwa kwa namba maalum.Pamoja na kuja hapa mara kadhaa lakini Amos hakuwahi kufika sehemu hii aliyoletwa .Yule mwanadada akabonyeza namba na mlango ukafunguka akamkaribisha Amos aingie ndani.Ndani ya chumba kile kulikuwa na watu sita.Amos akastuka baada ya kuwaona baadhi ya watu ambao hakuwa ametegemea kuwaona pale.Kwa sekunde kadhaa alionekana ni kama vile amepigwa na butwaa akiwashangaa watu wale aliowakuta mle ndani.
“ Karibu sana Amos kwani ni wewe tu ambaye tulikuwa tunakusubiri.” Akasema Jackson Matila
“ Ahsante sana.”akajibu Amos na kuwasalimu watu wale mle ndani kwa heshima kubwa halafu Jackson akaendelea
“ Amos sikukwambia kama kuna watu utakutanana nao leo na ndiyo maana umeonyesha kustuka sana.Tumekuwa tukionana mimi na wewe mara kwa mara lakini leo hii nimeona nikushirikishe katika kikao kimojawapo cha juu kabisa cha umoja wetu na ukutane na vigogo wa nchi hii.Naomba nichukue nafasi hii kufanya utambulisho mfupi.Wa kwanza kabisa ambaye unatakiwa umfahamu usiku huu ni rais wetu mstaafu mzee Deus Mkozumi,natumai unamfahamu lakini hujawahi kukutana naye ana kwa ana.Pia tunaye Profesa Rafael kujilwa,huyu ni waziri mkuu mstafu natumai naye pia unamfahamu.Tunaye pia Benard mkeka,huyu ni mtu mwenye wadhifa mkubwa katika chama,tunaye Generali Adam,tunaye pia Ndikana mluwo.” Akasema Jackson na kuendelea
“ Ndugu zangu huyu ni yule kijana wetu ambaye amekuwa akitufanyia kazi ya kutukusanyia taarifa za kila kinachoendelea ndani ya Ikulu anaitwa Captain Amos.Yeye ni mtu wa karibu sana na rais Dr Joshua na ndiye amekuwa msaada wetu mkubwa katika kupata taarifa nyingi.Karibu taarifa nyingi ninazowapatieni huwa zinatoka kwake.Nimeona leo hii nimualike katika kikao chetu kikubwa kabisa ili muweze kusikia kutoka kwake kuhusiana na hatua kubwa iliyofikiwa katika kuiokoa package E21 isiuzwe. Karibu sana Captain Amos iliuweze kutupa taarifa ya kina kuhusu nini kimefikiwa hadi hivi sasa kuhusiana na package E21” akasema Jackson na kuonyesha heshima mbele ya vigogo wale Amos akasimama.
“ Awali ya yote napenda sana nitoe shukrani za pekee kabisa kwa kunialika na mimi katika kikao hiki kikubwa na kukutana na watu wakubwa kama ninyi ambao sikutegemea kama siku moja ningeweza kukaa nanyi kama tulivyo hivi sasa.Kuhusiana na Package E21 ni kwamba mpaka sasa tunaendelea vizuri.Mipango yote iko safi.Mawasiliano yanaendelea kati ya rais na wanunuzi wanaoitaka package ile na pindi wakifikia makubaliano basi Dr Joshua atamkabidhi Dr Kgomba katibu wake ambaye ndiye atakayefanya makabidhiano yote na wanunuzi.Team SC41 nao wamepiga hatua tayari katika kuipata package hiyo na tayari wamekwisha mpandikiza mtu wao kwa viongozi wakuu.Wanamtumia msichana mmoja aitwaye Peniela ambaye tayari yuko katika mahusiano ya kimapenzi na Dr Joshua na usiku huu kabla sijaja hapa nimeuunganisha na Dr Kigomba na wameanzisha mahusiano tayari kwa hiyo watu hawa wote wawili tayari amewadhibiti na wote wamekufa wameoza kwake.Dr Kgomba akishakabidhiwa mzigo huo ,team SC41 kwa kumtumia Peniela watauchukua na halafu sisi tutauchukua mzigo huo toka kwao.Tayari kila kitu kimekwisha andaliwa na kinachosubiriwa ni mzigo huo ukabidhiwe kwa Dr Kigomba.” Akasema Amos na wote wakampigia makofi
“ Good.Kazi nzuri imefanyika lakini nina swali moja,” akasema Benard mkeka.
“ Unadhani hawa Team SC41 hawawezi kugundua kwamba pamoja na kuwa ni mtu wao lakini una mpango wa siri wa kuichukua package hiyo toka kwao?
“ Hapana hawawezi kugundua chochote.Isitoshe kwa hivi sasa Team SC41 haina nguvu sana kwani kiongozi wake mkuu John Mwaulaya anaumwa sana kwa hiyo nguvu yake si kama awali japokuwa bado wana nguvu lakini hawawezi kugundua lolote kuhusu mimi.Katika hilo ondoeni shaka kabisa.”akasema Amos
“ Huyu msichana peniela mna mawasiliano mazuri? Unaamini anaweza kuifanya kazi hii kikamilifu na kuipata hiyo package? Akauliza tena Benard Mkeka
“ Ninamuamini sana peniela,Ni msichana mwenye uwezo mkubwa na ndiye anayetegewa na team SC41 katika operesheni hii.Peniela amefanikiwa kumuweka Dr Joshua katika mikono yake na kumpeleka atakavyo na hivi sasa Dr Joshua haambiwi lolote kuhusu Peniela.Usiku huu Peniela amefanikiwa kumnasa tena Dr Kigomba kwa hiyo ni msichana mwenye uwezo mkubwa sana.Isitoshe katika operesheni hii hayuko peke yake,kuna watu nyuma yake kama mimi ambao tunamuelekeza njia za kupita ili kuipata package hiyo.” Akasema Amos
“ Sawa Amos tunakuachia suala hili wewe ulishughulikie na likamilike bila matatizo yoyote.Tunakutegemea sana.Hakikisha Package ile haiondoki nje ya mipaka yetu ” Akasema mzee Deus Mkozumi rais mstaafu wa Tanzania,akamtazama Amos kwa makini na kusema
“ Amos binafsi napenda nikupongeze kwa kazi nzuri unayoifanya na nimefurahi sana leo kukutana nawe ana kwa ana.Jackson amekuwa akinipa taarifa zako mara kwa mara kuhusu kazi unazozifanya japokuwa wakati mwingine ni katika mazingira ya hatari kubwa lakini unazifanya kwa umahiri mkubwa na tunazipata taarifa kwa wakati.Tumekuwa tukizifanyia kazi taarifa zako zote na kuhakikisha kwamba nchi inakwenda kadiri tunavyotaka sisi iende na si kwa matakwa ya mtu mmoja mjinga kama Dr Joshua” akasema Deus.Akanyamaza kidogo halafu akaendelea
“ Nilipata taarifa za kuhusiana na kitendo cha kikatili alichokifanya Dr Joshua cha kumuua mke wake Dr Flora kwa sababu tu ya kugundua kuhusiana na mpango wa kuiuza package E21. Dr Flora na mke wangu walikuwa marafiki wakubwa na mimi na familia yangu tuliumizwa mno na kifo kile.Nilitaarifiwa kwamba kuna jaji moja wa mahakama kuu ambaye amemuoa mtoto wa dr Joshua ananitwa jaji Elibariki alifanya uchunguzi na kugundua kilichomuua Dr Flora kwamba ni sumu lakini ilipogundulika kwamba tayari ameifahamu siri yakatolewa maelekezo kwamba auawe.Nilipopata taarifa hizo za kutaka kuuawa Elibariki ,nikatoa maelekezo kwamba zifanyike kila jitihada kuhakikisha kwamba jaji huyo anaokolewa na ninashukuru kwamba hilo ulilifanya vyema Amos na kufanikiwa kumuokoa Elibariki.Ninachotaka kufahamu ni maendeleo ya huyu jaji.Anaendelaje? Yuko sehemu salama kwani ni mtu ninayemuhitaji sana” Akauliza mzee Deus na kumshangaza kidogo Captain Amos kwani hakuwahi kufikiria kama maagizo yale ya kumuokoa jaji Elibariki yalitoka kwake.
“ Elibariki yuko sehemu salama .Siku ile alipookolewa aliomba apelekwe kwa Peniela ambako alikaa hadi usiku wa jana alipogundulika na kuondoka kwenda kujificha sehemu nyingine ambako ni salama zaidi kwake” akasema Amos
“ Peniela again? Akauliza Ndikana mluo huku akicheka
“ Elibariki na Peniela wana mahusiano ya siri ya kimapenzi” akasema Amos na kuwafanya watu wote mle ndani waangue kicheko.
“ Huyu Penielani ni msichana wa namna gani? Mbona kila mahala amepashika yeye? Dr Joshua,Dr Kigomba na hata jaji Elibariki ! Akauliza mzee Deus
“ Peniela ni msichana mwenye uzuri wa kipekee kabisa na kama nilivyowaeleza awali kwamba anautumia uzuri wake kumnasa mwanaume yeyote amtakaye.Team SC41 ndiye wanayemtegemea kutafuta taarifa toka kwa watu mbalimbali ” akasema Amos
“ Ok good.Nafurahi kusikia kwamba Elibariki anaendelea vizuri.Anatakiwa alindwe sana hasa kwa wakati huu ambao nina hakika nguvu kubwa inatumika kumtafuta.Siri anayoifahamu Elibariki ni kubwa na inatosha kabisa kumuangamiza Dr Joshua na ndiyo maana anatumia nguvu kubwa kumtafuta. Elibariki ni kijana ambaye nina mpango naye mkubwa sana na ndiyo maana nikataka aokolewe na awe salama na ninaagiza tena kwamba alindwe kwa kila namna ” akasema mzee Deus
“ Amos kwa kukuzidishia uelewa zaidi ni kwamba Dr Joshua ni mtu ambaye mimi nimemlea kisiasa ndani ya chama.Alikuwa ni muadilifu sana na mchapakazi.Nilimuandaa Dr Joshua kwa ajili ya kushika nafasi kubwa nchini kwani alionyesha uwezo wa juu sana wa uongozi katika nyadhifa mbali mbali alizopewa ndani na nje ya chama.Wakati kipindi changu cha uongozi kinakaribia ukingoni mchakato wa kumpata mrithi wangu ukaanza na bila kusita nilimpendekeza Dr Joshua kwani niliamini anaweza kukikalia kiti kile.Nilitaka mrithi wangu awe ni mtu ambaye atakuwa akifuata ushauri wangu kwangu kwani mimi nimehudumu ikulu kwa miaka mingi kabla sijawa rais na baadae nikawa rais.Nilichokitaka kikatimia na Dr Joshua akawa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.Baada tu ya kushika madaraka Dr Joshua alibadilika sana na amekuwa akifanya mambo mengi ya ajabu sana .Mwanzoni nilikuwa naye karibu nikimshauri namna ya kuongoza ofisi kubwa kama ile lakini baada ya muda hakutaka tena niwe nikimshauri lolote na nikaamua kukaa pembeni lakini hata hivyo sikutaka kabisa kujiweka pembeni na kumuacha afanye mambo namna anavyotaka yeye na ndiyo maana nikamuagiza Jackson akuingize Amos katika umoja wetu ili tuweze kupata kila taarifa ya kile anachokifanya Dr Joshua.Taarifa ile ya kutaka kuuza package E21 ilinistua sana.Naomba niwaeleze ukweli kwa sababu wakati wa uongozi wangu niliilinda kama mboni ya jicho.Hata mimi nilikumbana na vishawishi vingi vya kutaka kuiuza package ile lakini sikuwa tayari kufanya hivyo.Hapa majuzi nilimpigia simu nikijaribu kumuonya kwamba aachane na mpango wake huo wa kuiuza package ile lakini tulishindwa kuelewana na badala yake alinitolea maneno ya dharau na kashfa kubwa na zaidi sana alifikia hatua ya kutaka hadi kuniua.Alimtaka generali Adam huyu hapa ,kubuni mpango wa kuniua bila kujua kwamba Adam ni mtu wangu mimi na asingeweza kufanya jambo kama hilo.Amenisikitisha sana Dr Joshua na sintomvumilia tena na ninataka kumuonyesha kwamba mimi nina nguvu zaidi yake.Nataka kumuondoa katika madaraka mara tu zoezi la kuiuza package E21 litakaposhindikana. Hapa ndipo Elibariki anapokuja kuingia.Yeye ana ushahidi mzito sana wa kuweza kumtoa Elibariki madarakani na akafungwa miaka mingi na hata ikiwezekana maisha gerezani.Ninataka kumtoa madarakani kwa aibu.” akasema mzee Deus.Watu wote walikaa kimya kabisa wakimsikiliza.
“ Tukiachana na hilo la Dr Jason ,kuna jambo lingine kubwa ambalo ninataka kuwashirikisha nyote.Ni kwamba nimefikiria baada ya kumuondoa Dr Joshua madarakani ,huyu kijana jaji Elibariki ndiye tumsimamishe kugombea nafasi hii kwani anafaa sana.” Akasema Deus Mkozumi na watu wote mle ndani wakawa ni kama wamepigwa na mshangao
“ What ?!! akashangaa Benard Mkeka.Kauli ile ya Deus iliwastua sana wale wajumbe mle ndani ya kile chumba
“ Deus are you serious about this? Akauliza Profesa Raphael Kujilwa.
“ yes I’m serious.Nimepitia kwa umakini wasifu wa Elibariki na nimejiridhisha kwamba anafaa na anaweza.Umri wake unaruhusu kikatiba kugombea nafasi ya urais,nimchapakazi,na elimu ya kutosha kabisa na zaidi ya yote wakati huo uchaguzi utakapofanyika jina lake litakuwa juu sana kwani ndiye atakayefichua kila kitu alichokifanya Dr Joshua kwa umma kwa hiyo nafasi yake ya kushinda uchaguzi ni kubwa sana.”
“ Deus kauli yako imenistua sana japokuwa bado sijafahamu umeona nini hadiukafikiria hivyo laini ninachojiuliza hata kama sisi tutamkubali ndani ya chama je watamkubali ? Sina uhakika kama ndani ya chama anaweza kuwa na nafasi kwani hakuna anayemfahamu.”akasema Ndikana Mluwo
“Kukubalika ama kutokukubalika ndani ya chama si hoja yenye mashiko.Sisi tulipo hapa ndio chama na tunaweza tukafanya chochote .Kitakachofanyika ni kwamba mara tu baada ya kumuondoa Dr Joshua ,Elibariki ataachana na kaziyake ya ujaji na hivyo kuwa huru kuingia katika siasa. Guys mnaweza msikubaliane na mimi kuhusiana na suala hili lakini nawahakikishia kwamba nimekwisha ona mbali sana na Elibariki ni mtu ambaye atatufaa sana.Nina sababu zangu za kusema hivyo.Kwa sasa kipindi cha pili cha uongozi wa Dr Joshua kinaelekea ukingoni na tayari kuna makada wengi wamekwisha anza kujitafutia nafasi hiyo kwa hiyo tunatakiwa kumtafuta mtu ambaye ni wa tofauti sana na ambaye hakuna aliyemtarajia.Mtaona hapa kwamba Elibariki ni mtu sahihi kwa sababu kwanza hana kundi lolote katika chama na pili hana kashfa yoyote,na vile vile kitendo atakachokuwa amekifanya cha kufichua maovu ya Dr Joshua kitamuweka katika nafasi nzuri kuchaguliwa kwani kumg’oa rais madarakani si kitu chepesi.Sifa nyingine Elibariki bado kijana na ana nguvu za kutosha kwa hiyo atapata uungwaji mkono mkubwa sana toka kwa vijana.Ndugu zangu chama kinahitaji mageuzi makubwa na mageuzi haya yataanzia kwa kumuweka madarakani rais kijana kama Elibariki.Najua kila mmoja wenu akilitafakari suala hili kwa makini sana atakiona kile ninachomaanisha.” Akasema Mzee Deus na kikao kikaendelea hadi usiku mwingi na kisha wakatawanyika kwa makubaliano ya kukutana tena siku nyingine kulijadili kwa upana wake suala lile alilolipendekeza mzee Deus.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
SEASON 2


SEHEMU YA 32

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Mtaona hapa kwamba Elibariki ni mtu sahihi kwa sababu kwanza hana kundi lolote katika chama na pili hana kashfa yoyote,na vile vile kitendo atakachokuwa amekifanya cha kufichua maovu ya Dr Joshua kitamuweka katika nafasi nzuri kuchaguliwa kwani kumg’oa rais madarakani si kitu chepesi.Sifa nyingine Elibariki bado kijana na ana nguvu za kutosha kwa hiyo atapata uungwaji mkono mkubwa sana toka kwa vijana.Ndugu zangu chama kinahitaji mageuzi makubwa na mageuzi haya yataanzia kwa kumuweka madarakani rais kijana kama Elibariki.Najua kila mmoja wenu akilitafakari suala hili kwa makini sana atakiona kile ninachomaanisha.” Akasema Mzee Deus na kikao kikaendelea hadi usiku mwingi na kisha wakatawanyika kwa makubaliano ya kukutana tena siku nyingine kulijadili kwa upana wake suala lile alilolipendekeza mzee Deus.


ENDELEA……………….

Peniela aliwasili nyumbani kwa Mathew,mlinzi akampigia sImu Mathew na kumfahamisha kwamba peniela amewasili akamruhusu amfungulie geti aingie ndani.

“ Its hard to do this but I hve to.lazima niwaeleze ukweli akina Elibariki.Bila kufanya hivyo sintaweza kabisa kujitoa katika team SC41 na maisha yangu hayataweza kamwe kubadilika” akawaza Peniela na kushuka garini akaelekea mlangoni akabonyeza kengele .Katika chumba cha kazi kilichokuwa na mitambo na luninga kubwa tatu ukutani,Mathew na Anitha walikuwa walimkagua Peniela kupitia katika kifaa kilichofungwa pale mlangoniili kukagua kama ana silaha amakitu chochote kinachoweza kuwa kinarusha mawasiliano na kuyapeleka sehemu nyingine.
“ She’s clean” akasema Anitha baada ya kuridhika kwamba Peniela hakuwa na silaha walakitu chochote cha kurusha mawasilianokupeleka sehemu nyingine. Mathew akatoka na kwenda mlangoni kumlaki Peniela

“ karibu Peniela” akasema Mathew

“ Ahsante sana Mathew. Samahani kwa kuwasumbua usiku huu” akasema Peniela

“ usijali P eniela ,unakaribishwa muda wote.katika nyumba hii watu hawalali “ akasema Mathew na kumkaribisha Peniela sebuleni walikokuwa wamekaa jaji Elibariki na Jason.Mtu wa kwanza kusalimiana naye alikuwa ni jaji Elibariki ambaye alimfuata na kumbusu halafu akamsalimu na Jason kwa kumpa mkono kisha akaketi kitini
“ Samahani sana kwa kuwaweka hadi mida hii.Nilikuwa na shughuli moja ya muhimu sana iliyonichelewesha ” akasema Peniela
“Usijali Peniela,hata kama ungekuja asubuhi lazima tungekusubiri tu” akasema jaji Elibariki na wote wakacheka.

“ Ok.Mmeshindaje toka muda ule nilipowaacha? Are you ok now? Akauliza Peniela ambaye uso na sauti yake vilionyesha kwamba hakuwa akihitaji mzaha wowote
“ We’re good.Tuko sawa.Tumeongea na tumeyamaliza yale mambo” akasema Jason

“ Good..I’m so happy for that.You are real men” akasema Peniela na mara akatokea Anitha wakasalimiana.

“ Peniela unatumia kinywaji gani? Akauliza Anitha

“ Ahsante sana Anitha,naomba kama una whsky yoyote tafadhali” akasema Peniela Anitha akaenda kumletea mvinyo ,akanywa funda kubwa.Watu wote pale sebuleni walikuwa kimya wakisubiri kusikia Peniela anataka kuwaambia kitu gani
“ Ninashukuru kwamba ninyi nyote mko hapa .Nilikuwa nawahitaji sana nyote muwepo ili tuongee jambo moja muhimu sana” akaanzisha mazungumzo Peniela bila kupoteza wakati

“ Kwanza kabisa ninakushukuru Mathew kwa kunikaribisha hapa kwako .Ninashukuru vile vile kwa kuendelea kuhakikisha usalama wa Elibariki”akanyamaza na kunywa funda moja la mvinyo

“ Nina mambo mengi sana ambayo ningependa kuwaeleza usiku huu lakini kutokana na muda nitawaeleza mambo mawili au matatu makubwa ya muhimu kwa sasa.” Akanyamaza tena akawaangalia akina Mathew kisha akaendelea

“ Nadhani nyote mnafahamu kuhusiana na kesi ya mauaji iliyokuwa ikinikabili.Ninawashukuru sana Jason wakili wangu na jaji Elibariki kwa kunipigania na hatimaye nikawa huru.Baada ya kesi ile kumalizika jaji Elibariki na Jason walitaka kwenda ndani zaidi kulichimba suala lile na kumfahamu muuaji.Leo hii naomba niwaeleze ukweli kwamba sikutaka jambo lile lifanyike kwani tayari nilikuwa nikimfahamu muuaji.”akasema Peniela na wote mle ndani wakastushwa na kauli ile isipokuwa Mathew
“ Ulifahamu aliyemuua Edfson? Akauliza Jason

“ ndiyo nilifahamu mtu aliyemuua Edson na sikutaka kufumbua mdomo wangu kusema .Niliogopa ningeuawa kwani ni mtu mzito na mwenye nguvu” akasema Peniela

“ Who is that? Akauliza Jason.Peniela akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Ni mheshimiwa rais”
Kimya kifupi kikapita mle ndani na baada ya sekunde kadhaa akasema

“ Ulijuaje kama rais ndiye aliyemuua Edson? Akauliza jaji Elibariki

“ Nimekuja hapa kuwaelezeni ukweli wa kila kitu kwa hiyo msihofu nitawaeleza kila kitu kilivyo.”akasema na kukaa kimya kidogo akaendelea

“ Kabla sijaingia katika mahusiano ya kimapenzi na Edson ,tayari alikuwa katika mahusiano na mtoto wa rais aitwaye Anna na wakati huo mimi nilikuwa na mahusiano ya siri na mheshimiwa rais” akasema Peniela.Uso wa jaji Elibariki ukabadilika.Hakuwa ametegemea kusikia jambo kama lile.

“ Unasema ulikuwa na mahusiano na nani? Akauliza jaji Elibariki
“ Tafadhali usihamaki Elibariki utafahamu kila kitu hatua kwa hatua.Usikuhuu ni usiku utakaojaa ukwelimtupu wa kila jambo.Nilikuwa katika mahusiano na rais Dr Joshua na mpaka sasa bado niko katika mahusiano naye “

“ Shetan…..” jaji Elibariki alipandwana hasira za ghafla akainuka na kutaka kumfuata Peniela lakini Mathew akawahikumdaka akamzuia

“ Elibariki please calm down.Msikilize kwanza Peniela anataka kutueleza jambo gani.Tafadhali naomba usihamaki “akasema Mathew
“ Ahsante sana Mathew.Nafahamu umekasirika kwa sababu unanipenda,lakini naomba utulie na usikie kila kitu ninachotaka kuwaeleza” akasema Peniela

“ Endelea peniela” akasema Mathew

“ Wakati nikiwa katika mahusiano na mheshimiwa rais, siku moja alinialika katika sherehe moja kubwa iliyokuwa ikifanyika ikulu .Katika sherehe hiyo ndipo nilipokutana na Edson na urafiki wetu ukaanzia hapo na baadae tukawa wapenzi.Dr Joshau aligundua kuhusu mahusiano yangu na Edson na alikasirika sana na kupanga mpango ule wa kumuua Edson na mimi nikabebeshwa mzigo ule wa kesi, lengo lake likiwa ni kuniangamiza kabisa.Japo nilimfahamu muuaji lakini sikuthubutu kufumbua mdomo wangu kusema chochote kwa sababu endapo ningethubutu kufanya hivyo basi ningeuawa mara moja ”akasema Peniela na kukaa kimya kidogo huku Elibariki akiendelea kumuangalia kwa macho makali ya hasira

“ Ilitokeaje wewe na rais mkaingia katika mahusiano ya kimapenzi? akauliza Anitha

“ Ni hadithi ndefu kidogo ila nitawaeleza hilo baadae lakini kwa sasa naomba mniruhusu niwaeleze kile nilichokusudia kuwaeleza usiku huu ” akasema Peniela akawaangalia watu wote mle sebuleni na wote walikuwa kimya wakimtazama,akaendelea .

“ baada ya kesi ile iliyokuwa ikinikabili kumalizika na mahakama kuniachia huru,Jaji Elibariki na Jason waliamua kuanzisha uchunguzi ili kulichimba zaidi suala lile na kufahamu nani aliyemuua Edson kwani wote waliamini mimi si muuaji.Niliogopa kwa wao kujiingiza katika suala hili kwani Endapo wangelichimba jambo hili kwa ndani wangeweza kugundua kwamba rais ana mkono wake katika mauaji yale na wangekuwa katika hatari kubwa kwani ninamfahamu vizuri Dr Joshua .Elibariina Jason ni watu wangu wa karibu na wa muhimu sana.Wote wana nafasi kubwa sana ndani ya moyo wangu na katika maisha yangu kwa ujumla kwa hiyo sikuwa tayari kuwaona wakiingia katika matatizo makubwa na kuhatarisha maisha yao.Niliogopa kuwaeleza ukweli wa jambo hilo na kwa hiyo nikatafuta njia ya kuweza kuwavuruga wasiendelee na mpango wao na nikaamua kuwagombanisha.Wenyewe wanafahamu kitu kilichotokea na wakavurugana..Mtanisamehe sana Elibariki na Jason kwa nilichokifanya hadi mkagombana ,lakinisikuwa na njia nyingine ya kuweza kuwazuia msiendelee na mpango ule wa kulichimba kiundani suala la lile la mauaji ya Edson.” Akasema peniela .Elibariki alimuangalia Peniela kwa jicho kali.

“ Sikuwahi kuhisi kama Peniela anaweza kuwa namna hii.Dah ! ama kweli umdhaniaye siye,ndiye.Nilikuwa tayari kufanya kila linalowezekana iliniwe naye lakinikmbenilikuwa najiingiza katika mdomo wa joka kubwa bila kujua.Nilidanganywa na uzir wake wa nje lakini kumbe ndani hana hata chembe ya ubinadamu.Siku ile Jason aliponipiga na chupa kichwani ningeweza hata kupoteza maisha kumbe yote ilisababishwa na Peniela.”akawaza jaji Elibariki akiendela kumuangalia Peniela kwa chuki
“ Ulimuuliza Dr Joshua sababu ya kumuua Edson? Akauliza Mathew
“ Nilimuuliza na akaniambia kwamba alifikia maamuzi yake kutokana na mimi kumsaliti kwa kuanzisha mahusiano na Edson kwa hiyo alitaka wote wakose na mimi nikaozee gerezani na ndiyo maana nikabebeshwa mzigo wa ile kesi kubwa” akasema Peniela.Mathew akamtazama na kusema

“ Alikudanganya”
“ alinidanganya? Peniela akashangaa

“ Ndiyo.dr Joshua alikudanganya kuhusu sabau ya kumuua Edson”

“ Unajuaje kama alinidanganya? Akauliza Peniela
“Tayari tunafahamu kila kitu kuhusiana na kifo cha Edson na ninisababuya yeye kuuawa.”

“ You know? Peniela akazidi kushanga

“ How do you know? Who are you Mathew? Akauliza Peniela
“ Nadhani Elibariki ndiye anayeweza kukueleza kila kitu kuhusiana na mimi.Elibariki please tell Peniela everything’ akasema Mathew.Jaji Elibariki akamtazama Peniela na kusema
“ Kutokana na mambo mengi yasiyo ya kawaida niliyoyaona wakati wa usikilizwaji wa kesi iliyokuwa ikikukabili ,niliazimia kwamba lazima nilifanyie uchunguzi wa kina suala hili na nifahamu ukweli wake.Nilimshirikisha Jason wazo langu na kwa pamoja tukakubaliana kulifanyia uchunguzi suala hili.kwa kuwa sisi wawili hatuna ujuzi wowote wa kufanya mambo haya ya uchunguzi na sikutaka kulichunguza jambo hili kwa kutumia jeshi la polisi nililazimika kutafuta mtu ambaye ana ujuzi na uzoefu wa kutosha wa mambo haya na ndipo nilipomfuata Mathew na kumuomba msaada wake katika jambo hili.Mathew ni mzoefu wa siku nyingi katika kazi hizi,amekwisha fanya kazi katika idara ya ujasusi ya taifa na kwa sasa anafanya kazi zake binafsi” akasema jaji Elibariki na kuendelea
“ Mathew aliwaita wenzake wamsaidie kuifanya kazi hii na mmoja wao ni huyu hapa Anitha na Noah aliyepoteza maisha wakati akiniokoa katika lile shambulio . Kitendo cha Peniela kunivuruga mimi na Jason kwa kutugombanisha hakikuathiri chochote kuhusu mpango wetu wa kulichunguza sualahili ,kwahio Mathew na wenzakewaliendelea na uchunguzi wao.Ni hayo tu ninayoweza kusema kuhusiana na Mathew na kuhusu namna walivyochunguza atakueleza yeye mwenyewe” akasema Elibariki akionekana kuishiwa kabisa maneno ya kusema
“ Peniela nadhani sasa umenifahamu mimi ni nani na kazi yangu ni nini.” Akasema Mathew na Peniela akatingisha kichwa kukubaliana naye,Mathew akaendelea

“ Tumelichungza suala hili na tumegundua kwamba Edson aliuawa kwa amri ya rais lakini kilichopeleka auawe si kwa sababu ya wewe kuingia katika mahusiano naye bali ni kwa sababu nyingine kabisa.Tumegundua kwamba Edson alikuwa akishirikiana na watu Fulani ambao walimtumia katika kuiba nyaraka za siri Ikulu.Nyaraka hizo walipanga waziuze kwa mabilioni ya fedha.Kwa bahati mbaya yeye na watu wote aliokuwa akishirikiana nao wote wamekwisha fariki kwa sababu ya nyaraka hizo na kwa bahati nzuri nyaraka hizo tumezipata na kwa sasa tunazifanyia uchunguzi wa kina kuzifahamu zinahusianana na nini kwani zimeandikwa kwa lugha ya kisayansi na sisi hatuelewi ni kitu gani kilichoandikwamo.Nadhani sasa umeelewa sababu iliyopelekea kifocha Edson.” Akasema Mathew.Peniela alionekana kustushwa sana na taarifa ile.

“ sikuwa nikilifahamu jambohilohilo .Niliaminimanenoaliyoniambia Dr Joshua .Nashukuru kwa kunifahamisha ukweli.’ akasema Peniela.

“ Dr Joshua asingeweza kukueleza ukweli kwa sababu inaonekana nyaraka hizo zina kitu kikubwa sana ndani yake na ndiyo maana wote waliozishika wamepoteza maisha.” akasema Elibariki
Peniela akainama chini akaonekana kujawa na mawazo

“ Ilikuaje hadi ukaanzisha mahusiano na mheshimiwa rais?akauliza Mathew

“ Ni hadithi ndefu kidogo lakini nitawaeleza ukweli wa kila kitu kinachoendelea kwani nina hakika hata ninyi mpaka mmefikia hatua ya kufahamu kuhusiana na jambo hili basi mtakuwa mmekwisha fahamu mambo mengi”akasema Peniela.Akakaa kimyakidogona kuendelea

“ Mimi ni Team SC41.Sina hakika kama mnafahamu au mmekwisha sikia kuhusu Team SC41 “ akasema Peniela na kuzidi kuwachanga Elibariki na Jason ambao hawakuwa wakifahamu chochote kuhusiana na Team SC41.

“ we already know what team SC41 is” akasema Mathew

“ You know? Peniela akashangaa

“ Peniela we don’t know anthything.Kama Mathew anafahamu kuhusu hiyo team unayoisema ni yeye mwenyewe lakini sisi hatufahamu chochote kuhusianana hiyo team ” akasema jaji Elibariki
“ I’m sorry guys ,sikuwahi kuwaeleza chochote kwamba katika uchunguzi wetu tuligundua uwapo wa team SC41 lakini hakukuwa na ulazima wa kuwaeleza kwa sababu kikundi hiki hakikuhusika na kifo cha Edson ”akasema Mathew
“ Ulipaswa kutuweka wazi kuhusu kila kitu Elibariki. Kwa hiyo team SC41 ni akina nani? shughuli zao ni nini? Akauliza Elibariki.
“ Team SC41 ni kikundi cha siri kinachofanya kazi zake kwa siri hapa nchini na katika ukanda wa afrika mashariki.Kikundi hiki kilianzishwa kwa siri na serikali ya marekani kwa ajili ya kulinda maslahi yake katika ukanda huu wa afrika ya mashariki.Kazi kubwa ya kikundi hiki ni kuhakikisha kwamba maslahi ya Marekani yanalindwa na yanakuwa salama.Serikali ya Marekani imefanya uwekezaji mkubwa katika eneo la afrika mashariki kwa hiyo wameweka kikundi hiki makusudi ili kiwe ni kama jicho la kuhakikisha kwamba hakuna hatari yoyote katika uwekezaji wao.Team SC41 imekita mizizi yake ndani ya serikali na wanafahamu kila kinachoendelea ndani ya serikali na endapo kuna mpango wowote wa kuhujumu maslahi ya marekani basi watafahamu mara moja.Mimi ni mmoja wao japokuwa kazi yangu mimi ni tofauti na wengine.Kazi yangu mimi ni kutafuta taarifa Fulani toka kwa mtu.Endapo kuna mtu ambaye team SC41 wanahitaji kitu Fulani toka kwake basi hunitumia mimi.Hujenga mahusiano na mtu huyo na kisha huhakikisha kwamba nimekipata kitu hicho au taarifa hiyo inayotakiwa.” akasema Peniela

“ Kuingia katika mahusiano na Dr Joshua ulikuwa ni mpango wa team yako au ulipenda mwenyewe? Ama kuna kitu ulikuwa unakitafuta? Akauliza jaji Elibariki ambaye alionekana kuwa mkali sana.

“ Ulikuwa ni mpango wa TeamSC41 wala haikuwa ni kwa mapenzi yangu.Kuna kitu walikuwa wanakihitaji toka kwake na ndiyo maana wakanitumia mimikuanzishamahusiano naye” Akasema Peniela

“ Ni kitu gani mnachokitafuta kwa Dr Joshua? Akauliza Mathew

“ Package E21” akajibu Peniela

“ Package E 21?.Ni kitu gani hicho? Akauliza Mathew
“ Hata mimi sifahamu ni kitu gani na hakuna aliyewahi kunieleza package hiyo ina nini lakini inaonekana ni kitu chenye thamani kubwa kwa sababu Package hiyo inafichwa ikulu na hata hapo ikulu kwenyewe anayefahamu mahala ilipo ni rais peke yake .Dr Joshua anataka kuiuza package hiyo kwa matrilioniya fedha.Dr Flora mke wa rais aligundua kuhusu jambo analotaka kulifanya mume wake na alijitajhidi sana kumsihi mume wake asiiuze package hiyo lakini bila mafanikio na ndipo alipoamua kuwaeleza wanae kile anachotaka kukifanya baba yao na mchana wa siku ambayo alipanga kuonana na wanae jioni ili awaeleze anachokifanya baba yao akafariki dunia.Aliuawa ili asiweze kutoa siri”
“ What ?! Dr Flora aliuawa kwa sababu ya hiyo Package? Akashangaa jaji Elibariki.
“ Ndiyo.Dr Flora aliuawa ili asiweze kutoa siri hiyo.”akasema Peniela.Kila mtu alikuwa kimya pale sebuleni.
“ Una uhakika gani kwamba Dr Flora aliuawa ili asiweze kutoa siri? Akauliza Mathew
“ katika biashara ya package hiyo Dr Joshua anashirikiana na watu wengine wawili.Katibu wake Dr Kigomba na daktari wa familia ya rais anaitwa Captain Amos.Hawa ndio wanaofahamu kila kitu kuhusianana biashara nzima ya package hiyo.Captain Amos naye yuko team SC41 na ndiye anayetupa taarifa zote kuhusiana na kila kinachoendelea ikulu.Captain Amos ndiye aliyemchoma sindano ya sumu Dr Flora kwa amri ya rais.” Akasema Peniela

“Mawazo yangu yalikuwa sawa kabisa kwamba Dr Flora aliuawa.Nilitegemea tu kwamba lazima kifo chake kitakuwa kimesbabishwa na jambo kubwa na kama anavyosema Peniela nikwamba aligundua kuhusiana na hiyo package anayotaka kuiuza Dr Joshua na ndipo alipouawa.Package hiyoni ya nini? Inamahusiano yoyote na hizi nyaraka alizoziiba Edson? Mhh! Mambo haya yanazidi kuwa magumu.” Akawaza Mathew.
Jaji Elibariki alikuwa ameinama amekishika kichwa chake

“ Ouh Mungu wangu ! akasema Elibariki halafu akainua kichwa akasema
“Mathew tulikuwa sahihi kabisa kuhisi kwamba Dr Joshua atakuwa akihusika na kifo cha mkewe na ndiyo maana nguvu kubwa ikatumika kuhakikisha sababu ya kifo cha Dr flora haijulikani.Kumbe tulipompelekea ile taarifa yetu ya uchunguzi iliyobainishakwamba dr Flora aliuawa kwa sumu tulikuwa tunajipalia makaa ”akasema Elibariki na kumstua peniela
“ Mlifahamu kilichomuua Dr Flora? Akauliza Peniela

“Ndiyo tulifahamu kila kitu.”akasema Mathew
“ Badaa ya kifo cha Dr Flora ilitolewa taarifa kwamba mwili wake usifanyiwe uchunguzi wowote kubainisababuya kifo chake na badala yake ikatolewasababu ya jumla kwamba kilichomuua ni shinikizo la damu. Mke wa Elibariki aliingiwa na hofu kuhusu kifocha mama yake namazingira kilivyotokea hivyo akamuomba mume wake amsaidie kuweza kuufahamu ukweli.Elibariki likuja kwangu akaniomba nimsaidie kufanya uchunguzi wa kubaini kilichomuua Dr Florana nusura tungepoteze maisha yetu wakati wa kufanya uchunguzi huo lakini mwishowe tuliubaini ukweli .Tuligundua hadi aina ya sumu iliyomuua Dr Flora .Baada ya hapo Elibariki alimpelekea mheshmwia rais majibu yale ili ayafanyie kazi bila ya kufahamu kwamba ni yeye ndiye aliyekuwa nyuma ya yale mauaji”akasema Mathew
“I’m impressed with you guys.Namna mnavyofanya kazi zenu mmenifurahisha sana” akasema Peniela
“ Baada ya Dr Joshua kugundua kwamba tayari Elibariki amegundua kilichosababisha kifo cha dr Flora aliamuru auawe na ndipo lilipopangwa lile shambulio ambalo alinusurika kuuawa”akasemaMathew.Jaji Elibariki naye akasema

“ Katika shambulio lile alitokea mwanamke mmoja na kunichukua toka eneo la tukio na akanikabidhi kwako.Mpaka leo sijamfahamu mwanamke yule ni nani na kwa nini aliniokoa.Hakutak……”kabla Elibariihajaendelea Penielaakaingilia kati

“That’s Jessica.Naye ni team SC41.Alipewa maagizo ya kukuokoa na Amos .”akasema Peniela.
“ Dah ! nimechoka kwa kweli.Hawa team SC41 wako kila mahala ,but why they saved me? Akauliza Elibariki.Kabla Peniela hajajibu kitu Mathew akauliza

“ John mwaulaya anaendeleaje?
Swalilile lilimstua mno Peniela.Hakuwa ametegemea kama Mathew anamfahamu John
“ Umesema John mwaulaya? Akauliza peniela

“ Ndiyo.John Mwaulaya.is he ok? Akauliza Mathew

“ Do you know him?
“ yes I know him” akasema Mathew

“ John mwaulaya ni nani? Akauliza jaji elibariki

“ Ni kiongozi wa team SC41”akajibu mathew

“ Unafahamiana na kiongozi wa team SC41? akauliza Elibariki kwa mshangao

“ Ndiyo ninamfahamu.Japokuwa si marafiki lakini mimi na yeye tun historia .Nitawaeleza siku nyingine ninamfahamuje John mwaulaya lakini usiku huu ni usiku wa peniela ,ametueleza mambo makubwa kabisa na kutufunulia mambo mengi mazito.Peniela endelea kutueleza kile ulichokusudia kutueleza” akasema Mathew,Penielaakaendelea

“ baada ya kunusurika katika ajali ile ,Elbariki alikuja nyumbani kwangu kwani aliamini ni sehemu salama.Ni kweli ni sehemu salama na alikuwa salama hadi pale Jason alipokwenda kutoa taarifa polisi kwamba Elibariki yuko kwangu.Taarifa zile zilimfikia Amos naye akamtaarifu kiongozi wangu John mwaulaya aliyeamuru Jason akamatwe na aeleze kwa nini alitoa taarifa zile kwa jeshi la polisi.Alikuwa na wasi wasi kwamba yawezekana Jason akawa anafahamu mambo mengi kuhusu team SC41.Walimteka Jason na kumtesa na ndipo alipopata nafasi ya kunipigia simu na kunifahamisha kwamba ametekwa.Nilichukizwa mno na kitendo kile cha kuwateka na kuwatesa watu wangu wa karibu na hiyo ndiyo sababu niko hapa nikiwaeleza haya yote niliyowaeleza ambayo sikupaswa kuwaelezakitendo kile na hii ndiyo sababu niko hapa kwenu mida hii nikiwaeleza haya yote niliyowaeleza na nikihitaji msaada wenu.” akasema Peniela akaak kimya kidogona kusema tena

“ I need your help guys”

“Our help? Akauliza Mathew

“ yes. Your help.”

“ Unahitaji msaada gani? Akauliza Mathew
“ To take down Team SC41”

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
Teheheh, wale wa kamaoja ka kupigia mswaki, hiyoo
 
SEHEMU YA 33
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ baada ya kunusurika katika ajali ile ,Elbariki alikuja nyumbani kwangu kwani aliamini ni sehemu salama.Ni kweli ni sehemu salama na alikuwa salama hadi pale Jason alipokwenda kutoa taarifa polisi kwamba Elibariki yuko kwangu.Taarifa zile zilimfikia Amos naye akamtaarifu kiongozi wangu John mwaulaya aliyeamuru Jason akamatwe na aeleze kwa nini alitoa taarifa zile kwa jeshi la polisi.Alikuwa na wasi wasi kwamba yawezekana Jason akawa anafahamu mambo mengi kuhusu team SC41.Walimteka Jason na kumtesa na ndipo alipopata nafasi ya kunipigia simu na kunifahamisha kwamba ametekwa.Nilichukizwa mno na kitendo kile cha kuwateka na kuwatesa watu wangu wa karibu na hiyo ndiyo sababu niko hapa nikiwaeleza haya yote niliyowaeleza ambayo sikupaswa kuwaelezakitendo kile na hii ndiyo sababu niko hapa kwenu mida hii nikiwaeleza haya yote niliyowaeleza na nikihitaji msaada wenu.” akasema Peniela akaak kimya kidogona kusema tena
“ I need your help guys”
“Our help? Akauliza Mathew
“ yes. Your help.”
“ Unahitaji msaada gani? Akauliza Mathew
“ To take down Team SC41”
ENDELEA………………
Watu wote mle ndani walibaki kimya wakimtazama Peniela.Ni Mathew aliyefungua mdomo wake na kumuuliza
“ You want to take down Team SC41?
“ yes I do” akajibu Peniela
“ Nataka kuimaliza kabisa team Sc41” akasisitiza.Sauti na sura yake vilionyesha wazi kwamba alikuwa amedhamiria kufanya alichokisema.Mathew akamtazama kwa makini sana na kuuliza
“ Kwa nini unataka kuimaliza team SC41?
Peniela bila kusita akajibu
“ Sababu kubwa inayonifanya nitake kuimaliza team SC41 ni ili niwe huru.Ninataka nianze kuishi maisha mapya tofauti na haya ninayoishi sasa .Nataka kuishi maisha ya kawaida kama wenzangu.Baada ya kuingia team SC41 maisha yangu yaliharibika na ndoto zangu zote za maisha kuyeyuka.Mnionavyo hapa sina maisha ya kawadia kama wenzangu,siwezi kuwa na mpenzi,siwezi kuwa na familia na siwezi kufurahi kama wanawake wenzangu.Nimechoshwa na maisha haya,nimechoshwa na kuutumia mwili wangu kama bidhaa kwa faida ya Tweam SC41,ninataka kuachana na aina hii ya maisha na ili niachane nayo lazima nitoke team SC41 na hakuna namna ninayoweza kutoka Team SC41 zaidi ya kukimaliza kabisa kikundi hiki.John Mwaulaya ameniahidi kwamba ataniachia niwe huru lakini sina hakika kama atatimiza lengo lake na kwa hiyo lazima nifanye jitihada za kujiweka huru mimi mwenyewe na kuimaliza Team SC41 ndiyo njia pekee.I need your help guys.Nimewaeleza ukweli huu ambao sijawahi kumweleza mtu mwingine ili mnielewe na mnisaidie .” Akasema Peniela
“ kwani ilikuaje hadi ukajiunga na Team SC41? Akauliza Anitha
“ Ni hadithi ndefu kidogo. Lakini nitawaelezeni kwa ufupi ili na ninyi mpate picha.”akasema Peniela na kunyamaza kidogo halafu akaendelea
“ Mimi ni yatima.Nilipopata akili nilijikuta katika kituo cha kulelea watoto yatima.Mpaka leo hii sijawahi kupata taarifa zozote za kuhusu wazazi au ndugu zangu.Kitu nilichoambiwa na mama Bernadetha mlezi wangu ni kwamba nilipelekwa pale kituoni na mtu aitwaye John Mwaulaya ambaye ndiye mfadhili wangu amekuwa akinihudumia kwa kila kitu.Nikiwa pale kwa mama Bernadetha niliishi maisha mazuri,nilipata kila kitu nilichohitaji kiasi kwamba nilijiona sawa na watoto wengine wote.John mwaulaya alikuwa akinitumia kila kitu kupitia kwa mama Bernadetha.Nilimshukuru Mungu kwa kunijalia mfadhili kama yule ambaye alikuwa akinipatia kila kitu.” Peniela akanyamaza kidogo akanywa whysky na kuendelea
“ Nilianza masomo katika shule ya kimataifa,na gharama zote zililipwa na John.Nilikuwa ni mmoja wa wanafunzi wenye uwezo mkubwa darasani.Nilisoma vizuri hadi nilipofika darasa la saba.Kwa maisha niliyoishi ilikuwa vigumu kuamini kwamba nilikuwa ni mtoto nisiye na wazazi kwani niliishi maisha kama mtoto wa tajiri mkubwa.Katika miaka hii yote sikuwahi hata siku moja kuonana na mfadhili wangu John ingawa nilitaka sana kumuona walau niweze kumjua ni mtu wa namna gani .Pamoja na maombi hayo ya siku nyingi lakini John Mwaulaya hakuwahi kujitokeza hata siku moja nimuone na sikuelewa ni kwa nini.Nilipomuuliza mama Bernadetha alisema kwamba John ni mtu wa safari nyingi wa hiyo atakapopata nafasi nitaonana naye.Miaka ilikwenda hadi nilipohitimu darasa la saba.Nakumbuka siku ya sherehe ya kumaliza darasa la saba ndiyo siku ambayo nilifanikiwa kuisikia sauti ya John Mwaulaya.Siku hiyo nilichukuliwa na mama Bernadetha na akanipeleka katika jumba moja kubwa la kifahari akanieleza kwamba jumba lile ni langu nimepewa zawadi na John Mwaulaya kwa kumaliza darasa la saba.Jumba lile lilikuwa kubwa ,zuri na la kifahari sana na nilipewa pia wahudumu wa kunihudumia .Usiku wa siku ile John mwaulaya alinipigia simu akajitambulisha,nilifurahi sana kuisikia sauti yake.Niliendelea na masomo ya sekondari na huku akiendelea kunihudumia kwa kila kitu na hadi ninamaliza kidato cha sita bado sikuwa nimebahatika kuonana na John mwaulaya ana kwa ana.Nilipomaliza kidato cha sita na matokeo kutoka mazuri,John alinitaarifu kwamba alikuwa amenitafutia chuo nchini marekani .Nilifurahi sana na nikajiandaa na kuelekea marekani.Nilipofika kule nilipelekwa katika chuo ambacho kinafundisha masomo tofauti kabisa nay ale ambayo nilikwenda kuyasomea.Chuo hicho kinafundisha mambo yanayohusiana na Team SC41.Mwanzoni sikuwa tayari kujifunza kuhusu masuala hayo lakini nilikamatwa na kuingizwa katika chumba Fulani na kufungiwa humo na baada ya kutolewa mle nilijihisi mtu mpya kabisa kwani nilikubaliana na masomo yote yahusuyo Team SC41.Nilijifunza mafunzo yale kwa miaka miwili nikarejea Tanzania na kujiunga rasmi na team SC41 Tanzania.Hata baada ya kujiunga na teamSC41 bado sikuwahi kuonana na John mwaulaya hadi hivi majuzi nilipochukuliwa na kupelekwa mahala anakoishi nikaonana naye kwa mara ya kwanza akiwa anaumwa sana.” Akasema Peniela .
“ kumbe wana hadi chuo cha kujifunzia? Akashangaa Jason ambaye kwa muda wote wa mjadala ule alikuwa kimya
“ Ndiyo wana chuo tena kikubwa tu kinachotoa kozi mbali mbali.Team SC41 imesambaa katika sehemu mbali mbali duniani ambazo nchi ya Marekani imefanya uwekezaji mkubwa na ndiyo maana kuna chuo kabisa cha kujifuniza kuhusu kazi za Team SC41.Kuna mafunzomengi yanatolewa katika chuo hiki yakiwamo mafunzo ya kijeshi ,mafunzo ya kiintelijensia na mengine mengi.” Akasema peniela
“ Katika chumba hicho ulichoingizwa na ukatoka ukiwa na mtazamo mpya ni kitu gani hufanyika hadi kuwabadili watu mtazamo na kuwafanya wakubali kujiunga na Team SC41? Akauliza Anitha
“ hata mimi sielewi huwa nini kinafanyika lakini ukitoka mle unajiona ni mtu mpya kabisa.” Akasema Peniela
“ I know what they do” akasema Mathew
“ do you know? Akauliza jaji Elibariki
“ yes I know.” Akajibu Mathew
“ Kuna teknolojia ambayo huitumia katika hucheza na akili ya mtu na ukishatoka mle ndani basi akili yako tayari inakuwa imejazwa mambo mengi kuhusiana na team SC41 .” akasema Mathew
“ Nakubaliana nawe Mathew kwamba yawezekana ni kweli wakawa wanatumia teknolojia hiyo kwa sababu ukitoka tu ndani ya hicho chumba hata kama ulikuwa mbishi kiasi gani basi utafuata kila wanachokuelekeza na utajikuta unaipenda team SC41.” Akasema peniela
“ Kama wanawafanyia hivyo basi watu hawa ni mashetani kwani wana waharibu watu akili zao kwa faida ya nchi yao.Ninyi mnapata faida gani kama team SC41? Akauliza Anitha
“ faida kubwa ambayoninaweza kuisema tunaipata ni kuishi maisha mazuri kutokana na mishahara mikubwa wanayotulipa.Tunalipwa mamilioni ya fedha kama mishahara ambayo inatuwezesha kuishi maisha ya kifahari lakini mambo mengine yote tunayoyafanya ni kwa maslahi ya marekani.” Akasema Peniela.
“ Serikali yetu inafahamu chochote kuhusiana na kuwepo kwa kikundi hiki hapa nchini? Akauliza Jason
“ Hapana .Serijkali bado hawafahamu chochote kwa sababu kikundi hiki kinafanya shughuli zake kwa siri kubwa ingawa tayari kimekwisha kita mizizi hadi katika serikali kuu “
“ kwa hiyo kazi zao tunaweza kusema ni sawa na ujasusi? Akauliza jaji Elibariki
“ Tunaweza kusema kazi zao zinafanana na hizo ingawa wanachoangalia wao ni maslahi ya marekani pekee.Kama kuna hatari yoyote katika maslahi ya marekani basi tunawataarifu makao makuu.Mfano kama kuna mpango wowote wa kubadili mikataba ya uwekezaji au kuna chokochoko zozote za chini chini kuhusiana na uwekezaji uliofanywa na marekani hapa nchini basi taarifa hizo huzipata mara moja kwa sababu tayari kuna mizizi ndani ya serikali.Hata hivyo naomba mnielewe ndugu zangu kwamba Team SC41 inashughulika na mambo yale yahusuyo maslahi marekani tu.” Akasema Peniela
“ hata hivyo kikundi hiki bado ni hatari kwa usalama wa nchi yetu na tunatakiwa tukiondoe.Lakini tutawezaje kukiondoa ? Tutakapokigusa kikundi hiki tutakuwa tumeyagusa maslahi ya Marekani na kunaweza kukatokea mgogoro kati ya serikali yetu na serikali ya Marekani ” Akasema jaji Elibariki
“ Ndiyo manaa nimekuja hapa ili kupata mawazo yenu” akasema Peniela
“ peniela,we’ll help you take down team SC41 “ akasema Mathew
“ How ?! Elibariki akauliza
“ let me figure out how we can take down team SC41 lakini ninawahakikishia ndugu zangu lazima tutaiondoa .Bila hata Peniela kuleta ombi lake ,binafsi tayari nilikuwa katika mpango wa kuimaliza kabisa team SC41 ” Akasema Mathew
“ Ulikuwa na mpango huo? Akauliza Peniela
“ ndiyo nilikuwa na mpango huo”
“ kwa nini ulitaka kuiondoa team SC41? Akauliza jaji Elibariki
“ Ni hadithi ndefu kama nilivyo waambia awali .Mimi na John mwaulaya tuna historia ambayo ndiyo sababu iliyonifanya nitake kulipiza kisasi kwa kitendo walichonifanyia.” Akasema Mathew
“ What happened? Mna historia gani wewe na John mwaulaya? Akauliza Peniela.Mathew akainama akazama katika mawazo mengi ,wote wakabaki kimya wakimtazama,wakisubiri kusikia atasema nini.Baada ya kama dakika moja Mathew akainua kichwa na kusema
“ John mwaulaya na team yake ndiyo chanzo cha mimi kuishi maisha haya “akasema Mathew na kisha akawasimulia kila kitu kilichotokea hadi familia yake ikateketezwa.Hadithi ile ikamuumiza sana Peniela.
“ John is a monster” akasema Peniela
“ Kumbe ukatili wake hajauanza jana ,na tayari amekwisha umiza watu wengi .Sikutegemea kama angeweza kufanya ukatili mkubwa kiasi hiki. Hapo kabla nilikuwa na hamu sana ya kutaka kumfahamu John mwaulaya lakini kwa sasa sina hata hamu ya kumuona tena.He’s a monster.Ni kwa sababu yake leo hii mimi nimekuwa na maisha haya.Kama isingekuwa yeye leo hii mimi ningekuwa na maisha yangu mazuri tu yenye furaha.Ndani ya Team Sc41 hakuna mtu ambaye anaweza kusema kwamba maisha yake yana furaha.Wote maisha yetu yako hivi hivi na ukikosea kidogo tu basi hawakuachi wanakuua kimya kimya.Ni kikundi cha hatari sana hiki kwa hiyo ndugu zangu nahitaji sana msaada wenu ili kwa pamoja tuweze kukiangamiza kikundi hiki.Mimi niko tayari kutoa kila aina ya ushirikiano ili kwa pamoja tuweze kukimaliza kikundi hiki.Ninazifahamu siri nyingi za Team SC41 kwa hiyo basi nitawaeleza kila kitu kuhusiana na kikundi hiki ” akasema Peniela
“ Peniela nimekusikiliza kwa makini maongezi yako,na ninapenda kukupa pole sana kwa mambo yote yaliyokupata.Mwanzoni nilikuwa na hasira na wewe sana kwa mambo ambayo umeyafanya lakini kwa sasa nimekuelewa na niko tayari kuungana nawe katika kuiondoa hiyo team SC41.Pamoja na hayo kuna jambo nataka kuuliza,huyu John mfadhili wako hajawahi hata mara moja kukueleza chochote kuhusiana na asili yako? Akauliza jaji Elibariki
“ Elibariki nashukuru sana kwa kunielewa .Umeuliza kama vile ulikuwa katika akili yangu .Nina maswali mengi ya kumuuliza John mwaulaya na moja wapo ni hilo hapo la kuhusiana na wapi alinitoa hadi akanifikisha katika kituo kile.Nataka kufahamu asili yangu na mwenye kujua haya yote ni John pekee.”akasema Peniela
“ Hata hivyo” akaendelea
“ Siku ya kwanza niliyoonana naye alinipa kikasha Fulani ambacho alisema kwamba nisikifungue hadi pale nitakapokuwa nimeikamilisha operesheni 26B.Aliniambia kwamba kasha hilo haliko kamili kwa hiyo inanibidi nitafute makasha mengine mawili ili liweze kukamiliza na alinielekeza kwa mtu ambaye alisema nimuone na ndiye atakayenipa maelekezo yote kuhusiana na mahala makasha mengine yaliko.John alisema kwamba niyatunze sana makasha hayo kwani ndimo kuna kila kitu kuhusiana na mimi” akasema Peniela
“ Kasha hilo liko wapi? Akauliza Mathew
“ Nimelihifadhi katika sehemu salama”
“ Ok Good.Endelea kulihifadhi na baada ya kukamilisha kila kitu basi mimi binafsi nitakusaidia katika kuutafuta ukweli kuhusiana na asili yako,wazazi wako,na ndugu zako” akasema Mathew
“ Me too.Count me in” akasema jaji Elibariki
“ Nashukuruni sana jamani kwa kujitolea kunisaidia.Jambo hili limekuwa likiniumiza akili yangu kwa miaka mingi .Ninataka sana kufahamu mimi ni nani lakini sijui nianzie wapi.Natamani sana kulifungua kasha lile ili nifahamu kilichomo ndani lakini ninaogopa kwa sababu John alisema kwamba nilifungue kasha lile pale tu ambapo operesheni itakuwa imemalizika.Kwa sasa nimeanza kuwa na matumaini kwamba nitafahamu asili yangu.” Akasema Peniela
“ Peniela usijali.Ninakuhakiisghia kwamba tutakusaidia katika hilo suala na hata katika kuiondoa Team SC41.Lakini kuna jambo ambalo ninaliomba toka kwako kama mbadala wa kukusaidia mambo haya yote mawili”
“ Jambo gani Mathew? Akauliza Peniela
“ Ninaihitaji hiyo package pindi utakapoitwaa toka kwa Dr Kigomba” akasema Mathew.Peniela akashangaa na akabaki akimuangalia Mathew.Watu wote mle sebuleni wakabaki kimya wakisubiri kusikia atatoa jibu gani

PENIELA ATATOA JIBU GANI? TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………
 
SEASON 2
SEHEMUYA 34
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Me too.Count me in” akasema jaji Elibariki
“ Nashukuruni sana jamani kwa kujitolea kunisaidia.Jambo hili limekuwa likiniumiza akili yangu kwa miaka mingi .Ninataka sana kufahamu mimi ni nani lakini sijui nianzie wapi.Natamani sana kulifungua kasha lile ili nifahamu kilichomo ndani lakini ninaogopa kwa sababu John alisema kwamba nilifungue kasha lile pale tu ambapo operesheni itakuwa imemalizika.Kwa sasa nimeanza kuwa na matumaini kwamba nitafahamu asili yangu.” Akasema Peniela
“ Peniela usijali.Ninakuhakiisghia kwamba tutakusaidia katika hilo suala na hata katika kuiondoa Team SC41.Lakini kuna jambo ambalo ninaliomba toka kwako kama mbadala wa kukusaidia mambo haya yote mawili”
“ Jambo gani Mathew? Akauliza Peniela
“ Ninaihitaji hiyo package pindi utakapoitwaa toka kwa Dr Kigomba” akasema Mathew.Peniela akashangaa na akabaki akimuangalia Mathew.Watu wote mle sebuleni wakabaki kimya wakisubiri kusikia atatoa jibu gani


ENDELEA……………….
“ Team SC41 wameitafuta package hii kwa muda mrefu na kwa sasa ambapo wanakaribia kuipata watakuwa macho sana ili kuhakikisha kwamba inatua katika mikono yao.Hata hivyo nitafanya kila linalowezekana ili package hii iweze kutua katika mikono yetu.Mimi na ninyi tuko timu moja sasa kwa hiyo usijali Mathew nitahakikisha package hiyo unaipata.” Akasema Peniela
“ Ahsante sana Peniela .Ninakuhakikishia kwamba utakuwa salama tutakulinda hadi mwisho wa operesheni hii na tutafanikiwa kuiondoa kabisa Team SC41.Kwa sasa baada ya mjadala mrefu na kufahamu mambo mengi ambayo hatukuwa tumeyafahamu,tuna kazi kubwa tatu mbele yetu.Kazi ya kwanza ni kuitafuta hiyo package na kuhakikisha kwa gharama zozote zile tunaipata.Kazi ya pili baada ya kuipata packge hiyo ni kumuondoa Dr Joshua katika uogozi na kumfikisha katika vyombo vya sheria na kazi ya tatu ambayo lazima tuifanye ni kuiondoa Team SC41 .” akasema Mathew
“ Kitu tunachotakiwa kukifanya kwa nguvukuanzia sasa ni kukusanya ushahidi wa kutosha kuweza kumtia hatiani Dr Joshua.Yule ni mkuu wa nchi kwa hiyo kumshitaki kwa namna yoyote ile tunatakiwa tuwe na ushahidi mzito sana wa kumuhusisha na matukio makubwa ya kijinai.Tukio la kwanza ni katika kifo cha mkewe.Tuna uhakika mpaka hivi sasa kwamba amehusika lakini tunatakiwa tuwe na ushahidi mzito wa kuthibitisha ni kweli alihusika katika kifo cha mke wake.Tukifanikiwa kumpata katika hili basitutawezakumuangushakirahisi sana ” Akasema Mathew
“ Mathew kuna kitu nimekifikiria kinachoweza kuturahisishia kazi ” akasema Anitha
“.Ili kuweza kupata kile tunachokihitaji,tunatakiwa tuwatumie hawa watu wawili wa karibu na Dr Joshua.Kuna huyu Dr Kigomba na Captain Amos.Hawa watatusaidia sana kuweza kukipata kile tunachokitafuta.Mapendekezo yangu ni kwamba kwa kuwa sasa hivi Peniela ameiingia katika mahusiano na Dr Kigomba basi tuitumie vyema fursa hiyo .Kuna teknolojia ambayo tutaitumia na kuiweka katika simu ya Dr Kigomba na sisi tutakuwa tukifuatilia kila atakachokuwa akikiongea Dr Kigomba kupitia simu yake na vile vile kuna jambo lingine tutakalolifanya,tutaweka kifaa kidogo sana katika mkufu ambao Peniela atampatia kama zawadi ili awe akiuvaa kila siku.Kupitia saa hiyo tutaweza kufahamu mahala aliko na tutaweza pia kusikia kila atakachokiongea kwa hiyo itakuwa rahisi kwetu sisi kufahamu mahala aliko na vile vile kifa hiki kitatuwezesha sisi kusikia kila anachokiongea na myuyeyote .Hii itakuwa njia rahisi sana kunasa mawasiliano yake na Dr Joshua au na watu wengine na kwa hiyo hata atakapokuwa amepewa hiyo package basi itakuwa rahisi kwetu sisi kufahamu kila kitu.Jambo hili tutalifanya pia kwa Dr Joshua.Peniela atampatia mkufu ambao tutaweka kifaa kidogo sana ambacho kitatuwezesha sisi kusikia kila atakachokuwa akikiongea a vile vile tutaweza kumfuatilia kwa ukaribu sana.Nadhani hii inaweza kuwa njia rahisisana ya kufanikisha mpango wetu na kupata ushahidi wa k utosha dhidi ya Dr Joshua” akasema Anitha.
“ Ahsante Anitha kwa mawazo hayo mazuri.Natumai tukitumia njia hiyo tunaweza tukafanikiwa kwa wepesi sana.” Akasema Mathew
“ hata mimi nakubaliana na wazo hilo la Anitha” akasema Jaji Elibariki
“ Jason wewe unasemaje? Unaonekana uko kimya sana” akasema Mathew
“ Mimi pia sina kipingamizi na wazo hilo alilolitoa Anitha kwani teknolojia ndiyo njia pekee ya kutuwezesha kupata ushahidi wa uhakika na tunaouhitaji” akasema Jason
“ Ok vizuri.Kwa kuwa wote tunakubaliana na wazo alilolitoa Anitha,turudi sasa kwa muhusika mkuu wa jambo hili.Peniela kwa upande wako unasemaje? akauliza Mathew
“ mimi kwa upande wangu sina tatizo na ninashukuru kwa mawazo hayo mazuri ya Anitha.Mimi nitafanya kama mtakavyonielekeza .Lolote linalowezekana kufanyika kwa ajili ya kuimaliza team SC41 na kuwatia hatiani Dr Joshua na mtandao wake mimi niko tayari kulifanya.” Akasema peniela
“ nashukuru kusikia hivyo Penny”akasema Mathew.
“ Anitha atashughulikia suala hilo na hadi kesho mchana kila kitu kitakuwa tayari.Lini unategemea kuonana na Dr Kigomba?
“ Tumepanga tuonane kesho jioni”
“ Good.Kwa hiyo kesho mpaka hiyo kesho jioni kila kitu kitakuwa tayari na tutamaliza hili suala ” Akasema Mathew.
“ Mathew kuna mtu wa tatu ambaye naye anaweza akawa ni ushahidi mzuri sana wa kuweza kumtia hatiani Dr Joshua.Ni Captain Amos.Huyu ndiye aliyemuua Dr Flora kwa amri ya rais kwa hiyo ni mtumuhimu sana kwetu” akasema Peniela
“ Ni kweli Captain Amos ni muhimu sana katika jambo hili lakini kwa sasa nadhani tumuweke kwanza pembeni kwani yeye ndiye anayekupa maelekezo na taarifa zote kuhusiana na package hiyo.Tukimvuruga sasa tunaweza kuikosa hiyo package.Amos tutashughulikanaye baadae mwisho wa mchezo” akasema Mathew na kukawa kimya
“ Jamani nawaona tayari mmechoka.Umekuwa ni usiku mrefu lakini ulioambatana na mambo mengi makubwa .Nadhani ni wakati sasa wa kwenda kupumzika.Kesho tutaamkia katika mambo mengine mapya na inawezekana siku ya kesho ikawa ni siku ndefu sana.Mambo mengi yanaweza yakatokea kesho”akasema Mathew.
“ Mathew kabla ya kutawanyika nina jambo nataka kuongea na Elibariki na Jason pekee” akasema Peniela.Mathew wna Anitha wakaondoka pale sebuleni wakawaachia nafasi
“ Simulizi ya Peniela imenisismua sana.Sikutegemea kama historia yake iko namna hii. But Mathew do you trust her ? akauliza Anitha wakiwa katika chumba chao cha kazi
“ I do trust her.Peniela ametueleza ukweli halisi na hajaficha hata jambo moja.Ninaamini ana lengo la dhati la kuisambaratisha Team SC41.” Akasema Mathew
“Vizuri kama unamuamini.Lakini kuna kitu bado najiuliza sana,hiyo package itakuwa na nini ndani yake? Inaweza kuwa na uhusiano wowote na zile karatasi tulizozipata ambazo Edson aliziziiba ikulu? Akauliza Aitha
“ Hata mimi ninahisi hivyo,yawezekana zikawa na mahusiano Fulani na hiyo package anayoisema Peniela. Tukipata taarifa za kutoka kwa wale jamaa zangu niliowaomba msaada kuhusiana na nini kimeandikwa katika zile karatasi basi tutaweza kupata japo mwangaza .Nitawapigia simukeshoasubuhi kufahamu kama wamefanikiwa kufahamu kuhusiana na nini kimeandikwa katika karatasi zile“
Baada ya Mathew na Anitha kutoka sebuleni walibaki Peniela ,Elibariki na Jason.Peniela akawatazama usoni kwa zamu na kusema
“ Jamani nimeona nitumie fursa hii kuongea nanyi maneno machache usiku huu kabla ya kwenda kulala.Kwanza kabisa ninashukuru sana kwa kuzimaliza tofauti zenu na kuwa marafiki tena.Moyo wangu umefarijika sana.Mmeonyesha ukomavu mkubwa .” Akasema peniela akanyamaza kidogo na kuendelea
“ Usiku wa leo nimewaelezeni ukweli wangu na ninafikiri kwa hivi sasa ninyi nyote mmekwishanifahamu mimi ni nani baada ya kuwapa maelezo yale.Ninapenda kuchukua nafasi hii kuwaomba samahani sana kwa jambo nililowafanyia lakini nililifanya kwa nia njema tu ya kutaka kuwaweka mbalimbali ili uchunguzi wa kifo cha Edson usifanikiwe . Nilifahamu hatari iliyopo katika kulichunguza jambo hili.Pamoja na hayo nwapongeza sana kwa kusimama imara na hatimaye mmeweza kuufahamu ukweli.Hakunakati yenu aliyekuwa akinifahamu kwa undani.Kila nilichowaeleza ni cha kwelikabisa na ninaomba mniamini kwamba nina nia ya dhati ya kutaka kuiondoa team SC41 ili niweze kuwa huru.Katika hili ninawahitaji sana ninyi wawili mniunge mkono.Najua kila mmoja kwa sasa atakuwa bado ana hasira na mimi lakini ninaomba msifanye hivyo kwani nimekwisha waeleza sababu za mimi kufanya vile nilivyofanya.Hata hivyo kuna jambo ninataka niliweke wazi mbele yenu .” akasema peniela na kunyamza kidogo akawatazama wanaume wale waliokuwa kimya wakimsikiliza
“ Jason wewe ni mtu ambaye una nafasi kubwa sana katika maisha yangu.Umekuwa rafiki wa kweli.Umesimama na mimi hata kwa nyakati zile ambazo wengine hawakuweza.Thamani yako kwangu ni kubwa mno na siwezi kuielezea kamwe.Ninafahamu unanipenda kwa moyo wako wote na umenionyesha kwa vitendo ni namna gani unanipenda na hata mimi nakupenda sana .Elibariki nawe hali kadhalika una nafasi kubwa na ya kipekee kabisa katika moyo na maisha yangu.Umenionyesha kunipenda na kunijali.Ninyi nyote wawili ninawapenda sana..Ninaamini nyote pia mnanipenda kupita maelezo .Mimi kama binadamu ninahitaji kuwa na mararafiki,ninahitaji pia kuwa na mpenzi na ndiyo maana ninataka kufanya kila linalowezekana kuiondoa Team SC41 ili niweze kuwa huru kwa hiyo basi kwa kuwa ninyi nyote ninawapenda na ninyi nyote mnanipenda imenilazimu nifanye maamuzi ni yupi hasa ambaye ninataka niwe naye ” akanyamaza kidogo na kusema
“ Nitakuwa na Elibariki.Ninafahamu Elibariki ananipenda sana japokuwa tayari ana mke wake lakini ndiye ambaye moyo wangu umempenda na ndiye mwanaume ninayetaka kuanza naye maisha mapya.Jason ninaomba usinichukie mimi au Elibariki kwa maamuzi haya .Moyo wangu umenituma nifanye hivyo kwa hiyo nina amini kwamba mtaelewana na hakutakuwa na ugomvi tena kati yenu” akasema Peniela
Kimya kikubwa kikatawala mle ndani.Jason na Elibariki wakaangaliana .
“ Jason kuna chochote unachotaka kusema? Akauliza Peniela
“ Hapana.Sina chochote cha kusema.Nimekubaliana na maamuzi yako.Ninakupenda sana lakini ninaamini kwamba haikuwa bahati yangu ,ninaamini iko siku na mimi nitampata Yule ambaye atakuwa ameumbwa kwa ajili yangu.” Akasema Jason halafu akamgeukia Elibariki
“ Elibariki ninafahamu una mke wako wa ndoa lakini Peniela ameamua kukupenda.Umeisikia historia ya maisha yake imejaa mateso matupu.Peniela anahitaji kuanza maisha mapya yaliyojaa furaha na anahitaji mtu ambaye atamshika mkono na kumuondolea kumbu kumbu zote za nyuma,mtu ambaye atampenda na kumjali kwa moyo wake wote.Mtu ambaye atamuingiza katika ulimwengu mpya uliojaa kila aina ya furaha.Amekuchagua wewe japokuwa uko katika ndoa kwa sababu anaamini kwamba wewe ndiye mwenye sifa hizo.Wewe ndiye ambaye utampatia furaha ya maisha yake.Kwa hiyo nakuomba uwe muangalifu sana,nitakuwa nyuma yako kama kivuli na ukithubutu kumtoa chozi Peniela,I swear I’m going to take her away.” Akasema Jason.Jaji Elibariki akatabasamu na kusema
“ Ahsante sana Jason kwanza kwa kukubaliana na maamuzi ya Peniela na pili kwa kunikumbusha jukumu langu kubwa kwa Peniela.Huna haja ya kunifuata nyuma kama kivuli kwa sababu nina hakika hata siku moja Peniela hatatoa chozi.Nitafanya kila ninaloweza kulifanya kuhakikisha kwamba Peniela hatoi chozi.” Akasema jaji Elibariki .Peniela alikuwa akitabasamu
“ Thank you guys..NInashukuru sana.Ninyi ni wanaume wa ukweli mnayamaliza mambo kiume.Nimefurahi sana kuwa na watu kama ninyi katika maisha yangu.’ Akasema Peniela na kisha akainuka na kuwaomba Jason na Elibariki wasimame kisha wote wakakumbatiana.
“ Ahsanteni sana guys sasa ni wakati wa kupumzika kama alivyosema Mathew.Nadhani tutaonana kesho mchana” akasema Peniela
“ Are you sure you want to go? Akauliza Elibariki
“ Yes ! I have to go Elibariki.Tutaonana kesho.Nitandoka na Jason kwani gari lake liko pale kwangu” akasema Peniela.Mathew akaitwa wakamuaga na kuondoka kwa miadi ya kuonana tena kesho yake.
“ Peniela are you sure you did the right choice? Akauliza Jason wakiwa garini baada ya kuondoka nyumbani kwa Mathew
“ What choice? Akauliza Peniela
“ Kuingia katikamahusiano na Elibariki ambaye tayari ana mke wake wa ndoa”
Peniela akacheka kidogo na kusema
“ Nilidhani mambo yale tumekwisha yamaliza Jason “
“ Ndiyo yamekwisha lakini si unajua ninakujali sana na ninataka niwe na uhakika kama unakifahamu kitu unachotaka kukifanya.”
“ Nina uhakika na maamuzi yangu Jason naniko tayari kukabiliana na change moto zote zitakazojitokeza” Akajibu Peniela kwa ufupi
“ Sawa Penny lakini kumbuka siku zote kwamba mimi niko hapa na ninakupenda na nitakuwa tayari kukupokea muda wowote ukinihitaji.Ukihitaji mtu wa kuongea naye,kubadilishana mawazo,mtu wa kulia naye ,usiende mbali niko hapa ninakusubiri.” Akasema Jason
“ Nashukuru sana Jason.Una mchango mkubwa sana kwangu.Siku zote nitakujali na kukuthamini kama rafiki wa kweli” akasema Peniela na kisha safari ikaendelea.
Walifika nyumbani kwa Peniela Jason akachukua gari lake akaondoka na Peniela akaenda chumbani kwake kulala.Kabla ya kulala akaona ni bora ampigie simu Dr Joshua kumjulia hali na kumuonyesha ni namnagani anamjali.Akachukua simu na kupiga lakini simu ikaita bila kupokelewa,akapiga tena simu ikaita bila kupokelewa
“Yawezekana Dr Joshua atakuwa tayari amelala mida hii au atakuwa katika shughuli nyingine.Nitaongea naye hata kesho” akawaza Peniela na kuweka simu mezani akapanda kitandani.Kabla hajajilaza simu ikaanza kuita.
“ Its him” akasema Peniela na kuinuka akaenda akaichukua na kupokea
“ Hallow Dr Joshua akasema peniela
“ Hallow peniela.Hujambo malaika wangu? Umenistua kidogo kwa simu hii ya usiku mwingi.Nimeogopa nikadhani labda una tatizo “ akasema Dr Joshua
“ Usistuke Dr Joshua.Nimekosa kabisa usingizi nimekuwa na mawazo mengi nikikuwaza wewe na ndiyo maana nikaona ni vyema endapo nitakupigia walau nisikie sauti yako”
“ Nashukuru sana Peniela kwa kunikumbuka.Hata mimi nimekukumbuka na nilitamani sana kukupigia simu walau niisikie sauti yako lakini nilishindwa kutokana na kubanwa sana na vikao”
“ Pole sana Dr Joshua” akasema Peniela
“ Ahsante peniela” akajibu Dr Joshua na halafu kikapita kimya kifupi.Baada ya sekudne kadhaa Peniela akauliza
“ Vipi hali ya mwanao Flaviana?
“ Flaviana bado hali yake si nzuri.Nimeshauriana na madaktari na kesho atapelekwa nje ya nchi kwa matibabu zaidi.Nimeagiza apelekwe nchini afrika ya kusini.Nitafanya kila lililo ndani ya uwezo wangu kuhakikisha mwanangu anapona” akasema Dr Joshua
“ Pole sana Dr Joshua.Aliyefanya kitendo hiki Elibariki tayari amekamatwa?
“ Hapana bado hajakamatwa lakini tayari jeshi la polisi limekwisha pata fununu za mahala alikojificha kwa hiyo muda wowote nina hakika watamtia nguvuni” akasema Dr Joshua
“ Dr Joshua nafahamu uko katika wakati mgumu sana hivi sasa.Naomba ufahamu kwamba hauko peke yako.Niko pamoja nawe katika wakati huu mgumu.Ninakupenda ”
“ Nashukuru sana Peniela kwa kusimama pamoja nami hasa katika wakati huu mgumu.Ninakupenda sana “
“ Hata mimi nakupenda pia dr Joshua .Samahani sana kwa kukusumbua usiku huu.Nimefurahi nimesikia sauti yako.Sasa waweza kupumzika.” Akasema Peniela
“ Hata mimi nimefarijika sana kuisikia sauti yako Peniela .Ulale salama malaika wangu kesho nitakupigia simu kukutaarifu hali ya Flaviana inavyoendelea” akasema Dr Joshua wakaagana na kukata simu
“Huyu mzee angejua siku zake zinahesabika wala asingethubutu kuniita mimi malaika.Kama angenifahamu alitakiwa kuniita ziraili wake kwani hajui kilichomo moyoni mwangu” akawaza Peniela na kujitupa kitandani akalala.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO
 
SEHEMU YA 35
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Dr Joshua nafahamu uko katika wakati mgumu sana hivi sasa.Naomba ufahamu kwamba hauko peke yako.Niko pamoja nawe katika wakati huu mgumu.Ninakupenda ”
“ Nashukuru sana Peniela kwa kusimama pamoja nami hasa katika wakati huu mgumu.Ninakupenda sana “
“ Hata mimi nakupenda pia dr Joshua .Samahani sana kwa kukusumbua usiku huu.Nimefurahi nimesikia sauti yako.Sasa waweza kupumzika.” Akasema Peniela
“ Hata mimi nimefarijika sana kuisikia sauti yako Peniela .Ulale salama malaika wangu kesho nitakupigia simu kukutaarifu hali ya Flaviana inavyoendelea” akasema Dr Joshua wakaagana na kukata simu
“Huyu mzee angejua siku zake zinahesabika wala asingethubutu kuniita mimi malaika.Kama angenifahamu alitakiwa kuniita ziraili wake kwani hajui kilichomo moyoni mwangu” akawaza Peniela na kujitupa kitandani akalala.

ENDELEA……………….
Ulikuwa ni usiku mgumu sana kwa jaji Elibariki.Kila alipojaribu kufumba macho na kuusaka usingizi,picha ya peniela ilimjia
“ Ama kweli peniela ameniingia katika kila mshipa wa mwili wangu.Sipati usingizi nikimuwaza yeye tu” akawaza jaji Elibariki halafu akainuka na kukaa
“ Mke wangu Flaviana yuko hospitali akiyapigania maisha yake lakini akili yangu yote inamuwaza peniela tu.mwanamke huyu ana kitu gani cha kutupumbaza sisi wanaume kiasi hiki? Kila mwanaume ambaye anatembea naye basi hayuko tayari kuachana naye.Hii ni sababu iliyopelekea hata Jason atake kuniua siku ile kwa kunipiga na chupa kichwani.Peniela amefanikiwa hadi kumteka mkuu wa nchi na sasa ametua kwa katibu wake Dr Kigomba.Uwezo wake mkubwa wa kuweza kumnasa mwanaume yeyote umewafanya Team SC41 wamtumie sana katika shughuli zao nyingi .Sina hakika kama kuna mwanaume timamu ambaye anaweza akamkataa peniela.”akaendelea kuwaza jaji Elibariki na uso wake ukajenga tabasamu baada ya kuyakumbuka maneno aliyoyasema peniela mbele ya Jason

“ Nitakuwa na Elibariki.Ninafahamu Elibariki ananipenda sana japokuwa tayari ana mke wake lakini ndiye ambaye moyo wangu umempenda na ndiye mwanaume ninayetaka kuanza naye maisha mapya “

“ Katika wanaume wote amenichagua mimi niwe mpenzi wake.Ninajisikia furaha na fahari kubwa sana kwani hata mimi ninampenda sana peniela kwa moyo wangu wote.Najua nitakutana na changamoto nyingi lakini nitazishinda .kwa ajili yake niko tayari kwa jambo lolote lile” akawaza jaji Elibariki na mara sura ya mke wake Flaviana ikamjia
“ Naomba nisamehewe kwa mawazo haya lakini nina hakika kwa Flaviana nilikosea njia na ndiyo maana ndoa yetu imetawaliwa na migogoro isiyokwisha.Nyumba yetu imekuwa haina furaha hata kidogo.Kwa Peniela hali ni tofauti kabisa.Pamoja na matatizo yote tuliyonayo sasa hivi lakini tukikutana upendo wa dhati unajidhihirisha kati yetu.Ninaamini Peniela ndiye hasa mwanamke wa maisha yangu.Flaviana ni mke wangu lakini amenifanyia mambo mengi mabaya lakini nimekwisha msamehe kwa mambo yote aliyonifanyia ila sina hakika kama bado moyo wangu una mapenzi tena kwake.Namuombea Mungu apone na akishapona na masuala yangu yakamalizika basi sintakuwa na na la ziada zaidi ya kuhitimisha safari yetu ya maisha ya pamoja kama mume na mke ili nianze maisha mapya na Peniela.Nina hakika kwa wakati huo tayari Dr Joshua atakuwa amekwisha fikishwa mbele ya vyombo vya sheria na nina imani Flavian atakuwa akinichukia mno kwa kitendo hicho kwa hiyo hata kama tukiendelea pamoja we’ll never be happy .Ni bora tuachane na kila mmoja akaendelea na maisah yake”akaendelea kuwaza jaji Elibariki akainuka na kuchungulia nje halafu akakaa tena kitandani
“ Peniela ametueleza mambo makubwa na mazito usiku wa leo na nimemuelewa vizuri sana.pamoja na hayo kuna vitu ambavyo nimejiuliza sana kuhusiana maisha yake na sijapata jibu.Peniela ametoka wapi? John alimtoa wapi? Alimuokota au ilikuaje akafika mikononi mwake na kumpeleka katika kituo cha kulelea watoto yatima? Akajiuliza jaji Elibariki
“ Huyu mtu John mwaulaya atakuwa akifahamu kila kitu kuhusiana na Peniela.Kuna kila ulazima wa kumsaidia peniela kufahamu kuhusiana na asili yake.Ninahisi yawezekana labda team SC41 wakawa wakiiba watoto na kuwakuza ili wawatumie baadae kwa kazi zao kama walivyofanya kwa peniela.Nina wasiwasi yawezekana labda wazazi wa peniela wakawa bado wako hai .Nitawaeleza akina Elibariki asubuhi ili tulishughulikie jambo hili na kuufahamu ukweli kuhusu Peniela.”akawaza jaji Elibariki na kujilaza tena kitandani


******

Kumekucha tena,siku nyingine imeanza.Saa mbili za asubuhi gari moja la kifahari lenye rangi nyeupe likafunguliwa geti na kuingia katika nyumba ya John Mwaulaya.Toka ndani ya gari lile wakashuka vijana wawili waliovaa suti nzuri za gharama kubwa.Moja kwa moja wakaingia ndani na kukutana na Josh wakasalimiana na kwenda kukaa sebuleni.
“ Karibuni sana Jacob na Paul” akasema Josh akiwakaribisha wale vijana
“ Ahsante sana Josh.Vipi kuhusu hali ya mzee? Tunaweza kumuona na kumueleza kuhusiana na suala lile nililokwambia? Akauliza mmojawapo wa vijana wale
“ Jacob,mzee hali yake si nzuri sana kwa sasa na sina hakika kama litakuwa jambo la busara kumueleza mambo hayo kwa sasa.Kitu cha msingi tunachotakiwa kukifanya ni kuwapokea wageni hao na kuwaleta moja kwa moja kuja kumtazama John na kisha waendelee na mambo mengine “ akasema Josh
“ John ndiye kiongozi wetu mkuu na kwa sasa baada ya Osmund kufariki hatuna tena kiongozi mwingine wa kutuongoza.Pamoja na ugonjwa wake lakini John ndiye tunayemtegmea atuongoze.Ugeni huu ni mkubwa na lazima tumueleze” akasema Jacob.Josh akainama akafikiri kidogo na kusema
“ Hapana Jacob.Kwa hali ya John ilivyo kwa sasa hatutakiwi kumshirikisha katikamasuala yoyote ya kikazi.Mimi ndiye ninayeshinda na John na ninauelewa ukubwa wa ugonjwa wake.Hata hivyo kuna kitu gani ambacho hatukifahamu? Sisi tunaweza kujiongoza wenyewe kwani kila mmoja wetu anafahamu majukumu yake ya kazi…” akasema Josh halafu akawa ni kama mtu aliyekumbuka kitu Fulani na kusema
“ Nina wazo,kwa nini tusimfahamishe Peniela ?
“ peniela? Jacob akaonyesha kama kushangaa
“ Ndiyo .Peniela ni mtu ambaye anaifahamu vizuri sana team SC41.Ni mtu ambaye anaainiwa sana na ndiyo maana akapewa operesheni 26B.Nadhani Peniela ni mtu ambaye anafaa sana kutuongoza kwa wakati huu ambao John mwaulaya hajiwezi.Nina hakika hata John mwenyewe atakubaliana na maamuzi yetu ya kumtaka Peniela atuongoze kwa wakati huu” Akasema Josh na wale wenzake wakakubaliana naye.Bila kupoteza wakati Josh akachukua simu yake na kumpigia Peniela
“ Hallow Josh.habari yako? Akasema Peniela baada ya kupokea simu
“ habari yangu nzuri sana.Ninaendelea vizuri.” Akasema Josh
“ Josh nilitegemea baada ya tukio la jana hutanipigia simu tena.What is it this time? Kuna mtu mwingine umeelekezwa umteke? Akauliza peniela ambaye sauti yake ilionyesha wazi kwamba hakuwa ameifurahia simu ile toka kwa Josh
“ Peniela samahani kwa kukusumbua asubuhi hii na ninaomba tusahau yale yaliyotokea jana.Nimekupigia kukutaarifu kuhusu jambo moja muhimu sana”
“ jambo gani hilo Josh? akauliza Peniela
“ Kuna wageni wanakuja leo kutoka makao makuu marekani.Watu hawa wanakuja kwa ajili ya kazi maalum za kiofisi pamoja na kuja kumuangalia John mwaulaya kuhusiana na afya yake.Kwa sasa baada ya Osmund kufariki hatuna tena kiongozi mwingine ambaye anatuongoza kwani John mwaulaya bado hajiwezi.Kwa sasa hali yake katu si nzuri hata kidogo na kwa hiyo basi hatutaki kumuhusisha na masuala yoyote ya kuhusiana na Team Sc41 kwa maana hiyo tumeona tuwasiliane nawe ili uweze kulishughulikia suala hili la hawa wageni na vile vile uwe kiongozi wetu wa muda” akasema Josh.Ilimchukua Peniela muda kidogo kujibu
“ Wageni hao wako wangapi? Akauliza Peniela
“ wako wageni sita.”
“ Wanakuja saa ngapi? Akauliza Peniela
“ saa tano za asubuhi leo watakuwa wamefika” akasema Josh.Peniela akakaa kimya akafikiri na kusema
“ sawa nitafika hapo nyumbani sasa hivi.Nisubirini” akajibu peniela
“ Ahsante sana.By the way aren’t you going to ask? Akauliza Josh
“ To ask about what?
“ about how he’s doing?
Peniela akafikiri kidogo na kusema
“ How he’s doing?
“ bado hali yake si nzuri sana” akasema Josh
“ Ok .Ninakuja huko sasa hivi” akajibu peniela na kukata simu
“ Peniela amekubali na amesema anakuja muda si mrefu.Msiogope ndugu zangu hatujakosea kumtaarifu peniela.Hata John mwaulaya anamkubali na kumuamini sana peniela “ akasema Josh
“ mambo yameiva.Nadhani watu hawa anaowasema Josh watakuwa wanakuja kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wanaondoka na Package.Nakumbuka nilipoongea na Osmund kwa mara ya mwisho alinitaarifu kwamba imekuja taarifa toka makao makuu kwamba operesheni 26B lazima ikamilike ndani ya kipindi kifupi na alinitaka tukutane ili tuweze kupanga mikakati ya namna ya kuikamilisha operesheni hiyo.Sikupata bahati ya kuonana naye akafariki dunia.Ninadhani wageni hawa tu wanaokuja leo lengo lao ni kuja kuhakikisha kwamba operesheni hiyo inakamilika na wanaondoka na package. Natakiwa kuwasoma ni watu wa namna gani na wanafuata nini.”akawaza peniela na kisha akaamka na kuanza kujiandaa kuelekea nyumbani kwa John mwaulaya.

******

Sauti ya mtu aliyekuwa akiongea na simu karibu na mlango wa chumba chake ndiyo iliyomstua jaji Elibariki toka usingizini.Akainuka akajinyoosha na kukaa kitandani.Bado macho yake yalikuwa mazito kwani alichelewa sana kupata usingizi kutokana na mawazo mengi.Kitu cha kwanza kilichomjia akilini baada ya kuamka ni kuhusiana na hali ya mke wake Flaviana.
“ sijui mke wangu Flaviana atakuwa katika hali gani huko aliko.Natamani sana kujua maendeleo yake lakini sijui nitapata wapi taarifa .Maisha yangu sasa yamekuwa ya kujificha ndani na siwezi kuiweka sura yangu nje.Ninamchukia sana Dr Joshua yeye ndiye chanzo cha haya mambo yote.Mtu huyu asiye na huruma amemuua mke wake na sasa mwanae yuko mahututi hospitali akipigania maisha yake yote ni kwa sababu yake.Aliwatuma watu kuja kuniua na badala yake mwanae ndiye aliyepatwa na masahibu na mimi nimeangushiwa mzigo huu .Kwa kweli lazima ifanyike kila aina ya jitihada kuhakikisha kwamba Dr Joshua anafikishwa mbele ya mkono wa sheria na anaondolewa madarakani.Hana roho ya huruma hata kidogo.Lazima madhambi yake yote yaanikwe kwa umma ili wamjue rais wao ni mtu wa namna gani” akawaza jaji elibariki halafu akainuka akavaa fulana
“ Ngoja nikaongee na Mathew yeye anaweza akanisaidia kupata taarifa za maendeleo ya Flaviana.” Akawaza jaji Elibariki na kuufungua mlango na mara akakumbuka kitu
“ Nimekumbuka ,Peniela anaweza akajua hali ya mgonjwa inakwendaje kwa kumuuliza Dr Joshua.Ngoja nimwambie Mathew ampigie simu asubuhi hii niongee naye” akawaza jaji Elibariki na kuelekea katika chumba cha kazi ambamo alimkuta Anitha.Wakasalimiana na akamueleza kwamba Mathew bado alikuwa amelala.Moja kwa moja Elibariki akaenda kugonga chumbani kwa Mathew ambaye aliamka na kuufungua mlango
“ karibu sana Elibariki.Habari za toka jana? Akauliza Mathew
“ habari nzuri sana Mathew.Pole na uchovu.”
“ ahsante sana Elibariki karibu ndani “ akasema Mathew na jaji Elibariki akaingia ndani
“ Mathew samahani sana kwa kukuamsha” akaanzisha mazungumzo Elibariki
“ Usijali Eli.Hujanisumbua na tayari nilikwisha amka” akasema Mathew
“ Mathew kuna mambo mawili ambayo yamenileta hapa.Jambo la kwanza ninataka kufahamu hali ya mke wangu inavyoendelea huko hospitali .Ni vigumu kwa mimi kujua kinachoendelea lakini nimegundua kwamba tunaweza kumtumia Peniela ili kufahamu kinachoendelea hospitali.Yeye ana mahusiano na Dr Joshua kwa hiyo anaweza akampigia na kumuuliza hali ya mgonjwa inaendeleaje kwa hiyo ninakuomba umpigie simu Peniela ili tuone kama anaweza akatusaidia katika hilo.Jambo la pili ambalo nimekuwa nikilifikiria usiku kucha ni kuhusiana na Peniela.Nilimsikia vizuri sana jana maelezo yake na kuna mswali nimejiuliza.Ametokea wapi? John alimtoa wapi? Wazazi wake ni akina nani? Inawezekana Team Sc41 wakawa wakiwateka watoto na kisha kuwakuza na kisha baadae wakaja wakawatumia katika shughuli zao kama vile ilivyotokea kwa Peniela.Alichukuliwa na John na kupelekwa katika kituo cha kulelea watoto na kisha akaendelea kumuhudumia kwa kila kitu ikiwa ni pamoja na kumsomesha katika shule nzuri na za gharama kubwa lengo kubwa likiwa ni kuja kumtumia baadae kwa shughuli zao.Alipelekwa kusoma nchini Marekani na kule akapatiwa mafunzo ya Team SC41.Ninadhani yawezekana wakawepo wengi tu ndani ya Team SC41 walio na historia kama ya Peniela.Tunatakiwa tulichunguze suala hili tufahamu undani wake na tumsaidie Peniela kufahamu asili yake.Yawezekana wazazi wake wakawa bado hai na wakawa bado wanamtafuta mtoto wao aliyepotea.Unaonaje kuhusu suala hili Mathew? Akauliza jaji Elibariki
“ Elibariki wazo lako zuri na ninaweza kukubaliana na wewe kabisa kwamba yawezekana Team SC41 wakawa wakiwachukua watoto na kisha kuwakuza na baadae kuja kuwatumia katika shughuli zao.John Mwaulaya ana majibu kuhusiana na wapi alimtoa Peniela na wapi waliko wazazi wake.Kwa sasa itakuwa vigumu sana kwa John kuweka wazi jambo lolote lile kuhusiana na Peniela kwani kwa kufanya hivyo atakuwa akihatarisha operesheni yao ya kuipata package.Nimefikiria kitu kimoja hatuwezi kumsubiri John Mwaulaya lazima tuanze mapema kumsaidia Peniela kuutafuta ukweli kuhusiana na asili yake.Leo hii hatuna kazi kubwa mchana na nitakachokifanya nitakwenda katika ile nyumba ya kulelea watoto alikokulia Peniela na nitamuhoji mmiliki wa kituo hicho pengine tunaweza tukapata kitu cha kuweza kutusaidia kufahamu Peniela ametokea wapi.” Akasema Mathew
“ Hilo ni wazo zuri sana Mathew .Kuna ulazima mkubwa sana wa kufahamu Peniela ametokea wapi.Peniela ana nia ya dhati ya kuanza upya maisha yake na itapendeza endapo ataanza maisha yake upya huku akifahamu kuhusiana na asili yake” akasema Elibariki.Mathew akachukua simu na kumpigia Peniela
“ Hallow Mathew habari za toka jana? Akasema Peniela baada ya kupokea simu
“ Habari nzuri Peniela.Umeamkaje?
“ Nimeamka salama Mathew.Elibariki hajambo?
“ Mbona Elibariki peke yake? Sisi wengine hutukumbuki? Akauliza Mathew na kumfanya Peniela aangue kicheko
“ Mathew ninyi nyote ni watu wangu msijali.Wote wazima lakini?
“ Sisi sote wazima kabisa .Elibariki naye mzima sana.Huyu hapa ongea naye” akasema Mathew na kumpa Elibariki simu aongee na Peniela
“ Hallow Peniela habari yako?
“ Habari nzuri Elibariki.Umeamka salama?
“ Ndiyo Penny.Nimeamka salama .Vipi wewe umeamka salama?
“ Ndiyo nimeamka salama japokuwa kila nilipofumba macho ni sura yakot u ndiyo iliyokitawala kichwa changu” akasema Peniela halafu kikapita kimya kifupi Elibariki akasema
“ Peniela kuna jambo ninataka unisaidie.Ni kuhusu kupata taarifa za maendeleo ya Flaviana” akasema jaji Elibariki
“ Ouh tena nimekumbuka.Niliongea na Dr Joshua simuni nikamuuliza kuhusu Flaviana akasema kwamba hali yake bado si nzuri hata kidogo na ameshauriana na madaktari kwamba wamkimbize nje ya nchi kwa matibabu zaidi.Halafu kuna kitu kingine aliniambia .Alisema kwamba tayari jeshi la polisi wana fununu kuhusu mahala ulipo kwa hiyo muda wowote wanaweza wakakukamata.Nimeogopa sana kwa taarifa hizi.” Akasema Flaviana na kumstua sana jaji Elibariki ambaye alibaki kimya akiwaza
“ Kuna nini Elibariki mbona umestuka namna hiyo? Akauliza Mathew
“ Peniela anasema kaambiwa na Dr Joshua kwamba tayari jeshi la polisi wana fununu za mahala nilipojificha.I’m so scared Mathew” akasema jaji Elibarki.Mathew akamfanyia ishara ampatie ile simu
“ Hallo Peniela” akasema Mathew
“ Pafadhali naomba msiwe na wasi wasi wowote hata kama polisi wana fununu kwamba Elibariki yuko hapa kwangu lakini hakuna atakayeweza kumuona.Hapa ni sehemu salama kwake na ninarudia tena hakuna anayeweza kumuona wala kumpata.Ndani ya nyumba hii waweza kuishi hata maisha yako yote bila ya mtu mwingine kufahamu kwa hiyo naomba ondoa kabisa wasi wasi kuhusiana na Elibariki.Jambo la pili ninataka kufahamu kuhusu mahala ulikolelewa.Ulituambia kwamba ulilelewa katika kituo cha watoto yatima ni kituo gani hicho ulicholelewa?
“ Kwani kuna nini Mathew? Akauliza Peniela
“ Usiogope Peniela.Naomba unielekeze tafadhali” akasema Mathew na Peniela akamuelekeza
“ Ahsante sana Peniela .Kuhusu lile suala tuliloongea jana la kuhusiana na ile mikufu tutakayoweka vifaa vya kielektroniki itakuwa tayari hadi mchana wa leo.Kila kitu kikiwa tayari Anitha atakufahamisha na atakuletea vifaa hivyo ili kuepusha wewe kuonekana hapa mara kwa mara kwani yawezekana ukawa unafuatiliwa” akasema mathew
“ Sawa Mathew.Halafu kuna jambo nataka nikutaarifu”
“ Jambo gani Peniela?
“ Nimepigiwa simu asubuhi hii kuna watu wanakuja toka makao makuu ya Team Sc41 marekani na ninahisi wanakuja kuhakikisha operesheni inakamilika na kisha waondoke na package.Hivi sasa najiandaa ili nikawapokee uwanja wa ndege” akasema Peniela.Mathew akafikiri kidogo na kusema
“ Peniela wachunguze vizuri ni watu wa namna gani na wanadhamiria kufanya nini kisha unitaarifu mara moja” akasema Mathew na kukata simu akamgeukia Elibariki
“ Mambo yanaiva,kuna watu wanakuja toka marekani kuja kusimamia zoezi la uchukuliwaji wa package na kisha kuondoka nayo.Lakini ndani ya hiyo package kuna nini mpaka iwe ni package yenye umuhimu mkubwa kiasi hiki? Akauliza Mathew
“ Lazima kitakuwa ni kitu kikubwa chenye thamani kubwa sana “ akasema Elibariki

TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
 
poleni sana wakuu nilikuwa nashida kidogo na halotel jana wakanikatili kwenye network basi ikawa kimyaa.tunaliendeleza week end hii hakuna kutoka home wala kuchepuka. ni mwendo wa peniele tuu
Pole sana
 
Back
Top Bottom