Ph.D bila kupata Master

Ph.D bila kupata Master

Wanandugu,

Je, duniani kuna utaratibu wowote unaoweza kukufanya ukapata Ph.D bila kulazimika kupitia kwanza Masters? Kama inawezekana, ni institutions zipi zinao utaratibu huo?

Muulize Dr. Slaa, Katibu Mkuu wa chadema, ana PhD bila masters bila baccalaureate (bachelor) atakupa maujanja.
 
Inawezekana manake kuna Dr Padri yeye alisomea Biblia sasa hivi anajiita Dr

Nasikia Jk anatarajia kupewa shahada ya Udaktari (PhD ya ukiruka njia ulio tukuka)

Copy to zomba
 
Last edited by a moderator:
asante sana mkuu "the state" mungu akubariki. umenielezea vizuri sana, na kuna mtu ameniambia wanaopata admission harvard kutoka bongo wemesoma shule za kimataifa kama IST na lazima uwe na IB sasa wengine tunasoma local schools na vigezo ni vigumu.
 
asante sana mkuu "the state" mungu akubariki. umenielezea vizuri sana, na kuna mtu ameniambia wanaopata admission harvard kutoka bongo wemesoma shule za kimataifa kama IST na lazima uwe na IB sasa wengine tunasoma local schools na vigezo ni vigumu.

Usijali la fiesta. Kama nia yako ni kwenda havard usikate tamaa. Nenda US kasome bachelor inayoendana na ile unayoitamani ya Havard kwenye university yeyote hata kama ni ya kata na u-uperform vizuri. Hii itakusaidia kuingia kwenye system ya education ya US.Usisome diploma wala ndugu yake na diploma. Hii itakusaidia "ubebeke na utakuwa mwenzao''. After that, omba Havard kusoma bachelor inayoendana na ya kwako utaona jinsi watakavyokuchukua ki-urahisi mpaka utashangaa!. Na kama utakuwa uko serious na masomo, utapasua vizuri na watakupa scholarship za masters wao wenyewe na hata PhD as long as uko vizuri. Cha msingi u-focus kile unachokitafuta na umtangulize Mungu kwanza. However, maelezo yangu ni ya kibinadamu na experience. Ask God for a final answer.
 
Isidhaniwe utaratibu huo kuwa ni njia ya mkato kwa maana ya kufanya vitu vichache. Mara nyingi kunapokuwa na utaratibu huo, mwanafunzi atasoma kwanza masomo ya ku-qualify kwa masters degree. Halafu ataendelea kumpeleka kwenye masomo ya kufanya utafiti na kuandika tasnifu. Kwa hivyo basi, PhD hiyo itasomewa kwa si chini ya miaka minne.
 
bwana State that is excellent. Tungekuwa na wabongo design yako..hakika tungepiga hatua..personally maelezo yako nimeyapenda..very encouraging and supportive kwa wanaodhani kwenye kwenye hizi best unis ni miujiza..

Kwa uzoefu wangu, kwa kweli hizi shule safi za UK na US ziko VERY VERY competitive especially kwa masters na PhD. Mfano utakuta wanafunzi dunia nzima wanagombania nafasi lets say 30 au 50 za international students kuingia in one of these Unis kama Harvard au Yale au Stanford. Sasa hapa utakuta there are some of the brightest students kutoka China, Singapore..you name it! But again kama alivyosema State, God is the final answer. I always tell people..by applying you dont lose anything (though kwetu Tanzania hata hela ya application ni challenge!).

Kwa PhD....uzoefu wangu ni UK. Kwa hizi super elite institutions za UK kama Cambridge, Oxford, LSE, Imperial au UCL....na penyewe ngoma ni nzito. Mfano jamaa yangu ali-apply PhD pale LSE..and aliniambia out of 365 walichukua wanafunzi 8! (unfortunately hakupata). Kifupi its really competitive and by the way dont forget kwamba waingereza hata kwa funding ni wachungu sana!

Again, si lazima uende kwenye hizi super elite universities..you can always go to 'lower ranked unis' lakini..I would say..we all have dreams...kama tungeweza hakuna ambaye asingependa kwenda Harvard, Yale, Cambridge, Oxford au LSE.

Kwa vijana ambao bado mko ambitious, I would encourage you guys to work..really hard and keep on challenging frontiers of knowledge. Hakuna kilicho automatic. Na ukiapply shule..lets masters..well changanya..mfano ukiapply hizo super elites..weka na nyingine kama tano za kawaida! But again..ni vema ukajipima kwa kuangalia grades zako na CV yako kwa ujumla if they can earn you a spot in these best unis.

Otherwise..vijana wanaotafuta shule..keep on working..inawezekana..msikate tamaa. Maana hata wanokwenda kwenye hizi shule nzuri ni watu kama sisi. Ila ninachoona watanzania wengi wetu hatuchangamkii fursa..tunakata tamaa mapema..we rule ourselves out before we are ruled out!

NB: Before making your application ni muhimu sana ukacheck grammers na makosa madogo madogo kwenye CVs na documents nyinginezo. They speak volume on your behalf.
 
Wanandugu,

Je, duniani kuna utaratibu wowote unaoweza kukufanya ukapata Ph.D bila kulazimika kupitia kwanza Masters? Kama inawezekana, ni institutions zipi zinao utaratibu huo?

Nyie mabongo lala jadilini jinsi ya kupata elimu bora, kupata maji, huduma safi za afya kutwa kujadili watu wewe PhD ya Dr. Slaa ikifutwa itakupa maji? Itakupa elimu? Acheni ujinga taifa linateketea
 
Dr slaa
philosophy 3yrs(sawa na degree)
theology 3yrs(ongezea hapi degree nyngne- masters

yap; na anavigezo vya kusoma PHD: ingawa kwenye kwenye hzo course hapo juu kwenye system kikatoliki hawaiti degree wala masters
 
Mbona hamsemi kwamba Marehemu Prof Haroub Othman (Naomba kusahihishwa) pia alipata PhD bila kusoma Masterz?
Hizi ni sifa za kuingia PhD UDSM
Doctor of Philosophy (Ph.D.)
A candidate for admission to the Doctor of Philosophy degree shall hold the following qualifications:
a) An honours degree of the University of Dar es Salaam or an equivalent degree from a recognized University. Candidates who hold an unclassified degree e.g., M.D. should have at least a B grade average in the subject of intended Ph.D study.
AND

b) Masters degree of the University of Dar es Salaam or an equivalent Masters degree from a recognized university.
c) Candidates with a First Class or Upper Second class degree, or holders of a distinction or a credit in the case of unclassified degrees, may also be considered for Ph.D. registration. Such candidates have to initially register for the Masters degree and do at least one full year's postgraduate training. If they demonstrate outstanding performance, and obtain the authorisation of the Senate on the recommendation of the relevant College and DPGS Boards, they may upgrade their registration to Ph.D candidacy.
 
Swali zuri. Unaweza kupata PhD bila masters kama ambavyo unaweza kupata masters bila bachelor!. Southampton university kwa mfano wana kitu kinaitwa integrated degree(sio course zote) yaani mtu anaingia kuanza kusoma bachelor ya four years but kiukweli bachelor yake inakuwa ni three years ila mwaka wa nne unakuwa wa masters. At the end anapata masters but hapewi cheti cha bachelor anakuwa na cha masters tu (so inakuwa kama vile hajasoma bachelor). However, kuna baadhi ya vyuo ulaya unaweza kusoma masters ukiwa na diploma na mara nyingi ni zile za diploma za three years although za miaka miwili pia waweza kusoma masters kulingana na "content" ya diploma yako. I think journalism and mass comm ina-lead katika hizi degree.

Suala la kuruka kwenda PhD bila masters linawezekana si tu ulaya bali hata UDSM. Sio kweli kwamba ukiwa na first class pekee ndiyo utasoma PhD (a case of law pale UDSM kwa mfano) ila ni pale tu unakuwa umeregister kama mwanafunzi wa masters especially under thesis (not coursewok and dissertation) na wakati wa kuandaa thesis yako ukaona imekaa ki-PhD PhD (imevuka viwango vya masters masters) then utaipeleka department na department wakiipitia waka-confirm wanaipeleka senate na senate itakuruhusu ''kuvuka'' na kuwa PhD candidate (sio kukupa PhD hapohapo). Baada ya kukupa candidacy ya PhD, chuo kinafuta registration ya masters palepale (automatic cancellation). Kazi yako wewe ni kufanya thesis yako ya PhD na ukifanya viva ikapita wanakuaward PhD kama wanafunzi wengine wa PhD. Hivyo, at the end utakuwa na PhD bila masters.

Kwa vyuo vingine hasa South wao wakishakuona umefanya vizuri thesis yako ya masters wanaweza kukutongoza ili upublish paper kadhaa kama tatu hivi na vi-conference proceedings paper kadhaa then wanakwambia uvifanye viwe kitu kimoja (monography) then unapata PhD yako hata after 1 year. Ingawa hili linawezekana pia hata kama umeshakuwa awarded masters yako (hasa pia kama ulipublish zaidi ya paper walizokuwa wanazihitaji masters). This is also applicable hata EU na sehemu nyingine.

Kuhusu swala la division one form six (I assume ni NECTA na sio cambridge au IB) kupata admission havard, duke na vyuo vingine vya marekani inategemea na vitu vingi sana. Vyuo vya wenzetu wanaangalia mambo mengi sana ikiwemo lugha, uwezo wako kulingana na course unayokwenda kuchukua, cousre husika (masharti yanatofautiana), competition etc. Si division one pekee, hata two shida inakuwa competition hasa kwenye admission ya ''best'' universities kama Havard, MIT, Stanford, Princeton, Yale, Columbia, California Berkeley etc. But ukiwa na one yako nzuri, TOEFL nzuri sana, admission exam yao ukapass vizuri sana (incase wanataka ufanye paper), halafu ukawa financially muscular, unaweza kupata. Shida nyingine ni pale ambapo nafasi ni chache na unacompete na watu kutoka states zote za US, wako safi kila angle na hawajasoma system zaidi ya US inakuwa shida. Kumbuka mnacompete dunia nzima etc.

Sina experience ya bachelor but admission ya PhD economics havard au leading university in the world kama MIT huwa wanapokea 30 students au wakizidi sana 33 wakati walio-apply na wana sifa ni 900 kutoka kila sehemu duniani. GMAT yao kwa mfano ukitaka kusoma PhD au masters katika business huwa ni si chini ya score 730, au 740 na kuendelea kati ya 800!. Sasa hao ni wa maana kweli mdogo wangu?!!. BUT ASK GOD.YEYE NI KILA KITU.

thankx mwana forum... umetuelewesha mengi mno...!
 
Muulize Dr. Slaa, Katibu Mkuu wa chadema, ana PhD bila masters bila baccalaureate (bachelor) atakupa maujanja.

Duh!!! watu kwa ufukunyuzi hamjambo. Yaani na mbwembwe zote hana hata bachelor? Hii kali.
 
Inawezekana manake kuna Dr Padri yeye alisomea Biblia sasa hivi anajiita Dr

Unajua "course contents" za hiyo biblia(theology/divinity) au unafikiri ni sawa na hizo shahada zetu?...matatizo ya shule za kata ndiyo haya tunayashuhudia kwenye post kama yako hapo juu

The guy has specialized in canon law....or sorry, you have no idea, what is it?!..
 
duh kweli hapa sie wa shule za kata ticha mmoja huyo huyo kiswahili and physics tukae kimya kwanza kushuhudia mtanange
 
duh kweli hapa sie wa shule za kata ticha mmoja huyo huyo kiswahili and physics tukae kimya kwanza kushuhudia mtanange


Mhh! Eti ticha mmoja huyohuyo Physics na Kiswahili, umenichekesha sana kijana
 
Mhh! Eti ticha mmoja huyohuyo Physics na Kiswahili, umenichekesha sana kijana

acha tu kama huamini sikumoja tembelea shule za kata vijijini ujionee hali halisi, nadhani unaweza ukakubali kwanini matokeo yao ya mitihani yanakua sio mazuri.
 
acha tu kama huamini sikumoja tembelea shule za kata vijijini ujionee hali halisi, nadhani unaweza ukakubali kwanini matokeo yao ya mitihani yanakua sio mazuri.

Pamoja na sababu nyinginezo, unajua wanafunzi wengi waliokuwa wakipenda na kuwa "vinara" wa Physics pia walikuwa wakipasi kiswahili bila tabu, lakini kwa "waliobobea" katika kiswahili hawakuweza hata kidogo kupasi Physics, sasa ishu ni kwamba hawa vinara wa Physics+(Biology, Math, Chem.Geog) hawa wote aidha ni madaktari au mainjinia wazuri, hivyo sidhani kama wako huko kwenye hizo shule za kata; hii inaniaminisha kuwa huyo mwalimu anayefundisha Kiswahili na Physics, bila shaka specialization yake ni Kiswahili-Hahaha...(Only Fallacy of composition)
 
Back
Top Bottom