Penye nia pana njia: Ni wiki ya 5 sasa sijatia soda mdomoni, kumbe inawezakana kabisa

Hongera sana. Mimi siku ya tatu sasa sijapata kileo.
 
Mwaka wa 8 huu sinywi hayo matakataka. Sio soda, sio juice za kopo, sio energy drinks, sio aina yoyote ya kilevi. Vilevi vingine nje ya soda sijawahi kuvigusa toka nizaliwe. Ni maji tu.
Ila utakufa tu,alisikika mlevi mmoja
 
Soda siyo nzuri kiafya, ukiweza kupunguza au kuacha kabisa ni jambo jema kwa afya yako.

Tena atleast ukinywa unywe hizi soda sugar free kama Coca zero, sprite zero, pepsi bonge angalau unapunguza risk.

Kwenye hizi soda kuna sukari ya kufa mtu.
Hata hizo unakuwa ujapunguza risk, hizo zote ni kemikali. Yale yale unakuta mtu eti soda anywi ila anavuta sigara.
 
Mmh, mi nikajua fegi. Soda haina addiction.
 
kwann huli chips

Sent from my Infinix X572 using JamiiForums mobile app
Tatizo ni uandaaji tu, mafuta mengi halafu mafuta yenyewe yana cholesterol.

Ila siku hizi kuna mashine zinauzwa madukani hata game zipo unaweza kukaanga chips bila kutumia mafuta, hizo ni chips salama kabisa kuleni.
Mwamba hali chipsi ila anakula viazi mviringo.
Viazi ulaya vikipikwa ni chakula kizuri sana, wanawake wangekuwa wanajielewa hiki ndio kingekuwa chakula chao kikuu na siyo chips.

Viazi ulaya vya kupiga vina matokeo mazuri kwa kutengeneza hips za wanawake wala huitaji mchina.
 
Kuacha kunywa soda ni rahisi sana,
Kula chakula, kunywa juice ya matunda halisi.

Kisha baadae kunywa maji mengi ya kawaida ya uhitaji wa size ya body lako
Mimi matumizi yangu makubwa Ni maji, kwa 24 hrs nakunywa 1.5 lt chupa 6 au 7. Kwenda kwa watu lazima nibebe maji kwenye begi. Safarini napata tabu Sana maana nalazimika kutokunywa maji ili kuzuia kukojoa Mara kwa Mara. Je hii nayo Ni addiction?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…