Philip Mangula ang'atuka nafasi ya Umakamu Mwenyekiti CCM Taifa. Abdulrahman Kinana apendekezwa na Halmashauri Kuu kuchukua nafasi yake

Philip Mangula ang'atuka nafasi ya Umakamu Mwenyekiti CCM Taifa. Abdulrahman Kinana apendekezwa na Halmashauri Kuu kuchukua nafasi yake

Kinana ni kijana?

Kinana wa 1951 (71)
Mangula 1941 (81)

Hivi hawa wazee hawakuwekeza ujanani mpaka wawe na tamaa za uzeeni

Hivi kustaafu maana yake nini?
Mimi kapuku ila natarajia nikistaafu na 67 nimejiandalia mapumziko na kazi zangu mwenyewe
IMG_4770.jpg
 
Kwahiyo kuna watu wameshangaa upitaji wa hayo majina?? Kwamba hili swala hamkulitarajia au?

Hii nchi imeoza, na utawala wa huyu dada ni lazima watu wasage meno hasa wale wa kipato cha chini (watumishi wa umma).
 
Sasa Chadema huu ndo muda wenu wa kushine kama mtakuwa na akili. Nendeni kwa wananchi mjijenge. Maana ukweli sasa hii iliyopo ni serikali ya kufavor matajiri ambao ni minority hapa Tanzania.
Mkuu 'Victoire', naona umekuwa mpole!

Lakini naona bado huelewi vizuri. Ngoja nikusaidie kidogo.

Unaposema "CHADEMA waka-'shine,'" waka-'shine' kwa ajenda ipi? Huoni kuwa CCM ya Samia ndiyo CHADEMA ya Mbowe?

Labda useme kwamba CHADEMA waanze mikakati ya kujiingiza ndani ya CCM(CHADEMA) ya Samia.

Kukurahisishia zaidi ni kwamba, usione ajabu sana siasa zetu sasa zikawa kama zile za Kenya zilivyo sasa. Haya mavyama ya CCM, CHADEMA, ACT, CUF, yatakuwa ni vyombo tu vya kubeba watafuta fursa. Inapofika wakati wa kusaka uongozi, mavyama yote yanahaha kutafuta mahala pa kujibanza ili yawe kwenye ulaji. Kwa hiyo anza kutegemea , kwa mfano Muungano wa CCM na CHADEMA hapo 2025, na mambo yanakwenda 'smoothly' kama ugali na mlenda.

Umenielewa?

Jambo hili ni rahisi sana sasa kulieleza kwa wananchi, na hapo ndipo kila mtu atakapoanza kuimba 'Maza, Maza, Maza.....' , pengine hata wewe utakuwa ni kati ya hao waimbaji wa sifa za mama!

Mbowe, inawezekana tayari yupo huko Kenya (chuoni) kujifunza jinsi haya mambo yanavyofanya kazi.

Wewe na mimi hatukuwepo Mbowe alipoitwa Ikulu kujadili "mwafaka, haki, uhuru" Kuna maafikiano mazuri kuliko hayo?

Ngoja nikuache kwa sasa uyatafakari hayo.
 
Mangula ameachia nafasi ya umakamu mwenyekiti CCM, kaona isiwe tabu.

Ila hii Ni Mara ya Pili mzee anawekwa pembeni, sijajua ana tatizo gani na wenzio huko.

Nafasi imechukuliwa na Kinana

Membe karudishwa CCM

===

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Philip Mangula leo Alhamisi Machi 31, 2022 amewasilisha katika Halmashauri Kuu ya CCM barua ya kuachia nafasi hiyo.

Kikao Cha Halmashauri Kuu ya CCM kimependekeza jina la Katibu Mkuu wa zamani Abdulrahman Kinana kuteuliwa kupigiwa kura za kuwa Makamu Mwenyekiti CCM Bara ambapo atachukua nafasi ya Philip Mangula.

Kikao hicho kimefanyika leo 31 Machi 2022 Jijini Dodoma.


Pia soma;

1). Nashauri Makamu Mwenyekiti wa CCM Mzee Philip Mangula ang'atuke na akabidhi mikoba kwa Abdulrahman Kinana

2). Ukatibu Mkuu CCM: Nani anafaa kuchukua nafasi ya Daniel Chongolo? Kinana ndani

Akina kibajaji huko tumbo joto wasiyempenda huyooo mdogo mdogo anarudi sasa chama kimeshika hatamu.
 
Mangula ameachia nafasi ya umakamu mwenyekiti CCM, kaona isiwe tabu.

Ila hii Ni Mara ya Pili mzee anawekwa pembeni, sijajua ana tatizo gani na wenzio huko.

Nafasi imechukuliwa na Kinana

Membe karudishwa CCM

===

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Philip Mangula leo Alhamisi Machi 31, 2022 amewasilisha katika Halmashauri Kuu ya CCM barua ya kuachia nafasi hiyo.

Kikao Cha Halmashauri Kuu ya CCM kimependekeza jina la Katibu Mkuu wa zamani Abdulrahman Kinana kuteuliwa kupigiwa kura za kuwa Makamu Mwenyekiti CCM Bara ambapo atachukua nafasi ya Philip Mangula.

Kikao hicho kimefanyika leo 31 Machi 2022 Jijini Dodoma.


Pia soma;

1). Nashauri Makamu Mwenyekiti wa CCM Mzee Philip Mangula ang'atuke na akabidhi mikoba kwa Abdulrahman Kinana

2). Ukatibu Mkuu CCM: Nani anafaa kuchukua nafasi ya Daniel Chongolo? Kinana ndani

Master ni JK
 
Kwahiyo kuna watu wameshangaa upitaji wa hayo majina?? Kwamba hili swala hamkulitarajia au?

Hii nchi imeoza, na utawala wa huyu dada ni lazima watu wasage meno hasa wale wa kipato cha chini (watumishi wa umma).
Kuna kipindi watumishi wa umma wamesaga meno kama kipindi cha Jiwe?
 
Niko shule ya Msingi nasoma darasa la 5, Mh. Mangula alikuwa Mkuu wa Wilaya yetu ya Kwimba na tuliwahi kumwalika kwenye kata yetu kama mgeni rasmi kwenye sikukuu ya Sabasaba. Alikuja akiwa amevaa kombati za JWTZ. Wengi wasichokijua ni kwamba Mangula pia ni mwanajeshi wa JWTZ, ila wengi hawajui hilo
Ni kweli kaka nakumbuka pia,
 
Mangula ameachia nafasi ya umakamu mwenyekiti CCM, kaona isiwe tabu.

Ila hii Ni Mara ya Pili mzee anawekwa pembeni, sijajua ana tatizo gani na wenzio huko.

Nafasi imechukuliwa na Kinana

Membe karudishwa CCM

===

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Philip Mangula leo Alhamisi Machi 31, 2022 amewasilisha katika Halmashauri Kuu ya CCM barua ya kuachia nafasi hiyo.

Kikao Cha Halmashauri Kuu ya CCM kimependekeza jina la Katibu Mkuu wa zamani Abdulrahman Kinana kuteuliwa kupigiwa kura za kuwa Makamu Mwenyekiti CCM Bara ambapo atachukua nafasi ya Philip Mangula.

Kikao hicho kimefanyika leo 31 Machi 2022 Jijini Dodoma.


Pia soma;

1). Nashauri Makamu Mwenyekiti wa CCM Mzee Philip Mangula ang'atuke na akabidhi mikoba kwa Abdulrahman Kinana

2). Ukatibu Mkuu CCM: Nani anafaa kuchukua nafasi ya Daniel Chongolo? Kinana ndani

Sasa hivi ni CCM ya Kikwete. Mangula hawezi kufanyakazi na Kikwete. Ni mtu ambaye kuzunguka wengine hawezi. Kumbuka huyu ni katibu wa CCM wa kwanza msomi na baada ya hapo akaletwa mzee wa mipasho, Makamba na kuharibu maana ya katibu wa chama.
 

Abdulrahman Kinana kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Tembo , faru wajiandae kupotea na Ngorongoro sasa imeondoka vizuri.​

JPM angefufuka leo akatokea Dodoma kuna watu wangeogelea baharini kukimbilia kwao.​

Katiba yetu haijasema mtu akifufuka nn kitatokea hivyo uwezekano ni akija leo hatakuwa raisi. Itakuwa kama kipindi kabla hajawa kiongozi. Atafuata maelekezo ya samia au kuanzisha kikosi cha waasi.
 
Mm pia najiuliza Kama ww, sipo CCM Wala sio mfuasi wa mangula. Maana pia nilishangaa unakuwaje mtu mwenye 70+ anakuwa na nafasi kubwa hivyo.
Ni Kama Sasa ilivyo kwa Kinana 70+ bado nafasi kubwa Kama hiyo
Mimi sishangai kwa mtu wa umri huo kuwa na nafasi hiyo.

Tatizo Ni kuwa na mtu wa umri huo kila miaka nenda Rudi ni wewe huyo huyo.

Na hata ukistaafu au kujiuzulu watu wanashangaza, wanataka uendelee kuwa hapo wewe huyo huyo
 

Abdulrahman Kinana kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Tembo , faru wajiandae kupotea na Ngorongoro sasa imeondoka vizuri.​

JPM angefufuka leo akatokea Dodoma kuna watu wangeogelea baharini kukimbilia kwao.​

Daah... badala ya kujiimarisha kuiadhibu ccm na mifumo yake wewe unawaza wafu wafufuke?
#Shame
 
Back
Top Bottom