Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Utakuta hata hivyo vikao vya juu na vyenyewe vimejengwa kwa msingi wa rushwa!sasa ndio wakati wa vikao vya juu kuchunguza wagombea wote walio toa au kujihusisha na rushwa hata kama walipata Kura 100% waondolewe na lipitishwe jina ambalo halina makandokando.
HakikaUtakuta hata hivyo vikao vya juu na vyenyewe vimejengwa kwa msingi wa rushwa!
Mambo yamebadilika ndani ya CCM. Dosari kubwa ni jinsi mchakato wa kupata wagombea unavyoendeshwa ambapo hakuna tena muda wa mwanachama anayegombea kujieleza kwa undani na kumwaga sera na mipango yake ya maendeleo.
HAKUNA mgombea yoyote katika jimbo lolote aliyepata kura tano na kuendelea ambaye hajatoa rushwa kwa wajumbe wanaopiga kura, HAKUNA. Mambo ya umaarufu na sifa zingine yanafuata baadae. Na hii si siri hata wakuu wa chama wanajua.
Mwalimu Nyerere aliwahi kuonya huko nyuma kwamba sasa kwenye CCM pesa imekua ndio qualification ya mtu kuchaguliwa kwenye uongozi wakati hapo awali pesa ilikua ni disqualification.
Hatari yake ni kwamba inajenga utamaduni wa watu kununua kura na kununua chaguzi na hata wale malaya wa kisiasa wanatengenezwa na tabia hii ambayo imeachiwa iote mizizi kitu ambacho sio afya kwa mustakabali wa CCM yenyewe na nchi kwa ujumla.
Hatari kwa afya ya Taifa
Jina lisilokuwa na makandokando litapitishwaje wakati lina kura 0?lipitishwe jina ambalo halina makandokando.
CCM wasipochukua hatua madhubuti kukomesha hii hali watakua wameonyesha mfano mbaya kabisa na huku ni kufeli kwa ahadi yao ya kupambana na rushwaRushwa ilitawala mchakato wote wa kuwapata wagombea.
Umeona eeh!?Jina lisilokuwa na makandokando litapitishwaje wakati lina kura 0?
Mkuu hilo sahau. Tulia, Kabudi, Jaffo, Majaliwa, Mpango, Ndalichako, etc wote wakatwe kisa akina nonihino wameangukia pua?Ikibidi wapitishe majina ya wagombea wasafi hata kama italazimika kumchukua mtu aliyepata sifuri lakini hakutumia rushwa kwenye uchaguzi.
Kama hao nao walitumia rushwa kupata nafasi zao na kama kutakua na kusitasita kuwachukulia hatua basi vita dhidi ya rushwa haitafanikiwa kwasababu haipiganwi. Wakati wa CCM ya Mwl Nyerere hapakua na double standard za kuwapendelea baadhi ya watoa rushwa na kuwaonea wengineMkuu hilo sahau. Tulia, Kabudi, Jaffo, Majaliwa, Mpango, Ndalichako, etc wote wakatwe kisa akina nonihino wameangukia pua?
Mkuu rushwa ina harufu mbaya, rushwa inanuka japo haionekani wakati wanapeana kwa kificho au hadharani. Kinachoonekana ni matokeo ya rushwa. Nzi wa uchafu wa rushwa ni kuchagua watu watakaojenga taifa la mambumbumbu wachumia tumbo hata kama ni Phd holders, no msiba kwa taifaHujaweka hata evidence ya rushwa
Si mlisema kuwa Magufuli karejesha nidhamu na uzalendo?Mambo yamebadilika ndani ya CCM. Dosari kubwa ni jinsi mchakato wa kupata wagombea unavyoendeshwa ambapo hakuna tena muda wa mwanachama anayegombea kujieleza kwa undani na kumwaga sera na mipango yake ya maendeleo.
HAKUNA mgombea yoyote katika jimbo lolote aliyepata kura tano na kuendelea ambaye hajatoa rushwa kwa wajumbe wanaopiga kura, HAKUNA. Mambo ya umaarufu na sifa zingine yanafuata baadae. Na hii si siri hata wakuu wa chama wanajua.
Mwalimu Nyerere aliwahi kuonya huko nyuma kwamba sasa kwenye CCM pesa imekua ndio qualification ya mtu kuchaguliwa kwenye uongozi wakati hapo awali pesa ilikua ni disqualification.
Hatari yake ni kwamba inajenga utamaduni wa watu kununua kura na kununua chaguzi na hata wale malaya wa kisiasa wanatengenezwa na tabia hii ambayo imeachiwa iote mizizi kitu ambacho sio afya kwa mustakabali wa CCM yenyewe na nchi kwa ujumla.
Natamani ingekua hivyo mkuu. Kwamba wajumbe walipiga kura kwa maslahi mapana ya Chama na nchi bila ushawishi wa fedha na mali. Kwamba wangetoa ujumbe mzito kwa wagombea kua wanahitaji mgombea aliyekaribu na watu na aliyebeba agenda yao ya kupambana na umasikini, maradhi na ujingaHakuna cha fedha wala nini hiyo ilikuwa ni tathmini halisi ya jinsi sisi watiania tulivyokuwa tunajisikia wakubwa na kujikweza ndani ya mioyo yetu na jinsi jamii inavyokuona. Mtu yupo kwenye idara amejiona ni mkuubwa akirudi kwao likizo hata wale aliokua nao anawaona malofa, hashirikiani nao kwa lolote ni kujisifusifu tuu,unaondoka kazini kwa mbweembwe na vihela vyako ndio unajifanya unawagawia, wanavipiga na kukuzuga kuwa kura watakupa.Mwisho wa siku unaipata tathmini ya kuwa wewe ni nani kupitia kura za wazi za hadharani kuwa wewe ni SIFURI bin ZERO na kuonyesha ukomavu wa kidiplomasia walikuwa hawakuambii sasa wamepita nafasi kupitia sanduku la kura na sasa wamekuambia wewe ni sifuri sii lolote level ya ukubwa uliojikweza jamii bado inakuona kama sisimizi tuu.jirekebishe