Ph.D bila kupata Master

Ph.D bila kupata Master

Mhh! Eti ticha mmoja huyohuyo Physics na Kiswahili, umenichekesha sana kijana

hii kitu ni kawaida kwa shule za kata ambazo zina mwalimu mmoja wawili au watatu.mi mwenyewe kabla sijaacha ualimu nimewahi kufundisha biology form 2 na chemistry form 1. wakati masomo yangu ya kufundisha was geo na hist maana a level nilisoma arts,ila olevel nilisoma mkondo wa science,na a level nilosoma kwa credits za masomo ya sayansi ns arts baada ya combination kugoma kubalance ns hesabun nikala mswaki ambao sijui hadi leo hii ulitokea wapi. hii ndio bongo.
 
Yes, mi nafahamu watu wawili, lakini ni University za Ulaya. Kinachotokea ni kuwa mwanafunzi anaanza Masters programme lakini njiani kutokana na mwelekeo wa data na aina ya matokeo basi msimamizi wake anaweza kudai-kuipandisha daraja hiyo kazi ili iwe ya kutoa PhD. Kwa hilo mwanafunzi ataongeza aina fulani fulani ya "analysis" na mwelekeo wa kazi yote, akifaulu anapewa PhD yake.
 
Mkuu pascal acha mawazo ya kivivu kama unapenda ile tyto bas anza hata uganga wa jadi au wa tba mbadala uwe kama dk ndodi, dk rahabu au hata uwe profesa kama vile profesa maji marefu, coz unachokitaka kitakusumbua sana hata kwenye field au eneo lolote ama sivyo ukitunukiwa huo uende zako kuwa mbunge huko mambo ni rahis tu, mara kugonga meza au kusinzia kama kawa.
 
bwana State that is excellent. Tungekuwa na wabongo design yako..hakika tungepiga hatua..personally maelezo yako nimeyapenda..very encouraging and supportive kwa wanaodhani kwenye kwenye hizi best unis ni miujiza..

Kwa uzoefu wangu, kwa kweli hizi shule safi za UK na US ziko VERY VERY competitive especially kwa masters na PhD. Mfano utakuta wanafunzi dunia nzima wanagombania nafasi lets say 30 au 50 za international students kuingia in one of these Unis kama Harvard au Yale au Stanford. Sasa hapa utakuta there are some of the brightest students kutoka China, Singapore..you name it! But again kama alivyosema State, God is the final answer. I always tell people..by applying you dont lose anything (though kwetu Tanzania hata hela ya application ni challenge!).

Kwa PhD....uzoefu wangu ni UK. Kwa hizi super elite institutions za UK kama Cambridge, Oxford, LSE, Imperial au UCL....na penyewe ngoma ni nzito. Mfano jamaa yangu ali-apply PhD pale LSE..and aliniambia out of 365 walichukua wanafunzi 8! (unfortunately hakupata). Kifupi its really competitive and by the way dont forget kwamba waingereza hata kwa funding ni wachungu sana!

Again, si lazima uende kwenye hizi super elite universities..you can always go to 'lower ranked unis' lakini..I would say..we all have dreams...kama tungeweza hakuna ambaye asingependa kwenda Harvard, Yale, Cambridge, Oxford au LSE.

Kwa vijana ambao bado mko ambitious, I would encourage you guys to work..really hard and keep on challenging frontiers of knowledge. Hakuna kilicho automatic. Na ukiapply shule..lets masters..well changanya..mfano ukiapply hizo super elites..weka na nyingine kama tano za kawaida! But again..ni vema ukajipima kwa kuangalia grades zako na CV yako kwa ujumla if they can earn you a spot in these best unis.

Otherwise..vijana wanaotafuta shule..keep on working..inawezekana..msikate tamaa. Maana hata wanokwenda kwenye hizi shule nzuri ni watu kama sisi. Ila ninachoona watanzania wengi wetu hatuchangamkii fursa..tunakata tamaa mapema..we rule ourselves out before we are ruled out!

NB: Before making your application ni muhimu sana ukacheck grammers na makosa madogo madogo kwenye CVs na documents nyinginezo. They speak volume on your behalf.

Guys mko kama sio watanzania, relying on your moral assistance and encouragement, ki ukweli nimekua inspired na mawazo yenu! Mungu awatie nguvu kwa sababu najua sio mimi tu nliefaidika!!!
 
Usijali la fiesta. Kama nia yako ni kwenda havard usikate tamaa. Nenda US kasome bachelor inayoendana na ile unayoitamani ya Havard kwenye university yeyote hata kama ni ya kata na u-uperform vizuri. Hii itakusaidia kuingia kwenye system ya education ya US.Usisome diploma wala ndugu yake na diploma. Hii itakusaidia "ubebeke na utakuwa mwenzao''. After that, omba Havard kusoma bachelor inayoendana na ya kwako utaona jinsi watakavyokuchukua ki-urahisi mpaka utashangaa!. Na kama utakuwa uko serious na masomo, utapasua vizuri na watakupa scholarship za masters wao wenyewe na hata PhD as long as uko vizuri. Cha msingi u-focus kile unachokitafuta na umtangulize Mungu kwanza. However, maelezo yangu ni ya kibinadamu na experience. Ask God for a final answer.

The state japokuwa sijakuuliza mimi swali hili ninakushuru kwa lugha nzuri uliyoitumia kujibu maswali yote Mungu akubariki sana natamani kama ningekuona hongera sana kwa ustaarabu wako
 
There are so many universities vinavyo offer PhD without Msc, you just have to do your homeworks guys. I am doing this program, and this is my final year, I will put my publications in the near future!! If you are looking for Engineering Research Programs don't hersitate to contact me through my inbox.
 
Dah kuna misconceptions nyingi kidogo kwenye thread hii.

Kwa nchi ninayojua (marekani), ukiona mtu ana PhD lakini hana Masters, maana yake siyo ameruka Masters au amefanya ujanja.

Katika masomo mengi, hasa sayansi, vyuo vingi havina hata programu za Masters. Kwa mfano watu walioko na Masters ya Physics au Chemistry marekani ni wachache sana. Kwa Engineering ni sawa, lakini kwenye Basic Sciences (Physics, Chemistry, na Biology) ni wachache kabisa. Kwa sababu kama unataka kuwa mwanasayansi (tofauti na mhandisi) bila PhD huwezi kupata kazi za basic research.

Hivyo, ukimaliza bachelors ya Physics (kwa mfano) marekani, na unataka kuwa Physicist, lazima uende moja kwa moja kusoma PhD (ambayo inachukua muda wa miaka 5 mpaka 7, inategemea na spidi unayofanya dissertation yako).

Hautapata Masters, lakini kwa kweli coursework ya Masters ipo ndani ya hiyo PhD. Kwa hiyo mara nyingi ukikuta mtu anayo Masters ya somo la sayansi, alikuwa anasoma PhD lakini haikumaliza. Kama unasoma PhD na umemaliza coursework ya kutosha, ukitoka kwenye hiyo programu kabla ya kumaliza, chuo kitakupa Masters. Kwa kiingereza hiki kitu kinaitwa "consolation prize". Lakini hiyo Masters unaweza kupata tu kama umemaliza coursework ya kutosha na umeshafanya Masters Thesis.

Ushauri wangu ni kwamba msione mtu mwenye PhD lakini hana Masters amechukua shortcut. Hapana. Mara nyingi ukiwa accepted kwenye PhD program baada ya kumaliza bachelors, maana yake ni kwamba coursework ya Masters ipo ndani ya hiyo PhD.
 
Swali zuri. Unaweza kupata PhD bila masters kama ambavyo unaweza kupata masters bila bachelor!. Southampton university kwa mfano wana kitu kinaitwa integrated degree(sio course zote) yaani mtu anaingia kuanza kusoma bachelor ya four years but kiukweli bachelor yake inakuwa ni three years ila mwaka wa nne unakuwa wa masters. At the end anapata masters but hapewi cheti cha bachelor anakuwa na cha masters tu (so inakuwa kama vile hajasoma bachelor). However, kuna baadhi ya vyuo ulaya unaweza kusoma masters ukiwa na diploma na mara nyingi ni zile za diploma za three years although za miaka miwili pia waweza kusoma masters kulingana na "content" ya diploma yako. I think journalism and mass comm ina-lead katika hizi degree.

Suala la kuruka kwenda PhD bila masters linawezekana si tu ulaya bali hata UDSM. Sio kweli kwamba ukiwa na first class pekee ndiyo utasoma PhD (a case of law pale UDSM kwa mfano) ila ni pale tu unakuwa umeregister kama mwanafunzi wa masters especially under thesis (not coursewok and dissertation) na wakati wa kuandaa thesis yako ukaona imekaa ki-PhD PhD (imevuka viwango vya masters masters) then utaipeleka department na department wakiipitia waka-confirm wanaipeleka senate na senate itakuruhusu ''kuvuka'' na kuwa PhD candidate (sio kukupa PhD hapohapo). Baada ya kukupa candidacy ya PhD, chuo kinafuta registration ya masters palepale (automatic cancellation). Kazi yako wewe ni kufanya thesis yako ya PhD na ukifanya viva ikapita wanakuaward PhD kama wanafunzi wengine wa PhD. Hivyo, at the end utakuwa na PhD bila masters.

Kwa vyuo vingine hasa South wao wakishakuona umefanya vizuri thesis yako ya masters wanaweza kukutongoza ili upublish paper kadhaa kama tatu hivi na vi-conference proceedings paper kadhaa then wanakwambia uvifanye viwe kitu kimoja (monography) then unapata PhD yako hata after 1 year. Ingawa hili linawezekana pia hata kama umeshakuwa awarded masters yako (hasa pia kama ulipublish zaidi ya paper walizokuwa wanazihitaji masters). This is also applicable hata EU na sehemu nyingine.

Kuhusu swala la division one form six (I assume ni NECTA na sio cambridge au IB) kupata admission havard, duke na vyuo vingine vya marekani inategemea na vitu vingi sana. Vyuo vya wenzetu wanaangalia mambo mengi sana ikiwemo lugha, uwezo wako kulingana na course unayokwenda kuchukua, cousre husika (masharti yanatofautiana), competition etc. Si division one pekee, hata two shida inakuwa competition hasa kwenye admission ya ''best'' universities kama Havard, MIT, Stanford, Princeton, Yale, Columbia, California Berkeley etc. But ukiwa na one yako nzuri, TOEFL nzuri sana, admission exam yao ukapass vizuri sana (incase wanataka ufanye paper), halafu ukawa financially muscular, unaweza kupata. Shida nyingine ni pale ambapo nafasi ni chache na unacompete na watu kutoka states zote za US, wako safi kila angle na hawajasoma system zaidi ya US inakuwa shida. Kumbuka mnacompete dunia nzima etc.

Sina experience ya bachelor but admission ya PhD economics havard au leading university in the world kama MIT huwa wanapokea 30 students au wakizidi sana 33 wakati walio-apply na wana sifa ni 900 kutoka kila sehemu duniani. GMAT yao kwa mfano ukitaka kusoma PhD au masters katika business huwa ni si chini ya score 730, au 740 na kuendelea kati ya 800!. Sasa hao ni wa maana kweli mdogo wangu?!!. BUT ASK GOD.YEYE NI KILA KITU.
umemaliza kila kitu mkuu
 
Mbona wanasema kwa Tanzania ukisoma PhD bila kuwa na masters ukirudi TCU wanakudisqualify. Je, kuna mtu yoyote ambae imemtokea hii? Naomba uzoefu wenu wadau!
 
Wanandugu,

Je, duniani kuna utaratibu wowote unaoweza kukufanya ukapata Ph.D bila kulazimika kupitia kwanza Masters? Kama inawezekana, ni institutions zipi zinao utaratibu huo?
What important is competence in the subject matter. Unaweza ukawa na PhD 10 na bado ukaonekana kiazi. Dogo piga msuli usitafute njia ya mkato.
 
What important is competence in the subject matter. Unaweza ukawa na PhD 10 na bado ukaonekana kiazi. Dogo piga msuli usitafute njia ya mkato.
The vise versa is true! You can't be competent with standard seven education, still more education is needed to improve your competence!
 
Inawezekana kbs, hata Sumaye alikuwa na Diploma then akaenda kufanya Masters Degree kule Harvard
 
Kama inawezekana mbona vyuo havitangazi huo mfumo ukafahamika kwa wanaohitaji elimu ya aina hiyo kama ilivyo kwa degree zingine? Wekeni na link za hivyo vyuo vinavyotoa PhD bila kupitia masters!
 
Kama inawezekana mbona vyuo havitangazi huo mfumo ukafahamika kwa wanaohitaji elimu ya aina hiyo kama ilivyo kwa degree zingine? Wekeni na link za hivyo vyuo vinavyotoa PhD bila kupitia masters!

Angalia prospectus ya SUA ya last year utaona hiyo kitu
 
Umeleza vizuri sana.
Swali zuri. Unaweza kupata PhD bila masters kama ambavyo unaweza kupata masters bila bachelor!. Southampton university kwa mfano wana kitu kinaitwa integrated degree(sio course zote) yaani mtu anaingia kuanza kusoma bachelor ya four years but kiukweli bachelor yake inakuwa ni three years ila mwaka wa nne unakuwa wa masters. At the end anapata masters but hapewi cheti cha bachelor anakuwa na cha masters tu (so inakuwa kama vile hajasoma bachelor). However, kuna baadhi ya vyuo ulaya unaweza kusoma masters ukiwa na diploma na mara nyingi ni zile za diploma za three years although za miaka miwili pia waweza kusoma masters kulingana na "content" ya diploma yako. I think journalism and mass comm ina-lead katika hizi degree.

Suala la kuruka kwenda PhD bila masters linawezekana si tu ulaya bali hata UDSM. Sio kweli kwamba ukiwa na first class pekee ndiyo utasoma PhD (a case of law pale UDSM kwa mfano) ila ni pale tu unakuwa umeregister kama mwanafunzi wa masters especially under thesis (not coursewok and dissertation) na wakati wa kuandaa thesis yako ukaona imekaa ki-PhD PhD (imevuka viwango vya masters masters) then utaipeleka department na department wakiipitia waka-confirm wanaipeleka senate na senate itakuruhusu ''kuvuka'' na kuwa PhD candidate (sio kukupa PhD hapohapo). Baada ya kukupa candidacy ya PhD, chuo kinafuta registration ya masters palepale (automatic cancellation). Kazi yako wewe ni kufanya thesis yako ya PhD na ukifanya viva ikapita wanakuaward PhD kama wanafunzi wengine wa PhD. Hivyo, at the end utakuwa na PhD bila masters.

Kwa vyuo vingine hasa South wao wakishakuona umefanya vizuri thesis yako ya masters wanaweza kukutongoza ili upublish paper kadhaa kama tatu hivi na vi-conference proceedings paper kadhaa then wanakwambia uvifanye viwe kitu kimoja (monography) then unapata PhD yako hata after 1 year. Ingawa hili linawezekana pia hata kama umeshakuwa awarded masters yako (hasa pia kama ulipublish zaidi ya paper walizokuwa wanazihitaji masters). This is also applicable hata EU na sehemu nyingine.

Kuhusu swala la division one form six (I assume ni NECTA na sio cambridge au IB) kupata admission havard, duke na vyuo vingine vya marekani inategemea na vitu vingi sana. Vyuo vya wenzetu wanaangalia mambo mengi sana ikiwemo lugha, uwezo wako kulingana na course unayokwenda kuchukua, cousre husika (masharti yanatofautiana), competition etc. Si division one pekee, hata two shida inakuwa competition hasa kwenye admission ya ''best'' universities kama Havard, MIT, Stanford, Princeton, Yale, Columbia, California Berkeley etc. But ukiwa na one yako nzuri, TOEFL nzuri sana, admission exam yao ukapass vizuri sana (incase wanataka ufanye paper), halafu ukawa financially muscular, unaweza kupata. Shida nyingine ni pale ambapo nafasi ni chache na unacompete na watu kutoka states zote za US, wako safi kila angle na hawajasoma system zaidi ya US inakuwa shida. Kumbuka mnacompete dunia nzima etc.

Sina experience ya bachelor but admission ya PhD economics havard au leading university in the world kama MIT huwa wanapokea 30 students au wakizidi sana 33 wakati walio-apply na wana sifa ni 900 kutoka kila sehemu duniani. GMAT yao kwa mfano ukitaka kusoma PhD au masters katika business huwa ni si chini ya score 730, au 740 na kuendelea kati ya 800!. Sasa hao ni wa maana kweli mdogo wangu?!!. BUT ASK GOD.YEYE NI KILA KITU.
 
Back
Top Bottom