Pesa ni chanzo cha watu kuwa wavivu, pamoja na kutokuwa wazalishaji halisi; 'barter trade' irudi

Pesa ni chanzo cha watu kuwa wavivu, pamoja na kutokuwa wazalishaji halisi; 'barter trade' irudi

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Pesa sio kipimio sahihi cha uzalishaji wa vitu.

Chukulia mfano, mtu anaponda kokoto kwa kutumia mkono kwa siku 20 na kuweza kujaza tipa, na mwishowe analipwa laki 1; wakati huo huo mwingine ameudhuria kikao cha nusu saa tu, anapata laki 5; hii haiko sawa.

Mkulima anatumia muda mwingi kwenye kilimo, na baada ya mavuno, gunia anauza elfu 30 au 40; wakati huo huo boda boda anaingiza hiyo hela kwa siku; hii haiko sawa.

Fundi ujenzi anajenga boma lote kwa shilingi milioni moja, na kugawana hiyo pesa na vibarua wake; wakati huo huo, mwingine yuko ofisini anafanya kazi za kawaida anapata zaidi; hii sio sawa.

Kwa mazingira haya, bora mfumo wa kubadilishana vitu (barter trade), urudi; ukitaka gunia la mahindi, leta gunia la mpunga; ukitaka ng'ombe leta mbuzi watano; ukitaka mafuta leta asali lita 20; ukitaka kuku leta samaki n.k

Hii itafanya watu wazalishe vitu vinavyoonekana, na vyenye thamani halisia.​
 
Nawaza tu.
Wabunge watapokea posho za matikiti.
Mkandarasi analipwa ng'ombe
Unaenda saloon kunyoa/kusuka unalipa kwa vitunguu
Kanisani unatoa sadaka ya mifugo
Daladala unalipa nyanya
Ofisini unapata mshahara kwa mahindi
Kifurushi/bando unanunua kwa mchele
Simu unanunua kwa maharage ,tecno unabadilishana na mchicha
Bodaboda analipwa kwa dagaa
Kodi/tozo unalipa vitunguu swaumu (china walijaribu 😂😂 Chinese real-estate developers are accepting wheat, garlic, and peaches as down payments for properties as the market slumps and bond defaults mount



Vipi kuhusu wanoishi kwa kutegemea K na msambwanda watalipwaje? Prof mzabzab tupe majibu 😂😂





Kiufupi pesa ni karatasi ambayo watu wamekubaliana iwe na thamani fulani ya kufikirika. Mara nyingine naona suala la pesa mzungu alitutapeli 😂😂😂
 
Nawaza tu.
Wabunge watapokea posho za matikiti.
Mkandarasi analipwa ng'ombe
Unaenda saloon kunyoa/kusuka unalipa kwa vitunguu
Kanisani unatoa sadaka ya mifugo
Daladala unalipa nyanya
Ofisini unapata mshahara kwa mahindi
Kifurushi/bando unanunua kwa mchele
Simu unanunua kwa maharage ,tecno unabadilishana na mchicha
Bodaboda analipwa kwa dagaa



Vipi kuhusu wanoishi kwa kutegemea K na msambwanda watalipwaje? Prof mzabzab tupe majibu 😂😂





Kiufupi pesa ni karatasi ambayo watu wamekubaliana iwe na thamani fulani ya kufikirika. Mara nyingine naona suala la pesa mzungu alitutapeli 😂😂😂
Mapori yote yasingekuwepo, yangekuwa mashamba, kwa sababu kila mmoja ingemlazimu kuzalisha
 
Kikao cha nusu saa kinaweza kujenga au kuumiza mitaji ya wakulima wote wa nchi nzima. Au kinaweza kuwakomboa waponda kokoto wote nchi nzima.
Walitakiwa walipwe 5000 kwa sababu hawazalishi, zaidi ya kuwapangia hao watu cha kufanya
 
Kikao cha nusu saa kinaweza kujenga au kuumiza mitaji ya wakulima wote wa nchi nzima. Au kinaweza kuwakomboa waponda kokoto wote nchi nzima.
Ukiwaza haya masuala utachosha akili na mwili 😂



Ukiwaza sana utajiona wewe ni kama Chifu Mangungo. unahangaika sana kutafuta likaratasi lisilo na thamani halisi 😂
 
unamaanisha ukitaka kupata huduma ya CT-Scan upeleke mchele au mahindi, na hiyo hospitali ikitaka kununua mashine ya CT-Scan nje ipeleke maharage au?
Wapeleke dhahabu n.k
 
ko hata kituo changu cha afya kayenze, kipeleke dhahabu au vepe
Fedha inadumaza na haileti uzalishaji halisia, ndio maana mapori bado ni mengi; kwa asilimia kubwa watu hawazalishi mashambani, ndio maana vyakula vinapanda bei kila siku kutokana na uzalishaji kuwa mdogo; huku tukitegemea karatasi ndio ifanye maamuzi, kwenye chakula kilicholimwa na wachache.​
 
Fedha inadumaza na haileti uzalishaji halisia, ndio maana mapori bado ni mengi; kwa asilimia kubwa watu hawazalishi mashambani, ndio maana vyakula vinapanda bei kila siku kutokana na uzalishaji kuwa mdogo; huku tukitegemea karatasi ndio ifanye maamuzi, kwenye chakula kilicholimwa na wachache.​
Upo sahihi kiongozi. Fedha (karatasi la kiutapeli) ndio linatuhangaisha sana duniani. Yaani mpaka hilo karatasi ndio tunalipa thamani kuuuubwa kuliko chakula. Mfano ufungiwe kwenye chumba kwa miezi 6 bila kutoka ndani kuna trillion 50. Na mwingine afungiwe kwenye chumba kilicho jaa misosi mbalimbali,maji, jiko na sufuria kwa miezi sita. Nani ataishi? Si yule mwenye msosi. Sasa unaweza ukalinganisha chakula na karatasi la kiutapeli "fedha"



Kiufupi pesa ni karatasi la kiutapeli tu. Mzungu alitutapeli 😂😂😂


Ndio maana Yesu aliwasanua wanafunzi wake kuwa watafute ufalme wa mbinguni wa milele.
"Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa."
Mathayo 6 :33
 
Upo sahihi kiongozi. Fedha (karatasi la kiutapeli) ndio linatuhangaisha sana duniani. Yaani mpaka hilo karatasi ndio tunalipa thamani kuuuubwa kuliko chakula. Mfano ufungiwe kwenye chumba kwa miezi 6 bila kutoka ndani kuna trillion 50. Na mwingine afungiwe kwenye chumba kilicho jaa misosi mbalimbali,maji, jiko na sufuria kwa miezi sita. Nani ataishi? Si yule mwenye msosi. Sasa unaweza ukalinganisha chakula na karatasi la kiutapeli "fedha"



Kiufupi pesa ni karatasi la kiutapeli tu. Mzungu alitutapeli 😂😂😂


Ndio maana Yesu aliwasanua wanafunzi wake kuwa watafute ufalme wa mbinguni wa milele.
Kwa mfano, kwa wengi tulioko mijini, ukituuliza tunazalisha nini; wengi tutakujibu, tumeajiriwa na tunalipwa mishahara ndio inayotusaidia kununua mahitaji yetu.

Swali, lingine; kama hayo mahitaji hayapo au mwenye nayo hayuko tayari kubadilishana na hiyo fedha yako; maisha yatakuwaje?
 
Back
Top Bottom