Peniela (Story ya kijasusi)

Peniela (Story ya kijasusi)

PENIELA

SEASON 4

EPISODE 1


MTUNZI : PATRICK.CK



ILIPOISHIA SEASON 3


“ Elibariki nakushukuru sana kwa kunitoa usingizini.Sikujua kama nina maadui wakubwa namna hii tena walio karibu kabisa na mimi na ambao wangeweza hata kunimaliza sekund e yoyote .Kuanzia sasa wewe ndiye utakayekuwa mshirika wangu mkuu.I’ll give back to you all that I took from you.Nisaidie tuimalize biashara hii na ninakuahidi kwamba uakuwa ni mtu mkubwa sana. kuna jambo ambalo sikuwa nimelifikiria lakini kwa sasa limekuja akilini.I’ll make you the next president of Tanzania”
Jaji Elibariki alibaki mdomo wazi akimkodolea macho Dr Joshua asiamini kile alichoambiwa.

“ Umesema nini mzee? akauliza
“ kwa mambo uliyonifanyia jaji umenifanya nikuthamini ghafla kuliko watu wote kwani bila wewe ningeendelea na mipango yangu yote bila kufahamau chochote na mwisho wangu ungekuwa ni wa aibu kubwa.Ni wewe ambaye nilikuwa nimekuweka katika kundi la adui zangu wakubwa lakini ndiye umekuja na kunifumbua macho.kwa hili ulilolifanya nimesema kwamba nitakufanyia kitu ambacho sikuwa nimekusudia kukifanya.Nitakufanya uwe rais wa jamhuri ya muunganowa Tanzania.” Akasema Dr Joshua.jaji Elibarki machozi ya furaha yakamdondoka.

“ is this true Dr Joshua?
“ Ndiyo Elibarik.Uwezo huo ninao na nitafanya hivyo na hakuna anayeweza kunizuia kufanya hivyo.I’ll make you a very powerfull man in this country na nina hakikani wewe ambaye utaweza kuendelea kuyalinda maslahi yangu.Nilikuwa nafikiria sana ni nani ambaye ninaweza nikampa nchi na akaendelea kuyalinda maslahi yangu lakini nashukuru nimekupata wewe.Nina hakika wewe ni mtu sahihi kabisa na unafaa.”Akasema Dr Joshua.Jaji Elibariki akainuka na kwenda kumpa mkono akamshukuru

“ Dr Joshua sikuwahi kufikiri kuhusu jambo kama hili ! akasema kwa furaha jaji Elbariki
“kwa hiyo kama halikuwa katika ndoto zako anza sasa kuota kwamba umekuwa rais wa Tanzania kwani jambo hili linakwenda kutimia.Nitakuelekeza nini cha kufanya muda utakapofika lakini lazima ukae ukijua kwamba wewe ndiye utakayekuwa rais wa Tanzania baada ya mimi kuondoka madarakani.Lakini pamoja na hayo kuna jambo nataka nikuombe”

“Jambo gani Dr Joshua?
“ Samahani lakini kwa kulisema hili kabla hata hatujamzika Flaviana mkeo lakini ni ukweli ulio wazi kwamba Kwa sasa baada ya Falivana kututoka utabaki mwenyewe na kwa kuwa bado kijana lazima utaoa tena lakini mimi lengo langu kubwa ni kutaka familia yangu iendelee kukaa katika neema ya uongozi kwahiyo basi ninakutaka ujenge mazoea ya karibu na Anna mbaye naye kwa sasa yuko mwenyewe baada ya mpenziwake kufariki.Ninajua umenielewa ninaposema hivyo kwani ninataka utakapokuwa rais yeye awe ni mke wa rais na familia yetu iendelee kutawala.Unalionaje wazo hili? Akauliza Dr Joshua
“ Hilo ni wazo zuri Dr Joshua lakini naomba uniachie kwanza jambo hilo nilitafakari na kulifanyia kazi na nitakupa majibu”akasema Elibarik,.Dr Joshua akafungua mlango na kumuita msaidizi wake akamuomba amuite Dr Kigomba ambaye alifika mara moja .Dr Joshaua akamuangalia kwa macho makali kwa sekunde kadhaa kisha akasema
‘ Kigomba give me your phone” .Huku akishangaa Dr Kigomba akachukua simu yake na kumpatia Dr Joshua.

” Kuanzia sasa hautaitumia simu hii utatafuta simu nyingine.Vua na hiyo saa mkononi”akaamuru Dr Joshua
“ Dr Joshua whats going on? Akauliza Dr Kigomba kwa wasiwasi.

“ Kigomba nadhani umekwisha fahamu nini kinaendelea.Nilikupa kazi ya kumchunguza peniela na badala yake ukaanzisha mahusiano naye.Ulifanya kosa kubwa sana Kigomba”
“ Nani kakueleza habarihizo dr Joshua?
“ Kigomba tayari ninafahamu kila kitu kwa hiyo hakuna haja ya mabishano. Siku zote nimekuwa nkikuonya kuhusiana na udhaifu wako kwa wanawake lakini hukutaka kunisikia.”
“ Dr Joshua sikuelewi una maanisha nini” akasema Dr Kigomba.Dr Joshua akamtazama kwa macho makali na kusema
“ Kigomba unafahamu Peniela ni nani? Unafahamu ni kitu gani alichotufanyia kupitia kwako?
“ hapana Mr President.”akajibu Dr Kigomba

“ Peniela ni nyoka mkubwa na tayari ameunganisha simu yako katika program yao na wanasikia kila kitu unachokiongea kupitia simu yako.Kama hiyo haitoshi alikupa saa hii kama zawadi uivae lakini kwa taarifa yako saa hii imefungwa kifaa maalum ambacho kina uwezo wa kuwaonyesha kila mahala ulipo.Tumshukuru sana Elibariki ambaye ametufumbua macho na kama si yeye tusingeweza kujua chochote kinachoendelea” akasema Dr Joshua.Kigomba alibaki kimya akiwatazama.
“ I’m sorry Mr President,sikuwa ninafahamu lolote kuhusiana na alichokifanya Peniela.” Akasema Dr Kigomba

“ Kigomba mimi na wewe tutakuwa na maongezi yetu baadae lakini kwa sasa naomba nikufahamishe kwamba mipango yetu yote imekwisha gundulika na kama tusipochukua hatua za tahadhari angali bado mapema basi hatutaweza kufanikiwa.Cha kwanza tunachotakiw a kukifanya ni kumuhamisha kwa siri Hussein na ujumbe wake mapema kesho asubuhi na kesho hiyo hiyo jioni kila kitu kikamilike na Hussein aondoke nchini haraka na baada ya hapo tutaendelea na zoezi la kumsaka mtu aitwaye Mathew ambaye huyu ndiye adui yetu mkubwa sana kwa sasa.”akasema Dr Joshua

“Mr President ninaomba niuliz……………”Dr Kigomba akataka kuuliza swali lakini Dr Joshua akamzuia
“ Kigomba hakuna muda wa maswali sasa hivi.Anza sasa hivi kushughulikia hoteli ya kuwahamisha Hussein na ujumbe wake.Tutaongea baada ya mambo yote kukamilika” Akasema Dr Joshua na Dr Kigomba akatoka mle chumbani
Jaji Elibarikina Dr Joshua waliendelea na maongezi na ilipotimu saa tisa za usiku wakaagana.
“ Nenda kalale jaji kesho tuna siku ndefu sana.Kesho tutamzika Flaviana na kisha tutaendelea na mchakato mwingine.Tutaongea zaidi kesho lakini nakushukuru sana jaji.” Akasema Dr Joshua na kumuongoza jaji Elibariki kuelekea katika chumba maalum cha wageni

ENDELEA SEASON 4


Dr Joshua akarejea sebuleni kwake na kuketi sofani akavuta pumzi ndefu halafu akavua koti na kulegeza tai .Alihisi joto .Mambo aliyoelezwa na jaji Elibariki yalimchanganya mno.

“ I’m confused .Totaly confused !!!.... akawaza na kuinuka akaenda katika kabati kulimokuwa na chupa kadhaa za pombe kali akachukua moja akamimina katika glasi akagugumia yote na kukunja sura kutokana na ukali wa pombe ile,halafu akaenda moja kwa moja chumbani kwake ,akavua tai na kuitupa kitandani akasimama kwa sekunde kadhaa akionekana kujawa na mawazo mengi mara ghafla akaibinua m eza kwa hasira na kumwaga kila kilichokiwa juu yake
“ Aaaagghhhh…!!!!” akapiga ukulele kwa hasira huku akihema mfululizo,na uso wake ukiwa umeloa jasho.Mara mlango wake ukagongwa kwa nguvu akainuka na kwenda kuufungua akakutana na sura zenye wasi wasi za walinzi wake.

“ Is everything ok Mr President?..akauliza mmoja wao.
“ I’m fine guys..I’m ok dont worry” akajibu Dr Joshua
“ Are you sure Mr President?

“ Vijana nimewaambia I’m ok..Nimekunywa kidogo pombe kali ili kuondoa mawazo ya kifo cha mwanangu mpendwa .Msijali vijana wangu I’m fine ,so if you’ll excuse me I n eed to be alone” akasema Dr Joshua na kuufunga mlango wake akaketi sofani na kuinamisha kichwa akaweka mikono kichwani
“ Mambo aliyonieleza jaji Elibariki ni mazito na magumu kuyaamini lakini kwa namna alivyonieleza nalazimika niamini ila nimestushwa mno kusikia eti Peniela ametumwa kwangu na kikundi kiitwacho Team SC41 kwa lengo la kunichunguza na kuhakikisha wanakipata kirusi Aby” akawaza na kuivuta akilini sura ya Peniela

“ Hivi kweli Peniela anaweza akanifanyia hivi alivyosema Elibariki ? Sura yake ya kimalaika iliyojaa mahaba haionyeshi kabisa kama ni msichana anayeweza kufanya hayo aliyoyasema Elibariki.Peniela ni mwananmke nnayempenda mno ,tayari ameniin gia katika kila mshipa wa mwili wangu na ndiyo maana inaniwia ugumu sana kuamini maneno aliyoyasema Elibariki juu yake.” Kichwa cha Dr Joshua kikaendelea kuuma kwa mawazo mengi .Akayakumbuka maneno fulani aliyoambiwa na jaji Elibariki
“ Peniela ambaye umekuwa ukimuona kama malaika wako hakupendi hata chembe na ndiye anayeongoza mipango yote ya kukuangamiza.Anatumiwa na Team Sc41 ambao nio waliompa mafunzo na wakamuunganisha kwako makusudi kabisa wakimtumia Captain Amos.Walikuwa na lengo moja tu la kukipata kirusi Aby.Nakuhakikishia tena mheshimiwa rais kwamba Peniela ni mwanamke hatari sana ambaye hana mapenzi yoyote kwako bali anatumiwa kukumaliza.Kama huamini hiki ninachokwambia usichukue hatua zozote na utaona kitakachotokea.Peniela ni nyoka mwenye sumu kali ,anautumia uzuri wake ili kupata kile ambacho yeye na team yake wanakitaka kwa manufaa yao.Amekuwa akiwalaghai kimapenzi watu mbali mbali na mmoja wao ni katibu wako Dr Kigomba”
Dr Joshua akahisi kama vile kichwa kinapigwa na kitu kizito alipoyakumbuka maneno haya ya jaji Elibariki

“ Natamani nisimuamini Elibariki lakini kwa mambo aliyonieleza yananilazimisha nimuamini.Kwanza ni kweli nilimpata Peniela kwa kumpitia Captain Amos.Hakuna aliyekuwa analifahamu hili zaidi yangu na Amos.Kwa Elibariki kulifahamu hili ananilazimisha niamini kuwa kile anachokisema kinaweza kuwa kweli.Kitu kingine ni kuhusu Peniela na Kigomba kuwa katika mahusiano.Sikuwa nikilifahamu hili lakini Elibariki amenifumbua macho na hata Kigomba ameshindwa kukataa mbele yangu kwamba ana mahusiano na Peniela.Kitendo cha kufuatilia mawasiliano ya Kigomba na kujua nyendo zake zote kinanifanya niamini yale aliyonieleza Elibariki yanaweza kuwa kweli.Ni wazi Peniela anahusika katika jambo hili na kama alivyosema Elibariki ni kwamba Peniela anatumia uzuri wake kufanikisha mambo yake.Oh !! Peniela ..Peniela !! Why she did this to me?!! Alinipofusha kwa penzi lake zito nikajiona nimepata malaika kumbe niko na shetani mtoa roho.I’m so stupid to trust her that much.Kwa nini sikuwa mwangalifu na kuligundua hili toka mapema?..Dr Joshua akauma meno kwa hasira

“ Sijui nitampa nini jaji Elibariki kwa jambo hili kubwa alilonifanyia la kuwasaliti wenzake na kuja kunipa siri hizi ambazo zimenitoa katika usingizi mzito ulionifanya nisijtambue kwa kufunikwa na blanketi la penzi la Peniela.Kumbe nilikuwa najikaanga mwenyewe na mafuta yangu bila kujua.Hayakuwa maamuzi mepesi kuwasaliti wenzake na kuja kwangu na kwa hili I must reward him na zawadi kubwa kuliko zote ambayo naweza kumpatia ni kumfanya awe rais ajaye wa Tanzania.” Akasimama na kuzunguka zunguka mle chumbani

“ Yes ! I will make him a president of Tanzania.Uwezo huo ninao na Elibariki anafaa kabisa.Anaweza akakalia kiti vizuri na zaidi ya yote atakuwa anafuata yale yote nitakayokuwa namuelekeza.Hata kama kuna mambo mengi mabaya nimeyafanya wakati wa uongozi wangu akija mtu kama Elibariki atayafukia yote na nitaendelea kukaa kwa amani na salama nikitumia utajiri wangu.” Akaendelea kuwaza Dr Joshua halafu akamkumbuka Peniela
“ Oh Peniela sijui nikufanye nini pindi nikikuweka mikononi mwangu lakini pamoja na yote uliyonifanyia bado taswira yako imekitawala kichwa changu.Ninahisi yawezekana akawa anatumia uchawi kwani sijawahi kuchanganyikiwa kwa mwanaume yeyote kama alivyonichanganya Peniela namna hii.Ninamuwaza kila dakika japokuwa bado ninahasira naye..” akawaza Dr Joshua na kuanza kukumbuka namna alivyokutana na Peniela



2012 JOHANNESBURG – AFRIKA YA KUSINI


Mkutano mkubwa wa siku sita wa kujadili athari za mabadiliko ya tabia nchi kwa nchi masikini duniani ulikuwa unafanyika katika jiji la Johannesburg Afrika ya kusini.Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo uliongozwa na rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr Joshua ambaye alitarajiwa kutoa hotuba katika mkutano huo.
Akiwa jijini Johannesburg Dr Joshua alifikia katika hoteli ya kifahari ijulikanayo k ama four season hotel
Kazi ya kwanza aliyoifanya Dr Joshua akwa jijini Johannesburg ni kukutana na jumuia ya watanzania waishio nchini Afrika ya kusini Katika mkutano na wanajumuiya hao Dr Joshua aliwaasa wakumbuke kuwekeza nyumbani na vile vile kuzingatia sheria za nchi wanakoishi.Kwa upande wao watanzania waishio afrika ya kusini walimueleza rais changamoto wanazokutana nazo nchini afrika ya kusini ambazo rais aliwaahidi kuzifikisha sehemu husika ili zipatiwe majibu.Baada ya mkutano kumalizika Dr Joshua akaondoka akarejea hotelini alikofikia.
Tayari ilikwisha timu saa kumi na moja jioni.
Akiwa chumbani kwake amejipumzisha,Captain Amos daktari wa familia ya rais akaingia

“ Hallow Mr President” Amos akamsabahi Rais
“ Hallow Amos” akasema Dr Joshua .Captain Amos akaiendea chupa ya mvinyo mezani na kumimina katika glasi mbili akampatia moja Dr Joshua

“ Maneno uliyoyaongea katika kikao chako na wanajumuiya ya watanzania waishio afrika ya kusini yamewagusa sana na kwa namna walivyoguswa nina imani yale yote uliyowaeleza watayafanyia kazi.” Akasema Captain Amos
“ Niliona niwakumbushe umuhimu wa kuwekeza nyumbani na kuijenga nchi yao .Wengi wao wakiwa huku nje ya nchi husahau kabisa kwao.Tuachane na hayo, mambo yanakwendaje? Have you found me something? I’m getting bored in here”

“ Tena ni hilo lililonileta kwako mheshimiwa” akasema Amos na kumfanya Dr Joshua atabasamu

“ Tell me the good news Amos” akasema Dr Joshua
“ Good news is that I’ve found you something very special.Utakubaliana nami utakapomuona” akasema Amos
“ Nakuamini Amos.Ukimsifia mwanamke namna hiyo basi ni kifaa hasa.Tell me who is she?
Captain Amos akanywa funda moja la mvinyo na kusema

“ Her name is Peniela.Ni mtanzania ambaye amekuja Afrika ya kusini kibiashara .Anamiliki maduka makubwa mawili ya nguo na urembo.Nakuhakikishia Mr President she’s an angel.Hadhi yake ni ya juu mno .Naamini hata wewe ukimtia machoni utakubaliana nami”
“ Unafahamiana naye? Unamuamini? Unajua sitaki mtu ambaye anaweza kuwa kidomo domo .Si unajua hawa wanawake ikitokea akatembea na rais basi huanzisha matangazo ili ajulikane kila mtaa kuwa anatoka na rais wa nchi”

“ Usihofu kabisa kuhusu hilo mzee.Peniela ni mwanamke ninayefahamiana naye na niamuamini sana.Hana mambo kama hayo ya ajabu ajabu.”

“ Good to hear that then.Nashukuru kwa kunipa uhakika huo.Nakuamini sana Captan na ndiyo maana sijawahi kukuacha katika safari zangu zote za nje ya nchi”

“ Hata mimi nashukuru sana mzee kwa kuniamini na ninatumai sijawahi kukuangusha hata mara moja katika kila kazi unayonipa”
“ Ni kweli Amos hujawahi kuniangusha .Katika safari zote tunazosafiri nje ya nchi umekuwa unaniletea wanawake wazuri wenye hadhi yangu.Nipatapo safari kama hizi za nje ya nchi huwa ni fursa yangu na mimi kujivinjari na watoto wazuri.Kama ujuavyo mama yenu ni mgonjwa sana siku hizi halafu mahaba yamepungua kutokana na umri kwa hiyo ninapokuwa huku nje ninapata nafasi nzuri ya kujivinjari na damu changa.Nashukuru unalifahamu hitaji langu na kila mara umekuwa unaniletea aina ya wanawake ninaowataka” akasema Dr Joshua na Amos akatabasamu

“ Saa tatu za usiku baada ya chakula nitakuwa na maongezi na balozi wetu hapa afika ya kusni kwa hiyo nitamuhitaji Peniela kuanzia saa sita za usiku.Atakapowasili mkabidhi kwa Kareem na yeye atajua namna ya kumleta kwangu” akasema Dr Joshua halafu wakaendelea na maongezi mengne na baada ya muda Amos akaondoka na kumuacha Dr Joshua peke yake.
“ Peniela ..” akasema kwa sauti ndogo huku akitabasamu
“ Jina hili linafanya nijenge taswira ya mwanamke mwenye uzuri zaidi ya tausi.Amos amemsifia sana na kwa sifa zote zile nina hakika uzuri wake utakuwa zaidi ya Cleopatra Yule aliyewahi kuwa mtawala wa Misri ambaye vitabu vinatueleza kwamba alikuwa na uzuri usioelezeka.Halafu kuna kitu nimekuwa nakifikiria kwa muda mrefu.Kadiri siku zinavyozidi kusonga ndivyo mapenzi na mke wangu Flora yanazidi kupungua.Flora hana tena ule mvuto wake wa asili na kutokana na maradh ya moyo yanayomsumbua hana tena ule uwezo wa uweza kuniridhisha kitandani.Japokuwa umri wangu umekwenda lakini bado damu inanichemka na ninao uwezo mkubwa kitandani .Kama ni hivyo basi kwa nini nisitafute mwanamke mzuri mwenye hadhi ambaye atakuwa wangu moja kwa moja? Mwanamke huyo nitakuwa naonana naye kwa siri kila pale ninapokuwa na hamu ya kufanya mapenzi,mwanamke ambaye ataniliwaza na kuniondolea mawazo.Hili niI wazo la msingi na ninatakiwa kulipa uzito wa kipekee.Ngoja nimuone huyo Peniela ni mwanamnke wa aina gani na kama anaweza akanifaa kuwa naye katika mahusiano ya siri.Kama atafanikiwa kuniridhisha na kama ni mwanamke mwenye staha na si wale wanaitwa micharuko basi nitamfanya awe mpenzi wangu wa kudumu.Nitamfanyia mambo makubwa na kufanya aishi maisha ya kifahari “ akawaza Dr Joshua huku akiendelea kupata mvinyo taratibu


SAA SITA USIKU FOUR SEASON HOTEL


Saa sita na dakika saba za usiku gari moja lenye rangi nyeusi likainga katika hoteli ya four seasons .Toka ndani ya gari hilo akashuka daktari wa rais Captain Amos akiwa ameongozana na mwanamke mmoja mwenye uzuri wa kipekee.Alikuwa mwembamba ,mrefu wastani aliyevaa suti nzuri nyeusi iliyomkaa vyema.Moja kwa moja wakaelekea katika chumba cha rais ambako Captain Amos akakamkabidhi Yule mwanamke kwa Kareem mmoja wa walinzi wa rais.
“ Karibu sana Peniela” akasema Kareem baada ya kutambulishwa.Captain Amos akaondoka na Kareem akamuomba Peniela amfuate.Ulinzi ulikuwa mkali na kila aliyepita eneo lile alipokuwa rais alilazimika kusachiwa kwanza lakini Peniela alipita bila wasi wasi kwa kuwa alikuwa ameongozana na mlinzi wa rais Kareem.Katika mlango wa kuingilia chumba cha rais kulikuwa na walinzi ,Kareem akawapa ishara Fulani nao wakaitika kwa ishara halafu akaufunga mlango na kuingia sebuleni.
Dr Joshua alikuwa peke yake mle sebuleni akitazama Luninga,huku pembeni yake kukiwa na chupa ya mvinyo.Akageuza shingo kutazama mtu aliyeingia mle sebuleni .Kwa sekunde kadhaa akabaki ameduwaa akitazama mlangoni ambako alikuwa amesimama mlinzi wake kareem akiwa na Peniela

“ Oh my Gosh !!!..what a beautifull angel..” akanong’ona Dr Joshua huku akimkazia macho peniela.Alistushwa mno na uzuri wake.
“ Amos wa right.Peniela ana uzuri wa kipekee mno.Katika wanawake wote ambao amekuwa ananiletea kila tuwapo nje ya nchi hajawahi kuniletea mwanamke mzuri kama huyu.This is exactly the the type of woman I want.” Akaendelea kuwaza Dr Joshua huku akimkazia macho Peniela
“ Samahani mzee kwa usumbufu,nimekuletea mgeni.Anaitwa Peniela” akasema Kareem halafu akamgeukia Peniela

“ Peniela huyu ni Dr Joshua ,rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.”
Baada ya utambulisho ule Peniela akatembea kwa mwendo wake wa maringo na kumfuata Dr Joshua akamsalimu kwa adabu.

“ Hallo Mr President” akasema huku akitabasamu
“ Hallo Peniela.Karibu sana.Nimefurahi kukuona”
“ Hata mimi nimefurahi kukuona mheshimiwa rais” akasema Peniela ,halafu Dr Joshua akamgeukia Kareem
“ Kareem ahsante kwa kumfikisha mgeni wangu” akasema na Kareem akaondoka zake.Dr Joshua akaenda katika meza iliyosheheni vinywaji mbali mbali
“ Peniela unatumia kinywaji gani? Akauliza .Peniela akatabasamu na kusema
“ anything that you can choose for me” Sauti laini ya Peniela ikazidi kumpagawisha Dr Joshua.Akachukua chupa ya mvinyo na kumimina katika glasi mbili akampatia moja Peniela

“ Karibu sana peniela.Ninafuraha kubwa mno kuwa nawe kwa usiku huu.Amos alinieleza sifa nyingi juu yako na baada ya kukuona ninakubaliana naye”
“ Amos alikueleza nini kuhusu mimi? Akauliza Peniela

“ Kikubwa alichonieleza ni juu ya uzuri wako.Alinieleza kwamba peniela ni mzuri hata Yule Cleopatra wa Misri hafikii uzuri wako.Baada ya kukuona nakubaliana na kauli yake.You are an angel Peniela” akasema Dr Joshua na kumfanya Peniela atoe kicheko kidogo halafu akasema

“ Thank you”
Dr Joshua akanywa mvinyo funda moja halafu akasema
“ Pamoja na yote aliyonieleza Amos lakini nahitaji kukufahamu zaidi Peniela”

“ Unahitaji kufahamu kitu gani kuhusu mimi Mr President?
“ Just call me Dr Joshua .I need to know everything about you.Your life,relation ship,everything”

“ Why do you wat to know me Mr Presi…..Oh Sorry Dr Joshua? Amos told me its just a one night stand but now it looks like an interrogation” akasema Peniela.Dr Joshua akatabasamu na kusema
“ Usinielewe vibaya Peniela.Ni sawa alivyokueleza Amos ninahitaji mwanamke mrembo kwa usiku wa leo na katika siku hizi chache nitakazokuwa hapa afrika ya kusini kwa mkutano lakini hata hivyo si vibaya kufahamiana zaidi.”
Peniela akanywa funda dogo la mvinyo na kuuliza
“ Don’t you tust Amos?

“ I do trust Amos with my life lakini ukweli ni kwamba nina sababu zangu bnafsi za kutaka kukufahamu kiundani”
“ Can you tell me what are the reasons?
“ The only reason is that I want you to be my woman”
“ Your woman??!” akauliza Peniela
“ Yes my woman” akajibu Dr Joshua

“ Dr Joshua you have a wife so why do you need me to be your woman?

“ Mke wangu ni mgonwa siku hizi na hawezi kunihudumia .Nahitaji huduma za kimwili na kama mke wangu hana uwezo wa kunihudumia basi nalazimika kuzitafuta huduma hizo sehemu nyingine na ndiyo maana nahitaji mwanamke mzuri mwenye hadhi ya kutembea na rais.Peniela nataka uwe mwanamke huyo.Nitakupa kila kitu unachokihitaji katika maisha yako.I’ll make you the most beautifull woman in the world.I’ll give you all luxuries..” akasema Dr Joshua na kunyamaza baada ya Peniela kuangua kicheko.
“ Peniela I’m serious about this.Its not a joke.” Akasema Dr Joshua
“ I know Dr Joshua but if you need love and comfort from me I’m ready to give you but not in exchange for money or anything.Nina kila kitu ninachokihitaji katika maisha yangu labda nilichokuwa nimekikosa ni kutembea na rais wa nchi” akasema Peniela na wote wakaangua kicheko.Dr Joshua akamtazama Peniela kwa sekunde kadhaa na kusema

“ So what do you say Peniela?
“ Say what? Akauliza Peniela
“ Kuwa mpenzi wangu”

“ Naomba unipe muda wa kulifikiri jambo hili Dr Joshua.Unajua kuwa na mahusiano na rais si jambo jepesi kwa hiyo nahitaji kufikiria kwanza kabla sijasema lolote”
“ Are you scared to be in relation with me? Akauliza Dr Joshua na kumfanya Peniela aangue kicheko.
“ Ofcourse I’m scared.You are the most powerfull man in the country so I must be scared.”akasema Peniela.Waliendelea na maongezi mengine na mwishowe wakajikuta kitandani

Dr Joshua akafumba macho baada ya kumbu kumbu ile kumjia kichwani.

“ For the first time in my life I enjoyed sex with her.Sikuwahi kuyafurahia mapenzi hadi nilipo kutana na Peniela.Usiku ule nilipokutana na Peniela ulikuwa ni usiku wangu wa kwanza kuyafurahia mapenzi na Peniela ndiye mwanamke pekee ambaye nakiri kwamba amefanikiwa kunipa penzi lile la kiwango cha juu mno.Ni mwanamke pekee aliyefanikiwa kunichanganya na kuniteka akili.” Akaendelea kuwaza Dr Joshua.



TUKUTANE SEHEMU IJAYO
 
PENIELA

SEASON 4


EPISODE 2


MTUNZI : PATRICK.C


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ So what do you say Peniela?
“ Say what? Akauliza Peniela
“ Kuwa mpenzi wangu”

“ Naomba unipe muda wa kulifikiri jambo hili Dr Joshua.Unajua kuwa na mahusiano na rais si jambo jepesi kwa hiyo nahitaji kufikiria kwanza kabla sijasema lolote”
“ Are you scared to be in relation with me? Akauliza Dr Joshua na kumfanya Peniela aangue kicheko.
“ Ofcourse I’m scared.You are the most powerfull man in the country so I must be scared.”akasema Peniela.Waliendelea na maongezi mengine na mwishowe wakajikuta kitandani
Dr Joshua akafumba macho baada ya kumbu kumbu ile kumjia kichwani.
“ For the first time in my life I enjoyed sex with her.Sikuwahi kuyafurahia mapenzi hadi nilipo kutana na Peniela.Usiku ule nilipokutana na Peniela ulikuwa ni usiku wangu wa kwanza kuyafurahia mapenzi na Peniela ndiye mwanamke pekee ambaye nakiri kwamba amefanikiwa kunipa penzi lile la kiwango cha juu mno.Ni mwanamke pekee aliyefanikiwa kunichanganya na kuniteka akili.” Akaendelea kuwaza Dr Joshua.



ENDELEA……………………….


“ Kwa penzi ambalo Peniela amekuwa akinipa sikukumbuka tena kumchunguza na kumfahamu kiundani.Sikujua kumbe nilikuwa najipeleka mwenyewe katika mdomo wa mamba.Maelezo ya Elibariki yananifanya nikubaliane naye kwamba Peniela alipandikizwa kwangu kwa lengo maalum.Damn you Amos !!..Una bahati umekufa ama sivyo ningekuua kifo kibaya sana kwa usaliti ulioufanya.Ninachotakiwa kukifanya kwa sasa ni kuvuruga mipango yote niliyokuwa nimeipanga na kuipanga upya.This time I’ll be more carefull na nitashirkiana na watu ambao ninawaamini.Mtu pekee ambaye ninaweza nikamuamini kwa sasa ni jaji Elibariki.Nitashirikiana na huyu.Dr Kigomba is a traitor and weak siwezi tena kufanya naye kazi.Siwezi kumuamini tena mtu kama Yule wala kushirikiana naye katika jambo lolote .Nitaikamilisha mipango yangu kimya kimya na baadae baada ya kuhakikisha nimemkabidhi Hussein mzigo wake nitalazimika kumuondoa kabisa Kigomba ili kufagia kabisa nyayo zote zisibaki nyuma.Nilimuamini sana Kigomba lakini ameniudhi mno kwa kitendo chake cha kutembea na mwanamke wangu ninayempenda kuliko wote.Tamaa zake zimenilazimisha nimuweke katika kundi la maadui zangu.” Dr Joshua akaendelea kuwaza.

“ Sasa nimeanza kupata picha kwamba Peniela alipoanzisha siri na Yule kijana Edson hakuwa anampenda bali alichokuwa anakitafuta ni zile nyaraka za siri alizoziiba Edson toka katika maktaba yangu ya siri.Inaonekana hao team Sc41 ni mtandao mpana na ni watu wanaofahamu mambo mengi.Kuna haja ya kuchimba kiundani mtandao huu na kuufutilia mbali hapa nchini kwetu.Ninaapa nitahakikisha lazima ninaufuta mtandao huo wa team sc41 katika nchi yangu.” Akawaza Dr Joshua halafu akachukua simu yake akazitafuta namba za mkuu wa kitengo cha siri cha usalama wa nchi kilichomo ndani ya idara ya usalama wa taifa aitwaye Abel Mkokasule.
“ Hallo mheshimiwa rais” akasema Abel

“ Mr Abel,habari za usiku huu?
“ Habari nzuri mzee” akasema Abel

“ Abel nahitaji kukuona usiku huu hapa katika makazi yangu binafsi uliko msiba wa mwanangu Flaviana”
“ Sawa mheshimiwa rais nitafika hapo muda si mrefu” akasema Abel na Dr Joshua akakata simu
“ Pamoja na ugumu wote uliopo wa kuikamilisha biashara ya ile package lakini katu siwezi kukata tamaa na kuishia kati kati.Endapo nitashindwa kumpatia Hussein package ile nitalazimika kurejesha fedha zote alizotoa , jambo ambalo siko tayari kulifanya.Nitapambana hadi nihakikishe ninamkabidhi Hussein mzigo wake.Ili mpango huu ufanikiwe ninahitaji sana watu nitakao waamini na mmoja wao ni huyu Abel.Ni kijana mtiifu sana kwangu na hajawahi kuniangusha katika kila kazi niliyowahi kumpatia.Nitamuondoa Kigomba na nafasi yake ataichukua Abel” Akawaza Dr Joshua



*******
Uso wa Dr Kigomba ulibadilika mara tu alipotoka kuonana na rais Dr Joshua.Alikuwa amejawa na hasira ,akatafuta sehemu akakaa.Kichwa kilijaa mawazo mengi mno

“ Bado siamini kilichotokea.Jaji Elibariki ni mtu hatari na ni kikwazo kikubwa mno kwetu na tayari anazifahamu siri zetu nyingi na kikubwa anachokifahamu ni kuhusiana na kifo cha Dr Flora.Tumetumia gharama kubwa kumsaka kila kona hata tukadiriki kutumia vyombo vya dola na kwa sababu yake uhai wa watu umepotea akiwemo Flaviana.Dr Joshua anayafahamu haya yote lakini nashangaa sana kwa kuonekana ameongozana naye usiku huu, kama vile hakuna chochote kilichotokea.Whats going on here?? Akajiuliza Dr Kigomba
“ Lazima kuna kitu kinaendelea hapa si bure.Hainiingii akilini mtu ambaye Dr Joshua alikuwa halali akiwaza namnaya kumpata leo wanashikana mikono na kucheka pamoja kama watu marafiki.Halafu ninachojiuliza Elibarki alikuwa amejificha wapi? Amefahamuje kwamba nimefanya mapenzi na Peniela? Amefahamuje kama Peniela amenipa zawadi ya saa? I’m confused” Dr Kigomba ni kweli alionekana kuchanganyikiwa.Akainuka alipokuwa amekaa na kuanza kuzunguka zunguka
“ Elibariki amemueleza dr Joshua kuwa eti Peniela ameiunganisha simu yangu na mfumo wao unaowawezesha kufuatilia kila ninachokiongea katika simu yangu.Sijui taarifa hizi Elibariki amezitoa wapi kwa sababu ninavyokumbuka mimi Peniela hajawahi kugusa simu yangu.Huu ni uongo mkubwa ambao ameutunga Elibariki kwa sababu anazojua yeye mwenyewe.Kama zawadi ya saa ni kweli Peniela alinipa lakini hajawahi kugusa simu yangu hata mara moja.Kingine kinachonishangaza na kunifanya nijiulize maswali ,huyu jaji Elibariki amefahamuje mambo haya yote? Au yawezekena ni kweli wakawa na mahusiano na ndiyo maana Dr Joshua akanituma niende kumchunguza Peniela kama ana mahusiano na jaji Elibariki? Inawezekana kabisa kwamba jaji Elibariki na Peniela wana mahusiano na ndiyo maana amefahamu mambo yote ya kuhusu mimi na Peniela .Ninachopaswa kukifanya kwa sasa ni kufahamu mambo yote ambayo jaji Elibariki amemwambia Dr Joshua.Lazima kuna mambo mengi atakuwa amemw……” Dr Kigomba akastuka kidogo baada ya kumuona mtu mmoja mwenye mwili uliojengeka vyema akishuka ndani ya gari

“ Abel Mkokasule !!!..What is he doing here at this time? Akajiuliza
Mmoja wa walinzi wa rais akampokea Abel na kuongozana naye kuelekea ndani.

“ What’s going on here? Mimi si mtoto mdogo wa kushindwa kutambua kwamba kuna jambo linaloendelea hapa.Lazima kuna kitu kati ya Dr Joshua,jaji Elibariki na Abel Mkokasule.I need to find out” akawaza Dr Kigomba na kupiga hatua za haraka akaingia ndani lakini alipokaribia tu sebule ya Dr Joshua akazuiwa na walinzi .
“ Samahani mzee huruhusiwi kuingia humo sebuleni.Rais ana maongezi muhimu na mgeni wake.” Akasema mmoja wa walinzi

“ Mimi ni katibu wa rais na ninaruhusiwa kuingia sehemu yoyote aliko rais.Nina jambo la muhimu ninalotaka kuzungumza na rais sasa hivi”
“ Mzee itakulazimu usubiri hadi hapo rais atakapomaliza maongezi ndipo uonane naye” akasema mlinzi wa rais na kuzidi kumpandisha hasira Dr Kigomba
“ Nyie vijana hamnijui mimi ni nani? Don’t you all know me ? Samweli ,Victor nini nyote hamnifahamu mimi ni nani? Akasema Kigomba huku akiwataja kwa majina wale walinzi
“ We know who you are Sir,but that’s the order from president himself.” Akasema mmoja wa walinzi .Jibu lile likazidi kumnyong’onyeza Dr Kigomba akavuta pumzi ndefu na kusema

“ Ok nitaonana naye baadae” akasema na kuondoka kwa hasira
“ Mr President “ akasema Abel Mkokasule baada ya kuingia sebuleni kwa rais.
“ Mr Abel.Karibu sana.Ninashukuru umefika kwa wakati” akasema Dr Joshua wakapeana mikono na kuendelea na maongezi
“ Samahani sana Abel kwa kukuita muda kama huu ambao ni wa mpumziko.” Akasema Dr Joshua huku akimiminia Abel mvinyo katika glasi

“ Don’t worry Mr President .Muda wowote mimi niko kazini” akasema Abel halafu kila mmoja akanywa funda moja la mvinyo.
“ Mr President naomba nichukue nafasi hii kukupa pole sana kwa msiba mkubwa wa mwanao.Nakuahidi ushirikiano wangu mkubwa katika kuhakikisha wale wote waliosababisha kifo cha mwanao wanapatikana na kufikishwa katika mkono wa sheria” akasema Abel
“ Nashukuru sana Abel .Muda wowote nitakapohitaji msaada wako sintasita kukutaka unisaidie” akasema Dr Joshua.Akanyamaza na kunywa mvinyo kidogo halafu akaendelea
“ Abel nimekuita usiku huu nina kazi yangu ambayo nahitaji ifanywe na mtu makini ninayemuamini na wewe ndiye pekee ninayekuamini kuifanya kazi hiyo kwani umekwisha nifanyia kazi nyingi na hujawahi hata mara moja kuharibu kazi yangu yoyote” akasema

“ Ahsante sana kwa kuniamini mheshimiwa rais.Nakuahidi kuifanya kazi hiyo kwa uamini na weledi mkubwa” akasema Abel
“ Nina kazi mbili ama tatu ambazo nataka uzifanye.Kwanza nina mgeni wangu binafsi anaitwa Hussein Abdullah Hussein ambaye amefikia 790 hotel.Ameongozana na watu kama kumi hivi .Nataka kesho asubuhi na mapema ,Hussein na watu alioongozana nao wahamishwe hoteli na kupelekwa Rainbow hotel.Kazi ya pili nataka umsake Jessica Alfredo Yule anayefanya kazi katika idara ya usalama wa Taifa.Nadhani unamfahamu .Ukimpata mpeleke Dark house na umuhifadhi kule hadi nitakapokupa maelekezo mengine. Kuna vitu ninavihitaji toka kwake.Jambo la tatu nataka ufuatilie nyendo za Dr Kigomba.Nataka kufahamu anakutana na nani ,sehemu zote anazotembelea,nataka kufahamu kila anachokifanya.Ripoti hii naihitaji kila baada ya masaa matatu.Mambo hayo matatu yanahitaji utekelezaji wa haraka .Lakini lipo jambo la nne ambalo nataka unisaidie pia.Kuna msichana mmoja yuko mahala ameshikiliwa na ana taarifa za muhimu sana.Nataka naye umchukue na umuhifadhi dark house ili nizipate hizo taarifa alizonazo.Lakini hili litasubiri kidogo hadi nitakufahamisha litakapokuwa tayari.Nadhani umenielewa Abel”

“ Nimekuelewa mzee na ninakuahidi kwamba kazi hizo zote zitafanyika kwa ufanisi mkubwa na kwa kuzingatia muda”
“ Good.Naomba vile vile nikukumbushe kwamba usiri na umakini mkubwa vinatakiwa sana katika kufanikisha kazi hizi “ akasema Dr Joshua

“ Usihofu mzee.Hayo yote yatazingatiwa .” akasema Abel halafu wakaendelea na maongezi mengine na baadae wakaagana Abel akaondoka.
“ Namuamini sana Abel Mkokasule hajawahi kuniangusha.Endapo atanifanyia vizuri kazi hizi nilizompa kabla sijamaliza uongozi wangu lazima nihakikishe nimemuweka sehemu nzuri ikiwa ni shukrani yangu kwake kwa kazi nzuri “ akawaza Dr Joshua na kunywa funda kubwa la mvinyo
“ Baada ya kumalizana na Abel natakiwa pia kuongea na mkuu wa polisi ili kulimaliza suala la Elibariki kwani tayari vyombo vya dola vilikuwa vikimsaka akihusishwa na kifo cha Flaviana.Hakuna namna nyingine ninayoweza kumtumia Elibariki bila ya kumsafisha kwanza kutokana na tuhuma zilizokuwa zinamkabili za kusababisha kifo cha Flaviana.Lazima niyalambe matapishi yangu kwani nisipofanya hivyo kutatokea sintofahamu kubwa kuhusu suala hili la jaji Elibariki kuwa huru wakati vyombo vya dola vimekwisha tangaza kumtafuta kwa tuhuma za mauaji.Ni wakati kama huu ambao ninal;azimika kutumia nguvu na madaraka yangu kama rais wa nchi” akainuka na kwenda kuegemea meza

“ Kuna suala lingine pia. Rosemary Mkozumi alimtaja mtu mmoja anaitwa Mathew kwamba ndiye aliyemteka na kwamba ndiye anayeongoza harakati zote za kuhakikisha mipango yangu yote inakwama.Kwa mujibu wa jaji Elibariki huyu Mathew ni rafki yake na anafanya kazi za upelelezi wa kujitegemea na tayari anafahamu mambo yangu mengi .Kila kitu ninachokifanya huyu jamaa anakifahamu na ana mikakati mizito ya kuhakikisha hakuna mpango wangu hata mmoja unafanikiwa.Huyu pia ni mtu hatari sana kwangu na lazima nimtafute kwa nguvu zangu zote hadi apatikane.Nikimpata huyu nitakuwa nimempata pia Peniela kwani kwa maelezo ya jaji Elibariki wawili hawa wameungana a wanafanya kazi zao pamoja ili kuhakikisha mambo yangu hayafanikiwi na wanaipata package kabla sijamkabidhi Hussein.” Akawaza Dr Joshua na mara sura yake ikabadilika
“ Kila nikimtamka au kumuwaza Peniela mwili wote unanisisimka.Sifahamu ni hasira au nini kinanitokea nilitamkapo jina hili .Mpaka hapa nakiri kwamba Yule msichana ameniteka akili yangu kabisa.Tayari ameniingia katika kila mshipa wa mwili wangu na ndiyo maana mpaka sasa ninashindwa kupata jibu nimfanye kitu gani kwa jambo alilonifanyia.Natamani nimpatie adhabu kali mno lakini bado kuna sauti ndani yangu inaniambia Peniela hawezi kunifanyia mambo hayo aliyonieleza Elibariki.Yawezekana ni kutokana na mapenzi mazito niliyonayo kwa mwanamke huyu ndiyo maana moyo wangu unakuwa mzito kupata ni adhabu gani nimpatie. Peniela amekosea sana kwa mambo anayonifanyia kwani hiki ninachokifanya ni kwa ajili yetu mimi nay eye ili tuwe na maisha mazuri pindi nitakapomaliza kipindi changu cha uongozi.Nilimpa chaguo achague nchi yoyote duniani anayotaka kwenda kuishi na ningemnunulia nyumba ili aishi maisha a kifahari kama malkia ,sijui ni shetani gani amemuingia Peniela na kumfanyanya akatae maisha haya mazuri ambayo wanawake wengi wanayaota usiku na mchana.Why Peniela?? Akajiuliza Dr Joshua akainama akatafakari.
“Ninadhani inawezekana kabisa Peniela anafanya mambo haya si kwa kupenda bali kwa shinikizo.Kuna nguvu kubwa iliyo nyuma yake inayomwelekeza na kumsukuma nini cha kufanya.Ni Team SC41.Namfahamu Peniela ananipenda na yeye kama yeye hawezi katu kunifanyia mambo kama haya.Anafahamu fika kwamba ninampenda na nina nia nzuri kwake ” akakuna kichwa na kuzama tena mawazoni

“ Kwa mujibu wa jaji Elibariki ni kwamba Team Sc41 ni kikundi cha siri kinachofanya kazi zake kwa siri hapa nchini na katika nchi nyingine afrika na kazi yao kubwa ni kulinda maslahi ya Marekani.Kwa nini Deus Mkozumi wakati ananikabidhi ofisi hakunieleza chochote kuhusu jambo hili ? Nani kiongozi wa kikundi hiki hapa Tanzania? Je ni kweli kwamba kazi yao ni kulinda maslahi ya Marekani hapa nchini au wanafanya shughuli nyingine za ujasusi ?Hili jambo limenistua mno kwani inaonekana hawa team SC41 tayari wamekita mizizi yao hadi ndani kabisa ya serikali na ndiyo maana wana uwezo wa kufahamu kila kinachoendelea ndani ya serikali.Kama wameweza kuniingia hata mimi kwa kuwatumia watu wa karibu na ninaowaamini ,hawawezi kushindwa kwa viongozi wengine.Hii ni hatari mno kwa usalama wa nchi yetu.Katika hili ,serikali ya Marekani inatakiwa kutoa ufafanuzi wa kina ni kwa nini wanaruhusu kikundi hiki kifanye kazi kwa siri ndani ya nchi yetu? Halafu kingine kinachonishangaza kwanini hadi leo hii bado vyombo vyetu vya usalama havijaweza kugundua uwepo wa kikundi hiki hapa nchini? Akawaza Dr Joshua na kukunja sura kwa hasira

“ Lazima nikifutilie mbali kikundi hiki na potelea mbali kama nitaanzisha mgogoro na serikali ya marekani .Lazima Team SC41 waondolewe hapa nchini na kuhakikisha jambo kama hili halijirudii tena hapa nchini kwa siku zijazo.Ni kweli Marekani wamefanya uwekezaji mkubwa sana katika sekta ya mafuta na gesi hapa nchini lakini hiki si kigezo cha wao kufanya kila wanachokitaka hapa nchini.Hii ni nchi huru na ina sheria zake.Kitendo cha kuruhusu kikundi cha siri kuingia nchini na kufanya shughuli zake kwa siri ni kitendo cha uchokozi mkubwa.Hawakuwa na haja ya kufanya hivyo wakati tayari tumewahakikishia maslahi yao yatalindwa .Suala hili lazima lifikishwe katika vyombo vya usalama wa nchi lakini kabla ya kufanya hivyo lazima niongee kwanza na rais wa Marekani nimuulize kama analifahamu jambo hili na kwa nini hajanieleza.Hili si suala dogo na linaweza kuweka doa katika mahusiano mazuri tuliyonayo baina ya nchi zetu.Kesho mara tu baada ya mazishi nitaongea na rais wa Marekani kuhusu suala hili.Sikutegemea kabisa kama jambo hili lingefika hapa lilipofika na kuibua mambo haya mazito”
Kichwa cha Dr Joshua kikaendelea kuzunguka kwa mawazo mengi

“ Kama Team Sc41 tayari wanafahamu kuhusu mipango yangu ya kukiuza kirusi Aby basi ni wazi hata serikali ya Marekani watakuwa wanalifahamu jambo hili na wamekaa kimya wakitegemea kwamba wana kikundi chao hapa nchini wanachokitumia kukitafuta kirusi hicho.Je tayari wanafahamu kuwa ninataka kumuuzia Hussein ? Hapo awali niliwahi kufanya utafiti mdogo kuhusiana na Hussein nikagundua kwamba ni mtu ambaye anatajwa kuhusiana na mitandao ya kigaidi na ninajua lengo la kukitaka kirusi Aby kwa gharama zozote lazima wanataka kukitumia katika mambo ya kigaidi.Ninachojiuliza itakuaje iwapo wanataka kukitumia kirusi hicho kuishambulia Marekani? Itakuaje iwapo uchunguzi utafanyika na nikabainika kwamba ni mimi ndiye niliyemuuzia Hussein kirusi hicho? I’m confused” akaendelea kuwaza huku akinywa funda kadhaa za mvinyo
“ Pamoja na hatari iliyopo siwezi kuyaacha mabilioni haya mengi ambayo tayari nimekwisha yapokea.Potelea mbali kama Hussein na wenzake wanataka kukitumia kwa shughuli za kigaidi ama la mimi ninachohitaji ni pesa tu.Nimeitumia nchi hii kwa miaka kumi sasa na siwezi kustaafu nikiwa masikini.Nataka niwe na maisha mazuri baada ya kumaliza uongozi wangu.Zaidi ya yote hakuna mwenye ushahidi au atakayekuwa na ushahidi kuwa kirusi Aby kimetoka Tanzania.Nitaendelea na mipango yangu kama nilivyoipanga and nobody can stop me.Muda umekwenda sana ngoja nizungumze na kamanda wa polisi kuhusiana na suala la kumsafisha jaji Elibariki.



TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
 
PENIELA

SEASON 4


EPISODE 3

MTUNZI : PATRICK.CK



ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Hapo awali niliwahi kufanya utafiti mdogo kuhusiana na Hussein nikagundua kwamba ni mtu ambaye anatajwa kuhusiana na mitandao ya kigaidi na ninajua lengo la kukitaka kirusi Aby kwa gharama zozote lazima wanataka kukitumia katika mambo ya kigaidi.Ninachojiuliza itakuaje iwapo wanataka kukitumia kirusi hicho kuishambulia Marekani? Itakuaje iwapo uchunguzi utafanyika na nikabainika kwamba ni mimi ndiye niliyemuuzia Hussein kirusi hicho? I’m confused” akaendelea kuwaza huku akinywa funda kadhaa za mvinyo

“ Pamoja na hatari iliyopo siwezi kuyaacha mabilioni haya mengi ambayo tayari nimekwisha yapokea.Potelea mbali kama Hussein na wenzake wanataka kukitumia kwa shughuli za kigaidi ama la mimi ninachohitaji ni pesa tu.Nimeitumia nchi hii kwa miaka kumi sasa na siwezi kustaafu nikiwa masikini.Nataka niwe na maisha mazuri baada ya kumaliza uongozi wangu.Zaidi ya yote hakuna mwenye ushahidi au atakayekuwa na ushahidi kuwa kirusi Aby kimetoka Tanzania.Nitaendelea na mipango yangu kama nilivyoipanga and nobody can stop me.Muda umekwenda sana ngoja nizungumze na kamanda wa polisi kuhusiana na suala la kumsafisha jaji Elibariki.


ENDELEA………………..


Ni tayari usiku wa manane na karibu watu wote waliokuwepo katika makazi ya binafsi ya rais Dr Joshua ulipo msiba wa mwanae Flaviana ,walikuwa wamelala lakini kwa jaji Elibariki hali ilikuwa tofauti.Macho yake yalikuwa makavu na hakuhisi hata tone la usingizi.Kichwa chake kilikuwa kizito kwa mawazo mengi aliyokuwa nayo.
“ I don’t know if I’m doing the right thing” akawaza akiwa ameinama na mikono ikiwa kichwani.

“ Sikuwahi kufikiria hata mara moja kama siku moja nitajiunga na kikundi hiki cha mashetani wa nchi.Mtandao wa Dr Joshau naweza kuuita ni wa mashetani kwa namna wanavyofanya mambo yao ya kifedhuli bila kuwa na hata chembe ya huruma.Wanatoa roho za watu bila hata huruma yoyote.Wamelewa madaraka na wanafanya chochote wakitakacho katika nchi hii.Wapo wazalendo wachache ambao wameyatoa maish a yao sadaka kwa kupambana na mtandao huu na miongoni mwao ni Mathew na Anitha lakini badala ya kuwaunga mkono nimechagua kuwasaliti .Si kuwasaliti pekee bali nimezirudisha nyuma juhudi zao zote za kujaribu kulifutilia mbali kundi hili la mafisadi wanaoitafuna nchi bila huruma wakiongozwa na rais Dr Joshua.Mipango yao yote nimeiweka wazi kwa Dr Joshua na kwa sababu hiyo hawana tena namna nyingine ya kutimiza malengo yao na Dr Joshua lazia atafanikisha mpango wake wa kukiuza kirusi Aby.” Akawaza na kujipiga kichwani kwa hasira
“ Shetani gani amenipitia na kunishawishi kufanya hivi nilivyofanya? Akazidi kuumia kwa mawazo kila alipokumbuka kile alichokifanya.
“ Lakini sipaswi kujilaumu sana kwa nilichokifanya kwani sikuwa na namna nyingine ya kufanya .Tayari maji yalikwisha nifika shingoni na sikuwa na uwezo tena wa kupambana na Dr Joshua.Nilishika makali wakati yeye ana mpini kwa hiyo kwa namna yoyote ile lazima angenikata tu.Nilikuwa nataka kushindana na mtu mwenye nguvu kuliko wote hapa nchini.Vyombo vyote vya dola viko chini yake kwa hiyo nisingeweza kujificha kwa muda mrefu lazima ningepatikana tu.Nilikuwa najitengenezea mwenyewe njia ya kujipoteza katika ramani ya dunia kwa hiyo nilichokifanya kwa upande mmoja si sahihi lakini kwa upande wa pili ni sahihi.Hata vitani mwanajeshi anayeshindwa hujisalimisha .Vita nilivianzisha mimi mwenyewe kwa shauku yangu ya kutaka kufahamu mambo yasiyonihusu na sikujua kama vita hii ingenifiisha hapa.Nimepoteza mke wangu Flaviana na mimi mwenyewe nilikuwa katika hatari ya kupotea.Nilihitaji maisha yangu tena.Nilihitaji kuwa huru na ili hilo lifanikiwe njia pekee ilikuwa ni kunyanyua mikono na kujisalimisha.Najua Mathew na wenzake wataumizwa sana na jambo hili lakini sina namna nyingine ya kufanya ,tayari limekwisha tokea na kwa hilo lazima wakubaliane nalo.Hapo mwanzo hata shetani aliwahi kuwa malaika na akaasi kwa hiyo uasi sikuuanza mimi.I hope they’ll understand japokuwa sijui mwisho wake utakuaje kwani sina hakika kama Mathew ataliacha jambo hili lipite hivi hivi.Lazima atataka kulipiza kisasi .Namfahamu Mathew ni mtu mzuri sana lakini ukimkorofisha ni mbaya kuliko shetani.He will haunt me till the day he die.Kwa ajili ya usalama wangu nitamwomba Dr Joshua anipatie ulinzi wa kutosha Anyway nisipoteze muda kuwawaza akina Mathew kwani nguvu ya kuwadhibiti ninayo na isitoshe baadae mwaka huu nitakuwa rais wa Tanzania .Dr Joshua amenihakikishia hilo na uwezo huo anao kwa hiyo ninachopaswa kukiwaza sasa ni namna gani nitatokea mbele ya umma wa watanzania n a kujisafisha kwani hapa nilipo nina tuhuma za kusababisha kifo..Nitatakiwa kueleza nilinusurika vipi katika shambulio ,baada ya hapo nilikwenda wapi ,natakiwa vile vile kukanusha tuhuma za kuhusishwa na kifo cha Flaviana.lakini haya yote yanatajkiwa kufanywa na Dr Joshua kwani uwezo huo anao.Mtu pekee ambaye nitapata wakati mgumu kwake ni Anna.Nilimuhakikishia kwamba baba yake anahusika na vifo vya mama na dada yake .Nilimueleza vile vile kwamba hata mimi kunusurika kuuawa ulikuwa ni mpango wa Dr Joshua na washirika wake baada ya kugundua sababu ya kifo cha Dr Flora.Lakini ghafla ananiona nikiwa nimeongozana na baba yake mtu ambaye anataka kuniua.Ni wazi hapa kunahitajika maelezo ya kutosha sana kumfanya aniamini.Halafu Dr Joshua kuna kitu alinigusia.Alisema kwamba kwa kuwa anataka kunipigania ili niwe rais basi nianzishe mahusiano na Anna ili nitakapokuwa rais basi Anna awe katika nafasi ya uongozi.Sina hakika kama hilo litawezekana kwani mimi na Anna hatujawahi kuwa katika mahusiano mazuri kwa muda mrefu na tumeanza kuzungumza vizuri hivi majuzi .Baada ya tukio la kushambuliwa kwa Flaviana Mwanamke pekee ambaye moyo wangu uliridhia kuwa naye ni Peniela .Yule ana kila kitu ninachokihitaji kwa mwanamke lakini kwa bahati mbaya sintaweza kumpata tena.Anyway ngoja niachane na mawazo haya ili kichwa changu kipumzike .Kesho itakuwa ni siku yangu ndefu sana” akawaza jaji Elibariki na kujilaza kitandani



******



“ Nimestushwa sana baada ya kumuona baba akiwa na Elibariki.How it happened? Akajiuliza Anna ambaye alikosa kabisa usingizi.
“ Kwa mujibu wa maelezo aliyonipa Elibariki nikiwa afrika ya kusini alisema kwamba baba ndiye mhusika mkuu wa vifo vya mama na dada .Alinieleza kwamba hata yeye kutaka kuuawa ulikuwa ni mpango wa baba na ndiyo maana akaenda mafichoni.Kitendo cha kuibuka tena na kuonekana akiwa na baba kimenishangaza sana.Nini kinaendelea hapa? Lazima nifahamu kinachoendelea kati yao kwa sababu hainiingiii kabisa akilini kuwaona wawili hawa wakiwa wanaongozana pamoja .Tayari Elibariki anatafutwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mke wake iweje basi mtuhumiwa wa mauaji aonekane ameongozana na rais? Anna akazidi kuumiza kichwa kwa mawazo.


********

Hali ilikuwa ya ukimya mkubwa katika jumba la John Mwaulaya.Kila aliyekuwamo ndani ya jumba hili alionekana kuwa katika tafakari .Kilichotokea usiku ule kiliwastua wote.Kwa takribani masaa mawili sasa wageni waliotoka Marekani walikuwa wamejifungia katika mojawapo cha chumba wakijadiliana.Mlango wa chumba walimokuwamo ukafunguliwa na Nickson Strawberry akawataka watu wote wakusanyike sebuleni
“ Ndugu zangu poleni sana kwa mkasa mzito uliotokea .Usiku wa leo tumewapoteza wenzetu wanne katika shambulio na wengine wawili hali zao ni mbaya sana.Hatukutegemea jambo kama hili kutokea lakini limetokea. “ akanyamaza kidogo kisha akaendelea

“ Siku ya leo imekuwa ni ya majanga makubwa kwa Team SC41 kwani tumempoteza pia mtu muhimu sana katika kundi letu ,John Mwaulaya.Huyu ni mtu aliyeanzisha Team SC41 hapa Tanzania .Ni mtu anayeifahamu Team Sc41 kwa undani sana.John Mwaulaya amefariki katika wakati ambao mchango wake ulikuwa unahitajika sana ili kufanikisha operesheni 26B. Ili operesheni hii muhimu ifanikiwe kuna watu wawili ambao tuliwategemea sana na kuwaweka m stari wa mbele,Captain Amos na Peniela.Kwa bahati mbaya kwetu,Captain Amos hatumjui na kati yetu hakuna aliyewahi kumuona.Ni John Mwaulaya pekee aliyemuingiza Team SC41 na alikuwa anaripoti kwake kwa hiyo sisi itakuwa vigumu sana kumpata.Mtu pekee ambaye tumebaki tunamtegemea ni Peniela.Katika hali isiyo ya kawaida Peniela naye alianza kuonyesha ushirikiano mdogo kwetu na baada yua kifo cha John Mwaulaya alitoweka ikatulazimu kuanza kumfuatilia.Tulikuwa tunamtafuta kwa mambo mawili makubwa.Kwanza atupe muelekeo wa operesheni 26B kwa sababu yeye ndiye tuliyemtanguliza mbele .Pili ni kuhusiana na mazishi ya John Mwaulaya.Katika wosia wake John Mwaulaya ameandika kwamba baada ya kifo chake mali zake zote atakabidhiwa Peniela.Hii inatufanya tuamini kwamba Peniela alikuwa ni mtu muhimu sana kwa John kwa hiyo yeye ndiye atakayekuwa na sauti kubwa kuhusiana na namna ya kumzika John Mwaulaya.Baadae usiku kamera za siri zilizofungwa nyumbani kwake zikamnasa akiingia nyumbani kwake akiwa ameongozana na mwanaume mmoja.Haraka haraka tuliwatuma vijana wetu kumfuatilia.” Akanyamaza kidogo na kuendelea

“ Peniela na jamaa aliyeongozana naye hawakukaa sana mle ndani ,wakatoka na kuondoka ,vijana wetu wakawafuatilia ili kufahamu wanakwenda wapi.Kwa mujibu wa vijana wetu ilionekana Peniela na huyo mtu aliyekuwa naye,waling’amua kwamba wanafuatiliwa kwa hiyo wakajihami na ndiyo m aana kulitokea upinzani mkubwa na tukawapoteza wenzetu wanne.Hatukufanikiwa kumpata Peniela kwani alifanikiwa kutoroka na huyo mwenzake.Mwanaume ambaye alikuwa ameongozana na Peniela ametambuliwa na Dr Martin kwamba aliwahi kufika hapa nyumbani kwa John akiwa ameongozana na mwenzake na akamtolea John vitisho vya kumuua.Mtu huyu anaonekana kufahamiana na Peniela na jina lake anaitwa Mathew.Peniela na Mathew wanaonekana ni washirika na na kuna siri wanayo kwa hiyo ili kuipata package tunayoitafuta toka kwa Dr Joshua lazima tumpate Peniela kwa namna yoyote ile kwani ndiye kiungo pekee kati yetu na rais.Bila yeye hakuna kinachoweza kufanikiwa.Kwa sasa Peniela yuko katika mstuko baada ya makazi yake kuchomwa moto na tumefanya hivi ili kumfanya Peniela akose makazi na arejee kwetu.Kwa sasa kumpata Peniela ni kipaumbele cha juu kuliko vyote lazima tufanye kila lililo ndani ya uwezo wetu kuhakikisha tunampata kabla ya kesho mchana.Bila ya yeye juhudi zetu zote tulizozifanya kwa miaka kadhaa ili kuipata package hiyo zitakuwa ni bure.Hatuwezi kukubali hilo litokee kwa hiyo basi tutumie kila aina ya uwezo tulionao kuhakikisha Peniela anapatikana.” Akasema Nickson

“ Josh kesho asubuhi utashughulikia mazishi ya watu hawa tuliowapoteza.Kumbuka ni mazishi ya kimya kimya na asifahamu mtu yeyote.Vile vile kwa sasa wewe ndiye utakayekaimu uongozi wa Team SC41 kwa hapa Tanzania kwa hiyo waongoze wenzako kuhakikisha Peniela anapatikana.Sisi tunakwenda kuwataarifu ofisi kuu Marekani kilichotokea” akasema Nickson halafu akaongozana na wale wenzake wakaondoka kuelekea ofisi kuu ya Team SC41.
“ Siamini kama nimepewa uongozi wa Team SC41 Tanzani.Hili ni jukumu zito na na nimepewa kama mtego.Nahisi hawa jamaa wanahisi kitu Fulani kuhusu mimi na Peniela.Mimi ndiye niliyempigia simu kumfahamisha kwamba anafuatiliwa .Nashukuru niliwahi kumpa taarifa ile ambayo naamini imemsaidia sana kwani bila hivyo wale jamaa wangemkamata.Where is she now? Imeniuma sana kusikia eti nyumbayake wameichoma moto.Huu ni unyama mkubwa sana.Mtu kama Peniela hakupaswa kabisa kufanyiwa ukatili kama huu hasa kwa mambo makubwa ambayo ameyafanya katika Team SC41.Watu hawa ni wanyama na hawafai kabisa.Nadhani mwisho wa Team SC41 umewadia.Wamekose a sana kunipa uongozi .Nitamtafuta Peniela na kwa kushirikiana naye we’re going to take down team SC41 “ akawaza Josh na kuelekea chumbani kwa John Mwaulaya.



******


Gari walilopanda Mathew na Peniela lilitawaliwa na ukimya mkubwa.Dereva aliyekuwa anaendesha gari lile alionekana kutohitaji maongezi ya aina yoyote
“ Mathew who is this guy? Where are wre going? “ akauliza Peniela kwa kunong’ona

“ Vuta subira Peniela utafahamu kila kitu.Usiwe na wasi wasi ,we’re going somewhere safe” akasema Mathew.Peniela akamtazama kwa sekunde kadhaa na kusema
“ Thank you Mathew for everything.Thank you for saving my life”
Mathew hakujibu kitu akatabasamu halafu akalitazama jeraha lake lililokuwa linavuja damu
“ Damu hii inayomwagika haiwezi kupotea bure.Lazima ilipwe” akawaza halafu akakiegemeza kichwa katika kiti na kuzama katika tafakari nzito
“ Nini kimesababisha nyumba yangu kuungua moto? Ni team SC41 ndio waliofanya unyama huu.Nalazimika kuamini hivyo kwa sababu hata nyumba ya Peniela imechomwa moto pia na matukio haya yote yametokea kwa wakati mmoja.Team SC41 wanamtafuta Peniela wa gharama zozote zile kwani ndiye tegemeo lao kubwa katika kukipata kirusi Aby.Bila yeye hawataweza kufanikisha lolote.Nina hakika walimfuatilia Peniela na kugundua kwamba alikuwa nyumbani kwake na ndiyo maana wakaamua kufanya vile walivyofanya.Kwa mara ya pili tena team SC 41 wanateketeza makazi yangu kwa moto.Mara ya kwanza alikuwa ni John mwaulaya aliyeteketeza nyumba yangu kwa moto na familia yangu yote ikateketea.Safari hii wameiteketeza tena na …” picha ya Anitha ikamjia na kumfanya aume meno kwa uchungu
“ Oh my God !! Anitha ..!!. She was in there with Elibariki,Naomi and Rosemary Mkozumi.Are they all dead? Jamani Anitha n itamlilia kilio gani mimi? Amekuwa ni mtu wangu na mshirika wangu wa karibu mno.Ufanikishaji wa k azi zangu nyingi kwa kiasi kikubwa unamtegemea yeye.Anitha ni mwanamke jasiri asiyeogopa kitu.Kuna nyakati tumekumbana na hatari kubwa lakini bado alisimama bila woga na tukashinda.Sijawahi na sintakutana na mwanamke kama Anitha.Sitaki kabisa kuamini eti Anitha amekufa.I know her she knows how to fight.Nafsi yangu inakataa kabisa kukubali kwamba Anitha aliteketea ndani ya ule moto” akawaza Mathew

“ Lakini kama hakuteketea ndani ya ule moto yuko wapi ? Jaji Elibariki,Naomi na Rosemary Mkozumi wako wapi? Nao pia watakuwa wameteketea ? Rosemary Mkozumi ni mwanamke hatari kwa nchi yetu ambaye anashirikiana na mtandao wa kigaidi na kwa kupitia kwake tungeweza kufahamu mambo mengi na mipango yote ambayo imepangwa kutekelezwa na magaidi katika ukanda huu wa afrika mashariki.Kumpoteza Rose kutarudisha nyuma juhudi zote za kupambana n a ugaidi.Ngoja kwanza nitulize akili yangu na kutakapopambazuka tayari nitakuwa nimepata akili n ifanye nini lakini kwa yeyote aliyefanya unyama huu wa kunichomea nyumba kwa lengo la kuharibu mipango yangu amekosea sana na ameuwasha moto ambao hataweza kuuzima.Safari hii watauona upande wangu wa pili ulivyo” akawaza Mathew huku akiuma meno kwa hasira ,akageuka na kumtazama Peniela.

“ Namuonea huruma sana Peniela.Inaonekana katika maisha yake hajawahi kukutana na mikasa ya namna hii.Sura yake inaonyesha wazi amekata tamaa kabisa.Kilichotokea usiku huu kimemuogopesha mno.Hata hivyo nitamlinda .Sintaruhusu hatari yoyote imkaribie.Kwa maneno yake mwenyewe kabla hajakata roho ,John Mwaulaya alinisisitiza kwamba nimlinde Peniela kwa namna yoyote ile hata kama ni kwa kuyaweka maisha yangu hatarini.Thats what I’m going to do.Nitamlinda Peniela zaidi ya mboni yangu ya jicho” akawaza Mathew

“ Whats going to happen from tomorrow is a victory or death.Chochote kinaweza kutokea lakini nitapambana kuhakikisha Peniela anakuwa salama na mipango yetu yote inakwenda kama tulivyoipanga” akawaza Mathew akajaribu kuinua mkono akahisi maumivu makali

“ Nahtaj kulitibu jeraha hili haraka.” Akawaza Mathew na taratibu mwendo wa gari ukapungua,walikuwa wamelikaribia geti kubwa jeusi.Yule dereva akatoa kifaa kidogo akakielekezea katika geti na kubonyeza kidude Fulani chekundu na geti likaanza kufunguka wakaingia ndani.Lilikuwa ni jumba zuri la ghorofa moja llilozungukwa na taa nyingi ,mbele ya jumba lile kuliegeshwa gari tatu .dereva akawageukia akina Mathew

“ Safari yenu bado inaendelea.Mtaingia katika gari lingine na mtapelekwa mahala mnakotakiwa kwenda.Ila nawatahadharisha .There is only one rule you’ll have to obey.Follow instructions and don’t ask question.Tumeelewana?
Mathew na Peniela wakatazamana na kujibu kwa pamoja
“ Tumeelewana”

“ Good.Now follow me” akasema Yule dereva na kushuka garini akina Mathew nao wakashuka wakamfuata,akawaelekeza waingie katika mojawapo ya magari yaliyokuwa yameegeshwa nje ya jumba lile halafu yeye akaingia ndani.

“ Mathew who are these people? Do you real know them? Akauliza Peniela kwa wasi wasi
“ Relax Penny.We’re going to be fine” akajibu Mathew kwa ufupi.
“ Mathew mienendo ya hawa jamaa inanipa shaka sana na ndiyo maana nahitaji kufahamu kama tuko salama ama vipi.Kilichotutokea usiku wa leo kimenipa fundisho la kuwa na mipaka katika kumuanini mtu.Kwa hiyo Mathew naomba unieleze ukweli unawafahamu hawa watu?
Kabla Mathew hajajibu kitu ,mlango wa kuingilia ndani ya ile nyumba ukafunguliwa akatoka jamaa mmoja aliyevalia fulana nyeupe na kofia nyeupe pia akaingia garini
“ Hi “ akawasalimu akina Mathew bila hata ya kuwatazama usoni halafu akawasha gari.Hakupita katika geti lile waliloingilia badala yake akazunguka nyuma ya nyumba kulikokuwa na geti lingine wakaondoka
“ Watu hawa ni akina nani? Mathew amewafahamuje? Huku tunakoenda wanatupeleka wapi? Akajiuliza Peniela

“ Napatwa na wasi wasi sana hasa nikikumbuka kilichotokea usiku wa leo.Team SC41 wamenifanyia kitendo cha kinyama sana.Kila kitu changu wamekiteketeza na kuniacha kama nilivyo.Nyaraka zangu ,kumbu kumbu zangu zote za muhimu zimeteketea.Huu ni ukatili usiovumilika.Nimefanya mambo mengi na mengine ya hatari kubwa kwa ajili ya team SC41 lakini haya ndiyo malipo yake? Kwa namna yoyote ile lazima nihakikishe ninaimaliza Team Sc41.Hata hivyo namshukuru sana Josh kwani bila yeye kunistua kuwa ninafuatiliwa na team SC41 sijui n ini kingetokea.Baada ya kunikosa sasa ni zamu yao.Moto huu lazima uwageukie wao” Akawaza Peniela huku safari ikiendelea.
“ Nyumba yangu naamini imechomwa moto na Team Sc41 lakini nani kaichoma moto nyumba ya Mathew na kwa nini ? Je ni team SC41? Kama ni wao walifahamu vipi niko pale? Kwa upande Fulani nalazimika kuamini watakuwa ni wao kwani tukio la kuchomwa moto nyumba yangu na ile ya Mathew vimetokea kwa wakati m moja.Nahisi aliyechoma nyumba zetu tayari alikuwa anafahamu mipango yetu na alifahamu kuwa mimi na Mathew tuna mashirikiano na ndiyo maana akaamua kuchoma nyumba zetu ili kuvuruga mipango yetu yote.Halafu bado sijapata jibu,Anitha,jaji Elibariki,na Yule kahaba Naomi wamesalimika katika moto ule? Au nao wameteketea?Haitaniuma kabisa kama jaji Elibariki na Naomi watakuwa wameteketea kwa moto kwani wanastahili ila nitaumia sana kama Anitha atakuwa amefariki.Anitha hastahili kufa kifo kigumu kama cha moto..Nitashirikiana na Mathew kuhakikisha wale wote waliofanya kitendo hiki wanalipa uovu wao” akawaza Peniela na kugeuka akamtazama Mathew.

“ Sijawahi kukutana na mtu jasiri kama huyu katika maisha yangu lakini pamoja na ujasiri wake kwa mara ya kwanza nimeshuhudia akimwaga chozi.Kitendo alichofanyiwa cha kuchomewa nyumba yake kimemuumiza mno.Anatakiwa kupata faraja ili apunguze hasira na machungu aliyonayo.Kwa kuwa niko k aribu naye nitajitahidi kwa kila niwezavyo kuhakikisha kuwa anapata faraja.He needs someone by his side.Vile vile ninapaswa kumshukuru sana kwani bila ya yeye leo nisingeweza kuwaponyoka team SC41.He’s my hero and this is the man I deserve to be in love with.Ni mwanaume wa kipekee kabisa ambaye yuko tayari kuhatarisha maisha yake kwa ajili yaw engine.After everything is over I hope me and him we’re going to be together for good.Japokuwa tuko katika matatizo lakini lazima nikiri kwamba najihisi kuanza kumpenda Mathew.Sielewi kama h isia hizi ni za kweli kwa sababu hisia zangu zimekuwa zikibadilika mara kwa mara mare leo kwa huyu,kesho kwa huyu lakini naamini safari hii hisia zangu ni za kweli.Imekuwa ni kawaida yangu kila nimuonapo mwanaume mzuri akanivutia basi hutokea kumpenda .Siwezi kuendelea na maisha ya namna hii..Natakiwa kubadilika.Mabadiliko yataanzia kwa Mathew.Hisia kwamba ninampenda zinazidi kukita mizizi yake ndani ya moyo wangu japokuwa sifahamu kama na yeye anahisi chochote juu yangu.” Peniela akamtazama tena Mathew aliyeonekana kuzama katika mawazo mazito

“ Kuna jambo bado linanipa mawazo mengi.Mathew na John Mwaulaya waliongea nini pale hospitali? Kwa nini John hakutaka nisikie mazungumzo yao? Kuna kitu gani hakutaka nikifahamu? Kwa nini M athew amekuwa mgumu sana kunieleza kile alichoelezwa na John ? Hapa lazima kuna jambo kubwa ambalo John alimweleza Mathew kwani nakumbuka baada tu ya kumaliza maongezi yao kulikuwa na mabadiliko katika sura ya Mathew.Kwa mujibu wa maelezo aliyowahi kutupa Mathew ni kwamba Team Sc41 wakiongozwa na John mwaulaya waliiteketeza nyumba yake ka moto miaka kadhaa iliyopita a katika tukio hilo familia yote ya Mathew pia iliteketea kwa moto.Tukio hili lilimfanya Mathew na John Mwaulaya wawe maadui wakubwa na siku zote Mathe alikuwa anatafuta nafasi ya kulipiza kisasi.Kinachonishangaza na kunipa udadisi ni kwamba baada ya mazungumzo yao Mathew hakuonyesha tena ile hasira yake kubwa kwa John Mwaualaya.Kitu gani basi John alimweleza Mathew kiasi cha kumfanya asiwe tena na hasira juu yake?Haiwezekani watu waliokuwa maadui wakubwa waongee na kupeana mikono baada ya kumaliza maongezi yao bila ya kuwa na jambo muhimu lililomaliza tofauti zao.Kuna kitu hapa ambacho nakikosa na ambach o lazima nikifahamu” akawaza Penila
Gari lilivuka daraja la Nyerere na kuelekea the Blue city au jiji la bluu.Huu ni mji mpya kabisa wa kimataifa ulioko Kigamboni.Waliwasili katika jengo moja kubwa llilozungushiwa uzio na dereva akapunguza mwendo wa gari akawasha taa ya kushoto kuashiria kwamba alikuwa anaingia katika jengo lile.Juu ya geti kulibandikwa kibao kikubwa kilichosomeka Calvary Ministry.
“Church?!!!..Peniela akashangaa



TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
PENIELA

SEASON 4

EPISODE 4


MTUNZI : PATRICK.CK

CONTACT : 0764294499

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA


Kitu gani basi John alimweleza Mathew kiasi cha kumfanya asiwe tena na hasira juu yake?Haiwezekani watu waliokuwa maadui wakubwa waongee na kupeana mikono baada ya kumaliza maongezi yao bila ya kuwa na jambo muhimu lililomaliza tofauti zao.Kuna kitu hapa ambacho nakikosa na ambach o lazima nikifahamu” akawaza Peniela
. Gari lilivuka daraja la Nyerere na kuelekea the Blue city au jiji la bluu.Huu ni mji mpya kabisa wa kimataifa ulioko Kigamboni.Waliwasili katika jengo moja kubwa llilozungushiwa uzio na dereva akapunguza mwendo wa gari akawasha taa ya kushoto kuashiria kwamba alikuwa anaingia katika jengo lile.Juu ya geti kulibandikwa kibao kikubwa kilichosomeka Calvary Ministry.

“ Church?!!!..Peniela akashangaa




ENDELEA………………..




“ Tumekuja kufuata nini hapa kanisani? Akajiuliza Peniela wakati gari likivuka geti la kanisa na kufuata bara bara iliyoelekea kushoto iliyoelekea katika jumba moja kubwa la ghorofa lililokuwa mita kadhaa toka katika kanisa lile kubwa.Kwa upande wa kaskazini mwa kanisa kama mita mia tano hivi kulionekana majengo sita makubwa ya ghorofa .
“ Sijawahi fika mahali hapa.Tumefuata nini? Tumemfuata nani? Maswali yangu hayataweza kupata majibu kwani Yule jamaa kule tulikotoka alitupa sharti la kutouliza chochote. Ninachopaswa kufanya ni kunyamaza na kusubiri kujua kinachoendelea” Akawaza Peniela
Nje ya jengo lile walilokweda kulikuwa na magari mawili, dereva akaegesha karibu kabisa na zile gari mbili halafu akawageukia akina Mathew
“ We’re here.You can get out now.” Akasema huku akiufungua mlango akashuka.Mathew na Peniela nao wakashuka wakaongozana na Yule dereva hadi katika mlango mkubwa wa kuingilia ndani.Yule jamaa akatoa kadi na kuipitisha katika sehemu maalum ya kupitishia kadi na mlango ukafunguka wakaingia ndani,akawaongoza katika lifti wakapanda hadi ghorofa ya nne.Mara tu milango ya lifti iilipofunguka wakajikuta wakitazamana na watu wawili waliovalia suti nyeusi.Yule kijana akaongea nao kwa kama dakika mbili pembeni halafu mmoja wao akawafanyia ishara akina Mathew wawafuate.Namna mambo yalivyokuwa yanakwenda yalizidi kumpa maswali mengi Peniela lakini alipata nguvu kila alipomtazama Mathew na kumuoana akiwa hana hata chembe ya wasi wasi.
Walipelekwa katika sebule kubwa lililosheheni samani za kupendeza .Baada ya dakika nne wakatokea wanawake wawili waliovalia mavazi ya wauguzi na kuwataka akina Mathew waongozane nao.Kila maelekezo yalipotolewa Peniela alimtazama kwanza Mathew kabla ya kufanya chochote.Bila wasi wasi Mathew akainuka na kuanza kuwafuata wale akina dada Peniela naye akafuata nyuma yake huku wale jamaa wawili wenye suti nyeusi wakiwa nyuma yao.Walipanda ghorofa ya tano wakaingia katika chumba kimoja chenye vifaa kama hospitali.Mmoja wa wale wauguzi akamtaka Peniela amfuate katika chumba kingine.Peniela akasita na kumtazama Mathew

“ It’s ok Penny.Go…” akasema Mathew na Peniela akaongozana na yule muuguzi hadi katika chumba kingine ambacho nacho kilikuwa na vifaa kama vile vilivyokuwa katika chumba kile alikomuacha Mathew.Yule muuguzi akamtaka avue nguo zote na aingie katika bafu akaoga na kisha akamuelekeza apande katika kitanda na kumtaka asubiri hapo.
“ Hapa ni wapi? Watu hawa ni akina nani? Mbona mambo yao wanayafanya kimya kila bila ya maelezo yoyote?Mbona Mathew anaonekana kuwaamini sana amewafahamuje watu hawa? Anyway ngoja niendelee kuvumilia nione kitakachotokea”
Peniela akaondolewa mawazoni baada ya mlango kufunguliwa na mtu mmoja aliyevalia koti la kidaktari akaingia
“ Hallow naitwa Dr Lucious Wade.Nataka nikufanyie uchunguzi wa mwili wako ili nijue kama kuna tatizo lolote umelipata.Naomba uendelee kulala hapo hapo kitandani” akasema Dr Lucious aliyeongea kiingereza chenye lafudhi ya Marekani .Alikaa katika kiti na kutazama mambo kadhaa katika kompyuta yake halafu akabonyeza vitufe kadhaa na mtambo Fulani uliokuwa juu ukashuka taratibu na kumfunika Peniela

“ Oh my God ! haya ni mambo gani sasa? Akawaza peniela akwa amefunikwa na mtambo ule.Baada ya dakika tano mtambo ukapanda juu.Dr Lucious akaendelea kucheza na kompyuta yake halafu akainuka na kumfuata Peniela
“ Uchunguzi unaonyesha hauna tatizo lolote kwa ndani wala nje.Uko salama “ akasema na kumtaka Peniela ainuke pale kitandani

“ Ninyi ni akina nani? Peniela akashindwa kuvumilia akajikuta akiuliza swali.Dr Lucious akamtazama kwa sekunde kadhaa na kusema
“ Mlipokuwa mnaletwa huku hamkupewa masharti yoyote?
“ Tulipewa sharti la kutouliza chochote”
“ Vizuri.Zingatia sharti hilo” akasema Dr Lucious na kutoka..Dakika mbili baadae akaingia tena Yule muuguzi akamtaka Peniela amfuate wakaelekea sebuleni.Baada ya muda mfupi Mathew naye akaingia pale sebuleni .Tayari alikwishatibiwa jeraha lake.Wakiwa bado sebuleni wakaletewa chakula chepesi wakala kimya kimya huku wakisimamiwa na wale jamaa wawili wenye suti nyeusi na walipomaliza kula wakaombwa wapumzike na wasubiri maelekezo mengine.Zilipita dakika kama kumi hivi akaingia sebuleni mwanamke mmoja mrembo akawasalimu akina Mathew halafu akawaelekeza kwamba kesho ndipo watakapopata nafasi ya kuonana na askofu.

“ Ninyi ni wapenzi? Akauliza yule mwanamke na kabla Mathew hajajibu Peniela akajibu
“ Ndiyo sisi ni wapenzi”
“ Vizuri.Nilifikiria kuwatenganisha lakini kwa kuwa ninyi ni wapenzi itawalazimu mlale katika chumba kimoja.Twendeni nikawaonyeshe mahala pa kulala” akasema na kuinuka ,akina Mathew nao wakamfuata.Aliwapeleka katika chumba kikubwa na kizuri.

“ Hiki ndicho chumba mtakacholala.Endapo mtahitaji chochote mtabonyeza kitufe kile cha rangi ya kijani na endapo kuna tatizo lolote na mnahitaji msaada basi mtabonyeza kitufe chekundu.Msihofu hapa mko sehemu salama kuna ulinzi wa kutosha “ akasema Yule mama na kutoka akawaacha akina Mathew peke yao.Peniela hakutaka kupoteza wakati akamvaa Mathew kwa swali
“ Mathew tell me,whats going on? Who are these people?
Mathew akageuza shingo akamtazama na kusema
“ Usihofu Peniela we’re safe here.Go to sleep and wait for tomorrow.It’s going t be a very long day.Go to sleep” akasema Mathew .Peniela hakuwa na la kusema .
“ Sawa Mathew tulale tujiandae na siku ya kesho”
“ Lala Peniela mimi sintalala,nitakesha macho nataka nihakikishe usalama wako.” Akasema Mathew na kwenda kuketi katika sofa lililokuwamo mle chumbani.



******


Kwa zaidi ya saa moja Dr Joshua alikuwa anaongea na mkuu wa polisi kanda ya Dar es salaam simuni.Kikubwa walichokiongea ni namna ya kulimaliza suala la jaji Elibariki ambaye tayari anatuhumiwa kwa kosa la kusababisha kifo cha Flaviana.Ulikuwa ni mjadala mrefu lakini mwishowe wakaelewana na kamanda wa poliisi dar es salaam akakubali ombi la Dr Joshua la kumsafisha jaji Elibariki dhidi ya tuhuma zote zilizokuwa zinamkabili .

“ Uuupppphhh !!!...Dr Joshua akasha pumzi baada ya kumaliza kuongea na kamanda wa polisi kanda ya Dar es salaam
“ Haikuwa rahisi kumshawishi kamanda amsafishe jaji Elibariki.kweli ni kazi ngumu kwa sababu tayari umma wote wa Tanzania unafahamu kuwa yeye ndiye aliyesababisha kifo cha Flaviana.Inahitaji kazi ya ziada kumsafisha tena mbele ya umma kwamba hakutenda kosa lile alilokuwa anashukiwa kulifanya.Hata hivyo nashukuru amekubali na ataifanya hiyo kazi” akawaza Dr Joshua akachukua kitambaa na kujifuta jasho
“ I have many things to solve tonight.Next is Kigomba” akainuka na kufungua mlango akamtuma mlinzi wake akamuite Dr Kigomba.Haikuchukua muda Dr Kigomba akawasili na Dr Joshua akamfanyia ishara aketi

“ Kigomba tuna mambo mengi ya kuzungumza mimi na wewe lakini muda umekwenda sana kwa hiyo tutazungumza kwa kirefu baada ya kumaliza shughuli za msiba hapo kesho” akaanzisha mazungumzo Dr Joshua.Dr Kigoma hakujibu kitu akatikisa kichwa na kumpa nafasi Dr Joshua ya kuendelea
“ kwa usiku wa leo kuna mambo mawili au matatu ambayo nitakufahamisha .Jambo la kwanza ni kuhusu biashara yetu na Hussein.Kutokana na hali halisi ilivyo hivi sasa nimeamua kusimamisha kwanza kila kitu hadi hapo baadae hali itakapotulia.”
Kauli ile ikamstua Dr Kigomba na mshangao haukujificha katika uso wake.
“ Mr President how???...Why ??!! we’re so close to finish everything…” akasema Dr Kigomba
“ Kigomba you don’t know whats going on right now na ndiyo maana umestuka na unashangaa.Nimefanya maamuzi haya kwa faida yetu sisi .Endapo tutaendelea na mipango yetu tutakuwa tunajiweka katika matatizo makubwa”
“ Mr President can you explain to me why you are doing this? We’ve sacrificed a lot for this.Maisha ya watu yamepotea ,iweje kila kitu kivurugike katika usiku mmoja?
“ Dr Kigomba mpango wetu umevuja.Tayari kuna watu wanaofahamu kila tunachokfanya na kila hatua tunayoichukua.Wapo watu ambao hawalali wanakesha wanapanga mipango ya kuipata package hiyo” akasema Dr Joshua
“ Who are they? Do you know them? Akuliza Dr Kigomba.Dr Joshua akamtazama na kusema
“ Do you trust me Kigomba? Akauliza Dr Joshua na kusimama

“ I do trust you me President and you know that..”|

“ Good..Naomba basi uniamini ninapokwambia kwamba tuko katika hatari na tutaendelea kujiweka katika hatari kubwa endapo tutaendelea na mipango yetu.”
Dr Kgomba akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Dr Joshua kama hutanieleza ni akina nani hao wanaohatarisha mipango yetu na kukushawishi uahirishe kila kitu ,sintakubaliana nawe hata kidogo.Mimi ni mshirika wako katika suala hili na nina haki ya kufahamu kila kinachoendelea katika mpango wetu.Tayari Hussein amekwisha lipa fedha zote na tayari amekwisha wasili ili kuchukua mzigo wake unadhani nini kitatokea iwapo utaahirisha kumpatia mzigo wake? Akauliza Dr Kigomba na kutazamana na Dr Joshua

“ What’s happening Dr Joshua? What’s going on? Tell me the truth and I’ll understand you.Kuna mambo yametokea ghafla ambayo nashindwa kuyaelewa na kubwa ni suala la kuibuka kwa jaji Elibariki mtu ambaye sote tunamfahamu kwamba ndiye kikwazo namba moja kwetu na tayari tumetumia nguvu kubwa kumsaka ikiwamo hata kulitumia jeshi la polisi.Nchi nzima wanafahamu kwamba Elibariki anasakwa kwa tuhuma za kusababisha mauaji lakini ghafla anaibuka na unaonekana ukiwa umeongozana naye na baada ya yeye kutokea tu ndipo kila kitu kimevurugika.Why Mr president..why???....” akauliza Dr Kigomba.Dr Joshua akaonekana kukerwa na maneno yale ya Dr Kigomba.Akavuta pumzi ndefu n a kusema
“ Jaji Elibariki ameibuka toka huko alikokuwa na kuja kunifumbua macho kuhusiana na kinachoendelea.Nilikupa jukumu la kumchunguza Peniela na kumfahamu kwa undani badala yake ukasahau jukumu lako na kuanzisha mahusiano naye.You did a very stupid thing Dr Kigomba !!!!..
Dr Kigomba akahamaki kwa kauli ile ya Dr Joshua

“ Dr Joshua don’t insult me because of that prostitute.Mwanamke Yule ni kahaba na hakatai mwanaume yeyote mwenye pesa.Ni yeye ndiye aliyenitaka na mimi sikufanya ajizi nika…….” Dr Joshua hakutaka kumuacha Dr Kigomba amalize kile alichotaka kukisema ghafla akamrukia na kumkaba koo.

“ Iwe ni mara ya kwanza na ya mwisho kumsema vibaya Peniela mbele yangu.You don’t know anything about her.Ukithubutu siku nyingine kumtukana au kumdharau Peniela I swear I’ll forget that we’re friends and I will destroy you!!! Do you understand me Kigomba? Akauliza Dr Joshua kwa ukali
“ Yes I understand” akajibu Dr Kigomba
“ Good.” Akasema Dr Joshua na kumuachia Kigomba

“ Sasa nisikilize vizuri,kuanzia sasa mipango yetu yote naisitisha hadi hapo nitakapotoa maelekezo mengine kwa hiyo naomba siku nyingine usijaribu kubishana na mimi pale ninapokuwa nimetoa maamuzi yangu.Kwa sasa nenda kapumzike kesho tuna siku ndefu.Nitaongea nawe zaidi baada ya msiba kumalizika” akasema Dr Joshua.
“ Sawa Dr Joshua”
“ It’s Mr President don’t forget that..!!! akasema Dr Joshua
“ Sawa Mr President ila kabla sijaondoka nahitaji kufahamu jambo moja.Kama kila kitu kimesimama tunafanyaje basi kuhusu zile fedha ambazo tayari tumelipwa? Ni wazi fedha zile haziwezi kurudi kwa hiyo nahitaji nipatiwe mgao wangu kabisa ili hata kama baadae biashara ikiendelea iwe ni kumkabidhi tu Hussein mzigo wake.”
Dr Joshua akamtazama Dr Kigomba kwa hasira na kusema
“ Masuala ya fedha ile nitaamua hapo baadae ndiyo maana nikakwambia kwamba tutaongea zaidi hapo baadae tutakapokuwa tumepata muda mzuri lakini kwa sasa kila kitu nimekiweka pembeni ili tuone upepo unavyokwenda.Nenda kapumzike Kigomba tayari ni usiku mwingi” akasema Dr Joshua.

“ Ok Mheshimiwa rais tutaonana kesho. “ Akasema Dr Kigomba na kuondoka

“ Kisiki kingine hiki nimeking’oa.Kwa sasa baada ya kumuweka pembeni Kigomba,mambo yangu yakwenda vizuri bila wasi wasi na pesa yote itakuwa yangu peke yangu.Kesho nitazihamisha zile fedha zote kutoka katika ile akaunti zilimowekwa na kuziweka katika akaunti nyingine .Sitaki kugawana na mtu yeyote Yule.Ili kujihakikishia kwamba pesa yote inakuwa yangu kuna watu wawili au watatu ambao lazima niwafumbe midomo haraka sana .Kwanza ni Rosemary Mkozumi pamoja na mumewe Deus Mkozumi.Hawa ni watu hatari sana kwangu.Hawa wote wanafahamu kuhusu jambo hili na Deus aliwahi hata kunipigia simu na kunitolea vitisho.Niliwahi kuwa na mpango wa kumuua lakini yalitokea mambo mengi kwa haraka na kunisahaulisha lakini safari hii lazima nimuondoe.Dr KIgomba yeye japokuwa bado ni mshirika wangu wa karibu sana na bado sijamuingiza katika orodha ya watu wanaotakiwa kukatwa ndimi zao lakini naye nadhani anastahili kabisa kuondolewa kwani anayafahamu mambo yangu mengi na anaweza kuwa mtu hatari sana kwangu.” Dr Joshua akaondoka pale sebuleni akaelekea chumbani kwake kujipumzisha



******


Baada ya kuondoka katika makazi ya Dr Joshua ,Dr Kigomba alihisi kuchanganyikiwa .Mambo mengi yalizunguka ndani ya kichwa chake lakini kubwa ni lile la Dr Joshua kusimamisha mipango yao yote ya kuiuza package yenye kirusi Aby kwa Hussein.
“ Lazima kuna jambo linaloendelea hapa.Haiwezekani Dr Joshua aahirishe kila kitu katika hatua hizi za mwishoni .Kuna mchezo unataka kuchezeka hapa.Hata mimi ni mwerevu na tayari nimeng’amua kinachoendelea .Ni wazi Dr Joshua anataka aniondoe kimya kimya katika mpango wetu na pesa yote abaki nayo yeye mwenyewe.Kwa hilo amekosea sana” akawaza Dr Kigomba halafu akachukua simu yake na kumpigia Jacob Kateka mkuu wa idara ya usalama wa taifa.
“ Hallow Kigomba? Akasema Jacob

“ Halow Jacob,samahani sana ndugu yangu kwa kukuamsha najua umepumzika mida hii”
“ Usijali Kigomba.Niambie kulikoni usiku huu?
“ Jacob nahitaji kukuona usiku huu”
“ Usiku huu” akauliza Jacob kwa mshangao kidogo
“ Ndiyo Jacob.Kuna suala la dharura nataka tulijadili.Ni muhimu sana tafadhali “
Jacob akafikiri kwa muda halafu akauliza
“ Kwani wewe uko wapi mida hii Kigomba na unataka tuonane wapi?
“ Usisumbuke tafadhali ninakuja nyumbani kwako sasa hivi”
“ Sawa Kigomba utanikuta hapa ninakusubiri.” Akasema Jacob.Dr Kigomba akamuelekeza dereva wake sehemu anakotaka kwenda.
Barabara nyingi hazikuwa na magari usiku huu hivyo haikumchukua muda mrefu Dr Kigomba kuwasili nyumbani kwa Jacob Kateka.Walinzi tayari walikuwa na taarifa zake hivyo mara tu alipofika geti likafunguliwa akaingia ndani.Jacob akamlaki Dr Kigomba akamkaribisha sebuleni
“ Karibu sana Dr Kigomba” akaanzisha mazungumzo Jacob
“ Ahsante Jacob.Samahani sana kwa kukusumbua usiku huu mkubwa.”
“ Bila samahani Kigomba.” Akajibu Jacob
Dr Kigomba akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Jacob nimekuja kwako usiku huu kuna jambo nataka nikueleze na nitaomba nitakachokueleza kibaki kati yangu na wewe.”
“ Usihofu Kigomba ,chochote tutakachokiongea hakitatoka nje ya kuta hizi.”

“ Good.” Akasema Dr Kigomba halafu zikapita sekunde kadhaa akasema
“ Dr Joshua amekupigia simu usiku huu?
“ Hapana sijapokea simu yoyote toka kwa mheshimiwa rais usiku wa leo.’

“ Vipi kuhusu Abel Mkokasule amekupigia simu usiku huu? Hajakutaarifu chochote?
“ Abel Mkokasule?!!..Jacob akashangaa
“Ndiyo.Hajakueleza chochote?
“ Hapana .Sijawasiliana kabisa na Abel siku nzima ya jana.Kwani kuna nini Kigomba?
“ Usiku huu Abel ameitwa ikulu na rais walikuwa na kikao cha siri “ akasema na kunyamaza

“ Abel anaongoza kitengo ambacho kiko chini ya ofisi ya rais na anaripoti moja kwa moja kwa rais.Kwa hiyo si ajabu kukutana usiku huu” akasema Jacob
“ Nalifahamu hilo lakini kikao cha leo hakikuwa kwa ajili ya mambo ya kawaida ya kikazi.Kuna jambo Dr Joshua alimuitia Abel.”

“ Ni jambo gani hilo? Unalifahamu?

“ Ndiyo ninalifahamu.Kuna biashara mimi na Dr Joshua tulikuwa tunaifanya.Kuna kitu tulikuwa tunataka kukiuza.Ni Package ambayo imehifadhiwa ikulu”
“ Hebu subiri kidogo Dr Kigomba.Unasema kuna package ambayo mnataka kuiuza? Kuna nini ndani ya package hiyo ? akauliza Jaco
“ Hata mimi sifahamu kuna nini ndani ya hiyo package ,anayefahamu ni Dr Joshua pekee lakini ninachofahamu mimi ni kwamba kilichomo ndani ya hiyo inayoitwa package kuna kitu cha thamani kubwa sana kwani fedha ambazo tulitegemea kupata kwa mauzo ya hiyo package ni nyingi mno.Its billions of money.Hapa siongelei bilioni mbili, tatu ,kumi au ishirini ni mamia ya mabilioni.” Akasema Dr Kigomba na kumfanya Jacob astuke

“ Dah ! basi kuna kitu cha thamani kubwa sana ndani ya hiyo package.” Akasema Jacob

“ ndiyo hivyo Jacob.Kuna kitu cha thamani kubwa mno.Mimi na Dr Joshua tumeshughulikia mchakato wa kuiuza package hiyo toka mwanzo na hadi kufikia hatua ya kukabidhiwa pesa na hatua iliyokuwa imebaki ni kumkabidhi mnunuzi aitwaye Hussein mzigo wake kwani tayari amekuja nchini kwa ajili ya kuuchukua lakini ghafla yakatokea mabadiliko usiku huu.Dr Joshua anadai kwamba kuna mambo yametokea na anasitisha biashara yetu.Nimemtaka anieleze ni mambo gani hayo yaliyotokea lakini hakuwa tayari kunieleza.Ninachofahamu mimi hakuna jambo lolote katika biashara yetu ile lililotokea bali ni njia ya Dr Joshua kuniondoa katika mpango halafu pesa zote abaki nazo yeye mwenyewe.” Akanyamaza wakatazamana kwa sekunde kadhaa
“ Kigomba kwa nini umeamua kunieleza mambo haya yote? Akauliza Jacob
“ Kwa sababu nataka tuungane na tufanye kitu kuhusiana na jambo hili” akasema Dr Kigomba bila kupepesa macho.
“ Unataka tuungane na tufanye kitu.” Akasema Jacob na kufkiri kidogo halafu akauliza
“What do you want me to do?

“ Nataka tutafute namna ya kuipata package hiyo na kuiuza “

“ Unataka tufanye nini?? Akauliza Jacob kwa mshangao
“ Nataka tuchukue biashara ile sisi wawili.Jacob nakuhakikishia package hiyo ina thamani kubwa.Ni fedha ambayo watakula hadi watoto wa vitukuu wetu.”

“ Kigomba bado umeniacha njia panda kwa maneno hayo uliyoniambia .Naomba unifafanulie kwa kina ili nielewe nini hasa unachokihitaji” akasema Jacob.Dr Kigomba akamueleza Jacob kwa kirefu kila kitu kiivyo
“ Kwa hiyo Jacob nahitaji kufahamu jambo moja tu kutoka kwako,kama umekubali tufanye jambo hili lenye manufaa makubwa kwetu na kwa vizazi vyetu.”
Jacob akafikiri kidogo na kusema

“ Kidogo nimeanza kukuelewa Kigomba lakini bado sijafahamu uhusika wangu ndani ya mpango huo endapo nitaamua kuubali.”
“ Usiogope kuhusu hilo.Ninachohitaji kukifahamu kwanza ni iwapo umekubali kujiunga nami katika mpango huu”
“ Kigomba ninakuamini na ninaamini kitu ulichonieleza ni cha kweli.Kama isingekuwa kweli usingenifuata usiku huu.I need money and we all need money na kwa kiwango hicho ulichonitajia ni wazi hakuna anayeweza kukataa labda awe malaika,kwa hiyo nimekubali kujiunga nawe na kikubwa kinachonifanya nikubali bila kusita ni kwa sababu ninamchukia sana Dr Joshua.Kitu kikubwa ninachokitaka ni sisi kukaa na kupanga mikakati namna ya kufanya kuipata hiyo package”
“ Nafurahi sana kusikia hivyo Jacob.Kwa kuwa hivi sasa muda umekwenda sana ,nitaonana nawe kesho ili tuongee zaidi na nikupe maelezo ya kina kuhusu mpango huu na kwa pamoja tuone nini cha kufanya.Narudia tena kukuhakikishia Jacob kwamba endapo mpango huu utafanikiwa basi tutaingia katika orodha ya mabilionea kwa hiyo nakuomba usije ukabadili mawazo” akasema Dr Kigomba
“ Only a fool can do that.Nakuhakikishia Kigomba siwezi kubadili mawazo.Nimekuwa mtiifu katika kazi yangu lakini hakuna chochote cha maana nilichokipata zaidi ya kujenga maadui wengi.Nadhani ni wakati wangu na mimi kufanya mambo ambayo wengine wanafanya yaani kujitengenezea maisha mazuri baada ya kustaafu” akasema Jacob

“ Ahsante Jacob kwa kuwa na muono huo.Muda wa uzalendo umepita na sasa ni wakati wa kujijengea maisha mazuri baada ya kustaafu.Tutaongea vizuri zaidi na kwa kirefu kesho.” Akasema Dr Kigomba na kisha wakaagana na Dr Kigomba akaondoka kuelekea nyumbani kwake

“ Kama ulifikiri una akili sana,ulikuwa unajidanganya Dr Joshua .Sasa nitakuonyesha kwamba kuna watu wana akili zaidi yako” akawaza Dr Kigomba wakati akielekea nyumbani kwake kupumzika.



TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
 
PENIELA
SEASON 4
EPISODE 5
MTUNZI : PATRICK.CK

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

Narudia tena kukuhakikishia Jacob kwamba endapo mpango huu utafanikiwa basi tutaingia katika orodha ya mabilionea kwa hiyo nakuomba usije ukabadili mawazo” akasema Dr Kigomba

“ Only a fool can do that.Nakuhakikishia Kigomba siwezi kubadili mawazo.Nimekuwa mtiifu katika kazi yangu lakini hakuna chochote cha maana nilichokipata zaidi ya kujenga maadui wengi.Nadhani ni wakati wangu na mimi kufanya mambo ambayo wengine wanafanya yaani kujitengenezea maisha mazuri baada ya kustaafu” akasema Jacob

“ Ahsante Jacob kwa kuwa na muono huo.Muda wa uzalendo umepita na sasa ni wakati wa kujijengea maisha mazuri baada ya kustaafu.Tutaongea vizuri zaidi na kwa kirefu kesho.” Akasema Dr Kigomba na kisha wakaagana na Dr Kigomba akaondoka kuelekea nyumbani kwake

“ Kama ulifikiri una akili sana,ulikuwa unajidanganya Dr Joshua .Sasa nitakuonyesha kwamba kuna watu wana akili zaidi yako” akawaza Dr Kigomba wakati akielekea nyumbani kwake kupumzika.

ENDELEA………………..

Kumekucha Tanzania .Taarifa ,kubwa iliyoliamsha taifa asubuhi hii ni tukio la polisi kupambana na majambazi wenye silaha katika msitu wa Makenge na kufanikiwa kuwaua majambazi wanne.Kwa mujibu wa kamanda wa polisi kanda ya Dare s salaam aliyehojiwa na waandishi wa habari muda mfupi baada ya tukio lile kutokea ni kwamba walipokea taarifa kuhusu kuwapo kwa kambi ya majambazi katika msitu wa Makenge kutoka kwa jaji Eibariki.

Kamanda Yule aliendelea kusema kwamba jaji huyo wa mahakama kuu ambayealikuwa anatuhumiwa kwa mauaji ya mke wake ambaye ni mtoto wa rais,alikuwa ametekwa na watu hao siku kadhaa zilizopita na alipelekwa katika msitu wa Makenge ambako alifichwa katika pango

“ Akiwa mafichoni“ akaendelea mkuu wa polisi kanda ya Dare s salaam
“ Watu wale walimtaka jaji Elibariki ampigie simu mke wake na kumtaka afike mahala walikopanga.Lengo lao lilikuwa ni kumteka Flaviana mtoto wa rais na kudai kiasi kikubwa cha fedha kutoka kwa rais ili wamuachie.

Jaji Elibariki alifanya kama alivyoelekezwa na Flaviana alipofika sehemu walikopanga wakutane majambazi wale walijitokeza na kutaka kumteka lakini kwa bahati nzuri alikuwa ameongozana na walinzi na hapo ndipo walipoanza kushambuliana na katika tukio hilo Flaviana alijeruhiwa kwa risasi akafariki akiwa katika matibabu nchini Afrika ya kusini.

Jaji Elibariki ,alifanikiwa kutoroka toka mafichoni alikokuwa anashikiliwa na majambazi hayo na kunipigia simu akanifahamisha kila kitu na kutuelekeza mahala wanakojificha majambazio hao .Usiku wa kuamkia leo polisi walivamia maficho ya majambazi hayo na pakatokea majibizano ya risasi kwa zaidi ya nusu saa lakini polisi walifanikiwa kuwadhibiti .

Majambazi wanne waliuawa na wawili walifanikiwa kutoroka.Katika eneo walilotumia majambazi hayo kama maficho yao kulikutwa na silaha mbili aina ya smg , na risasi mia moja na kumi.Kwa sasa jeshi la polisi linaendelea na msako mkali kuwatafuta majambazi waliotoroka pamoja na mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Mathew ambaye inasemekana ndiye anayeshirikiana na majambazi hayo na kuwasaidia katika kufanikisha mipango yao ya kihalifu”

Hii ilikuwa ni taarifa fupi iliyotolewa na kamanda wa polisi kanda ya Dar es salaam kwa baadhi ya waandishi wa habari,muda mfupi baada ya kutokea kwa tukio lile la majambazi na polisi kushambuliana kwa risasi katika msitu wa Makenge tukio lililotokea mida ya saa kumi na moja za alfajiri.

Dr Joshua ambaye kwa kawaida huwa hakosi kutazama taarifa ya habari .Aliitazama taarifa hii iliyopewa umuhimu mkubwa akatabasamu

“ he did it…!! Akasema kwa furaha

“ hawa ndio watu ninaopenda kufanya nao kazi.Ukimpa maelekezo yanafanyika kama unavyotaka.Nimeongea naye jana usiku na usiku huo huo akatafuta namna ya kulimaliza suala ambalo lilikuwa linanila sana akili yangu.I’m very Impressed .

Kabla ya uongozi wangu kumalizika lazima na huyu kamanda wa kanda ya Dare s salaam nimuache katika nafasi nzuri.” Akawaza Dr Joshua na kuchukua simu akazitafuta namba za kamanda wa polisi kanda ya Dar es salaam akampigia
“ hallow mzee.” Akasema Kamanda wa polisi baada ya kupokea simu

“ Habari yako Kamanda”

“ Habari nzuri sana mzee.Samahani nimechelewa kukupigia simu kukutaarifu kuhusiana na kukamilika kwa ile kazi uliyonipa”

“ Usijali kuhusu hilo kamanda,nimeona katika taarifa ya habari muda mfupi uliopita.Thank you so much”

“ Mzee,jana baada ya kumaliza kuzungumza nawe ,nilianza kuchekecha akili namna ya kufanya nikakumbuka niliwahi kupewa taarifa za kuwapo kwa majambazi wanaotumia msitu wa Makenge kama maficho yao .Taarifa hii haikuwa imefanyiwa kazi bado kwa hiyo nilikuwa nayo mimi pekee hivyo niliwaandaa vijana na kuwapa maelekezo na mimi mwenyewe nikaongozana nao hadi katika msitu wa Makenge na kweli tulifanikiwa kuwakuta majambazi hao tukawavamia na kushambuliana nao tukawaua wanne, wawili wakatoroka.

Hiyo ilikuwa ni njia nyepesi niliyoweza kuifanya ya kumsafisha tena Elibariki na kumuondoa katika zile tuhuma zilizokuwa zinamkabili.Kwa sasa mpira umerushwa kwa huyu Mathew na Elibariki amesafishika na hahusiki tena katika tuko lolote.

Nitaonana naye na kumpa maelekezo ya namna ya kuzungumza na waandishi wa habari ambao watapenda kumuhoji au mtu yeyote atakayemuuliza kuhusuana na tukio hili lakini hadi hapo nitakapokuwa nimeongea naye naomba asihojiwe na mtu yeyote Yule au chombo chochote cha habari”

“ Kamanda nimefurahi sana kwa namna ulivyo mbunifu.Sitaki nikuahidi chochote kwa sasa ila naomba unisubiri kwa kama wiki mbili hivi na utaona nitakachokufanyia.Watu watiifu kama ninyi mnastahili pongezi ya kiwango cha juu mo” akasema Dr Joshua

“ Nashukuru sana mheshimiwa rais” akasema Kamanda wa polisi
“ Hata mimi nashukuru sana na kwa kuwa hivi sasa bado nimebanwa na mambo mengi nitakuita hivi karibuni ili tujadili kuhusiana na huyu Mathew.”

“ Hakuna shaka mzee.Muda wowote ukinihitaji utanipa taarifa”

“ Ahsante kamanda .Nakukumbusha vile vile kuwa leo ni siku ya mazishi ya mwanangu na kutakuwepo na wageni mbali mbali marafiki zangu wa kutoka nje ya nchi kwa hiyo naomba suala la ulinzi lipewe kipaumbele kikubwa.”

“ Tayari nimekwisha toa maelekezo ya kuwepo kwa ulinzi wa kutosha eneo hilo kwa hiyo usihofu mheshimiwa “ akasema kamanda wa polis Dar es salaam wakaagana Dr Joshua akakata simu.

“ Lazima nimfanyie mambo makubwa huyu kamanda kwa namna alivyonisaidia katika suala hili.Kitakachofuata baada ya Elibariki kusafishika ni kuanza kumuandaa kwa ajili ya kushika madaraka makubwa.Najua kuna taratibu zake kwa mtu kama Elibariki ambaye ni jaji wa mahakama kuu kuingia katika mambo ya siasa lakini hilo si tatizo litakalonisumbua.

Elibariki kwa sasa tayari jina lake linafahamika,kwanza kama mhalifu na sasa anajulikana kama shujaa.Nitawaita wanamtandao wangu ili kwa pamoja tuanze kulijadili suala hili la kumuandaa Elibariki kwa nafasi ya urais” akawaza Dr Joshua.

“ Ngoja kwanza niachane na mambo haya ya jaji Elibariki,leo ni siku ndefu na ngumu.Ninamzika mwanangu Flaviana” akanyamaza na kuinamana na kuzama katika mawazo

“ Sikutegemea kama suala hili lingenifikisha hapa.Sikujua kama jambo hili lingewapoteza mke na wanangu.Hakuna wa kumlaumu kwa haya yote yaliyotokea,kwani ilikuwa ni lazima yatokee.Ninachopaswa kukifanya kwa sasa ni kuhakikisha lengo langu halikwami na ninafanikiwa kulimaliza suala la package .

Siko tayari kuyakosa mabilioni yale ya fedha ambayo tayari yametua mikononi mwangu.” Akawaza Dr Joshua halafu akaanza kujiandaa kwa ajili ya siku hiyo.Wakati akijiandaa mara mlango ukagongwa,akatoka na kukutana na mwanae Anna
“ Anna,how are you my princess??

“ I’m fine dady” akajibu Anna na kuingia akateti sofani

“ Nashukuru umekuja Anna kwani nilikuwa natazamia kukuita asubuhi hii ili tuongee kuhusiana na siku ya leo” akasema Dr Joshua halafu akanyamaza kidogo akamtazama Anna aliyekuwa amesawajika sana na kuendelea

“ Leo ni siku nyingine ngumu kwetu kama familia.Tunakwenda kumpumzisha dada yako Flaviana.Its hard but we have to be strong.Anna nakuomba sana uwe jasiri siku ya leo”

“ I’m trying dady.Najaribu sana kuwa jasiri lakini najikuta nashindwa .Why this is happening to us? Why always us” Anna akasema huku akilia

“ Usilie Anna.Kila jambo hutokea kwa sababu maalum na kifo ni mapenzi ya Mungu.Hatuwezi kujua Mungu ana makusudi gani kutuchukulia wapendwa wetu wawili ndani ya kipindi kifupi.Hata kabla ya arobaini ya mama yako haijawadia,ametutoka tena dada yako.

Japo ni mapenzi ya Mungu na yeye ndiye mwenye kutoa na kutwaa lakini inauma sana” akasema Dr Joshua na kuinama akionyesha majonzi makubwa.Sekunde kadhaa za ukimya zikapita Anna akainua kichwa na kusema
“ Who will be next??.
Swali lile likamstua Dr Joshua
“ Umesemaje Anna?

“ Nimeuliza nani atafuata kati yetu? Alianza mama ,akafuata Flaviana na sasa tumebaki wawili mimi na wewe kwa hiyo nani atakayefuata? Akauliza Anna.Dr Joshua akamtazama mwanae kwa sekunde kadhaa akashidwa ampe jibu gani
“ kwa nini umeuliza hivyo Anna?

“ kwa sababu naona kama kuna kitu kinaiandama familia yetu na ndiyo maana najiuliza hivyo”
Ukimya ukatanda mle ndani.Baada ya muda Anna akasema
“ Anyway dady forget what I said. Mambo haya yaliyotokea yamenichanganya mno akili yangu.Kitu kikubwa kilichonileta hapa kwako asubuhi hii ni kutaka kufahamu kuhusu jaji Elibariki.Nimemuona uko naye jana usiku.What is he doing here? Kwa nini hakamatwi? Akauliza Anna

“ Mimi ndiye ninayepaswa kulaumiwa kwa kutokukufahamisha mapema kuhusu jaji Elibariki.There is an explanation” akasema Dr Joshua
“ Explanation? What explanation dady?? He killed my sister so what can you explain to me? Akauliza Anna
“ Calm down Anna.Umetazama taarifa ya habari leo asubuhi?
“ Hapana sijaitazama.Kuna nini ?

“ Basi kama ungekuwa umetazama tayari ungekuwa na jibu Elibariki siye aliyemuua Flaviana”

“ What ???!! Anna akashangaa
“ Ndiyo Anna,Elibariki siye aliyemuua Flaviana”

“ Dady I don’t understand what you are talking about. Jeshi la polisi walilithibitisha hilo na wakaanzisha msako wa kumsaka Elibariki ,nini kimetokea ?

“ Ukweli umebainika kwamba Elibariki alitekwa na watu wasiojulikana na kwenda kufichwa katika msitu wa Makenge.Lengo kuu la watu hao ni kujipatia fedha na ndiyo maana wakamtumia ili awasiliane na Flaviana wakapanga wakutane sehemu ambako wale majambazi walikuwa wamejipanga ili wamteke Flaviana.

Kwa bahati nzuri kulikuwa na walinzi wa siri ambao walikuwa wanamlinda Flaviana ambao walipambana vilivyo na majambazi hao na katika mapambano hayo Flaviana akajeruhiwa kwa risasi.Jana Elibariki alifanikiwa kuwaponyoka majambazi wale na kukimbia na mtu wakwanza kumpigia simu baada ya kutoroka alikuwa ni mimi.

Alinieleza kila kitu na mahala alipo nikampiga simu kamanda wa polisi kanda ya Dare s salaam nikamtaarifu kuhusu suala hili na usiku wa kuamkia leo polisi walivamia maficho ya majambazi hao na kufanikiwa kuwaua watatu na wawili wakakimbia.

Kwa sasa jeshi la plisi linawasaka majambazi yaliyokimbia pamoja na mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Mathew ambaye ndiye mfadhili wao.Kwa maana hiyo basi jaji Elibariki hahusiki kabisa na kifo cha dada yako.” Akasema Dr Joshua wakabaki wanatamana.Anna akataka kusema kitu lakini mlango ukafunguliwa akaingia mlinzi wa rais

“ Mzee kuna mgeni wako amefika anakusubiri pindi ukimaliza maongezi”
“ Ni nani? Akauliza Dr Joshua
“ Abel mkokasule”
Dr Joshua hakutaka kupoteza muda akamtaka Anna aende akajiandae ili yeye apate muda wa kuongea na mgeni wake .Anna akatoka japo kwa shingo upande.

“ hallow Abel,karibu sana “ akasema Dr Joshua
“ Ahsante sana mzee.Samahani kwa kukuvamia asubuhi asubuhi namna hii.
“ Bila samahani Abel.I hope you have something for me this morning”
“ Ndiyo mzee” akajibu Abel

“ Tell me good news Abel..” akasema Dr Joshua huku akitabasamu
“ Tulipoachana jana usiku niliwapanga vijana wangu na tukaanza kazi mara moja.Kama ulivyoelekeza ,usiku huo huo tulianza kumfuatilia Dr Kigomba.Alipotoka hapa kwako,aliekea moja kwa moja kwa mkurugenzi wa idara ya usalama wa taifa Jacob kateka” akasema Abel.
“ Alikwenda kuonana na Jacob Kateka?..Dr Joshua akashangaa

“ Ndiyo mzee”

“ Alikwenda kumueleza kitu gani? Mlifanikiwa kunasa maongezi yao?
“ Hapana mzee hatukufaikiwa kunasa maongezi yao”
Taarifa ile ikaonekana kumchanganya kidogo Dr Joshua

“ Kama baada ya kutoka hapa alikwenda kuonana na Jacob basi lazima kuna jambo alikwenda kumueleza.Waliongea mambo gani? Naanza kuhisi lazima Kigomba atakuwa amemueleza Jacob kuhusiana na mpango wetu.Kigomba anaanza kudhihirisha ni kwa namna gani alivyo hatari kwangu.

Anafahamu mambo yangu mengi na anafahamu mipango yangu yote na ninahisi atakuwa na mipango ya siri ya kunivurugia mipango yangu.Natakiwa kufahamu kitu ambacho wawili hawa wanakipanga na kikubwa zaidi natakiwa kumshughulikia Kigomba haraka iwezekanavyo .

Endapo nitamuacha huyu jamaa basi lazima kuna jambo anapanga kulifanya.Na kama amemweleza Jacob basi lazima wawili hawa watakuwa wameungana na kupanga njama za kunihujumu.I’m going to deal with them “

“ Mr President..!!” Abel Mkosasule akamstua Dr Joshua toka mawazoni

“ Oh Samahani Abel kuna jambo nilikuwa nawaza.Ahsante sana kwa taarifa hii.Endeleeni kumfuatilia Kigomba kila aendako na kila anachokifanya kisha unipe taarifa.Nataka kufahamu watu anaokutana nao na kama ikiwezekana nataka kujua hadi kile wanachokiongea.

Kitu kingine ambacho kinaweza kuwasaidieni kumpata vizuri Kigomba ni kwamba ni mdhaifu mno kwa wanawake.Utumieni udhaifu huo kufanikisha kazi yenu” akasema Dr Joshua

“ Ahsante sana mzee kwa wazo hilo.Tutaendelea kumfuatilia Kigomba na nitakupa taarifa kamili jioni ya leo.Tukiachana na suala la Kigomba kuna kazi ulinipatia ya kumpata Jessica na kumpeleka Dark house.Napenda kukutaarifu pia kuwa alfajiri ya leo tumefanikiwa kumpata na tayari amepelekwa dark house tunasubiri maelekezo yako”
Dr Joshua akaachia tabasamu kubwa na kusema

“ Good Job Abel.Najuta kwa nini nisingekutumia wewe toka awali,ninsingefika hapa nilipofika”

“ Unasemaje mzee? Akauliza Abel

“ Oh sorry,forget what I said.Kazi nzuri sana umeifanya Abel .Endelea kumuweka Jessica Dark house hadi hapo nitakapokupa maelekezo mengine.Jioni ya leo nataka tuonane kuna kazi ambayo nataka uifanye.

Nilikudokeza kwamba kuna mtu yuko sehemu Fulani anashikiliwa kwa hiyo nataka mtu huyo akachukuliwe toka mahala hapo naye pia apelekwe dark house.Ni kazi ya hatari kidogo kutokana na mahala aliko huyo mtu kuwa ni sehemu yenye ulinzi mkali kwa hiyo waweke tayari vijana wako” akasema Dr Joshua

“ Usijali Dr Joshua.Vijana wako tayari kwa kazi muda wowote”
“ Ahsante sana Abel kwa taarifa nzuri.Nenda kaendelee na kazi na tutaonana hapa jioni ya leo.Nitakufahamisha muda nitakaokuwa na nafasi” akasema Dr Joshua na kuagana na Abel akaondoka

“ Dr Kigomba alikwenda kufanya nini nyumbani kwa Jacob usiku ule mwingi? Kuna kitu gani kinaendelea kati yao? Naanza kuhisi Kigomba kuna jambo analipanga na Jacob na lazima jambo lenyewe litakuwa ni kuhusiana na ile package.

Ngoja kwanza nimalize shughuli za msiba wa mwanangu halafu nitaamua niwafanye nini lakini wakae wanajua kwamba kama wana mipango yoyote mibaya juu yangu wanajisumbua bure kwani hawatafanikiwa .Kushindana nami ni sawa na kushindana na moto wa nyika..

Mimi ndiye raia namba moja hapa nchini na kila kitu kipo ch…..” Mlio wa simu ukamstua Dr Joshua akaichukua na kutazama mpigaji.Alizifahamu namba zile ni namba za zamani za Dr Kigomba

“ Hallow Kigomba” akasema Dr Joshua
“ Mr President habari za asubuhi ?
“ Habari nzuri Kigomba.Kuhusu ile simu yako nataka kuikabidhi kwa vijana wetu wa usalama waifanyie uchunguzi na kubaini kama kweli imeunganishwa halafu utarejeshewa.Habari za toka jana?

“ Habari nzuri mheshimiwa rais.Nitashukuru sana mzee kama nitarejeshewa simu yangu kwani watu wengi wanaifahamu ile namba wananitafuta na kunikosa” akasema Dr Kigomba na kunyamaza kidogo halafu akasema

“ Dr Joshua kuna jambo limenistua na ndiyo maana nimekupigia simu.Nimekuja katika hii hoteli ambako Hussein na ujumbe wake walifikia kwa lengo la kutaka kuhakikisha wako salama lakini kitu cha kushangaza Hussein na ujumbe wake wamehamishwa alfajiri ya leo.Unafahamu chochote kuhusu jambo hili? Akauliza Dr Kigomba

“ Ndiyo ninafahamu Kigomba na mimi ndiye niliyetoa maelekezo hayo”
Kupitia spika za simu Dr Kigomba akasikika akishusha pumzi.
“ Kigomba kuna tatizo lolote kwani? Akauliza Dr Joshua
“ Hakuna tatizo Dr Joshua kama wamehamishwa kwa amri yako.Naweza ukaniambia wamehamishiwa wapi?

“ No I cant tell you now.” Akasema Dr Joshua na kuzidi kumkasirisha Dr Kigomba
“ Dr Joshua whats going on? Kwa nini unanificha na hutaki kunieleza kitu gani kinachoendelea ? Don’t you trust me?
“ Kigomba nimekwisha kueleza kwamba subiri kwanza tuyamalize masuala ya msiba halafu tutakaa na nitakueleza kila kitu kinachoendelea.Do you understand me Kigomba? Akauliza Dr Joshua.
“ Yes I do” akajibu Dr Kigomba
`
“ Good.Now come over here.I’m waiting for you.Shughuli zinatakiwa kuanza mapema” akasema Dr Joshua na kukata simu
“ Damn ! you Joshua.Unajifanya wewe una akili sana basi nitakuonyesha namna ulivyo mjinga!!.akawaza Dr Kigomba akiwa garini akielekea kwa Dr Joshua .Akachukua simu na kumpigia Jacob Kateka.

“ Habari za asubuhi Dr Kigomba? Akauliza Jacob baada ya kupokea simu

“ Habari nzuri Jacob.Nimekupigia simu kukufahamisha kuhusu sarakasi za Yule mtu wetu,Nimetoka katika hoteli niliyokuwa nimewatafutia Hussein ana ujumbe wake,nimekuta wameamishwa hoteli alfajiri ya leo.

Nimempigia simu Dr Joshua nikamuuliza kama analifahamu jambo hili akasema kwamba ni yeye aliyetoa amri ya kuwahamisha Hussein na ujumbe wake na amegoma kabisa kunieleza mahala alikowahamishia.Zote hizi ni harakati zake za kutaka kuniengua katika mpango wetu na kumiliki kila kitu mwenyewe.

Nitakuja kuonana nawe jioni ya leo ili tupange mikakati mizito nini tufanye” akasema Dr Kigomba akaagana na Jacob Kateka kwa miadi ya kuonana jioni.


TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
Hii ni kama movie moja ya Wisley Sniper inaitwa Murder at 16......yaaan copy and paste
 
Usiku mwema japo Mathew na Peniela wapo Ukimyani. Elibariki kashaanza kufikiria namna ya kujirudi kwa Mathew. Naona Dr Joshua akituma kikosi kazi cha kumvamia Rosemary.
Kesho Mchana weka tatu hivi mkuu.

Lege waishi arusha nini maana leo hakuna umeme kabisa yaani hapa powerbank ndo imemalizika chaji.
 
Back
Top Bottom