Petition ya kumfanya Ibrahim Traore kuwa Rais wa Afrika iliyoungana

Petition ya kumfanya Ibrahim Traore kuwa Rais wa Afrika iliyoungana

Ofcourse Dunia inaenda kuwa na serikali moja, ila si leo, labda wajukuu wa vitukuu vyako ndo watashuhudia hilo maana lazima Tech ifike kiwango cha kuweza kucontrol raia mpaka vijijini ndani huko sasa ndo kwanzaa tunapambana na AI.
Tafuta taarifa mkuu,it is much much sooner than you think.
 
Ni mapema sana kuamua hilo ikumbukwe Africa ni zaid ya Burkina Faso,,waafrika mpunguze mihemuko.
Kwa nini unadhani ni mapema?Kwa hiyo unafurahi kuendelea na viongozi hawa matapeli na wezi tulio nao?
 
Hiyo link ya petition Iko wapi mkuu maana naona umetupeleka youtube
 
Haiwezekani. Ili uongoze dunia lazima kuwe na mambo ambayo yatacontrol unaowaongoza otherwise labda liwe ni igizo la kuongoza.
Vitu vyote vya kuiongoza Dunia vipo.United Nations ipo na organizations zote major zipo.Unajua kwa nini UN ipo,WHO?ILO?UNICEF nk.nk.?Amkeni.Unajua concept ya Globalization Ina maana gani.Everything is there for you to see,but you don't,poleni sana.
 
mkutano mkuu uliofanyika TZ aligoma kwenda akatuma muwakilishi si undezi huo.. pelekeni hooja kama hizi maliwatoni
 
Muungano wa Afrika kuwa taifa moja kamwe hauwezi kutokea!

Hiyo ni njozi tu inayosikika vizuri masikioni lakini isiyo na uhalisia wowote ule.

Wenyewe kwa wenyewe tu ndani ya vinchi vyenu hamuelewani, seuze bara zima liongozwe na mtu mmoja?

Watu wa Bulawayo wana nini cha kufanana na watu wa Akwa Ibom?
 
Vitu vyote vya kuiongoza Dunia vipo.United Nations ipo na organizations zote major zipo.Unajua kwa nini UN ipo,WHO?ILO?UNICEF nk.nk.?Amkeni.Unajua concept ya Globalization Ina maana gani.Everything is there for you to see,but you don't,poleni sana.
One gvt ina shida gani?
 
Plan Yao ni 2030 mkuu.
hivi akili mnawekaga wapi? Hayo mambo ya New world order ni upuuzi ulioanza muda mrefu na ulifeli tangu enzi za vita za wazungu walizoziita world war 1&2 ambapo waliunda kila mbinu za kuufanya ulimwengu uwe kitu kimoja huku wakiusimika uongozi wa taifa moja kubwa kutawala mataifa mengine, hilo lilifeli.

Kama walifeli katika kipindi cha giza la ukoloni na ujima ndio waweze hivi leo?

Mambo ya kutawala ulimwengu kupitia Order ya kikundi kimoja chenye sheria zake na plan zake hilo haliwezekani kwa sasa, labda miaka 300 ijayo.

Kwanini haiwezekani?, kwasababu hayo mambo ya new world order yameletwa na watu magharibi wakiwepo hao fake jews, na baadhi ya Muslims, ambapo kwasasa hawa kwa upande waliopo unaofungamana na USA wanapata pingamizi kubwa kutimiza sheria&plan zao kutoka mataifa mengi yenye nguvu kama vile Russia,China, Iran, North Korea, Cuba, India, na baadhi kutoka Afrika,

Suala la kuutawala ulimwengu kwa Sheria moja na kanuni moja si jepesi kama mnavyodanganywa humo makanisani na misikitin, kuutawala ulimwengu na kila mtu inahijika nguvu kubwa ya kitechnolojia, ushawishi, ambapo kwa sasa hiyo nguvu haipo na haijawai kuwepo acheni kudanganywa.

Ili uutawale ulimwengu ni lazima mataifa yote makuu kama Russia, china, India, USA, UK, Canada, German, France, Italy, Japan, UAE, Saud Arabia, Qatar, Iran, South+North Korea, wakubali kuweka tofauti zao na wakubaliane kufanya jambo moja, jambo ambalo kwasasa haliwezekani wala dalili za kuwezekana kwake hakupo.

Ili uutawale ulimwengu vile vile ni lazma uwe na control ya Afrika nzima, ambako kuna population ya watu wengi ambao hawapo hata katika database ya control ya kimaeneo, tamaduni, sheria, hiyo technology ya kuamlisha kila mtu afuate mambo fulani hamna kwa sasa.
 
Back
Top Bottom