mrengo wa kushoto
Senior Member
- Sep 27, 2015
- 100
- 185
Lengo zima la mifuko ya jamii ni kumkinga na kumlinda mwanachama wake dhidi ya majanga.
Majanga ni vitu vyoote vinavyoweza kuondoa au kupunguza uwezo wa mtu kuzalisha.
Moja ya janga kubwa ni UZEE.Tunaliita ni janga kwasababu tunaamini huna uwezo wa kuzalisha na kuchangia kiuchumi kama ulivyokuwa kijana.
Fedha ya pensheni ya uzeeni inalengo la kukupinguzia ukali wa maisha katika kile kipindi baada ya kustaafu, kwasababu huwezi kumrithisha mtoto wako kazi yako kama mfanyabiashara itabidi uwe na chanzo cha kipato walao kidogo cha kukusaidia.
Kelele nyingi zipo kwenye swala la Kikokotoo kipi kitumike kitakacholeta tija zaidi kwa mstaafu kati 25/75 ambapo lumpsum (pensheni kubwa) ya 25% kwa pensheni ya kila mwezi ya 75% na hivyo hivyo kwa 33%/67%, 75%/25% ya kiasi cha jumla cha michango pamoja na interest(gawio) la miaka yote ya uchangiaji.
Serekali ipo sahihi kabisa kuweka kikokotoo kilichopo na kwa upande wangu ningependa kingeshushwa zaidi ya hapo tukarudi kwenye 25% ya lumpsum(pensheni kubwa) na 75% (pensheni ya kila mwezi)
KWANINI? Mfano unamichango ya mill 100 katika kipindi chako cha kuajiriwa.
Ukapewa 25mill kama pensheni kubwa na ile 75mill ikigawanywa kwa miaka 10 inakiwa 7.5 kwa mwaka na ukiigawanya 7.5 /miezi 12 unakuwa na laki 625,000 kila mwezi kwa maisha yako yote yaliyobaki hata kama utaishi miaka 60 mingine.
Ukinipa 75 mil na labda sikuwahi kushika hata 10mill kwenye maisha na ajira yangu kwa pamoja,kweli nitafurahia mwaka wangu wa kwanza lakini kumbuka sina nguvu za kuzalisha kama nilivyokuwa kijana,akili maono siyo sawa na vijana siwezi kwenda kuanza kuparangana Kariakoo au karume kwenda china kuafat mzigo na kadhaliaka.
Kitu kikubwa nitaanza kuuliza biashara za kufanya na kuanza kujaribu jaribu. Hapo utapigwa sana na baada ya miaka mi3 hela inaweza kuwa haionekani. Kumbuka nimebakiza 25mill kwenye pensheni ya kila mwezi.
25mill/10miaka= 2.5mill na 2.5mill/12miezi inakuwa 208,000 kwa mwezi.
Anaeishi kwa 625,000 na anaeishi kwa 208,000 kwa mwezi tofauti inaanza kuonekana baada ya miaka 3_4.
Hapo tunajenga wazee tegemezi,ombaomba na waliokosa muelekeo kila siku kulalamikia watoto wao. Hapo ukute bado anasomesha, hajajenga etc.
Unapokuwa huna hela mipango inakuwa mingi lakini ukiipata na hujawahi kuishika wengi malengo yanapotea kabisa na kuitumia vibaya wakijua kesho itakuwepo.
Majanga ni vitu vyoote vinavyoweza kuondoa au kupunguza uwezo wa mtu kuzalisha.
Moja ya janga kubwa ni UZEE.Tunaliita ni janga kwasababu tunaamini huna uwezo wa kuzalisha na kuchangia kiuchumi kama ulivyokuwa kijana.
Fedha ya pensheni ya uzeeni inalengo la kukupinguzia ukali wa maisha katika kile kipindi baada ya kustaafu, kwasababu huwezi kumrithisha mtoto wako kazi yako kama mfanyabiashara itabidi uwe na chanzo cha kipato walao kidogo cha kukusaidia.
Kelele nyingi zipo kwenye swala la Kikokotoo kipi kitumike kitakacholeta tija zaidi kwa mstaafu kati 25/75 ambapo lumpsum (pensheni kubwa) ya 25% kwa pensheni ya kila mwezi ya 75% na hivyo hivyo kwa 33%/67%, 75%/25% ya kiasi cha jumla cha michango pamoja na interest(gawio) la miaka yote ya uchangiaji.
Serekali ipo sahihi kabisa kuweka kikokotoo kilichopo na kwa upande wangu ningependa kingeshushwa zaidi ya hapo tukarudi kwenye 25% ya lumpsum(pensheni kubwa) na 75% (pensheni ya kila mwezi)
KWANINI? Mfano unamichango ya mill 100 katika kipindi chako cha kuajiriwa.
Ukapewa 25mill kama pensheni kubwa na ile 75mill ikigawanywa kwa miaka 10 inakiwa 7.5 kwa mwaka na ukiigawanya 7.5 /miezi 12 unakuwa na laki 625,000 kila mwezi kwa maisha yako yote yaliyobaki hata kama utaishi miaka 60 mingine.
Ukinipa 75 mil na labda sikuwahi kushika hata 10mill kwenye maisha na ajira yangu kwa pamoja,kweli nitafurahia mwaka wangu wa kwanza lakini kumbuka sina nguvu za kuzalisha kama nilivyokuwa kijana,akili maono siyo sawa na vijana siwezi kwenda kuanza kuparangana Kariakoo au karume kwenda china kuafat mzigo na kadhaliaka.
Kitu kikubwa nitaanza kuuliza biashara za kufanya na kuanza kujaribu jaribu. Hapo utapigwa sana na baada ya miaka mi3 hela inaweza kuwa haionekani. Kumbuka nimebakiza 25mill kwenye pensheni ya kila mwezi.
25mill/10miaka= 2.5mill na 2.5mill/12miezi inakuwa 208,000 kwa mwezi.
Anaeishi kwa 625,000 na anaeishi kwa 208,000 kwa mwezi tofauti inaanza kuonekana baada ya miaka 3_4.
Hapo tunajenga wazee tegemezi,ombaomba na waliokosa muelekeo kila siku kulalamikia watoto wao. Hapo ukute bado anasomesha, hajajenga etc.
Unapokuwa huna hela mipango inakuwa mingi lakini ukiipata na hujawahi kuishika wengi malengo yanapotea kabisa na kuitumia vibaya wakijua kesho itakuwepo.