Peter Madeleka awaburuta Mahakamani Jaji Biswalo Mganga na Kamishina wa uhamiaji Anna Makakala

Peter Madeleka awaburuta Mahakamani Jaji Biswalo Mganga na Kamishina wa uhamiaji Anna Makakala

Jamaa anaoenda kiki za kipuuzi sana

USSR
Hapana hii kesi itajibu maswali mengi sana acha tuone mwisho wake itachimbua hadi hela zilikuwa zinaenda wapi maana cag alionyesha kuna shaka kwenye mfumo mzima wa plea bargaining na vile vile itaweka records sawa kwa maamuzi yoyote yatakayofikia siyo kiki ila ni shule wote tutapata kujifunza espeally wadau wa sheria
 
Na wewe unajua? Mbona huchambui?
nichambue nini sasa ndugu, wakati mchakato wa s.128 na 129 ya CPA ukiisha, atatakiwa kuwepo prosecutor, anaweza kuwa private prosecutor au hata public. hakimu hawezi kuwa prosecutor mwenyewe. na kesi yeyote ikifunguliwa, iwe ya private au public prosecution, DPP anaweza kuvamia muda wowote na kutoa nolle prosequi bila kuhitajika kutoa sababu yeyote ya kufanya hivyo, atakwambia tu ni kwa maslahi ya uma basi. sasa hapo kuna uhai wa kesi kweli?

na mchakato wa kumwondolea Mganga J hadhi ya kuwa jaji hadi awe mtu wa kawaida umweke lock up au asimame kizimbani, sio wa kitoto na huwa haupo kwenye mambo kama aliyolet amadeleka. usifikiri pale alipo Mganga utaenda na kumkamata kama utakavyokamatwa wewe ukifanya kosa, lazima tume iundwe na ipendekeze avuliwe ujaji kwanza awe mtu wa kawaida.

zaidi ya yote, hayo aliyoyaweka kwenye complaint madeleka, yeye mwenyewe alikiri kwenye plea bagarning na kusaini kwamba ni kweli alikosea, na akalipa fungu la 2m. sasa utakuja leo kweli usema mganga na hao wenzake walikuwa namakosa? yepi sasa? kwa mtu mwenye akili ya kawaida tu. NImeamini watanzania wengi sana wajinga mno kwenye sheria ndio maana huwa mnafungwa kama kuku.
 

Kupitia ukurasa wake rasmi wa X (Twitter) Peter Madeleka anaandika

HAWAKO juu ya SHERIA na wala HAWANA KINGA ya kutoshitakiwa KIJINAI. Naishukuru Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kwa KUIPOKEA kesi hii kwa ADMISSION No. AD/RM/ARS/91511/2023
View attachment 2840791
To keep the Record Right!

Hawa vijana akina Madeleka Historia itawakumbuka na kuwazawadia mambo bora
 
Huyu jamaa yuko Moto sana soon watamla kichwa
Kwani Si tunakubaliana hakuna aliye juu ya Sheria kwa mujibu w Katiba ya Tanzania?

Sasa kwanini mnawaza Kula vichwa vya binadamu wenzenu??
Ni madaraka tu au kuna kingine mkuu?
 
madeleka kuna uwezekano mkubwa ana shida ya afya ya akili. msaidieni mlio karibu naye. kwahiyo anategemea kumshitaki mh Jaji mbele ya Hakimu? na kesi yake hiyo si nilisikia kwamba alikiri yeye mwenyewe kwa plea bargaining?
Kwani Mkuu Sheria inasema Jaji hawezi kutenda Kosa au Jinai?

Au kuna mahali sheria za Nchi zinataja kuwa Jaji au Hakimu kamwe hatotenda kosa lolotw la jinai hata kama akiua au akiiba?
 
Tumasubirii sarakasiiii......pia tujifunze kitu kipyaa kwenye jinai na sheria za nchin na katiba
Hi ndio akili sasa.

Kuna watu walishajifanya miungu watu na ndio hao.utawaoma wameshupaa kumshangaa Wakili Madereka.

Hata Trump leo anaripoti Polisi na Mahakama kwa makosa aliyotenda.

Kwanini sisi Wafrika tuko hivi?
 
Kiki unawaza wewe chawa mwenzako anawaza nchi kua na utawala wa sheria.na ni haki yake kama anaona kuna kitu katendewa isivyo haki.mahakama ndiyo itakayotafsiri anatafuta haki au kiki.
Sahihi
 
Kwani Mkuu Sheria inasema Jaji hawezi kutenda Kosa au Jinai?

Au kuna mahali sheria za Nchi zinataja kuwa Jaji au Hakimu kamwe hatotenda kosa lolotw la jinai hata kama akiua au akiiba?
Kile kitu Mganga na hao wote walichofanya, walikifanya in the course of their duties, sio kama wao binafsi, DPP huwa hashitaki mtu kibinafsi, ni mwakilishi wa Jamhuri, pale anasimama sio kama yeye binafsi bali ni jamhuri, hivyo Madeleka alishtakiwa na jamhuri, hakushitakiwa na hao. na alishtakiwa baadaya huyo DPP kupelekewa jalada la ushahidi na wapelelezi. mbona hajawaweka wapelelezi? dpp huwa haamki tu na kushtaki mtu, basis yake ni ushahidi unaoletwa na wapelelezi.

pili, Jaji ana immunity, hawezi kushtakiwa kwa mambo aliyoyafanya kama Jaji katika kazi zake za kila siku.labda kwa mambo ya kibinafsi kama vile ameua mtu, amepiga mtu n.k. ila yale yote anayafanya akiwa Mahakamani, hata hakimu ana immunity, hawezi kushtakiwa. basi tuseme Mganga J hayo atakuwa aliyafanya akiwa bado hajawa Jaji, alikuwa DPP, lakini sasaivi ameshakuwa Jaji, hata kwenda kumwona pale unahitaji appointment, huwezi kumshtaki jaji hadi tume ya kumchunguza iundwe na imshauri aliyemteua kutengua ujaji wake ili awe raia wa kawaida. ila akiwa jaji huwezi kumshtaki, lazima umvue kwanza ujaji wake. sasa madeleka anaamini anaweza kumvua Mganga J ujaji wake kwa kufungua mashtaka ambayo Mganga aliletewa jalada la upelelezi na wapelelezi, na akiwa Mahakamani Madeleka mwenyewe akaandika barua kuiomba Mahakama kwamba anataka kuongea na DPP akiri kosa kwa plea bargaining, akaandika barua, akatia saini kwenye plea bargaining agreement, akalipa pesa na kutoka. NI rais gani ataunda tume kuchunguza Jaji katika mazingira ambayo madeleka mwenyewe alikiri kosa Mahakamani?

plea bargaining ni sawa na kukiri kosa, sasa mtu unakiri alafu uje kesho useme ulishtakiwa kimakosa? kweli?

huyu dogo tulishamwambia, anatakiwa kukaa chini ya uangalizi wa watu kama kina Tundu Lisu au Kibatala, hao wangemsaidia. hivi unafikiri Tundu Lisu hajui hayo yote? kwanini yeye au kibatala hawajafungua mashtaka kama hayo? wanajua ni upuuzi, unajidharaulisha na unadharaulisha tasnia ya sheria. inatakiwa hata ukiwa Mahakamani watu waseme kweli huyu kaleta kitu cha maana, sio kuleta upupu ambao ni sawa na wa watu ambao hawajasoma sheria.
 
Kwani Si tunakubaliana hakuna aliye juu ya Sheria kwa mujibu w Katoba ya Tanzania?

Sasa kwanini mnawaza Kula vichwa vya binadamu wenzenu??
Ni madaraka tu au kuna kingine mkuu?
Mkuu tuna historia mbaya wa watetezi kama hawa wa haki za watu wanapotezwa kwa makusudi
 
nichambue nini sasa ndugu, wakati mchakato wa s.128 na 129 ya CPA ukiisha, atatakiwa kuwepo prosecutor, anaweza kuwa private prosecutor au hata public. hakimu hawezi kuwa prosecutor mwenyewe. na kesi yeyote ikifunguliwa, iwe ya private au public prosecution, DPP anaweza kuvamia muda wowote na kutoa nolle prosequi bila kuhitajika kutoa sababu yeyote ya kufanya hivyo, atakwambia tu ni kwa maslahi ya uma basi. sasa hapo kuna uhai wa kesi kweli?

na mchakato wa kumwondolea Mganga J hadhi ya kuwa jaji hadi awe mtu wa kawaida umweke lock up au asimame kizimbani, sio wa kitoto na huwa haupo kwenye mambo kama aliyolet amadeleka. usifikiri pale alipo Mganga utaenda na kumkamata kama utakavyokamatwa wewe ukifanya kosa, lazima tume iundwe na ipendekeze avuliwe ujaji kwanza awe mtu wa kawaida.

zaidi ya yote, hayo aliyoyaweka kwenye complaint madeleka, yeye mwenyewe alikiri kwenye plea bagarning na kusaini kwamba ni kweli alikosea, na akalipa fungu la 2m. sasa utakuja leo kweli usema mganga na hao wenzake walikuwa namakosa? yepi sasa? kwa mtu mwenye akili ya kawaida tu. NImeamini watanzania wengi sana wajinga mno kwenye sheria ndio maana huwa mnafungwa kama kuku.
Wajinga tunashukuru ufafanuzi ingawa umemalizia na matusi.
 

Kupitia ukurasa wake rasmi wa X (Twitter) Peter Madeleka anaandika

HAWAKO juu ya SHERIA na wala HAWANA KINGA ya kutoshitakiwa KIJINAI. Naishukuru Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kwa KUIPOKEA kesi hii kwa ADMISSION No. AD/RM/ARS/91511/2023
View attachment 2840791
Katika Taaluma ya Sheria, unafungua kesi ngumu anbayo itakutangaza kibiashara ili kuvuta wateja wa kesi za kawaida. Hata ukishindwa na jamhuri lakini unapata faida ya kujitangaza na kufahamika kwa wadau
 
nichambue nini sasa ndugu, wakati mchakato wa s.128 na 129 ya CPA ukiisha, atatakiwa kuwepo prosecutor, anaweza kuwa private prosecutor au hata public. hakimu hawezi kuwa prosecutor mwenyewe. na kesi yeyote ikifunguliwa, iwe ya private au public prosecution, DPP anaweza kuvamia muda wowote na kutoa nolle prosequi bila kuhitajika kutoa sababu yeyote ya kufanya hivyo, atakwambia tu ni kwa maslahi ya uma basi. sasa hapo kuna uhai wa kesi kweli?

na mchakato wa kumwondolea Mganga J hadhi ya kuwa jaji hadi awe mtu wa kawaida umweke lock up au asimame kizimbani, sio wa kitoto na huwa haupo kwenye mambo kama aliyolet amadeleka. usifikiri pale alipo Mganga utaenda na kumkamata kama utakavyokamatwa wewe ukifanya kosa, lazima tume iundwe na ipendekeze avuliwe ujaji kwanza awe mtu wa kawaida.

zaidi ya yote, hayo aliyoyaweka kwenye complaint madeleka, yeye mwenyewe alikiri kwenye plea bagarning na kusaini kwamba ni kweli alikosea, na akalipa fungu la 2m. sasa utakuja leo kweli usema mganga na hao wenzake walikuwa namakosa? yepi sasa? kwa mtu mwenye akili ya kawaida tu. NImeamini watanzania wengi sana wajinga mno kwenye sheria ndio maana huwa mnafungwa kama kuku.
Tunafungwa kama Kuku huku mafisadi na wezi wana neeemeka.
Is that what you mean mr presenter?
 
Back
Top Bottom