Peter Zakaria aanza kurudisha mali zote alizonunua yeye na mkewe serikalini


Nadhani wanaJF na watanzania wanao uwezo wa kufuatilia ni wapi mali hizi zinarejeshwa na kwa manufaa ya nani.ukichukua muda utaujua ukweli na hoja yako itakuwa imejibiwa.
mimi siangalii wanarejesha vipi bali matokeo kuwa zinarudi...walichukua bila uhalali na warudishe kwa style hiyo hiyo
 
Wote hao tunawafuata mkuu. Wasikupe tabu hakuna mali ya serikali itakayopotea. Kwali ule msemo wa lazima mali iliyoibwa kuna sehem yakutoke umeusahau
Hapo kwenye red mkuu wangu nakumbuka sana, alisema tatokea mahali popote palipo wazi (hapa alitaka kusema tunapotolea haja kubwa). Hivyo na wao wajiandae kuzitolea kwenye tundu lolote lililo wazi!!
 
Mwelekeo mzuri, pia mali ya watanzania inayo milikiwa na CCM irejeshwe kwa wananchi bila ucheleweshaji. HAPA kazi tu.
 
Zakaria kaingia choo cha kike,dah,sijui kilichomponza ni nini.Unajiingiza kwenye mgogoro na TISS! Yangu macho.
 
Ukisema huangalii wanarejesha vipi ila matokeo, unajua umeipa ruhusa serikali kukupiga risasi kwa minajiki ya ujambazi ambao hujaufanya bila serikali kuhojiwa lolote?

Unaelewa kwamba process inaathiri matokeo na hutakiwi kusema hujali process, unajali matokeo tu?
 
Reactions: Cyb
Wafuatilie wapi? Kwenye serikali ambayo haitaki kuhojiwa, haitaki uwazi, inafanya mambonje ya sheria na utaratibu na bajeti?
 
Mali za umma zirudishwe kwanza mambo ya dhamana baadae.
 
Tatizo nililogundua hapa ni kwamba wana habari hawajatoa taarifa ya kutosha kwa umma na matokeo yake baadhi ya watu wanasema mambo ambayo hata hayapo kabisa. Ngoja nitoe ufafanuzi kidogo kama ifuatavyo:-

1. Mali za NCU zote zilizouzwa kwa watu mbalimbali "kimagumashi" zilitakiwa kurudishwa serikalini tangu mwaka jana na agizo hilo lilitolewa kwa watu wote walionunua mali hizo.

2. Wale wote walionunua mali za NCU na wakatii agizo la serikali la kuzirejesha bila pingamizi lolote, wote wapo huru uraiani.

3. Hata hivyo, wale wote walioweka pingamizi juu ya urudishwaji wa mali za NCU, wote wapo korokoloni wakiongozwa na mke wa Zakaria, mdogo wake na sasa Zakaria mwenyewe.

4. Binafsi maamuzi ya serikali nayaunga mkono 100% na pia nawasii Watanzania watambue kwamba Serikali hii ya awamu ya tano ipo makini mno na maamuzi yoyote inayofanya ni kwa maslahi ya umma.

5. Kwa kumalizia, wenye akili wote walitumia mali za NCU kujitajirisha kwa miaka yote walipokuwa wamiliki wa mali hizo. Leo walivyopewa fursa ya kuzirejesha, hata kama taratibu zilizotumika zinaonekana za kibabe, kwao ilikuwa salama sana kuzirudisha na ndio sababu wengi wamezirejesha kwa hiari yao wenyewe.
 
Tundu Lisu alishasema kuwa wakiwamaliza wapinzani watawageukia makada wa ccm sasa ndiyo hayo
 
Tundu Lisu alishasema kuwa wakiwamaliza wapinzani watawageukia makada wa ccm sasa ndiyo hayo
Kwahiyo ulidhani kuwa CCM ndio kinga ama!?

CCM ni chama tu na kama wanachama wake watafanya uhalifu, basi watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Ikiwa huko upinzani mmezoea kulindana kwa mambo ya kihalifu kisa tu ni upinzani, basi hampaswi hata kusogelea Ikulu.
 
Umefufuka wewe Hamida
 
Kama shida ni kununua mali za NCU mbona akina Simon Kisenha wako nje wanapeta na ma UDART tu? Wote wakamatwe na hata waliouza nyumba za serikali kwa bei ya kutupwa na wenyewe wakamatwe kwa uhujumu uchumi!!
Kisena and co washarudisha hima New Era waliyouziwa na Samsoni ni suala la muda tu nadhani hata udart wapo shakani
 
kukosa International standars kunatokana na kutokuwa na exposure kwa asilimia kubwa ya wananchi.
 
kukosa International standars kunatokana na kutokuwa na exposure kwa asilimia kubwa ya wananchi.
Kuna kukosa exposure, halafu kuna utamaduni wa "hewalla bwana" hata kwa wale wachache wenye exposure.

Nina uhakika hata kama 1% ya Watanzania wote wana exposure, hao ni takriban watu 500,000.

Wanatosha sana kuanzisha kizungumkuti, ambacho hatujakisikia.

Washakubali matokeo.
 
hewala kweli ni dasturi yetu.Na uzuri wanaotutawala wanayajua vyema mapungufu yetu na namna ya kuya exploit.ila umenifikirisha sana kuhusu suala la kutotumia international standards kwenye kufanya ulinganyo,matokeo yake tumaridhika na kudanganyika na vitu substandard.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…