Pep Guardiola ndio Kocha Bora kwa sasa Duniani

Mbona kwenye La Liga Mou alisanda kwa Pep hata EPL pia
Jose Mourinho ndiye alimfukuzisha kazi Pep Kiparangoto pale Hispania baada ya kupigwa nnje ndani kwa wiki 1 tu huku Real Madrid ikitwaa EPL na Copa Del Rey, fuatilia vizuri kumbukumbu za mwaka wa mwisho Pep kuifundisha Barcelona utanishukuru.

Pep anamuheshimu sana Mourinho kwenye mechi za mtoano na anamwelewa vyema sana kuwa Special One huwa hacheki na kima akiwa kwenye hatua hizo.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Stone, Everton, benardo monaco , Ederson wapi? Akanji

Tuache unafiki jamaa anajua kutafuta wachezaji wazuri

Hao wachezaji sio beikubwa ila kawatengeneza ata Alvarez unajua alikotoka!
 
Pep Guardiola ni genius nilianza kuliona hilo tangu alipoanza kukinoa kikosi cha Barça
Pep nilianza kumchukia akiwa Barca kwa ishu ya Yaya Toure, akaja kurikera tena kwa ishu ya Ronaldinho akamalizia kunitibua nafsi alivyozinguana na Et'oo.
Alivyohamia Mancity akanitibua tena kwa bifu lake na Yaya Toure, ila yote kwa yote hata umchukie Guardiola kwa kiasi gani ila ni lazima umkubali kimoyomoyo na umpe heshima yake kama kocha bora zaidi duniani kwa sasa.
 
Nani katengeneza hiyo team yenye quality players
 
●Sababu ya Pep kuondoka Barça:
Ngoja kwanza nikupe sababu ya Pep kuondoka Barça. Baada ya Barça kutolewa na Chelsea kwenye UEFA msimu wa 2011/2012, Pep alitangaza kuwa ataondoka Barça mwishoni mwa msimu huo. Hivyo kusema Mou ndiye aliyemfukuzisha kazi sio sahihi kabisa.

Tuanze sasa historia nzuri kati ya Pep na Mou pale Spain

▪︎RMA walimsajili Mourinho mwaka 2010

▪︎Pep akaondoka Barça 2012

Tupitie rekodi zao za misimu miwili waliyokutana 2010/2011 na 2011/2012

MSIMU WA 2010/2011 (Pep vs Mou)
(1)Walipokutana kwa mara ya kwanza kwenye la liga RMA alilamba goli 5-0 pale Camp Noú msimu huo Barça wakabeba kombe la La Liga

(2)Kwenye semi final ya UEFA wakakutana Barça na RMA. Barça akamtoa RMA kwa aggregate ya 3-1, Barça akanyanyua UEFA msimu huo.

(3)Mwaka huo RMA chini ya Mou waliambulia Copa del Rey tu

MSIMU WA 2011/2012 (Pep vs Mou)
(1)Barça na RMA walikutana kwenye Spanish Super Cup. Barça wakashinda 5-4 in aggregate

(2)Msimu huu Barça chini ya Pep walishinda kombe la Copa del Rey na Spanish Super Cup

(3)RMA walinyanyua kombe la La Liga

Kwa takwimu hizo ni nani alikuwa bora Pep au Mou?
 
Alitaka wachezaji wenye nidhamu. Na hii ni kanuni ya kwanza ili uwe kocha mzuri

Ronaldinho alipokuwa star alianza kuwa mtu wa night life yeye na Deco. Hata viwango vyao vikashuka

Ikiwa angewafukuza halafu Barça isifanye vizuri sawa lakini aliwafukuza na akatengeneza kikosi bora zaidi
 
Mwanzo kwa yale mapenzi yetu kwa hao wachezaji tulikua hatulioni hilo zaidi ya kumuona kama ni mbaguzi tu wa rangi, maana wachezaji karibia wengi aliokua anazinguana nao walikua ni weusi.
Ila sasa hivi ndio tunaelewa kua Pep alikua kwenye msimamo sahihi, maana kocha akishindwa kusimamia nidhamu ya timu ni vigumu sana kupata mafanikio.
 
Uko sahihi
 
Mourinho alipewa Madrd ina Ronaldo,modric,benzema,ozil na mastaa kibao alifanya nini?
 
Acha kinyesi maua
 
Stone, Everton, benardo monaco , Ederson wapi? Akanji

Tuache unafiki jamaa anajua kutafuta wachezaji wazuri

Hao wachezaji sio beikubwa ila kawatengeneza ata Alvarez unajua alikotoka!
Kwahiyo tukimpa tot atabeba ubingwa?? Alaf pep hajatengeneza mchezaj yoyote,hao wote kawachukua wapo kwenye form zaoo
 
Weusi wamejazana crystal palace timu imekuwa kama timu ya taifa ya ghana wanafuga rasta tu pale
 
Ni kama scolari alivyoamua kumuacha romario WC ya 2002 na kumchukua dinho nchini kwake watu walisema sana ili mwisho wa siku kombe akalibeba
Kocha anatakiwa awe na misimamo yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…