Peniela (Story ya kijasusi)

Peniela (Story ya kijasusi)

Story nzuri sanaaaaa....sasa kwa shingo upande ngoja niende kwa Jojo Danny
 
kamamwenyewe aliamua kuisa

mbaza kwenye fb na kundi lake la watsapp sio mbaya na sie hapa jf tukiburudika na soon anatoa kitabuu baada ya ushauri sana wa wadau juu ya kitabu
Mkuu hicho kitabu kikitoka kumbuka kunitonya japo inbox plse
 
hahaha mkuu kwa jins watu walivyokuwa busy JF wakipigana vikuombo na story ya peniele hatari tupu.

ipo story nyingine ya kijasusi ya mwandishi nguri wa story za taharuki HUSSEN TUWA inaitwa WIMBO WA GAIDI itabidi ikiisha hii tufanye mpango tuibwage hapa nayo
Kuna hadithi yake inaitwa mkimbizi ile story sikuwahi kuimaliza ni nzuri mno
 
LEGE nakushukuru sana sasa ni mchana ukimaliza lunch mwaga tena ili itupeleke mpaka jioni maana jumatatu job.Ahsante kwa kuwa unapenda kushauriwa na unajali washabiki wako.keep it up
 
LEGE sasa ikiisha hii tu bandika hiyo ya GAIDI na by the time gaidi inaisha unakuwa na kitu kingine.Kwa wale ambao tunapenda movie za kijasusi na kiterrorist hapandio home.LEGE umetufikisha .salute
 
mkimbizi mm ninacho kitabu chake nimeisoma mwanzo mwisho .kuna nyingine mtafiti,mtuhumiwa,mdunguaji,utata, na now ya kijasusi ni wimbo wa gaidi ushawahi zisoma hizo
Mkuu una hazina ya kutosha jitendee haki basi ili tufaidi hasa sisi mateja wa story hizo
 
Alafu mkuu shusha basi cha mchana huu mpaka jioni ili tulale mapema usiku😉😉
 
PENIELA SEASON 3

SEHEMUYA 16

ILIPOISHA SEHEMUILIYOPITA
“ Nitakuwa nikikufahamisha kila kitu kuhusiana na kinachoendelea lakini kuna jambo nitaomba ulifanyie uchunguzi.Ninataka unisaidie kufanya utafiti Rosema Mkozumi yuko wapi ? Idara yenu ya usalama wa taifa mnazo nyenzo za kuweza kupata taarifa mapema sana kwa hiyo nisaidie kufahamu mahala aliko Rosemary .Can you do that for me? Akauliza Vincent
“ Niachie suala hilo nitalifanyia kazi .Nitafuatilia ofisini ili nione kama kuna taarifa zozote zimepatikana kuhusu mahala alipo Rose.” akasema Jesica
“ Ahsante sana Jesica.Lifanyie kazi sualahlo kwani nina wasiwasi sana na kutoweka huku kwa kutatanisha kwa Rose .Yule ni mtu anayetufahamu sana sisi na anayafahamumamboyetu mengi kamasisi tunavyoyafahamu yak wake “: akasema Vincent akaagana na Jesica.
“ Sasa kidogo ninaweza kuvuta pumzi baada ya kuwa na uhakika Amos ametoweka.Huyu alikuwa ni mtu muhimu mno kwa Deus na ndiye alikuwa anamtegemea sana katika mpango wake.Kwa sasa mipango yake haitaweza kufanikiwa tena na ni nafasi yetu kumuandaa mtu wetu ambaye atatusaidia sana endapoatashika madaraka “ akawaza Vincent.


ENDELEA……………………

Mathew akaingIa chumbani kwake akalifungua kabati ambao huhifadhi baadhiya vifaa vyake mbalimbaLi.Akachukua sanduku moja la kijani pamoja na vifaa kadhaa akatoka mle chumbani na kuelekea katika chumba alimolazwa Rosemary Mkozumi.Akakinyonga kitasa na kuingia ndani.Rosemary alipomuona akainuka na kukaa kitandani.Alikuwa na hasira kali sana “ Who are you? Kwan in umeniweka humu? Nani kakutuma ufanye hivi? Akauliza kwa ukali Rosemary.Mathew hakumjibu kitu akaviweka vifaa vyake mezani akavuta kiti na kuketi akamtazama Rosemary kwa sekudne kadhaa kisha akasema
“ Hello Rosemary! “ Sina haja ya salamu yako.Tafadhali kijana naomba usijitafutie matatizo zaidi.Mpaka sasa tayari umekwishajiingiza katika matatizo makubwa.Umemuua Henry na kama vile haitoshi umeniteka na kunifungia humu chumbani.Unadiriki kumteka nyara mke wa rais? Umelipwa shilingi ngapikijana wangu hata ukakubali kujihatarisha namna hii? Tafadhali naomba uniachie huru haraka sana na nitaangalia namna ya kukusamehe na kukusaidia kukutoa katika janga hili ulilojitumbukiza bila kujua....” akasema Rosemar y Mkozumi kwa sauti ya juu .Mathew akamtazama kwa makini na kusema
“ Rosemary Mkozumi just relax…”
“ Kijana naomba tafadhali usiendelee na upuuzi wako unaotaka kuufanya.Nani lakini kakutuma unifanyie hivi? Unashirikiana na akina nani? Hao waliokutuma wamekuingiza katika tanuru la moto na wewe kwa tamaa zako ukakubali kuingia na kuungua .Ninakuonya kwa ara nyingine kijana tafadhali naomba unifungue haraka sana miguu yangu inaumia” akasema Rosemary.
“ Rosemary tafadhali naomba uniskilize kwa makinisanana sihitaji mzaha hata kidogo” Akasema Mathew.
“ Ninaitwa Mathew,ni mchunguzi wa kujitegemea.Nimewahi kufanya kazi katika idara ya usalama wa taifa Tanzania idara ya kupambana na kuzuia ugaidi na baadae nikaacha kazi hiyo na kuanza kufaya kazi zangu binafsi za kiuchunguzi.Mwezi wa pili mwaka jana kijana mmoja aitwaye Edson aliyekuwa akifanya kazi katika idara ya mawasiliano ikulu aliuawa na watu wasiojulikana lakinikesi hiyo ya mauaji ikamuangukia mpenzi wake aliyeitwa Peniela.Mahakama ilimuachia huru Peniela baada ya kuridhika kwamba hakuw ana hatia na hakumuua Edson kama ilivyodaiwa.Nilikabidhiwa jukumu la kumtafuta muuaji halisi wa Edson .Katika uchunguzi wangu niligundua kwamba Edson alishiriki katika uibwaji wa nyaraka nyeti sana toka ikulu.Niligundua kwamba ili kulifanikisah jambo lile Edson hakuwa peke yake alikuwa akishirikiana na watu wawili Mzee Kitwana na Mzee Matiku ambao kwa sasa wote ni marehemu.Nyaraka hizo zilizoibwa zilikuw ana kanuni za kutengeneza kirusi hatari sana ambacho kinaweza kusababisha maangamizi makubwa sana kwa binadamu.Nimelichimba suala hilikwa undani zaidi na kugundua kwamba mtu aliyetaka kuzinunua karatasi hizo anaitwa Habib Soud raia wa Saudi Arabia .Habib anatajwa kuvifadhili vikundi kadhaa vya kigaidi nahivyo kunifanya niamini kwamba yawezekanaalizihitaji karatasizile kwa ajili ya kutengeneza kirusi kile ili wakitumie kwa mambo ya kigaidi.Sikuishia hapo nilimchunguza Habib na kugundua kwamba amekuwa na mawasiliano nawe ya mara kwa mara .Nimegundua pia kwamba wewe ndiye uliyeratibu na kufanikisha mpango mzima wa kuibwa kwa karatasi hizo ikulu kwa kumtumia Edson na baadaya kuzipata karatasi hizo uliwazunguka washirika wako na kuwamaliza ili ubaki na karatasihizo na pesa yote itokanayo na mauzo ya karatasi hizo uipate peke yako.Ili kuendelea kuuficha uhusika wako katika suala hili kumbu umbu za mawasilianokatiyako na washirika wako wakuu katika suala hili yaani mzee Kitwana na matiku zilifutwa kabisa .” Akasema Mathew na uso wa Rosemary ukabadilika .Mathew akaendelea.
“ Kwa bahati mbaya pamoja na kuwaua washirika wako lakinihukufanikiwa kuzipata nyarakazile kwani ziifichwa na mmoja wa washirika wako.baadaya kuona jambo lile limeshindikana hukukata tamaa ukaingia tena katika biashara nyingine namtu mmoja anaitwa samir Asaad.Umekuwa ukiwasiliana na Samir na katika mojawapo ya barua pepeuliyomtumia Samir umemuhakikishia kwamba muda si mrefu toka sasa utafanikiwa kuupata mzigo anaoutaka kwani una mawasiliano ya karibu na mtu wa karibu na rais .Baadae tukagundua kwamba mtu uliyemtaja kuwa karibu na rais ambaye umekuwa na mawasiliano naye ni Captain Amos ambaye ni daktariwa familia ya rais.Tulimpata Captain Amos na wakati tukimfanyia mahojiano ,alitokea mtu na kumpiga risasi akamuua na hili lilifanyika makusudi ili Captain Amos asiweze kutoa siri.” Mathew akanyamaza akamtazama Rose ambaye matone ya jasho yalionekana usoni pake.
“ Amos is dead?! Akauliza Rosemary kwa msahngao mkubwa
“ yes ..he’s dead” akasema Mathew.Rose akainamisha kichwa kwa masikitiko
“ Rosemary kuna mambo mengi ambayo ninyafahamu kuhusu wewe namtandaowako nasitaki kpoteza muda kuyaongelea hapa.Ninachokihitaji toka kwako nikunipatiamajibu sahihiya kila nitakachokuuliza kaini kama hutanipa ushrikiano wa kutosha na kuniletea jeuri sahau kabisa kutoka hapa ukiwa hai.” Akasema Mathew na kunyamaza kidogo halafu akasema
“Kitu cha kwanza ninachotaka toka kwako nataka kufahamu ,ukiacha wale washirika wako walikwisha fariki,nani mwingine ambaye umeshirikiana naye katika kuziiba karatasi zile ikulu? akaulizia Mathew .Rosemary Mkozumi akasonya na kubetua midomo kwa dharau akasema
“ You go to hell,wewe na huyo aliyekutuma!! .Mathew akamuangalia na kusema
“ Rose ninakukumbusha kwa mara nyingine kwamba hapa ulipo ni nusu ya jehanamu kwa hiyo nataka unijibu kiufasaha kila nitakachokuuliza na kitakachokuokoa ukaweza kutoka humu ndani ni ukweli..Tell me the truth and you’ll get out of here alive..Ninarudia tena nilichokuuliza mwanzo,nina kila ushahidi kuthibitisha kwamba ulihusika katika kuratibu mpango wa kuziiba karatasi zile ikulu.Ninataka kufahamu ni akina nani wengine ulioshirikiana nao kulifanikisha jambo hili ukiacha wale ambao wamekwisha fariki? Akauliza Mathew.
“ You go to hell you witch..nakuhurumia sana wewe kijana kwa nini unakubali kutumiwa kirahisi namna hiyo ? tafadhali achana na huu upuuzi unaoufanya.Mwambie aliyekutuma kwamba hawezi kupambana na Rosemary..” akasema Rosemary kwa dharau
“ Hakuna mtu aliyenituma bali ninafanya kazi hii kwa niabaya serikaliya jamhuri ya muungano wa Tanzania na si mtu binafsi kama unavyodhani..” akasema Mathew.Rose akacheka kwa dharau na kusema “ Serikali !! Unafahamu serikali ni nani? Poor boy hujui hata unachokiongea.Tafadhali naomba unifungue niondoke zangu na nitakusamehe,lakini ukiendelea kunishikilia hapa kwako kwa dakika kumi zijazo ninakuapia kijana sintakusamehe hata kidogo.”akasema Rosemary
“ Vitisho vyako havitaweza kukusaidia hata kidogo Rose.Nakuonya kwa mara ya mwisho kwamba utatoka humu ndani ukiwa salama endapo utanipa majibu ya kile ninachokitaka.Ukileta jeuri ninakuapia Rose hautatoka humu ndani salama.” Akasema Mathew na Rose akaukunja uso wake
“ Kijana kwa nini unakuwa mgumu kunielewa? Kwa nini unaendelea kuhatarisha maisha yako na kujiweka katika matatizo makubwa? Ninakwambiwa kwamba ndani ya muda mfupi ujao utajutia hiki unachokifanya .Sintokusamehe kabisa na wala usidhani kwamba h iyo serikali unayodai unafanya kazi kwa niabayake watakusaida kitu .Iam the government! ….Akasema kwa ukali Rose. Mathew akainuka na kumsogelea karibu. “ Rose ninafahamu kwamba unalengo la kugombea urais na kwa sasa mimi ndiye nitakayeamua kama jambo hilo litafanikiwa ama vipi.Endapo sintaridhika na majibu yako ndoto hiyo kubwa haitatimia kamwe.Nita…” Ghafla Mathew akastuka baada ya kutemewa mate usoni
“ I’ve told you go to hell you black devil !! akasema kwa ukali Rosemary.Mathew akamtazama Rosemary kwa hasira na kusema
“ umefanya kosa kubwa sana.Ni bora ungekutana na mtoa roho kuliko mimi.Sasa kwa kuwa umekataa kunijibu kwa hiari yako na umeonyesha kiburi ,nitakulazimisha kunijbu kwa nguvu” akasema Mathew na kuchukua ndoo ya maji akammwagia Rosemary na kumloanisha chapa chapa
“ Are you crazy?!!.I swear I’ll never forgive you for this ”akafoka Rose.Mathew akalifungua lile sanduku halafu akatoa vifaa kadhaa akaviweka mezani.Akachukukua vyuma Fulani viwili vyenye nyaya akavichomeka katika lile sanduku halafu akaliunganisha katika umeme kisha akavigusanisha vyuma vile vikatoa cheche.Rosemary Mkozumi akatumbua macho “ Unataka kufanya nini? Akauliza.Mathew hakumjibu kitu akarekebisha kiasi cha umeme anaouhitaji na kisha akasogea kitandani na kugusisha vyuma vile vyenye umeme katika pingu aliyofungiwa Rosemary mguuni.. "Aaaaaggggghhhhh!!!!!!!!!!!!!!!...”Rosemary akapiga kelele kubwa..Mathew akatulia kidogo halafu akarudia tena zoezi lile..Rose akaendelea kupiga kelele kubwa
“ Give me the names!!...akasema kwa ukali Mathew.Halafu akatulia
“ Give me the names!! nani u nashirikiana nao? Akauliza .
“ There is..there..iiii..there are no names..” akasema Rosemary huku akitetemeka mwili.mathew akagusisha tena vyuma vile katika pingu na kuendelea kumtesa Rosemary..
“ Stop that.!!.please stoooop !!!!!..” akalia Rose.Mathew akasimama
“ Ni akina nani ulishiriana nao katika mpango ule? Akauliza Mathew. “No one..sijashirikiana na mtu yeyote na wala siufahamu huo mpango unaousema..” akasema Rose huku akitweta.
“ This is not working…!!! Akasema Mathew kwa sauti ndogo.Akavua shati na kubakiwa na fulana ya ndani akamshika Rosemary kwa nguvu akamfunga mikono yake kwa pingu.
“ Nilikuonya toka mwanzo kwamba usiombe ukutane na mimi lakini ukapuuza.Utanieleza kila kitu leo ”akasema Mathew halafu akachukua kisu na kukata kijisehemu kidogo katika kidole cha mguu wa kulia wa Rose halafu akachukua bomba la sindano akavuta dawa fulani nyeupe toka katika kichupa kidogo na kudondoshea matone kadhaa mahala palipokuwa panatoa damu.Rose akagalagala pale kitandani huku akipiga kelele kubwa kwa maumivu aliyoyasiki..Mathew akachukua gundi na kumfunga mdomo ili asiweze kutoa ukelele halafu akadondoshea tena matone kadhaa mahala alipopakata..Rosemary akaendelea kugugumia kwa maumivu makubwa.Mathew akamfungua ile gundi aliyomfunga nayo mdomo akamuuliza
“ Uko tayari kuniambia ninachokihitaji?Akiwa ndani ya maumivu makali sana akasema
“ You go to hell you devil !! Mathew akamfunga tena mdomo na kumkata kidogo shingonihalafu akadondoshea matone kadhaa mahala alipokata..Rose akaruka ruka kana kwamba anakata roho.Mathew akamuangalia halafu akamfungua ile gundi mdomoni. “ Utanijibu nilichokuuliza? Akauliza Mathew lakini Rose hakumjibu kitu akabaki analia kwa maumivu makali.
“ C’mon Rose ..nijibu haraka nilichokuuliza !!!! akasema Mathew kwa ukali Rose akaendelea kulia kwa maumivu makali sana aliyoyasikia.
“ Dah ! sijawahi kukutana na mwanamke mwenye roho ngumu kama huyu mama.Lakini leo hii atanieleza kila kitu ninachotaka.”akawaza Mathew.Akaelekea mezani kwake na kuchukua kifaa kidogo cha kukatia akakiwasha na kukijaribu
“R ose umetaka mwenyewe tufike hapa tulipofika na nilikuonya toka mapema kwamba usiombe ukutane na mimi.I’ m a monster na ninachokwenda kukufanyia kitabaki katika kumbu kmbu za uzao wako daima.Nitakukata kidole kimoja kimoja nikianzia na vidole vya miguu na halafu nitakuja mikononi na halafu nitanyunyiza dawa hii inayouma na utajihisi kamaumetupwa katika shimo la moto kwani mwili wote utawaka moto kwa maumivu utakayoyasikia..Utasikia maumivu makali mno ambayo hujawahi kuyasikia toka umezaliwa.Ukitaka nisifanye hivyo nijibu haraka kile nilichokuuliza” akasema Mathew lakini Rosemary hakujibu kitu bado aliendelea kulia kwa maumivu makali.Mathew akachukua kile kifaa akakiwasha na kisha akakishika kidole cha mwisho cha mguu wa kulia wa Rosemary na kukikata. Rosemary akapiga ukulele mkubwa sana
“ C’mon Rose,usinilazimishe nikakufanyia hivi.Niambie kile ninachokitaka” akasema Mathew kwa ukali.Bado Rose aliendelea kugalagala huku akilia kwa maumivu makali mno.
“ Bado anaendelea kuwa na kiburi ..leo lazima nimbadilishe sura yake..Atanieleza tu .” akawaza Mathew na kukishika tena kidole kinachofuata akakata.Rose akapiga ukele mkubwa hadi sauti ikaanza kumkwama..
“ Please stop !!.stop hurting me !!!!!!!!!!..akasema Rosemary..
“ Are you ready to tell me what I want? akauliza Mathew
“ I will tell you..i will tell you everything ..stop hurting me…” akasema Rose huku bado akiendelea kulia kwa maumivu makali.Mathew akachukua bandeji na kufunga mguu ule wenye majeraha halafu akamchoma sindano ya kupunguza maumivu.
“ Now tell me everything” akasema Mathew
“ I will tell you everything you want..please don’t hurt me




ROSE ATAMUALEZA NINI MATHEW? TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………
 
PENIELA SEASON 3

SEHEMU YA 17

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Rosemary akapiga ukulele mkubwa sana
“ C’mon Rose,usinilazimishe nikakufanyia hivi.Niambie kile ninachokitaka” akasema Mathew kwa ukali.Bado Rose aliendelea kugalagala huku akilia kwa maumivu makali mno.
“ Bado anaendelea kuwa na kiburi ..leo lazima nimbadilishe sura yake..Atanieleza tu .” akawaza Mathew na kukishika tena kidole kinachofuata akakata.Rose akapiga ukele mkubwa hadi sauti ikaanza kumkwama.. “ Please stop !!.stop hurting me !!!!!!!!!!..akasema Rosemary..
“ Are you ready to tell me what I want? akauliza Mathew
“ I will tell you..i will tell you everything ..stop hurting me…” akasema Rose huku bado akiendelea kulia kwa maumivu makali.Mathew akachukua bandeji na kufunga mguu ule wenye majeraha halafu akamchoma sindano ya kupunguza maumivu.
“ Now tell me everything” akasema Mathew
“ I will tell you everything you want..please don’t hurt me

ENDELEA………………

“ Ni kweli mimi ndiye niliyeratibu mpango ule wa kuziiba nyaraka zile toka ikulu.Nilifahamiana na Habib Soud alipokuja Tanzania kutembelea mbuga za wanyama.Wakati huo mume wangu Deus alikuwa katika kujiandaa kuhitimisha awamu ya mwisho ya uongozi wake na kumuachia Dr Joshua.Akiwa katika mapumziko yake Habib akatembelea ofisi za taasisi yangu na akadai kwamba amefurahishwa na kazi ninayoifanya kupitia taasisi yangu ya kuwainua wanawake kiuchumi na hivyo anataka kunipa sapoti.Ni kweli alianza kutoa misaada mingi sana ya mamilioni ya fedha na akawa ndiye mfadhili mkuu wa taasisi yangu.Tulijenga urafiki mkubwa .Siku moja aliniomba tukutane Dubai ili anitambulishe kwa matajiri wakubwa ambao wako tayari kuendelea kuifadhili taasisi yangu.Ni kweli alinitambulisha kwa mabilionea wakubwa sana ambao sikuwahi kuota kama siku moja ningeweza kukaa nao na kula nao chakula.Matajiri wale waliniahidi kunisaidia sana ili taasisi yangu iwe ya kimataifa na kusaidia wanawake sehemu mbali mbali za dunia.Baada ya kuachana na matajiri wale wakubwa,Habib akanifuata na kuniomba tuongee faragha akaniambia kwamba matajiri wale wako tayari kunisaidia sana na watamwaga pesa nyingi sana kwa taasisi yangu lakini kuna kitu kidogo wanakihitaji toka kwangu. Aliniambia kwamba kuna nyaraka Fulani za siri zinahifadhiwa ikulu na ambazo natakiwa kufanya juhudi nizipate.Hakunieleza kwa nini wanazihitaji karatasi zile ila alisema ni za muhimu sana kwao.Alinihakikishia kwamba endapo ningefanikiwa kuzipata karatasi zile basi ningeingia katika ulimwengu wa mabilionea.Ili kunithibitishia kwamba hawakuwa wakitania muda ule ule nikaingiziwa katika akaunti ya taasisi yangu kiasi cha shilingi milioni mia mbili.” akasema Rosemary na kuuma meno kwa maumivu makali aliyoyasikia. “ Please do something on my leg..I feel pain like hell !..umeniumiza sana wewe kijana I swear utanijua mimi ni nani ndani ya muda mfupi nikitoka hapa!! Akasema kwa ukali Rose huku akigugumia kwa maumivu makali.Mathew akachukua tena kichupa kingine cha dawa akaivuta katika bomba la sindano na kumchoma Rose katika mguu wake ule uliokuwa unavuja damu na mguu wote ukawa na ganzi hakusikia tena maumivu.
“ Sasa endelea na maelezo yako” akasema Mathew
“ Damu yote hii iliyomwagika haitakwenda bure lazima utailipa tu..How a handsome guy like you could be such a monster!!..
“ Rose naomba tafadhali usiendelee kunipotezea wakati wangu.Endelea kunipa maelezo au unataka nianze tena kazi yangu? Akasema Mathew kwa ukali.
“ Ok ! Ok!..dont hurt me any more you monster.nitakueleza unachotaka.” Akasema Rose akamtazama Mathew kisha akaendelea
“ Nilirejea Dar es salaam kwa lengo moja tu la kuzitafuta hizo karatasi mahala zilikofichwa.Niliishi ikulu kwa miaka kumi lakini kuna sehemu za siri ambazo sizifahamu.Suala lile nisingeweza kumuuliza mume wangu Deus ambaye kwa wakati huo tayari alikwisha staafu kwani ninamfahamu Yule mzee ni mtu muadilifu sana na asingeweza kunipa siri kama hiyo kwa hiyo nikaanza kutengeneza mtandao wa watu wa karibu na rais ambao niliamini wangeweza kunipatia taarifa za mahala zilipo hizo karatasi na nikafanikiwa kumpata Captain Amos.Huyu ndiye aliyeweza kunisaidia kufahamu mahala zilipo hizo nyaraka na ndiye aliyefanikisha mpango mzima wa kuzipata .Kwa bahati mbaya baada ya kufanikiwa kuzipata karatasi hizo watu niliowashirikisha katika mpango huu wakaingiwa na tamaa na kuzungukana wao kwa wao wakauana bila sababu . Taarifa za upotevu wa nyaraka zile zilifika hadi ikulu na Edson akauawa.Aliyemuua Edson ni Captain Amos ili kuuficha uhusika wake katika wizi ule kwani endapo rais angefahamu kwamba naye alishiriki katika wizi ule basi asingeweza kumuamini tena “
“ Wait !..” akasema Mathew
“ Kwa hiyo unaniambia kwamba Captain Amos ndiye aliyemuua Edson na si Dr Joshua? Akauliza Mathew
“ Ndiyo ! Edson aliuliwa na Amos ..” akasema Rose
“ Ok endelea…..
“ Kutokana na sintofahamu ile baina ya washirika wangu,karatasi zile zilipotea katika mazingira ya kutatanisha sana na mpaka leo hii sifahamu ziko wapi na biashara yetu ilishindwa kufanikiwa” Akasema Rose.Mathew akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Uliwahi kufahamu nini kiliandikwa katika nyaraka zile?
“ Sikuwahi kuzitia mikononi nyaraka zile na wala sifahamu nini kiliandikwamo.Nimesikia kwa mara ya kwanza leo hii toka kwako kwamba nyaraka zile zilikuwa na kanuni za kutengeneza kirusi” akasema Rose
“ Ndiyo.Karatasi zile zilikuwa na kanuni ambazo zinaelekeza namna ya kutengeneza kirusi hatari ambacho kinaweza kutumika katika maangamizi makubwa.” Akasema Mathew
“ Unafahamu kama Habib anahusishwa na kufadhili vikundi vya kigaidi? Akauliza Mathew
“ Hapana sikuwa na habari hizo.Mimi nilimfahamu Habib kama mfanya biashara wa mafuta na sikujua kama alikuwa anajihusisha na kufadhili vikundi vya kigaidi.”
“ Ukiacha karatasi hizo ambazo ulitaka kumuuzia Habib kuna mambo gani mengine ambayo amewahi kukuomba umsaidie? Au mliyoshiriiana kuyafanya?
“ Hakuna” akajibu Rose
“ Rose naomba ufahamu kwamba Habib na kundi lake walikuwa wanakutumia kwa faida yao na mitandao yao ya kigaidi na endapo wangefanikiwa kuzipata karatasi zile walizokuomba uwatafutie basi wangeweza kutengeneza kirusi hatari na wangefanya mashambulizi makubwa sana ambayo yangesababisha maangamizi makubwa duniani.Kwa kitendo hicho ulichokifanya uliiweka nchi yetu katika hatari kubwa na kukuweka wazi , hata wewe kwa hivi sasa unachunguzwa na mashirika makubwa ya ujasusi duniani kama C.I.A kutokana na ukaribu wako na ukaribu wako na Habib Soud.” Baada ya kusikia vile sura ya Rose ikajikunja.Alistushwa sana na taarifa ile ya kwamba anachunguzwa na C.I.A
“ To be honest I didn’t know if Habib is a terrorist “ akajitetea Rose
“ Lazima ulifahamu ,laini kwa tamaa ya fedha ukaamua kushirikiana naye.Kwa kushirikiana na mshukiwa wa kufadhili ugaidi ni wazi kwamba hata wewe mwenyewe unashiriki katika mambo hayo.Na kama suala hili likifahamika kwa umma basi taswira yako nzuri uliyoijenga katika jamii ya ndani na nje ya nchi itaharibika na mpango wako wa kugombea urais hautafanikiwa.All that you’ve worked hard for all these years will lost because you cant escape a very long sentence.Hebu jiulize Rose ungejisikiaje kama ungesikia maelfu ya watu wameuawa kutokana na kirusi kilichotengenezwa kwa karatasi zile ambazo wewe uliziuza kwa magaidi? Akauliza Mathew
“ I swer I didn’t know anything.Habib hakuwa tayari kunieleza kwa nini alizihitaji karatasi hizo na mimi sikuhoji kwani shida yangu kwa wakati huo ilikuwa ni fedha tu kwa hiyo sikujali hata kidogo kujua nini kimeandikwamo.Tafadhali naomba uniamini ninachokwambia” akasema Rose
“ Siwezi kukuamini hata kidogo Rose.You are a professional liar.Maisha yako yametawaliwa na uongo mkubwa. Unawadanganya watu kwa kuwapa misaada ya fedha ambazo zinatoka kwa magaidi.Unadhani wakilifahamu jambo hili watakufanya nini? Ndiyo maana nilikueleza toka mwanzo kwamba hatima ya maisha yako iko mikononi mwangu kwa sasa kwa hiyo ninahitaji maelezo yenye kuniridhisha ama sivyo I will destroy you” akasema Mathew
“ Please help me.Nimekuamini wewe ni mchunguzi makini sana na ndiyo maana nimekueleza kila kitu bila kukuficha kwa hiyo tafadhali naomba sana sala hili lisitoke nje ya kuta za nyumba hii.Lets put this between us.I ‘m giving you a chance to make a deal ”
“ A deal !!..Mathew akacheka kidogo
“ Rose lazima ukutane na mkono wa sheria lakini endapo ukinieleza ukweli mambo ambayo ninayataka basi ninaweza kulifiria ombi lako” “ Kitu gani unataka kufahamu?
“ Ni mambo mengi ambayo ninahitaji kuyafahamu toka kwako lakini nataka kwanza kumfahamu kiundani huyu Habib Soud na kama kuna mambo mengine ambayo umewahi kushirikiana naye.Ukinisaidia kumpata Habib nami nitakusaidia katika suala hili na hakuna atakayefahamu chochote.” Akasema Mathew.Rose akafumba macho na baada ya sekunde kadhaa akafumbua macho na kutazama mguu wake na damu iliyokuwa imetapakaa pale kitandani na kusema
“Ok kuna jambo lingine .Baada ya ule mpango wa mwanzo wa kuzipata karatsi zile kushindikana Habib alinikabidhi kwa binamu yake anaitwa Samir Asaad.Huyu naye ni kijana tajiri sana na ni mmoja wa mabilionea niliokutana nao Dubai.Huyu alinieleza kwamba kuna mzigo Fulani ambao rais wa Tanzania yaani Dr Joshua anataka kuwauzia watu Fulani ambao hakunitajia ni akina nani.Alinieleza kwamba kama nikifanikiwa kuupata mzigo huo ambao rais anataka kuuza basi nitakuwa bilionea.Nilikubali kwa kuwa ninao mtandao wa kutosha hata ndani ya ikulu.Kuwa kumtumia Amos ambaye ni mtu wa karibu na rais niliweza kufahamu mambo mengi kuhusiana na biashara hiyo anayotaka kuifanya rais na tayari kuna mikakati mikubwa ya kuweza kuipata. “ akasema Rose
“ Amos au Samir waliwahi kukueleza kwamba ni kitu gai hicho ambacho Dr Joshua anataka kuuza?
“ Hakuna anayefahamu kuna nini ndani yake lakini inaonekana ni kitu chenye thamani kubwa sana kiasi kwamba Samir yuko tayari kutoa fedha nyingi mno kukipata kifurushi hicho.Sikuhitaji kujua ndani kuna nini mimi shida yangu ni fedha tu .Nahitaji sana Fedha kwa ajili ya kuanza maandalizi ya kampeni ya kunipeleka ikulu.“ akasema Rose na mara mlango ukagongwa kwa nguvu .Mathew akainuka na kwenda kuufungua akakutana na Anitha jaji Elibarki pamoja na Peniela
“ What ! Kuna nini mbona wote mko hapa akauliza Mathew
“ Tulisikia kilio kikubwa tukaja hapa mlangoni kujua kinachoendelea.Whats going on ? akaulizia jaji Elibariki
“ Hamkutakiwa kuwa hapa Elibariki.Ninapotafuta taarifa Fulani wakati mwingine ninalazimika kwenda mbali zaidi na kutumia kila aina ya mateso kuweza kuipata taarifa hiyo.”
“ Mathew tuachane na hayo.Nilikuwa ofisini nikiendelea kucunguza simu na kompyuta ya Amos pamoja na ile ya Rosemary.Kuna mambo nimeyagundua.Naomba twende ofisini” Akasema Anitha kisha wakaongozana kuelekea ofisini.
“ Kuna nini Anitha? Akauliza Mathew
“ Jambo la kwanza nimegundua kwamba kuna mawimbi yasiyoya kawaida yanatoka hapa ndani.”
“ Sijakuelewa Anitha unazungumzia mawimbi gani? akauliza Mathew Anitha akaanza kuwaelekeza kwa kutumia luninga kubwa iliyokuwa ukutani
“ Kompyuta yangu ina mfumo wa kuweza kutambua aina mbali mbali za mawimbi yaliyoko katika eneo nilipo.Mfumo unanionyesha kwamba kuna mawimbi Fulani yasiyo ya kawaida yanatoka ndani ya nyumba hii ambao si mawimbi ya simu.Ulimchunguza vizuri Rose kama hana kifaa chochote cha kielektroniki ambacho kinaweza kuelekeza kufahamu mahala alipo? Akauliza Anitha
“ Nilimsachi vizuri na sikukumkuta na kitu chochote zaidi ya simu yake” akasema Mathew
“ wait ! “ akasema Peniela
“ ninavyohamu mimi marais na wake zao huwekewa vifaa fulani vidogo ndani ya miili yao kwa ajili ya kuwafuatilia kila mahala waliko.Huyu aliwahi kuwa make wa rais yawezekana bado kifaa hicho kipo mwilini mwake” akasema Peniela .Mathew akamtazama na kusema
“ Peniela can be right” akasema na kulifungua kabati akatoa kifaa Fulani na kwa kasi akeelekea katika chumba alimo Rosemary Mkozumi na kuanza kukipitisha kifaa kile katika sehemu mbalimbali za mwili wa Rose na mara alipofika katika mkono wa kushoto kidude kile kikatoa mlio wa kengele na kuwasha taa ya kijani
“ Got it! Akasema Mathew
“ Ndiyo maana Rose alikuwa anajiamini sana kamba muda wowote watu wake wanaweza wakafika kumuokoa kumbe alifahamu kwamba ana kifaa kinachowaelekeza watu wake mahala alipo.Ahsante sana Anitha kwa kuligundua hili.Tulikuwa katik ahatari kubwa” Akawaza Mathew akachukua kisu kidogo na kuushika mkono wa Rose ambaye alikuwa ametumbua macho asiamini kilichokuwa kinatokea
“ Unataka kufanya nini? Akauliza Rose kwa mshangao.Mathew bila kumsemesha kitu akapasua sehemu ya mkono akaingiza mkasi mdogo na kutoa kidude Fulani kidogo .Rosemary akabaki anashangaa huku akigugumia kwa maumivu makali.Haraka haraka Mathew akalitibu lile jaraha akalifunga na kutoka mle chumbani.
“ Ahsante sana Anitha kwa kuligundua hili. kifaa hiki katika mwili wa Rose watu wake kumfuatilia kila mahala aliko.Tunachotakiwa kukifanya hivi sasa ni kwenda kukitupa mbali kifaa hiki.Ngoja niende nitarejea ndani ya muda mfupi” akasema Mathew na kuingia katika nyumba ya gari akachukua piki piki yake kubwa na kutoka mbio
“ Rose hakusita kunieleza kuhusu mambo yake ya siri kwa kujua kwamba muda si mrefu watru wake wangeweza kutuvamia na kumuokoa. Namshukuru sana Anitha kwa kuligundua hili” akawaza Mathew
“ Hata hivyo maelezo aliyonipa yamenipa mwanga kidogo kuhusu suala hili ingawa bado ninahitaji kufahamu zaidi.Kupenda kwake pesa kumemtokea puani na amejikuta akitua katika mikono yangu.” akawaza Mathew na mara akajikuta ametokea katika kijikanisa kimoja kidogo kikuu kuu ambacho hakikuonekana kama kinatumika kwa ibada.Akashuka katika piki piki yake na kuchungulia ndani ya lile kanisa hakukuwa na mtu yeyote nyuma ya kanisa lile kulikuwa na kijito cha maji ,akakitupia kile kifaa ndani ya kanisa halafu akarejea mahala alikopaki piki piki yake Akapanda na kabla hajaondoka gari mbili zikawasili kwa kasi eneo lile wakashuka watu watano na mmoja wao akiwa na kifaa Fulani kilichoonekana kumpa malekezo.Mathew akawatambua watu wale walikuwa ni kutoka usalama wa taifa kutokana na magari yao
“ Ouh thank you Lord. Kama tungechelewa kidogo wangeweza kutuvamia pale nyumbani kwani kifaa kile kilikuwa kinawaelekeza mahala Rose alipo” akawaza Mathew akiwa juu ya piki piki yake.Wale jamaa wakaelekea hadi katika mlango wa kanisa na kwa kasi ya aina yake wakavunja kufuli wakaingia ndani na wote wakapigwa na butwaa. Kanisa lile lilikuwa tupu. Mathew akatabasamu na kuwasha piki piki yake akaondoka.


TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………
 
PENIELA SEASON 3

SEHEMU YA 18

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Mathew na mara akajikuta ametokea katika kijikanisa kimoja kidogo kikuu kuu ambacho hakikuonekana kama kinatumika kwa ibada.Akashuka katika piki piki yake na kuchungulia ndani ya lile kanisa hakukuwa na mtu yeyote nyuma ya kanisa lile kulikuwa na kijito cha maji ,akakitupia kile kifaa ndani ya kanisa halafu akarejea mahala alikopaki piki piki yake Akapanda na kabla hajaondoka gari mbili zikawasili kwa kasi eneo lile wakashuka watu watano na mmoja wao akiwa na kifaa Fulani kilichoonekana kumpa malekezo.Mathew akawatambua watu wale walikuwa ni kutoka usalama wa taifa kutokana na magari yao
“ Ouh thank you Lord. Kama tungechelewa kidogo wangeweza kutuvamia pale nyumbani kwani kifaa kile kilikuwa kinawaelekeza mahala Rose alipo” akawaza Mathew akiwa juu ya piki piki yake.Wale jamaa wakaelekea hadi katika mlango wa kanisa na kwa kasi ya aina yake wakavunja kufuli wakaingia ndani na wote wakapigwa na butwaa. Kanisa lile lilikuwa tupu. Mathew akatabasamu na kuwasha piki piki yake akaondoka.


ENDELEA…………………..

“ Anitha Thank you so much for saving us” akasema Mathew baada ya kurejea nyumbani.
“ Kama usingegundua mapema kuhusu kuwepo kwa kifaa kile chenye kurusha mawimbi na kumuwezesha Rosemary kuonekana kila mahala alipo tungevamiwa na sijui nin kingetokea hapa leo.” Akasema Matheq
“ Nilipofika tu katika kile kijikanisa kikuukuu karibu na njia panda ya kwenda kiwanda cha sabuni nikakitupa kile kifaa ndaniya lile kanisa na haikuchukua muda zikatokea gari mbili ambazo zote ni za usalama wa taifa wakashuka watu watano ambao na walikuwa na kifaa Fulani mithili ya kompyuta ndogo ambacho kiliwapa maelekezo ya mahala kifaa kile tulichokitoa mkononimwa Rosemary kilipo.Walivamia kanisani na kumkosa Rose wote wakapigwa na butwaa wasijue wafanye nini.Niliwaacha hapo wakishangaa nikaondoka zangu.kwa hiyo ahsante sana Anitha.Good job” akasema Mathew na kumpongeza Anitha
“ Ahsante sana Mathew.” Akasema Anitha
“ Ulipomuhoji Rosemary ulifanikiwa kupata chochote kutoka kwake? Akauliza jaji Elibariki
“ Rosemary alifahamu fika kwamba watu wake walikuwa wanamfuatili ili kufahamu mahala alipo kwa hiyo nina hakika alichonieleza hakikuwa cha kweli hata kidogo.Alitaka kuvuta muda ili kuwapa nafasi watu wake waweze kufika na kumchukua.Guys huyu mama ana mtandao mkubwa sana.Sasa ninayaamini maneno aliyonieleza Eva kuhusu huyu mama.Hata hivyo nitakwenda tena kumuhoji kwa mara ya pili .This time she will tell the truth” akasema Mathew
“ Mathew please don’t hurt her anymore.Amekwisha umia sana” akasema jaji Elibarki
“ kama atanieleza ukweli sintamfanya chochote .Yule mama ana roho ya ujasiri sana na bila kutumia nguvuna ukatili kidogo hawezei kutueleza chochote.Naombeni dakika kumi nikamuhoji tena na safari hii tutafahamu kila kitu..” akasema Mathew na kuelekea tena katika chumba alimo Rosemary mkozumi.Akamtazama kwa hasira na kusema
“ Now its just you and me..Watu wako uliowategemea waje wakuokoe hawatakuona tena.Mipango yako imeshindikana.Ninachokihitaji toka kwako sasa hivi ni ukweli.Awali uliniambaimambomengi lakini yote yalikuwa ni uongo mtupu.Nitalianza zoezi langu upya hadi pale utakaponieleza kile ambacho ninakihitaji.Kabla sijafanya hivyo tafadhali naomba unieleze kwa undani kuhusu habib Soud na kuhusiana na karatasizile zilizoibwa ikulu” Akasema Mathew .Rosemary hakumjibu kitu .Mathew akakiwasha kile kifaa cha kukatia.
“ Please don’t hurt me.Umekwiha niumiza sana npaka sasa.” Akaomba Rose
“ I’ll continue hurting you hadi pale utakaponieleza kile ninachokitaka.Nilikukata vidole viwili sasa ninaendela na vilivyobaki.Nitakukata kimoja kimoja hadi utakapokuwa tayari kunieleza ukweli” akasema Mathew na kuanza kuifungua bandeji aliyoifunga katika mguu wa Rose wenye majeraha ya kukatwa vidole
“ Ok Ok tusifike huko tafadhali. Let me tell you one thing.You need me” akasema Rose
“ Ninachokihitaji toka kwako ni majibu ya maswali yangu tu na si vinginevyo..”akasema Mathew
“ You need me because I know so many thing than anyone and I’ll tell you everything I know “
“ Ok tellme” akasema Mathew
“ We must have a deal first”
“ a deal? Siwezi kuwa na makubaliano yoyote na wewe Rose” akasema Mathew
“ kama hutaki makubaliano na mimi then you wont know anything.” Akasema Rosemary.Mathew akafikiri kidogo na kusema
“ Ok tellme everything na kama utakachoniambia kitaniridhisha basi nitaona kama nitakubaliana nawe” akasema Mathew.Rosemary akanyamaza kidogo na kusema
“ It’s true I lied to you about Habib…Ninamfahamu vizuri habib.Ninafahamu kwamba anahusika na mambo ya kigaidi .”akasema Rose na Mathew akamuangalia kwa macho makali
“ Ninafahamu Habib anawindwa sana na mataifa ya kigeni na hasa marekani.C.I.A wanamuwinda usiku na mchana lakini mpaka sasa hawajawahi kugundua chochote kuhusu Habib.Ninafahamu mipango yake ya sasa na baadae ,ninaufahamu mtandao wake,ninafahamu mambo mengi sana ya habib kuliko mtu mwingine.I’m an asset you can’t afford to lose. Accept the deal” akasema Rose
“So you are working with terrorist!! You Devil !! Akasema Mathew kwa hasira
“ If you want to know everything please accept the deal otherwise I’m not going to tell you anything” akasema Rose
“ Rose you know I don’t work like that..above all siwezi kufanya makubaliano na mtu anayeshirikiana na magaidi.How could you do that Rose?
“ are you accepting my deal or not? Akauliza Rose
“ Rose mimi sifanyi kazi kwa shinikizo.Kama hutaki kunieleza kwa hiari yako utanieleza kwa lazima” akasema Mathew na kuiwasha ile mashine yake ya kukatia
“ Nitaendelea kukukata kidole kimoja kimoja na utanieleza kila kitu” “ Go ahead.kill me.Do you think I’m afraid of death? I’m not afraid of death so go ahead and kill me but if you kill me you’ll never know anything that you need to know.” akasema Rose.Mathew akamuangalia kwa makini akataka kusema kitu na mara mlango ukagongwa,Mathew akaufungua ,alikuwa ni Anitha
“ Mathew there is something you need to know ”akasema Anitha kisha wakaongozana na Mathew hadi ofisini.
“ Kuna nini Anitha? Akauliza Mathew
“ Kuna mambo nimeyapata.Amos na Deus mkozumi walikuwa na mawasilaino”
“ What?!! Wanafahmaiana?! Mathew akashangaa
“Ndiyo walikuwa wanafahimiana.Kumbukumbu zinaonyesha kwamba leo asubuhi ,Amos alimpigia simu Deus Mkozumi mara tatu bila Deus kupokea hivyo akamtumia ujumbe mfupi uliosomeka hivi

“ mzee shikamoo.Nimekupiga simu lakini haipokelewi.Naomba unipigie ukipata ujumbe huu ni muhimu sana”

“ haikuishia hapo” Anitha akendelea
“ Baadae Deus akamtumia Amos ujumbe uliosomeka hivi
” Anitha akamuonyesha Mathew ujumbe ambao Deus alimtumia Captain Amos ambao ulisomeka hivi

“ Amos nimeshindwa kukupigia niko katika kikao kizito cha viongozi wa Chama .naomba tuonane saa moja jioni Rozina Hotel kuna mambo ya muhimu sana ya kuongea kuhus ule mpango wetu”

“ Amos was a bastard !! akasema peniela kwa hasira “ Sikutegemea kama yuko namna hii.Nimsaliti mkubwa sana Yule “
“ Nimeshangaa sana kusikia kwamba Amos na Deus ni washirika.kwa sasa nimepata picha Fulani.Kabla hajauawa Amos alisema alimwambia Peniela kwamba wana mipango mikubwa kuhusiana na Elibariki na peniela na ilionyesha wazi kuna kikundi cha watu aliokuwa anashirikiana nao katika kupanga mipango hiyo lakinihakuweza kuwataja,sasa ninaamini Deus ni mmoja wa watu waliokuwa wakishirikiana na Amos.Kumbukeni pia katika maelezo yake dr Joshua alimtaarifu Kigomba kwamba mmoja wa watu hatari sana katika mpango wao ni Deus ambaye aliwahi hta kumpigia simu na kumtahadharisha kuhusiana na mpango wake wa kuiuza hiyo package.Ni wazi dues alikuwa anamtumia Amos katika kupata taarifa kutoka ikulu na kufanikisha mambo mbalimbali.” aKasema Mathew
“ Deus ni rais mstaafu kwa maana hiyo nashawishika kuamini kwamba anafahamu kilichomo ndani ya package hiyo ndiyo maana amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba package hiyo haiuzwi.Mzee huyu anaonekana kufahamu mambo mengi sana.Dont you think its time to find him? Akauliza peniela
“ Hata mimi nilikuwa na wazo kama lako Peniela.We need to find Deus.Kuna mambo mengi ambayo tunaweza kufahamu kutoka kwake.Tatizo ni namna ya kumpata.Tutalijadili baadae jambo hili tuone namna tutkavyoweza kumpata”akasema Mathew
“ Kuna jambo lingine vile vile nimeligundua kwa Rosemary..” akasema Anitha
“ Nimechunguza pia mawasiliano yake ,nimegundua amekuwa na mawasiliano ya karibu sana na mtu aitwaye Hasheem Abdullah.Taarifa zinaonyesha kwamba Rose amekuwa akituma kiasi kikubwa cha pesa kwa huyu mtu mara kwa mara .Hasheem ana akaunti katika benki mbali mbali za hapa nchini na nje ya nchi.Baada ya kuligundua hio nimetafuta taarifa za hasheem ni nani nikagundua kwamba huyu ni mmoja wa watu walio katika orodha ya watu wanaotafutwa kwa kuratibu matukiombalimbali ya kigaidi katika eneo la afrika mashariki na kati..” “ Oh my God!! Akasema Mathew kwa mshangao
“ Huyu hasheem ni raia wa nchi gani? Akauliza Mathew
“ taarifa hazijaonyesha uraia wake” akajibu Anitha
“ Nilihisi toka awali kwamba Rosemary Mkozumi lazima anajihusisha katika mambo ya kigaidi.Kama amekuwa na ushirika na magaidi basi lazima hata yeye mwenyewe atakuwa anajihusisha kwa namna moja au nyingine na mambo hayo.dah ! Nivigumu sana kuamini kama mke wa rais anaweza kujihusisha na mambo kama haya.Hii ni aibu kubwa kwa taifa.”akasema Mathew
“ Tayari suala hili limebadilika tena na sasa limeingia katika ugaidi.Lini mambo haya yatafika mwisho na tuvute pumzi? akauliza jaji Elibariki akionekana kukata tamaa
“ usihofu Elibariki,wanasema giza linapokuwa nene ujue kunakaribia kupambazuka.Na hata sisi tunapoanza kukabiliana magumu mengi tujue tunakaribia kufika mwishoni..Tusikate tamaa.Tuendelee kupmbana.Kuna mambo kadhaa ambayo tunatakiwa kuyafanya lakini kabla hatujafanya chochote,tunatakiwa kumuhoji Rosemary atueleze huyu Hasheem ni nani na tuufahamu mtandao wote anaoshirikiana nao.Anitha na Elibariki endeleeni kuchunguza zaidi kompyuta ya Rosemary na Captain Amos.Nadhanibado kuna mambo mengi tutayafahamu . Peniela twende ndani tukaendelee kumuhoji Rose.”akasema Mathew wakarejea tena katika chumba alimo Rose.Mara tu Rose alipomuona peniela akastuka.
“ You ?! akasema Rose kwa mshangao
“ Hello Rose.Do you know me? Akauliza Peniela
“ Yes I know you.You are Peniela.Kumbe na wewe uko na huyu kijana? Who are you guys? Akauliza Rosemary
“ Usijali utatufahamu tu sisi ni akina nani” akasema Peniela
“ Gosh ! sikutegemea kabisa kama siku moja nitaonana nawe ana kwa ana.”akasema Rose
“ Rose nimekuja hapa kwa jambo moja tuna ninataka kufahamu Hasheem Abdullah ni nani? Akauliza Mathew huku sura yake ikionyesha kwamba hakuhitaji masihara.
“ Hasheem Abdullah? Rosemary akaonyesha mstuko mkubwa
“ Ni nani Hasheem Abdullah? Umekuwa ukimtumia pesa nyingi mara kwa mara” Rosemary akanyamaza kimya “ Rose nakuuliza kwa mara ya mwisho hasheem Abdullah ni nani? “ hakuna chochote ambacho ninaweza nikakueleza kijana .Fanya unachokitaka na hata kama ni kuniua fanya hivyo haraka lakini sintakueleza chochote kama sintapata kile ninachokihitaji” akasema Rose.
“ Rose nadhani bado hujanielewa.Hakuna chochote nitakachojadiliana nawe .Utanieleza kila kitu ninachokihitaji” akasema Mathew na kuichukua mashine yake ya kukatia akaiwasha. “ tayari umenikata vidole viwili umekwiwha nitia ulemavu .Endelea kukata na vingine vilivyobaki ukimaliza njoo katika shingo yangu uniue kabisa lakini katu sintakueleza kitu chochote kama sintapata kile ninachokitaka “akasema Rose.Mathew akaushika mguu wa Rose ule alioukata vidole viwili.Peniela akaona namna vidole vya Rosemary vilivyokatwa akastuka.
“ Mathew ,Rosemary anataka nini? Akauliza Peniela
“ hajanieleza bado anahitaji kitu gani lakini siko tayari kufanya makubalino yoyote naye.She will talk” akasema Mathew kwa hasira huku akijiandaa kuendelea kukata vidole vya mguu.
“ Mathew wait!!..akasema Peniela na kumuomba Mathew watoke nje ya kile chumba wakaongee . “ Mathew hata ukimtesa vipi huyu mama hataweza kusema chochote.Muulize anataka nini na kama analolitaka liko ndani ya uwezo wako accept the deal.” Akasema Peniela
“ Peniela we cant accept any deal ..”
“ Listen to me Mathew,msikie kwanza anataka nini.Rose ana taarifa muhimu sana ambazo hatuwezi kukubali kuzikosa.Huyu ni msaada mkubwa kwetu “ akasema Peniela.Mathew akainama akafikiri kidogo na kusema
“ Ok ngoja tumsikie anataka kitu gani” akasema Mathew na kuingia tena ndani
“ Ok tell me what do you want? Akauliza Mathew
“ are you ready to accept the deal? Akauliza Rose
“ Ninataka kwanza kusikia ni kitu gani unachokihitaji” akasema MathewRose akamgeukia Peniela na kumfanyia ishara atoke nje
“ No she stays” akasema Mathew
“ Fine “ akajibu Rosemary
“ Nitawapa taarifa zote mnazozitaka kuhusiana na Habib na mtandao wake wote lakini kuna mambo ambayo ninahitaji kufanyiwa.” akasema Rose na kunyamaza kidogo kisha akasema
“ Ninataka kinga ya kutokukamatwa kwa kosa lolote lile iliyosainiwa na rais wa Tanzania na vile vile ninataka nipelekwe katika nchi ambayo nitaichagua mwenyewe. …”
“What?!!!!.....Mathew akauliza kwa mshangao
“ Nimesema kwamba ninataka kinga ya kutokukamatwa kwa kosa lolote lile iliyosainiwa na rais wa Tanzania na vile vile ninataka nipelekwe katika nchi ambayo nitaichagua mwenyewe pamoja na ulinzi kama ukilifanikisha hilo nitakueleza kila kitu..” Mathew akamsogelea na kumtazama
“ You are crazy…Siwezi kukubali jambo kama hilo litokee.I cant accept the deal.” Akasema Mathew
“ Hayo ndiyo masharti yangu .Kama hutaki kuyakubali basi sintafumbua mdomo wangu tena.I’m ready to die” akasema Rosemary
“ You are going to tell me everything I want ” akasema Mathew na kuelekea katika meza iliyokuwa na vifaa vya kutesea
“ Mathew can we talk outside?akasema Peniela.Wakatoka ndani ya kile chumba
“ Mathew accept the deal” akasema Peniela
“ Peniela !! akasema Mathew
“ Please Mathew Accept the deal…mpaka hapa hakuna namna unayoweza kafanya ili aweze kukueleza kile unachokitaka.Chaguo ni moja tu Mathew ,tukitaka atueleze kile tunachokitaka lazima tukubaliane na matakwa yake.Rose ni mjanja sana anafahamu kwamba taarifa alizonazo ndizo kinga yake ya mwisho kwa hiyo anaicheza vizuri karata yake ya mwisho .Anafahamukabisa kwamba hawa watu anaoshirikiana nao wakigundua kwambaametoa siri zao watamuua ndiyo maana anataka aende mahala kusikojulikana akajifiche.”akasema peniela
“ Peniela hapana hatuwezi kufanya hivyo…We cant let her go just like that” akasema Mathew
“ Mathew tafadhali nisikilize.Rose anashirikiana na magaidi na anazifahamu siri zao nyingi kwa hiyo tukikubaliana na matakwa yake na akatueleza kile tunachokitafuta atakuwa ameokoa maisha ya watu wengi.Kumbuka nyaraka zile ziliibwa toka ikulu ambazo ni nyaraka hatari sana,ni vipi iwapo watakuwa tayari walizipata karatasi zile na wamekwisha zitumia kutengeneza kirusi hicho? Mathew accept that deal ili tuweze kufahamu mengi kutoka kwa Rose.” Akasema Peniela.Mathew akainama akafikiri na kusema
“ hata kama tukikubali matakwa yake how are we going to do it? Anataka hati ya inga iliyosainiwa na rais,tutafanyaje kuweza kuipata hati hiyo?
“ Hilo ni suala dogo kwangu.Kama ukikubali niachie mimi kila kitu nitakifanya.” akasema peniela
“ How are you going to do it? Rais yuko nje ya nchi hivi sasa na wakati huo huo ana msiba wa mwanae na sisi tunahitaj taarifa toka kwa Rose haraka iwezekanavyo na kingine hatakiwi kabisa kufahamu kuhus kinachoendelea ..I’m confused !! akasema mathew
“ Leave everything to me Mathew.Ninajua nitakavyofanya na rais atasaini hati hiyo” akasema peniela
“ sawa peniela nimekubali kwa sababu yako lakini roho inaniuma sana kumuacha mtu huyu anayeshirikiana na magaidi aondoke….”akasema Mathew na kisha wakarejea chumbani kwa Rose “ Ok Rose.I accept the deal” akasema Mathew
“ Good..”akajibu Rose


TUKUTANE SEHEMUIJAYO………
 
mkimbizi mm ninacho kitabu chake nimeisoma mwanzo mwisho .kuna nyingine mtafiti,mtuhumiwa,mdunguaji,utata, na now ya kijasusi ni wimbo wa gaidi ushawahi zisoma hizo
LEGE Mungu anakuona,andika ili kuokoa fasihi andishi ambayo kwa kiasi kikubwa imeshamezwa na movie za kikorea!
Mimi ni muumini mkubwa wa fasihi andishi na mentor wangu ni marehemu Edie Ganzel though na wengine wapo!
 
PENIELA SEASON 3

SEHEMU YA 19

ILIPOISHIA SEHEMU ILYOPITA
“ hata kama tukikubali matakwa yake how are we going to do it? Anataka hati ya inga iliyosainiwa na rais,tutafanyaje kuweza kuipata hati hiyo?
“ Hilo ni suala dogo kwangu.Kama ukikubali niachie mimi kila kitu nitakifanya.” akasema peniela
“ How are you going to do it? Rais yuko nje ya nchi hivi sasa na wakati huo huo ana msiba wa mwanae na sisi tunahitaj taarifa toka kwa Rose haraka iwezekanavyo na kingine hatakiwi kabisa kufahamu kuhus kinachoendelea ..I’m confused !! akasema mathew
“ Leave everything to me Mathew.Ninajua nitakavyofanya na rais atasaini hati hiyo” akasema peniela
“ sawa peniela nimekubali kwa sababu yako lakini roho inaniuma sana kumuacha mtu huyu anayeshirikiana na magaidi aondoke….”akasema Mathew na kisha wakarejea chumbani kwa Rose “ Ok Rose.I accept the deal” akasema Mathew “ Good..”akajibu Rose


ENDELEA…………………….

“ Suala lako litashughulikiwa na litakapokuwa tayari hati hiyo unayoitaka italetwa hapa.Lakini wakati tunasubiri hilo lifanyike,nataka unipe maelezo ya kuhusiana na huyu mtu Hasheem Abdulah ni nani ? akauliza Mathew
“ Save your breath ..Siwezi kukwambia kitu chochote bila ya kuona kile ninachokihitaji.And please find me a doctor immediately umeniumiza sana.!! Akasema kwa ukali Vicky.Peniela akamtazama Mathew na kusema “ Mathew she can’t tell us anything.” Mathew akamtazama Rose kwa hasira na kusema
“ I’ll be right back.” “ Tafadhali naomba mnifungue hizi pingu mlizonifunga “ akafoka Rose huku akilia Mathew na Anitha wakatoka mle chumbani na kumuacha Rose akilia kwa maumivu wakarejea ofisini walikokuwapo Anitha na jaji Elibariki
“ Amesema chochote? Akauliza jaji Elibariki
“ hapana hajasema chochote but we made a deal with her ”
“ a deal ? akauliza Elibariki kwa mshangao
“ Yes .Tumefanya makubaliano naye ili atueleze mamboya muhimu anayoyafahamu kuhusiana na habib na mtandao wake wa kgaidi.Hakuna namna tunayoweza kumfanya akatupa taarifa hizo zaidi ya kukubaliana na anachokitaka.”akasema Mathew
“ Anataka nni? Akauliza Elibariki ambaye hakuonekana kufurahishwa na kitendo kile cha Mathew kufanya makubaliano na Rose.
“ Anataka hati ya kinga ya kutokushtakiwa kwa kosa lolote iliyosaiwa na rais, na vile vile anataka apelekwe katika nchi anayoitaka pamoja na ulinzi.”
“ That’s impossible.We can’t do that” akasema jaji Elibariki
“ Elibariki hatuna namna nyingine ya kufanya zaidi ya kumtimizia matakwa yake ili aweze kutupa taarifa za muhimu sana.” Akasema Peniela
“ hata kama ana taarifa za muhimu lakini huyu mama anashirikiana na magaidi na anazifahamu siri zao nyingi ,we cant just let her go like that..Anatakiwa ateswe na atasema ukweli”
“ Elibariki,jambo tulilolifanya halikuwa rahisi hata kwangu mimi .Rose anashirikiana na magaidi na tayari amekwisha pata ujasiri wa kigaidi wa kutokusema chochote hata akiteswa vipi.Siku zote magaidi wako tayari kufa kuliko kusema chochote.Hata tukitumia njia gani Rose hataweza kusema chochote.Njia pekee ya kupata taarifa toka kwa Rose ni kumtimizia kile anachokitaka.”
“ how are we going to do that? Tutaipataje hiyo hati iliyosainiwa ana rais? Akauliza jaji Elibariki
“ I’ll do that “ akajibu Peniela.Jaji Elibariki akamgeukia na kumkodolea macho “ Peniela hili si suala dogo kama unavyolichukulia..Hili ni suala kubwa na hawezi kulifanya yeye mwenyewe ,atashirikishwa pia mwanasheria mkuu naye alifahamu suala hili na aweke sahihi yake.Endapo jambo hili likifika huko kote halitakuwa siri tena.Kila kitu kitakuwa wazi na chochote tunachokifanya.” Akasema jaji Elibariki
“ Kwa hiyo jaji Elibariki wewe ndiye mjuzi wa sheria hapa unatushauri tufanye nini? Akauliza Mathew.
“ Mimi kwa ushauri wangu ni kwamba suala hili la Rosemary tuliweke kwanza pembeni kisha tuendelee na suala letu la awali. La kuitafuta package toka kwa Dr Joshua.Tukifanikiwa kuipata package na kupata ushahidi unaojitosheleza wa kutuwezesha kumuangusha Dr Joshua tutapata nafasi ya kuonana na mtu atakayeshika nafasi ya urais na atatusadia katika kulifanikisha suala hilo.lakini kwa sasa ninashauri kwanba tusichanganye mambo mengi kwa wakati mmoja tutajikuta tumekwama.” Akasema jaji Elibariki
“ Elibariki anaweza kuwa sahihi..Tuliweke pembeni suala hili la Rosemary.Tuendelee kumshikilia Rosemary na kuhakikisha anakuwa chini ya ulinzi mkali hadi hapo tutakapolifanikisha kwanza suala la kuipata package.”
“ Rosemary kwa sasa lzima atakuwa anasakwa kial kona na vyombo vya usalama. kuendelea kumuweka hapa kwa muda mrefu inawezakuwa ni hatari kubwa kwa usalama wetu.Wewe mwenyewe umetuhakikishia kwamba watu uliokutana nao waliokuwa wakifuatilia taarifa za kile kifaa tulichokigundua mwilini mwa Rose ni watu wa usalama wa taifa basi ni wasi kuna juhudi kubwa sana zinafanyika kuweza kumpata Rose..Tukisema tusubiri mpaka hapo tutakapokamilisha kwanza suala la kuipata package toka kwa Dr Joshua tunaweza tukajikuta tumempoteza na tukashindwa kupata taarifa za muhimu toka kwake.Guys let us finish this once and for all..” akashauri Peniela
“ Nakubaliana nawe Peniela kwamba watu wa Rosemary kwa sasa hawalali wakimtafuta na leo hii nusura wangeweza kumfikia kama tusingefanikiwa kugundua kifaa kile cha kuonyesha kila mahala alipo .Hata hivyo nadhani tukubaliane na jaji Elibariki kwamba tuliweke pebeni kwanza suala la Rosemary na tuendelee na mipango yetu ya awwali ya kuipata package toka kwa Dr Joshua.Kuhusu usalama wa Rosemary naoba niwatoe wasiwasi kwamba hapa kwangu kuna sehemu salama kabisa ambayo hakuna mtu anayeifahamu na tutamuweka huko na atakuwa salama hadi hapo tutakapokuwa tayari kulishughulikia suala lake”akasema Mathew
“ Damn you Mathew umejiandaa sana katika jumba lako hili.Umekamilika kwa kila kiru” Akasema Peniela
“ Ninafahamu ugumu wa kazi zangu na ndiyo maan nikajitahidi kujikamilisha kwa kila kitu.Tukiachana na hayo kuna kitu kingine ambacho tunatakiwa tukijadili..Rosemary alikuwa anashirikiana na Captain Amos na walikuwa katika mpango wa kuipata package kutoka kwa Dr Joshua.kwa sasa Captain Amos amefariki na Rosemary tunaye hapa kwa maana hiyo mipango yao yote kuhusiana na Package imevurugika.Tumegundua pia kwamba Captain Amos alikuwa ana mawasiliano na Deus Mkozumi rais wa zamani wa Tanzania na ambaye alikuwa ni mume wa Rose.Katika maelezo yake kabla hajapigwa risasi alimueleza Peniela kwamba wana mpango mkubwa unaomuhusu Peniela na jaji Elibariki kwa maana hiyo basi ninashawishika kuamini kwamba Deus Mkozumi atakuwa akifahamu mpango huu aliousema Amos.Inaonekana wazi kwamba huku nako kuna mtandao mwingine .Mkumbuke pia kwamba Dr Joshua alimtaja Deus kama mmoja wa watu ambao ni maadui wakubwa katika kufanikisha uuzwaji wa hiyo package kwa maana hiyo Dues atakuwa akilifahamu vyema sana suala hili.Nadhani ni wakati muafaka sasa wa kumtafuta mzee huyu na kufahamu mambo mengi kutoka kwake” akasema Mathew
“ Deus Mkozumi ni rais mstaafu,ana ulimzi mkali kila aendapo na nyumbani kwake pia,kumpata mtu kama huyu haliwezi kuwa jambo rahisi hata kidogo.Huyu naye ana mtandao mkubwa wa watu wenye nguvu na hatari na wana mipango mikubwa juu yetu kwa hiyo si watu wa kuwafuata kirahisi rahisi.” Akasema jaji Elibariki
“ Ni kweli kumpata Deus Mkozumi si rahisi lakini jambo hili haliwezi kutushinda.Tunaweza kumpata”akasema Mathew
“ Tutampataje Deus?akauliza jaji Elibarii.Mathew akamgeukia Peniela
“ No ! Mathew we cant use her ..”akasema Elibariki “ Hatuna namna nyingine ya kufanya Elibariki ili kumpata Deus zaidi ya kumtumia Peniela.” Akasema Mathew
“ Mathew ,we cant put her at risk again.Peniela amenusurika leo hii katika shambulio,I’ve lost my wife today,and I cant lose Peniela again” akasema jaji Elibariki.Mathew akamtazama na kusema
“ Eli Can we talk outside?Wakatoka nje ya kile chumba
“ Elibariki tuko kati kati ya vita.Tunatakiwa tutumie kila aina ya mbinu na silaha tulizonazo katika kupambana.Wewe na Peniela kuna mipango inapangwa juu yenu na kikundi cha watu ambao wanawafuatilia.Maisha yenu yako hatarini kwani hatufahamu watu hao wana mipango gani juu yenu.Kwa hali halisi ilivyo ni wazi kwamba hatuwezi kumfikia Deus Mkozumi isipokuwa kwa kumtumia Peniela Pekee.She can penetrate any where.She’s good at this.She was trained for this .Kwa hiyo usiwe na wasiwasi hata kidogo kuhusu usalama wake..Kitu kingine nafahamu unampenda sana Peniela lakini tunapokuwa katika kazi kama hizi ,masuala ya mapenzi tunayaweka pembeni na hutakiwi kabisa kuonyesha hisia zako hata kama unampenda mtu yeyote .Peniela mwenyewe yuko tayari kuifanya kazi yoyote ile na haogopi lakini kitendo ulichokifanya cha kuingilia kati na kumzuia kwamba asishirikishwe katika kumtafuta Deus kimemshangaza hata yeye pia.Wanawake wale mle ndani wanatutegemea sisi kuwaongoza katika kulimaliza suala hili lakini kama tutashindwa kuonyesha namna bora ya kufanya maamuzi tutawavunja moyo kwani tayari wamekwisha jitoa maisha yao katika kuhakikisha tunalifanikisha jambo hili.” Akasema Mathew
“ Mathew I’m sorry kama nilikukwaza kwa kauli ile lakini nilijikuta nikishindwa kujizuia .Ninampenda sana Peniela na tukio lililotokea mchana alipokwenda kuonana na Amos lilinistua na kuniogopesha sana .Please forgive me and lets do what needs to be done” akasema jaji Elibariki
“ Are we good? Akauliza Mathew
“ We’re good”akajibu jaji Elibariki kisha wakarejea tena ndani ya ofisi
“ Are you guys ok? Akauliza Peniela
“ we’re fine.”akajibu jaji Elibariki
“ kwa hiyo nini kinachoendela saa hivi? Akauliza Peniela
“ Kitu kinachotakiwa kufanyka kwa sasa ni kumtafuta Deus Mkozumi.Yeye anafahamu mambo mengi sana na kama tukimpata basi atatusaidia kupiga hatua kubwa.Peniela utaifanya hii kazi.You will go meet Deus Mkozumi” akasema Mathew
“ Ni jinsi gani ataonana na Deus? Akauliza jaji Elibariki
“ Usihofu Elibariki,they call me an insect because I can penetrate anywhere. Kwa kuwa namba za simu za Deus tunazo hapa,I’ll call him and set a meeting.Kuhusu nitakwenda kuongea naye nini hilo ni nyie mtapanga.”akasema Peniela
“ say something Anitha “akasema Mathew
“ Peniela atakapokwenda kuonana na Deus tutamuwekea kifaa cha mawasiliano sikioni .Atavaa gauni la rangi nyeusi na sehemu ya kifuani katika titi la kulia tutaweka ua jeusi na ndani ya ua hilo kutakuwa na kamera ndogo ambayo itatuwezesha sisi kutazama kila kitu kinachoendelea kati yako na Deus.Tutayafuatilia maongezi yenu na tutakuwa tunakueleza nini cha kufanya.Endapo tutaona kama kuna tatizo lolote la kiusalama tutakutaarifu “ akasema Anitha
“ Hata hivyo hatutakuwa mbali na mahala utakapokuwa kwa ajiki ya msaada wa dharura pindi ukihitajika” akasema Mathew
“ Ok guys.muda umekwenda sana Nipeni namba za Deus nimpigie.”akasemaPeniela.Anitha akaziandika namba za simu za Deus katika simu yake halafu akapiga kisha akampatia Peniela akaiweka simu sikioni
“ hallow”ikasema sauti nzito ya kiume upande wa pili “hallow” akasema peniela
“naongea na nani? “ Unaongea na Peniela hapa.Naongea na nani?akauliza Peniela
“Kwani wewe umempigia nani? Akauliza tena Yule jamaa upande wa pili
“ Ninahitaji kuongea na Mr Deus Mkozumi tafadhali.” Kimya kifupi kikapita halafu yule jamaa akauliza
“ Umeipata wapi hii namba? Nani kakupatia namba hii?
“ It doesn’t matter nimeipata wapi ila kama Deus yupo ninaomba niongee naye“ akasemaPeniela.Kikapita kima kifupi tena Yule jamaa akauliza
“ Umesema unaitwa nani vile?
“Peniela.mwambie Peniela anahitaji kuongea naye” Baada ya dakika mbili Peniela akasikia sauti nyingine ambayo haikuwa nzito sana kama ile ya mwanzo
“ Hallow” ikasema sauti ile
“Hallow”akasemaPeniela
“ Are you Peniela?
“ Yes I am Peniela.Are you Deus Mkozumi? Akauliza Peniela
“ Yes Iam Deus..Umeipata wapi namba hii? Akauliza Deus
“ Mzee Deus nina shida na wewe ndiyo maana nikaitafuta namba hii hadi nikaipata.”
“ Una shida na mimi ! Shida gani hiyo?akauliza Deus “ Siwezi kukueleza simuni mzee.Nahitaji kuonana nawe tuongee”
“Peniela ,ingekuwa vizuri ungenieleza suala ambalo unataka tukune tuliongelee ili niweze kupima na kuona kama lina uzito gani.Unajua mimi ni mtu mwenye shughuli nyingi kwa hiyo kama ukitaka kuonana na mimi lazima nivunje baadhi ya mipango yangu kwa hiyo naomba unieleze ili nipate walau picha.”
“ Deus ninafahamu wewe ni mtu mwenye shughuli nyingi lakini hadi nimeamua kukupigia basi fahamu suala lenyewe ni kubwa hivyo naomba usilipuuzie tafadhali.Nahitaji sana kuonana nawe” Kikapita kimya kifupi kisha Deus akauliza
“ Unataka tuonane lini na wapi?
“ Tuonane leo hii jioni kuanzia saa mbili za usiku..Kuhusu mahala pa kukutana utaamua wewe mwenyewe tukutane wapi mahala ambako unaamini ni salama.”akasema Peniela.Baada ya sekunde kadhaa Deus akasema
“ Tukutane Iyumba country club saa mbili kamili. Katika geti la kuingilia jitambulishe kama mgeni wa namba ishirini na saba utapelekwa mahala nitakapokuwepo.Ila hakikisha kwamba jambo unalotaka kunieleza ni jambo kubwa .”
“ Ahsante sana mzee.Nitafika mida hiyo bila kukosa “akasema Peniela na kukata simu.
“ Good.You did great! Akasema Mathew
“ Deus hajaonyesha kustushwa kabisa na ulivyompigia simu na hii inadhihirisha wazi maneno ya Amos kwamba they know you already .Ok hatua muda mwingi sana hivyo maandalizi yaanze mara moja.Anitha anza kuandaa program zako halafu ukamchagulie Peniela gauni zuri la kuvaa usiku wa leo .”
“ Anitha ninaomba simu niwasiliane na josh kumpa taarifa kwamba sintakuwepo jioni ya leo.Nina hakika watakuwa wamenitafuta sana mpaka mida hii kwani hata simu yangu nimeizima kabisa ili wasiweze kujua mahala niliko” akasema Peniela akachukua simu na kumpigia Josh “hallow Josh.Its me Peniela” akasema peniela baada ya Josh kupokea simu “ peniela where are you? Kila kitu kimesimama hapa hawa watu wanakusubiri wewe.wanahaha wanakutafuta lakini hakuna anayejua uko wapi na simu yako umeizima kabisa.Tafadhali naomba uje hapa mara moja ili taratibu za msiba wa John ziweze kufanyika”akasema Josh
“Josh I cant come right now.I’m at the middle of something.” Akasema Peniela “kwa hiyo itakuwaje?akauliza Josh
“waambie nimekupigia simu na nimekutaarifu kwamba sintaweza kufika leo tuonane kesho”akasema peniela
‘ Ok peniela ngoja niwataarifu”akasema Josh na kukata simu
“kwema huko? Hakuna tatizo lolote?
“ hakuna tatizo ila kila kitu kimesimama wananisubiri mimi ili tuweze kupanga kuhusiana na suala la msiba wa John.” “ sawa utalishughulikia suala hilo kesho lakini kwa leo lazima tushughulikie kwanza suala la Deus.”akasema Mathew kisha akageuka kutaka kutoka mle ofisnini lakini Anitha akamuita.
“Kuna simu inapigwa katika namba ya Dr Kigomba.Inaonyesha ni simu kutoka afrika ya kusini.Yawezekana akawa ni Dr Joshua”akasema Anitha na wote wakatega sikio kusikia simu ile.
“ hallow Mr President”akasema Dr Kigomba
“ Kigomba nipe taarifa za huko.mambo yanakwendaje? Akauliza Dr Joshua “Huku kila kitu kinakwnda vizuri.Maandalizi yanaendelea.Vipi ninyi huko?
“ Huku hakuna habari mpya .Nimekupigia ili kufahamu umefikia wapi na maandalizi ya msiba”
“Kila kitu kimekwenda vizuri na tayari shughuli zinaendelea pale katika nyumba ya familia.Taarifa zimesambaa haraka sana na mpaka hivi sasa waombolezaji ni wengi mno.Kifo hiki cha Flaviana kimewagusa watu wengi sana na ndiyo maana wamejitokeza kwa wingi namna hii ndani ya muda mfupi.”akasema Dr Kigomba
“ kwa kweli kifo cha Flaviana kinaumiza sana na hata mimi kimeniumiza sana lakini yote hii ni katika kuhakikisha kwamba mpango wetu unafanikiwa.Anyway tuachane na hayo tutajadili kwa undani nikirejea.Tutawasili na mwili esho saa tano asubuhi.Watangazie.”akasema Dr Joshua.
“ Sawa Mr President.Tumekwisha fahamishwa hilo na mwenyekiti wa kamati ya mazishi na kila kitu kwa ajili ya kuupokea mwili kimeandaliwa...”
“ sawa Kigomba sina mengi ya kukwambia kwa sasa ila tutaongea mambo mengi nikishafika huko kesho.Ila nimeongea na Hussein atafika kesho saa mbili za usiku tayari kwa kuuchukua mzigo wake.Nataka tulimalize suala hili ili maisha mengine yaendelee.Nimechoshwa na kuwapoteza watu wangu kila kukicha kwa sababu ya biashara hii.Nitakupigia baadae Dr KIgomba”
“ Dr Joshua before you go,kuna jambo ambalo sina hakika kama umekwishapata taarifa zake”
“jambo gani?
“ Amos is dead” “Amos is dead? how?Who killed him?
“ Mpaka sasa haijafahamika ni nani lakini inaonyesha aliyemuua is very professional assassin”
“ Mungu wangu ! !!Dr Joshua akastuka
“ tuki hilo limetokea muda gani? Mbona asubuhi ya leo nimewasiliana na Amos ?
“ Tukio limetokea mchana wa leo Mlimba lodge”Zikapita sekunde kadhaa kisha Dr Joshua akasema “Nimestushwa sana Kigomba kwa taarifa hizi.Ngoja nizungumze na mkuu wa polisi nifahamu kama kuna hatua yoyote imefikiwa kuchunguza waliomuua Amos.Kigomba kwa mara ya kwanza nimeogopa sana.Kama Amos ameuawa basi watu walionfaya hivyo wako karibu sana kutufikia na sisi pia.Please make sure hakuna kitu chochote ambacho kinaweza kutuunganisha sisi na Amos.Kigomba this is a very serious matter and take it very seriously.Nitakupigia baada ya masaa mawili kujua kinachoendelea na tutaongea zaidi”
“ sawa Mr President lakini wa mujibu wa taarifa za polisi watu waliofanya mauaji hayo wameondoka na kompyuta na simu ya Amos.” “Kigomba something is going on.Kuna kitu kinatafutwa kwa Amos.We need to hurry.Tunatakiwa tuimalize biashara yetu haraka iwekanavyo .Ntakupigia tena baadae kidogo”akasema Dr Joshua na kukata simu.


PENIELA ATAFANIKIWA KUONANA NA DEUS MKOZUMI? TUKUTANE SEHEMU IJAYO….
 
PENIELA SEASON 3

SEHEMU YA 20

ILIPOISHAI SEHEMU ILIYOPITA
“Nimestushwa sana Kigomba kwa taarifa hizi.Ngoja nizungumze na mkuu wa polisi nifahamu kama kuna hatua yoyote imefikiwa kuchunguza waliomuua Amos.Kigomba kwa mara ya kwanza nimeogopa sana.Kama Amos ameuawa basi watu walionfaya hivyo wako karibu sana kutufikia na sisi pia.Please make sure hakuna kitu chochote ambacho kinaweza kutuunganisha sisi na Amos.Kigomba this is a very serious matter and take it very seriously.Nitakupigia baada ya masaa mawili kujua kinachoendelea na tutaongea zaidi”
“ sawa Mr President lakini wa mujibu wa taarifa za polisi watu waliofanya mauaji hayo wameondoka na kompyuta na simu ya Amos.” “Kigomba something is going on.Kuna kitu kinatafutwa kwa Amos.We need to hurry.Tunatakiwa tuimalize biashara yetu haraka iwekanavyo .Ntakupigia tena baadae kidogo”akasema Dr Joshua na kukata simu.


ENDELEA…………………….

“ Vifo vilivyotokea mfululizo vimemuogopesha sana Dr Joshua nandiyo maana anataka kuitoa package hiyo haraka kwani ana wasiwasi kwamba kuna watu wengine wanaoitolea macho package hiyo.Kwa maelezo yake mwenyewe alikiri kwamba anataka makabidhiano yafanyike haraka pindi tu akirejea kutoka afrila ya kusini kwani tayari pesa imekiwsha ingizwa katika akaunti zao za sri walizofungua nje ya nchi.Amemtaja Hussein kwamba atawasili kesho jioni na huyu inaonekana ndiye ambaye anakuja kukabidhwa package hiyo.Kwahiyo jamani ile kazi yetu ya msingi iko mbioni kukamilika.Umakini wa hali ya juu sana unahitajika.Tutakaa na kulijadili hilo baadae kidogo lakini kwa sasa tuanze kumuandaa Peniela kwa ajili ya kwenda kuonana na Deus Mkozumi.” Akasema Mathew kisha akamuomba jaji Elibariki aongozane naye wakaelekea katika chumba alimo Rosemary.Mara tu walipoingia mle chumbani Rosemary akastuka sana baada ya kumuona jaji Elibariki “I know you !! akasema Rose. “ unanifahamu? Akauliza jaji Elibariki.Hakutegemea kama Rose angemtambua
“ Elibariki ,right? Jaji Elibariki..Ninakufahamu sana.Kumbe na wewe uko na hawa mashetani.Who are you guys? Akauliza Rose akishangaa sana kumuona jaj Elibariki pale. Mathew akafungua mlango uliokuwa pembeni na ndani ya chumba kile kukaonekana vifaa mbalimbali akatoa kiti cha magurudumu na kukisogeza karibu na kitanda alicholazwa Rose.Akamfungua pingu na kumuomba Elibariki amsaidiea kumuinua Rose wakamuweka katika kile kiti.
“ Mnanipeleka wapi? Akauliza Rose.Mathew akakisukuma kiti kile hadi chumbani kwake halafu akaenda katika kisanduku Fulani kilichokuwa ukutani kilichokuwa na muundo kama simu akabonyeza namba kadhaa na mara kabati kubwa la vitabu likasogea pembeni na ukaonekana mlango.Mathew akaufungua ule mlango nakulionekana kuna ngazi za kushuka chini.Mathew akamuamuru Elibariki amfuate waksshuka ngazi kuelekea chini..Elibariki na Rose wakabaki wanashangaa.
“ who are you ? Hii nyumba ya chini ni kwa ajili gani?akauliza Rose lakini Mathew hakumjibu kitu..Waliingia katika chumba kimoja kikubwa kilichokuwa na kitanda kikubwa meza ya kulia chakula,meza ya kusomea,kabati kubwa la nguo bila kusahau Luninga kubwa iliyokuwa ukutani.Wakamnyanyua Rose na kumuweka kitandani.
“ Rose suala lako uliloliomba tunalishughulikia na litakapokuwa tayari tutakutaarifu lakini mpaka wakati huo this will be your new home.Hii ni nyumba iliyoko chini ya ardhi .Nobody will know you are here.Usihofu sisi si watu makatili kama unavyodhani lakini huwa tunalazimika kuwa wakali kwa watu kama ninyi ambao mnashirikiana na magaidi.Kwa sasa pumzikanitakuwa na maongezi nawe baadae” Akasema Mathew huku akimfunga pingu za mikono na miguu.
“ Mpaka lini mtaendelea kunifunga pingu hizi ? akauliza kwa ukali Rose
“ Mpaka hapo tutakapopata kila tunachokihitaji toka kwako”akasema Mathew.
“ tafadhali naomba msinifunge namna hii,.Mnanitesa sana.Vipi kama nikihitaji kujisaidia “ akaomba Rose
“ Jisaidie hapo hapo.You deserve to be in chain mpaka hapo rais atakaporejea na hatujui atarejea lini yawezekana ikawa ni kesho,wiki ijayo,baada ya miezi au hata mwaka “ akasema Mathew na kisha wakatoka mle chumbani wakimuacha Rose akiangua kilio
“ Mathew umejiandaa sana.Sikutegema kama nyumba yako inaweza kuwa na mambo mengi ya siri namna hii”akasema Elibariki
“ Kutokana na kazi ninayoifanya,nimelazimika kutengeneza nyumb aiwe namna hii ili kuniwezesha kufanya kazi zangu bila wasiwasi.”akasema Mathew wakati wakipanda ngazi kurejea sebuleni.Wakaelekea ofisini alikuwemo Anitha peke yake.
“ peniela yuko wapi? akauliza Mathew
“ Nimempeleka chumbani anajaribu mavazi,can you check on her Mathew if she’s ready ? kuna kitu ninamalizia katika komyuta hapa”akaomba Anitha..Mathew akatoka na kuelekea katika chumba cha Anitha akaufungua mlango na kuchungulia ndani.Akapatwa na mstuko wa ghafla kwa alichokiona ndani..Peniela alikuwa amegeukia katika kioo akijipodoa.Alikuwa na nguo za ndani pekee.
“ ouh my gosh ! akasema Mathew kwa sauti ndogo na kubaki anamkodolea macho binti Yule mwenye uzuri usioelezeka..
“ Ndiyo maana kumbe wanaume wanachanganyikiwa kwa ajili yake.She’s hot !!
akawaza huku akiwa amejisahau kabisa akiendelea kumtazama Peniela..Kupitia kioo cha kujitazamia Peniela alimuona Mathew namna alivyostuka baada ya kumkuta katika hali ile.Hakutaka kumstua akamuacha aendelee kumtazama. kwa makusudi akainama kujipaka mafuta miguuni.Mathew akaufunga mlango na kusimama pale nje kwa sekunde kadhaa
“ Dah ! Kitu gani kimeniambia nije huku chumbani hadi nimekutana na mambo haya? Nimekwisha mzoea Anitha mara nyingi tu huwa ninamshuhudia akiwa mtupu lakini hakuna chochote kinachonitokea ila kwa peniela imekuwa tofauti kabisa.Nimepata msisimko wa ajabu.This woman have got smething special to attract men” akawaza na kupiga hatua za haraka haraka kuelekea chumbani kwake kwani tayari ikulu kulikwisha kasirika na mambo yalikwisha haribika..Haraka haraka akaingia bafuni akaoga na kubadili nguo kisha akafungua kasiki lake ambalo huhifadhia vifaa mbalimbali na silaha akachagua vitu ambavyo wangevihitaji kwa usiku ule na kutoka akaeleka ofisini ambako Anitha alikuwa anamalizia kuweka sawa program kadhaa katika kompyuta yake..
“ is everything ready? akauliza Mathew
“ Nimeshamaliza kuweka kila kitu tayari.” Akasema Anitha. Na mara akatokea Peniela akiwa katika gauni jeusi la Anitha lililomkaa vyema sana.
“ dah ! Peniela !! Huyu mwanamke amebarikiwa uzuri wa ajabu sana.Sikuwahi kuifahamu siri yake ya kuwadatisha wanaume kiasi hiki leo nimegundua.Mtoto huyu akiwa hana nguo huwezi amini ni binadamu wa kawaida.She looks like an angel”akawaza Mathew huku akimtazama Peniela
“ hello Mathew How do I look?akauliza Penela
“ You look wonderful..unafanana sana na malaika” akasema Mathew na wote wakacheka.
“ Anitha mimi niko tayari sasa ni zamu yako kuniandaa”akasema Peniela.Anitha akafungua kisanduku kidogo akatoa vidude Fulani vinne kama vispika vidogo akachukua kimoja na kukipachika sikioni kwa Peniela halafu kingine akampatia Mathew na kingine akaweka katika sikio lake
“Hivi ni vifaa vya mawasiliano ambavyo vitawezesha kuwasiliana .Kupitia vifaahivi tutasikia kila utakakachokiongea na Deus na sisi tutakuongoza nini ukiseme .Usifanye chochote bila ya maelekezo yetu.”akasema Anitha halafu akafungua kiboksi kidogo akatoa kijiua kidogo cheusi akakipachika katika sehemu ya titi la kulia .
“ Hili ukilitazama ni kama ua linaloongeza urembo katika nguo uliyovaa lakini kidude hiki katikati ya ua kinachoonekana kama pini ya ua ni kamera ambayo ndiyo itatuwezesha sisi kutazama kila kitu kitakachofanyika ukiwa na Deus.Kwa kujaribu Mathew mpeleke chumbani kwa Naomi akaongee naye jambo lolote ili tuijaribu kamera” .Akasema Anitha
“ Lets us go.I’ll show you the room” akasema Mathew na kumuongoza Peniela kueleka katika chumba cha Naomi akagonga mlango Naomi akafungua Peniela akaingia Kila walichokiongea Peniela na Naomi kikaonekana katika kompyta ndogo ya Anitha
“ Kila kitu kinakwenda vizuri .kwa upande wangu nimemaliza”akasemaAnitha.Mathew akamfuata Peniela chumbani kwa Naomi akamtaarifu kwamba kila kitu tayari na wanaweza wakaondoka halafu akaongea na Naomi akamfahamisha kwamba wanatoka kidogo kuna mahala wanaelekea na watarejea baadae kisha akatoka hadi katika nyumba yake ya magari akatoa gari moja ambao hulitumia mara chache sana.Mle ndani alikuwa na magari sita
“ hili ndilo gari analostahili kulitumia Peniela leo.Anastahili gari kama hili.She’s ana angel”akawaza Mathew akilijaribu gari.Aliporidhika liko vizuri akarejea ndani.
“ Kila kitu tayari we can leave now.Elibariki utaangalia kila kitu hapa ndani.Utamuangalia Naomi na endapo kuna tatizo lolote utatujulisha mara moja kwa kutumia simu ile ofisini” akasema Mathew
“ Mathew tafadhali kuwa makini sana.Take good care of peniela. “ akasisitiza Elibariki “ I will” akasema Mathew.Elibariki na peniela wakakumbatiana kwa muda
“ Please be carefull Peniela.”akasema Elibariki
“ I will Eli” akajibu Peniela akumbusu Elibariki kisha akaongozana na Mathew na anitha kueleka nje.Peniela akaingia katika gari aliloandaliwa na kutangulia.Mathew na Anitha wakafuata nyuma yake.Elibariki akafunga geti na kurejea ndani akajilaza sofani. Mawazo mengi kuhusiana na kinachoendelea.
“ Sikuwahi kuota kama siku moja maisha yangu yanaweza yakabadilika na kuwa hivi..Mtu niliyekuwa ninaheshimika leo hii nimejificha humu ndani ninasakwa kila kona ya nchi..” Mara Elibariki akastuliwa toka mawazoni na mtu aliyeingia pale sebuleni alikuwa ni Naomi.
“ Hallow” akasema Naomi
“umenistua sana ,nilikuwa nimezama katika mawazo mengi.”akasema jaji Elibariki.
‘” Pole..”akajibu Naomi huku akicheka kidogo kisha akaenda kuketi sofani
“ Wamekwenda wapi akina Peniela?akauliza Naomi
“ Kuna mahala wamekwenda na watarejea muda si mrefu sana.Kuna kitu unahitaji? Chakula tayari kipo jikoni.Mfumo wa hapa ukihisi njaa unakwenda mwenyewe jikoni unatafuta chakula unachokitaka unakula.Vyakula vingi vya hapa ni vya maboksi .Ndani ya nyumba hii watu wanafanya kazi muda wote kiasi kwamba hawakumbuki hata kula kwa hiyo kama unahisi njaa tafadhali nenda jikoni utaangalia wewe mwenyewe unataka kula kitu gani” akasema jaji Elibariki.
“ Nadhani nyumba hii mnahitaji sana mtu wa kuwasaidia,kuwapikia n.k.Sura zote zinaonekana sura za kazi .Kesho nitakwenda kununua mahitaji ya ndani.Hamuwezi mkafanyakazi mkasahau kula..Anyway tuachane na hayo wewe ni jaji si ndiyo?
“ Ndiyo mimi ni jaji wa mahakama kuu.naitwa jaji Elibariki.”
“ Nimefurahi kukufahamu.Mbona hukuambatana na akina Mathew? Akauliza Naomi
“ Sitakiwi kuonekana huko nje”akajibu Elbariki kwa ufupi
“ Unatafutwa? Ulifanya nini?
“ Ni hadithi ndefu sana ambayo siwezi kukuelezea kwa sasa” akajibu Elibariki.Kikapita kimya kifupi Naomi akauliza
“ Mke wako anafahamu kama unaishi hapa?
“ Sina mke” akajibu Elibariki
“ Huna mke? Naomi akashangaa
“ Ndiyo sina mke kwa sasa.She’s dead”akasema Elibariki.
“ Pole sana jaji .Sikulifahamu hilo.” Akasema naomi
“ yah ni mapenzi ya Mungu.”
" Kwa hiyo una mpango gani hivi sasa kuhus maisha yako? Hufikirii kuoa tena?bado kijana sana” Akauliza Naomi
“ kwa sasa ni mapema sana kusema chochote kuhusu mpango wa kuoa tena kwa sababu hata mke wangu bado hajazikwa” akasema Elibaliki na kumstua sana Naomi
“Ina maana amefariki si muda mrefu?
" Asubuhi ya leo” akajibu Elibariki “leo ?!! Naomi akazidi kushangaa “Ndiyo .”
“ Kwa hiyo huruhusiwi hata kuhudhuria msiba? “ kama nilivyokwambia awali kwamba siruhusiwi kabisa hata kuonekana huko nje.Ninasakwa kila kona”
“Ulifanya nini?
“ni hadthi ndefu sana .Nitakusimulia siku nyingine.”
“ jamani pole sana jaji.Mungu akupe nguvu katika kipindi hiki kigumu.” Akasema Naomi na kuinuka akelekea jikoni akafungu fungua makabati kuangalia kuna kitu gani ambacho wanaweza kula kwa usiku ule
“ Kweli hii ni nyumba ya watu wa kazi .Vyakula vyao vyote ni vile vya makopo.Nataka nimtengenezee jaji Chakula aweze kula..Kwa hali aliyo nayo anatakiwa apate chakula ili awe na nguvu.Namuonea huruma sana yule kaka.Kufiwa si jambo dogo” akawaza Naomi huku akiwasha jiko na kuanza kutengeneza chakula.
“ Ninamshukuru sana Mathew kwa kuniweka huru kasi hiki.Nitafurahi sana kama nikiendelea kukaa hapa kwake siku zote.Ninahisi amani sana nikiwa ndani ya numba hii.Mathew ni mtu mzuri na ana moyo wa huruma.Hata watu anaofanya nao kazi vile vile ni watu wazuri sana.” Akawaza Naomi na mara akamkmbuka Elibariki
“He’s so handsome…sijui kwa nini ametokea kunivutia sana yule jaji...Nitajitahidi nijenge ukaribu naye..” akaendelea kuwaza Baada ya kama dakika kumi na tano chakula kikawa tayari akabeba sahani mbili na kwenda nazo sebuleni.
‘” jaji karibu chakula” akasema “ Wow Naomi kumbe ni mpishi mzuri .Chakula kinanukia sana.lakini hata hivyo ahsante sina hamu ya kula.” Akasema jaji Elibariki
“ jaji lazima ule chakula ili upate nguvu ya kukabiliana na wakati huu mgumu ulio nao” akasema Naomi
“ Naomi najitahidi sana kujilazimisha lakini chakula hakipiti.” Akasema Elibarii
“ sawa jaji naomba nikulishe mimi kwa mkono wangu kitapita tu”akasema Naomi na kwenda kukaa karibu na jaji Elibariki akachukua kijiko na kumuwekea jaji Elibariki chakula mdomoni.Elibariki akacheka kidogo kisha akasema
“ Ahsante sana Naomi.naomba niendelee kula mwenyewe.” Akasema jaji Elibariki
“ hapana jaji.Kaa utulie .Nataka nihakkishe umekula chakula chote hiki umekimaliza” akasema Naomi na kuendelea na zoezi lake na akahakikisha Elibariki amemaliza chakula chote
“ nashukuru sana mdogo wangu kwa chakula.Bila wewe nisingekuwa na nguvu ya kutia chochote tumboni.”akasema jaji Elibariki. Waliendelea kukaa pale sebuleni wakitazama filamu kisha Naomi akasema
“ Its bored in here.twende tukakae pale katika bwawa la kuogelea” Jaji Elibariki hakupenda kwenda nje lakin Naomi akamshika mkono akamvuta naakakubali kuinuka wakaeleka katika bwawa la kuogelea ,. “ Unajua kuogelea? .” akauliza Naomi
“ ndiyo ninaweza lakini nina muda mrefu sana sijaogelea”
“ Ok let’s swim.” “Not today naom......“ Kabla hajamalizia sentensi yake Naomi akamsukumia Elibariki ndani ya maji naye akajitupia majini na kuzama chini kisha akaibuka na kumfuata Elibariki aliyekuwa amejiegemeza katika kingo za bwawa lile
“ Naomi mbona we mtundu sana.Nimekwambia leo sijisikii kuogelea” akasema jaji Elibariki
“ najua una matatizo jaji hata mimi nina matatizo yangu tenamakubwa tu lakini pamoja na matatizo tuliyonayo ninataka uchangamke na uondoe mawazo.Maisha lazima yaendelee.”akasema Naomi na kumsogelea Elibariki.Wakaangaliana usoni kwa sekunde kadhaa.halafu kiuchokozi akaupeleka mkono wake kunako ikulu ya Elibariki
“ Naomi unafanya nini?
“ Shhhhh !!!.akasema Naomi
“ watu wote hawapo tuko peke yetu hakuna ubaya kama tukistarehe nakupunguza mawazo tuliyo nayo.” Akasema Naomi huku akiendelea kumchezea Elibariki maungoni

TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………….
 
Back
Top Bottom