Pesa za biashara kuchukuliwa zote kwenye droo ya kuhifadhia pesa kimazingira

Pesa za biashara kuchukuliwa zote kwenye droo ya kuhifadhia pesa kimazingira

Njia za Giza Biashara ipo nyumbani na nakaa mm ma Wife tu
Hakuna cha njia za giza

Mbona wanasema kwenye nguvu za giza pesa haina thamani na ndio maana wachawi wanaweza kuja kukukaba wakakuta mezani kuna milioni na home wamepika tembele lakini wakaiacha

Wewe hela umepoteza kwa njia ya kawaida tu zidisha umakini. Otherwise umetapeliwa bila kujua.
 
chuma ulete mkuu
kuna kastory kafupi dada yangu kama miezi miwili hivi imepita kahamia mitaa ya manzese baresa sasa siku ya kwanza kaamka anafanya usafi sebuleni akaokota elfu 30 akaificha akijua shemeji ndo kaidondosha, siku ya pili akaokota tena elfu 30 na siku ya tatu vile vile akaogopa akaamua kumwambia mume wake. siku ya nne akaokota tena hali hiyo ikaenda mpaka siku saba yaani wiki kila siku wanaokota elfu 30 eneo lile lile. baada ya wiki wakasikia hodi mzee kumbe ndo alikuwa mpangaji kabla ya wao kuingia akawaambia kuwa kuna mzigo wake aliusahau amekuja kuuchukua wao kwa haraka wakajua zile hela wakataka kumpa hela akakataa akawaambia wamruhusu aingie ndani achukue mzigo wake. waka mruhusu kumbe kuna sehemu aliweka ka kamba keusi kanining'inia akakachukua akawashukuru na pesa akawaachia. toka hapo hawakuokota tena pesa. uchawi hupo jamani tumwombe sana Mungu.
Dah!
 
Ninachojua chumaulete wabachukua asilimia tuu na sio mzigo wote... Hebu acheki humo ndani kama hakuna panya

Hili la pesa za mauzo kuondoka sote limenitafakarisha
mkuu limeninyima usingizii now DUKANI nakava mwenyewe sitakiii aingie mtu mwengine
 
Back
Top Bottom