PENIELA SEASON 3
SEHEMU YA 19
ILIPOISHIA SEHEMU ILYOPITA
“ hata kama tukikubali matakwa yake how are we going to do it? Anataka hati ya inga iliyosainiwa na rais,tutafanyaje kuweza kuipata hati hiyo?
“ Hilo ni suala dogo kwangu.Kama ukikubali niachie mimi kila kitu nitakifanya.” akasema peniela
“ How are you going to do it? Rais yuko nje ya nchi hivi sasa na wakati huo huo ana msiba wa mwanae na sisi tunahitaj taarifa toka kwa Rose haraka iwezekanavyo na kingine hatakiwi kabisa kufahamu kuhus kinachoendelea ..I’m confused !! akasema mathew
“ Leave everything to me Mathew.Ninajua nitakavyofanya na rais atasaini hati hiyo” akasema peniela
“ sawa peniela nimekubali kwa sababu yako lakini roho inaniuma sana kumuacha mtu huyu anayeshirikiana na magaidi aondoke….”akasema Mathew na kisha wakarejea chumbani kwa Rose “ Ok Rose.I accept the deal” akasema Mathew “ Good..”akajibu Rose
ENDELEA…………………….
“ Suala lako litashughulikiwa na litakapokuwa tayari hati hiyo unayoitaka italetwa hapa.Lakini wakati tunasubiri hilo lifanyike,nataka unipe maelezo ya kuhusiana na huyu mtu Hasheem Abdulah ni nani ? akauliza Mathew
“ Save your breath ..Siwezi kukwambia kitu chochote bila ya kuona kile ninachokihitaji.And please find me a doctor immediately umeniumiza sana.!! Akasema kwa ukali Vicky.Peniela akamtazama Mathew na kusema “ Mathew she can’t tell us anything.” Mathew akamtazama Rose kwa hasira na kusema
“ I’ll be right back.” “ Tafadhali naomba mnifungue hizi pingu mlizonifunga “ akafoka Rose huku akilia Mathew na Anitha wakatoka mle chumbani na kumuacha Rose akilia kwa maumivu wakarejea ofisini walikokuwapo Anitha na jaji Elibariki
“ Amesema chochote? Akauliza jaji Elibariki
“ hapana hajasema chochote but we made a deal with her ”
“ a deal ? akauliza Elibariki kwa mshangao
“ Yes .Tumefanya makubaliano naye ili atueleze mamboya muhimu anayoyafahamu kuhusiana na habib na mtandao wake wa kgaidi.Hakuna namna tunayoweza kumfanya akatupa taarifa hizo zaidi ya kukubaliana na anachokitaka.”akasema Mathew
“ Anataka nni? Akauliza Elibariki ambaye hakuonekana kufurahishwa na kitendo kile cha Mathew kufanya makubaliano na Rose.
“ Anataka hati ya kinga ya kutokushtakiwa kwa kosa lolote iliyosaiwa na rais, na vile vile anataka apelekwe katika nchi anayoitaka pamoja na ulinzi.”
“ That’s impossible.We can’t do that” akasema jaji Elibariki
“ Elibariki hatuna namna nyingine ya kufanya zaidi ya kumtimizia matakwa yake ili aweze kutupa taarifa za muhimu sana.” Akasema Peniela
“ hata kama ana taarifa za muhimu lakini huyu mama anashirikiana na magaidi na anazifahamu siri zao nyingi ,we cant just let her go like that..Anatakiwa ateswe na atasema ukweli”
“ Elibariki,jambo tulilolifanya halikuwa rahisi hata kwangu mimi .Rose anashirikiana na magaidi na tayari amekwisha pata ujasiri wa kigaidi wa kutokusema chochote hata akiteswa vipi.Siku zote magaidi wako tayari kufa kuliko kusema chochote.Hata tukitumia njia gani Rose hataweza kusema chochote.Njia pekee ya kupata taarifa toka kwa Rose ni kumtimizia kile anachokitaka.”
“ how are we going to do that? Tutaipataje hiyo hati iliyosainiwa ana rais? Akauliza jaji Elibariki
“ I’ll do that “ akajibu Peniela.Jaji Elibariki akamgeukia na kumkodolea macho “ Peniela hili si suala dogo kama unavyolichukulia..Hili ni suala kubwa na hawezi kulifanya yeye mwenyewe ,atashirikishwa pia mwanasheria mkuu naye alifahamu suala hili na aweke sahihi yake.Endapo jambo hili likifika huko kote halitakuwa siri tena.Kila kitu kitakuwa wazi na chochote tunachokifanya.” Akasema jaji Elibariki
“ Kwa hiyo jaji Elibariki wewe ndiye mjuzi wa sheria hapa unatushauri tufanye nini? Akauliza Mathew.
“ Mimi kwa ushauri wangu ni kwamba suala hili la Rosemary tuliweke kwanza pembeni kisha tuendelee na suala letu la awali. La kuitafuta package toka kwa Dr Joshua.Tukifanikiwa kuipata package na kupata ushahidi unaojitosheleza wa kutuwezesha kumuangusha Dr Joshua tutapata nafasi ya kuonana na mtu atakayeshika nafasi ya urais na atatusadia katika kulifanikisha suala hilo.lakini kwa sasa ninashauri kwanba tusichanganye mambo mengi kwa wakati mmoja tutajikuta tumekwama.” Akasema jaji Elibariki
“ Elibariki anaweza kuwa sahihi..Tuliweke pembeni suala hili la Rosemary.Tuendelee kumshikilia Rosemary na kuhakikisha anakuwa chini ya ulinzi mkali hadi hapo tutakapolifanikisha kwanza suala la kuipata package.”
“ Rosemary kwa sasa lzima atakuwa anasakwa kial kona na vyombo vya usalama. kuendelea kumuweka hapa kwa muda mrefu inawezakuwa ni hatari kubwa kwa usalama wetu.Wewe mwenyewe umetuhakikishia kwamba watu uliokutana nao waliokuwa wakifuatilia taarifa za kile kifaa tulichokigundua mwilini mwa Rose ni watu wa usalama wa taifa basi ni wasi kuna juhudi kubwa sana zinafanyika kuweza kumpata Rose..Tukisema tusubiri mpaka hapo tutakapokamilisha kwanza suala la kuipata package toka kwa Dr Joshua tunaweza tukajikuta tumempoteza na tukashindwa kupata taarifa za muhimu toka kwake.Guys let us finish this once and for all..” akashauri Peniela
“ Nakubaliana nawe Peniela kwamba watu wa Rosemary kwa sasa hawalali wakimtafuta na leo hii nusura wangeweza kumfikia kama tusingefanikiwa kugundua kifaa kile cha kuonyesha kila mahala alipo .Hata hivyo nadhani tukubaliane na jaji Elibariki kwamba tuliweke pebeni kwanza suala la Rosemary na tuendelee na mipango yetu ya awwali ya kuipata package toka kwa Dr Joshua.Kuhusu usalama wa Rosemary naoba niwatoe wasiwasi kwamba hapa kwangu kuna sehemu salama kabisa ambayo hakuna mtu anayeifahamu na tutamuweka huko na atakuwa salama hadi hapo tutakapokuwa tayari kulishughulikia suala lake”akasema Mathew
“ Damn you Mathew umejiandaa sana katika jumba lako hili.Umekamilika kwa kila kiru” Akasema Peniela
“ Ninafahamu ugumu wa kazi zangu na ndiyo maan nikajitahidi kujikamilisha kwa kila kitu.Tukiachana na hayo kuna kitu kingine ambacho tunatakiwa tukijadili..Rosemary alikuwa anashirikiana na Captain Amos na walikuwa katika mpango wa kuipata package kutoka kwa Dr Joshua.kwa sasa Captain Amos amefariki na Rosemary tunaye hapa kwa maana hiyo mipango yao yote kuhusiana na Package imevurugika.Tumegundua pia kwamba Captain Amos alikuwa ana mawasiliano na Deus Mkozumi rais wa zamani wa Tanzania na ambaye alikuwa ni mume wa Rose.Katika maelezo yake kabla hajapigwa risasi alimueleza Peniela kwamba wana mpango mkubwa unaomuhusu Peniela na jaji Elibariki kwa maana hiyo basi ninashawishika kuamini kwamba Deus Mkozumi atakuwa akifahamu mpango huu aliousema Amos.Inaonekana wazi kwamba huku nako kuna mtandao mwingine .Mkumbuke pia kwamba Dr Joshua alimtaja Deus kama mmoja wa watu ambao ni maadui wakubwa katika kufanikisha uuzwaji wa hiyo package kwa maana hiyo Dues atakuwa akilifahamu vyema sana suala hili.Nadhani ni wakati muafaka sasa wa kumtafuta mzee huyu na kufahamu mambo mengi kutoka kwake” akasema Mathew
“ Deus Mkozumi ni rais mstaafu,ana ulimzi mkali kila aendapo na nyumbani kwake pia,kumpata mtu kama huyu haliwezi kuwa jambo rahisi hata kidogo.Huyu naye ana mtandao mkubwa wa watu wenye nguvu na hatari na wana mipango mikubwa juu yetu kwa hiyo si watu wa kuwafuata kirahisi rahisi.” Akasema jaji Elibariki
“ Ni kweli kumpata Deus Mkozumi si rahisi lakini jambo hili haliwezi kutushinda.Tunaweza kumpata”akasema Mathew
“ Tutampataje Deus?akauliza jaji Elibarii.Mathew akamgeukia Peniela
“ No ! Mathew we cant use her ..”akasema Elibariki “ Hatuna namna nyingine ya kufanya Elibariki ili kumpata Deus zaidi ya kumtumia Peniela.” Akasema Mathew
“ Mathew ,we cant put her at risk again.Peniela amenusurika leo hii katika shambulio,I’ve lost my wife today,and I cant lose Peniela again” akasema jaji Elibariki.Mathew akamtazama na kusema
“ Eli Can we talk outside?Wakatoka nje ya kile chumba
“ Elibariki tuko kati kati ya vita.Tunatakiwa tutumie kila aina ya mbinu na silaha tulizonazo katika kupambana.Wewe na Peniela kuna mipango inapangwa juu yenu na kikundi cha watu ambao wanawafuatilia.Maisha yenu yako hatarini kwani hatufahamu watu hao wana mipango gani juu yenu.Kwa hali halisi ilivyo ni wazi kwamba hatuwezi kumfikia Deus Mkozumi isipokuwa kwa kumtumia Peniela Pekee.She can penetrate any where.She’s good at this.She was trained for this .Kwa hiyo usiwe na wasiwasi hata kidogo kuhusu usalama wake..Kitu kingine nafahamu unampenda sana Peniela lakini tunapokuwa katika kazi kama hizi ,masuala ya mapenzi tunayaweka pembeni na hutakiwi kabisa kuonyesha hisia zako hata kama unampenda mtu yeyote .Peniela mwenyewe yuko tayari kuifanya kazi yoyote ile na haogopi lakini kitendo ulichokifanya cha kuingilia kati na kumzuia kwamba asishirikishwe katika kumtafuta Deus kimemshangaza hata yeye pia.Wanawake wale mle ndani wanatutegemea sisi kuwaongoza katika kulimaliza suala hili lakini kama tutashindwa kuonyesha namna bora ya kufanya maamuzi tutawavunja moyo kwani tayari wamekwisha jitoa maisha yao katika kuhakikisha tunalifanikisha jambo hili.” Akasema Mathew
“ Mathew I’m sorry kama nilikukwaza kwa kauli ile lakini nilijikuta nikishindwa kujizuia .Ninampenda sana Peniela na tukio lililotokea mchana alipokwenda kuonana na Amos lilinistua na kuniogopesha sana .Please forgive me and lets do what needs to be done” akasema jaji Elibariki
“ Are we good? Akauliza Mathew
“ We’re good”akajibu jaji Elibariki kisha wakarejea tena ndani ya ofisi
“ Are you guys ok? Akauliza Peniela
“ we’re fine.”akajibu jaji Elibariki
“ kwa hiyo nini kinachoendela saa hivi? Akauliza Peniela
“ Kitu kinachotakiwa kufanyka kwa sasa ni kumtafuta Deus Mkozumi.Yeye anafahamu mambo mengi sana na kama tukimpata basi atatusaidia kupiga hatua kubwa.Peniela utaifanya hii kazi.You will go meet Deus Mkozumi” akasema Mathew
“ Ni jinsi gani ataonana na Deus? Akauliza jaji Elibariki
“ Usihofu Elibariki,they call me an insect because I can penetrate anywhere. Kwa kuwa namba za simu za Deus tunazo hapa,I’ll call him and set a meeting.Kuhusu nitakwenda kuongea naye nini hilo ni nyie mtapanga.”akasema Peniela
“ say something Anitha “akasema Mathew
“ Peniela atakapokwenda kuonana na Deus tutamuwekea kifaa cha mawasiliano sikioni .Atavaa gauni la rangi nyeusi na sehemu ya kifuani katika titi la kulia tutaweka ua jeusi na ndani ya ua hilo kutakuwa na kamera ndogo ambayo itatuwezesha sisi kutazama kila kitu kinachoendelea kati yako na Deus.Tutayafuatilia maongezi yenu na tutakuwa tunakueleza nini cha kufanya.Endapo tutaona kama kuna tatizo lolote la kiusalama tutakutaarifu “ akasema Anitha
“ Hata hivyo hatutakuwa mbali na mahala utakapokuwa kwa ajiki ya msaada wa dharura pindi ukihitajika” akasema Mathew
“ Ok guys.muda umekwenda sana Nipeni namba za Deus nimpigie.”akasemaPeniela.Anitha akaziandika namba za simu za Deus katika simu yake halafu akapiga kisha akampatia Peniela akaiweka simu sikioni
“ hallow”ikasema sauti nzito ya kiume upande wa pili “hallow” akasema peniela
“naongea na nani? “ Unaongea na Peniela hapa.Naongea na nani?akauliza Peniela
“Kwani wewe umempigia nani? Akauliza tena Yule jamaa upande wa pili
“ Ninahitaji kuongea na Mr Deus Mkozumi tafadhali.” Kimya kifupi kikapita halafu yule jamaa akauliza
“ Umeipata wapi hii namba? Nani kakupatia namba hii?
“ It doesn’t matter nimeipata wapi ila kama Deus yupo ninaomba niongee naye“ akasemaPeniela.Kikapita kima kifupi tena Yule jamaa akauliza
“ Umesema unaitwa nani vile?
“Peniela.mwambie Peniela anahitaji kuongea naye” Baada ya dakika mbili Peniela akasikia sauti nyingine ambayo haikuwa nzito sana kama ile ya mwanzo
“ Hallow” ikasema sauti ile
“Hallow”akasemaPeniela
“ Are you Peniela?
“ Yes I am Peniela.Are you Deus Mkozumi? Akauliza Peniela
“ Yes Iam Deus..Umeipata wapi namba hii? Akauliza Deus
“ Mzee Deus nina shida na wewe ndiyo maana nikaitafuta namba hii hadi nikaipata.”
“ Una shida na mimi ! Shida gani hiyo?akauliza Deus “ Siwezi kukueleza simuni mzee.Nahitaji kuonana nawe tuongee”
“Peniela ,ingekuwa vizuri ungenieleza suala ambalo unataka tukune tuliongelee ili niweze kupima na kuona kama lina uzito gani.Unajua mimi ni mtu mwenye shughuli nyingi kwa hiyo kama ukitaka kuonana na mimi lazima nivunje baadhi ya mipango yangu kwa hiyo naomba unieleze ili nipate walau picha.”
“ Deus ninafahamu wewe ni mtu mwenye shughuli nyingi lakini hadi nimeamua kukupigia basi fahamu suala lenyewe ni kubwa hivyo naomba usilipuuzie tafadhali.Nahitaji sana kuonana nawe” Kikapita kimya kifupi kisha Deus akauliza
“ Unataka tuonane lini na wapi?
“ Tuonane leo hii jioni kuanzia saa mbili za usiku..Kuhusu mahala pa kukutana utaamua wewe mwenyewe tukutane wapi mahala ambako unaamini ni salama.”akasema Peniela.Baada ya sekunde kadhaa Deus akasema
“ Tukutane Iyumba country club saa mbili kamili. Katika geti la kuingilia jitambulishe kama mgeni wa namba ishirini na saba utapelekwa mahala nitakapokuwepo.Ila hakikisha kwamba jambo unalotaka kunieleza ni jambo kubwa .”
“ Ahsante sana mzee.Nitafika mida hiyo bila kukosa “akasema Peniela na kukata simu.
“ Good.You did great! Akasema Mathew
“ Deus hajaonyesha kustushwa kabisa na ulivyompigia simu na hii inadhihirisha wazi maneno ya Amos kwamba they know you already .Ok hatua muda mwingi sana hivyo maandalizi yaanze mara moja.Anitha anza kuandaa program zako halafu ukamchagulie Peniela gauni zuri la kuvaa usiku wa leo .”
“ Anitha ninaomba simu niwasiliane na josh kumpa taarifa kwamba sintakuwepo jioni ya leo.Nina hakika watakuwa wamenitafuta sana mpaka mida hii kwani hata simu yangu nimeizima kabisa ili wasiweze kujua mahala niliko” akasema Peniela akachukua simu na kumpigia Josh “hallow Josh.Its me Peniela” akasema peniela baada ya Josh kupokea simu “ peniela where are you? Kila kitu kimesimama hapa hawa watu wanakusubiri wewe.wanahaha wanakutafuta lakini hakuna anayejua uko wapi na simu yako umeizima kabisa.Tafadhali naomba uje hapa mara moja ili taratibu za msiba wa John ziweze kufanyika”akasema Josh
“Josh I cant come right now.I’m at the middle of something.” Akasema Peniela “kwa hiyo itakuwaje?akauliza Josh
“waambie nimekupigia simu na nimekutaarifu kwamba sintaweza kufika leo tuonane kesho”akasema peniela
‘ Ok peniela ngoja niwataarifu”akasema Josh na kukata simu
“kwema huko? Hakuna tatizo lolote?
“ hakuna tatizo ila kila kitu kimesimama wananisubiri mimi ili tuweze kupanga kuhusiana na suala la msiba wa John.” “ sawa utalishughulikia suala hilo kesho lakini kwa leo lazima tushughulikie kwanza suala la Deus.”akasema Mathew kisha akageuka kutaka kutoka mle ofisnini lakini Anitha akamuita.
“Kuna simu inapigwa katika namba ya Dr Kigomba.Inaonyesha ni simu kutoka afrika ya kusini.Yawezekana akawa ni Dr Joshua”akasema Anitha na wote wakatega sikio kusikia simu ile.
“ hallow Mr President”akasema Dr Kigomba
“ Kigomba nipe taarifa za huko.mambo yanakwendaje? Akauliza Dr Joshua “Huku kila kitu kinakwnda vizuri.Maandalizi yanaendelea.Vipi ninyi huko?
“ Huku hakuna habari mpya .Nimekupigia ili kufahamu umefikia wapi na maandalizi ya msiba”
“Kila kitu kimekwenda vizuri na tayari shughuli zinaendelea pale katika nyumba ya familia.Taarifa zimesambaa haraka sana na mpaka hivi sasa waombolezaji ni wengi mno.Kifo hiki cha Flaviana kimewagusa watu wengi sana na ndiyo maana wamejitokeza kwa wingi namna hii ndani ya muda mfupi.”akasema Dr Kigomba
“ kwa kweli kifo cha Flaviana kinaumiza sana na hata mimi kimeniumiza sana lakini yote hii ni katika kuhakikisha kwamba mpango wetu unafanikiwa.Anyway tuachane na hayo tutajadili kwa undani nikirejea.Tutawasili na mwili esho saa tano asubuhi.Watangazie.”akasema Dr Joshua.
“ Sawa Mr President.Tumekwisha fahamishwa hilo na mwenyekiti wa kamati ya mazishi na kila kitu kwa ajili ya kuupokea mwili kimeandaliwa...”
“ sawa Kigomba sina mengi ya kukwambia kwa sasa ila tutaongea mambo mengi nikishafika huko kesho.Ila nimeongea na Hussein atafika kesho saa mbili za usiku tayari kwa kuuchukua mzigo wake.Nataka tulimalize suala hili ili maisha mengine yaendelee.Nimechoshwa na kuwapoteza watu wangu kila kukicha kwa sababu ya biashara hii.Nitakupigia baadae Dr KIgomba”
“ Dr Joshua before you go,kuna jambo ambalo sina hakika kama umekwishapata taarifa zake”
“jambo gani?
“ Amos is dead” “Amos is dead? how?Who killed him?
“ Mpaka sasa haijafahamika ni nani lakini inaonyesha aliyemuua is very professional assassin”
“ Mungu wangu ! !!Dr Joshua akastuka
“ tuki hilo limetokea muda gani? Mbona asubuhi ya leo nimewasiliana na Amos ?
“ Tukio limetokea mchana wa leo Mlimba lodge”Zikapita sekunde kadhaa kisha Dr Joshua akasema “Nimestushwa sana Kigomba kwa taarifa hizi.Ngoja nizungumze na mkuu wa polisi nifahamu kama kuna hatua yoyote imefikiwa kuchunguza waliomuua Amos.Kigomba kwa mara ya kwanza nimeogopa sana.Kama Amos ameuawa basi watu walionfaya hivyo wako karibu sana kutufikia na sisi pia.Please make sure hakuna kitu chochote ambacho kinaweza kutuunganisha sisi na Amos.Kigomba this is a very serious matter and take it very seriously.Nitakupigia baada ya masaa mawili kujua kinachoendelea na tutaongea zaidi”
“ sawa Mr President lakini wa mujibu wa taarifa za polisi watu waliofanya mauaji hayo wameondoka na kompyuta na simu ya Amos.” “Kigomba something is going on.Kuna kitu kinatafutwa kwa Amos.We need to hurry.Tunatakiwa tuimalize biashara yetu haraka iwekanavyo .Ntakupigia tena baadae kidogo”akasema Dr Joshua na kukata simu.
PENIELA ATAFANIKIWA KUONANA NA DEUS MKOZUMI? TUKUTANE SEHEMU IJAYO….