Picha: Ephrahim Kibonde wa Clouds FM atiwa nguvuni

Picha: Ephrahim Kibonde wa Clouds FM atiwa nguvuni

Ni kama vile anasema oya usinipige picha, tutaonana wabaya, mi nagombea ubunge mwakani, sasa watu wakijua 0713 yangu ipo hatarini watasemaje.

Hahahah,,yani mule mule kudadaek,,tigo iko hatarin kuliwa,,hapo ndo umeua mkuu
 
Habari JF lovers,
Hii ishu ya Kibonde ni kama ime kick sana, kwamba alijaribu kuvunja sheria huku akiwa amelewa,
The fact is Kibonde alikua anatengeneza Tangazo la Usalama Barabarani "TII SHERIA BILA SHURUTI"

Wanauzi sana watu wanaokuja kupinga lengo lao ni kuprovoke watu ili wajiridhishe ni kweli kakamatwa au la? cha kushangaza huyo anayepinga hana hata facts hata moja ya kutetea upu.pu wake! haya alikuwa anafanya tangazo je alikuwa anarecordiwa na satellite?
attachment.php
 
Pia lazima mjue kwamba Clouds FM wanacheza na saikoloji za watu, kitu mtavyokipokea ndo wao hugeuza, sio mda sana yaliandikwa mengi kwamba watangazaji wa clouds wamepigana studio lakini nani aliye kanusha?
Magazeti na mitandao mingi ya kijamii ili wapa kick......

This is what called stunt making

Mkuu wewe ni mbishi kama............(ngoja niishie hapo maana naona burn inaninyemelea).
 
pole sana. soma hapa mchini
ELIZABETH HOMBO WATANGAZAJI maarufu wa redio nchini, Ephraim Kibonde na Gadner G. Habash, wametiwa mbaroni katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, jijini Dar es Salaam baada ya kudaiwa kusababisha ajali na kukaidi amri ya askari wa usalama barabarani.
Kibonde ambaye amejizolea umaarufu kupitia kipindi cha ‘Jahazi’ kinachorushwa na kituo cha redio cha Clouds Fm akiwa na mtangazaji mwenzake wa Radio Times, Gadner, walikutwa na mkasa huo jana saa 12 asubuhi katika eneo la Makumbusho.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, zilieleza kuwa Kibonde ambaye alikuwa dereva wa gari hilo aligonga kwa nyuma gari lililokuwa likiendeshwa na raia wa kigeni (mzungu).
Akizungumza na gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani, Kamanda Wambura alisema baada ya Kibonde kusababisha ajali hiyo, alikaidi amri ya askari wa usalama barabarani iliyomtaka asimame ili wapime na badala yake aliondoa gari kwa mwendo kasi hali iliyoashiria alikuwa amekimbia.
Alisema baada ya kukaidi amri hiyo, askari aliyekuwepo eneo la tukio naye alipanda gari jingine kwa nia ya kumfukuza na kwamba alipofika eneo la Mwenge alifanikiwa kumsimamisha na kisha kupanda katika gari lake ili warudi eneo ilikotokea ajali.
Kwa mujibu wa Wambura, baada ya askari huyo kupanda kwenye gari la Kibonde, mtangazaji huyo hakurudi kwenye eneo la tukio na badala yake aliendelea kukata mitaa mingine.
“Bahati nzuri askari wetu huyo alikuwa anawasiliana na wenzake, walipofika eneo la Ubungo Mataa wakawawekea kizuizi kilichowasaidia kuwakamata.
“…Nilipata taarifa hizo za Kibonde nikiwa kwenye kikao, ni kweli alisababisha ajali majira ya saa 12 asubuhi pale Makumbusho na alimgonga Mzungu ambaye hata hivyo sikuishika namba ya gari lake,” alisema Kamanda Wambura.
Alieleza kuwa baada ya askari wa Ubungo kufanikiwa kuwakamata, waliwafikisha katika kituo cha Polisi cha Oysterbay na walibaini kuwa watangazaji hao walikuwa wamelewa.
“Walipofikishwa kituoni na kutakiwa kupimwa ulevi waligoma… kwa sababu Kibonde alikuwa hana uwezo wa kuendesha tena gari na walikuwa wanatoa lugha chafu za matusi kwa askari wetu,” alisema.
Alipoulizwa kuwa ni sheria zipi walizozivunja, Kamanda Wambura aliyataja makosa matano, ambayo ni kusababisha ajali, kutokutii amri ya askari, kukimbia na kutoroka na askari, kutoa lugha chafu za matusi na kukataa kupimwa ulevi.
Kamanda Wambura alisema kwa sasa wanaendelea na upelelezi wa tukio hilo, na baada ya kuukamilisha watapeleka jalada kwa wakili wa serikali ili watangazaji hao washitakiwe.
Akiwazungumzia watangazaji hao, Kamanda Wambura alisema kuwa wao wanawaona kama wahalifu wa makosa ya jinai na kamwe hawatawachukulia kama watu maarufu.
“Sisi hatutajali kama watangazaji hao ni watu maarufu, na kwamba mbele ya uso wa sheria hakuna umaarufu,” alisisitiza Wambura ambaye hadi tunakwenda mitamboni jana jioni alisema watangazaji hao walikuwa bado rumande.

Askari wamesahau kosa la kibonde kumteka askari mwenzao .
 
Pia lazima mjue kwamba Clouds FM wanacheza na saikoloji za watu, kitu mtavyokipokea ndo wao hugeuza, sio mda sana yaliandikwa mengi kwamba watangazaji wa clouds wamepigana studio lakini nani aliye kanusha?
Magazeti na mitandao mingi ya kijamii ili wapa kick......

This is what called stunt making

pambaafff...
 
Wadau,

Mnapenda sana UMBEA,muda sijui mnatoa wapi?. Je Mkiambiwa kua walikua wanatengeneza TANGAZO la kutii sheria bila shurti?.

Halafu mnasema nchi yenu masikini. Tanzania itaachaje kuwa masikini kama sample ya watu wake ni aina YENU humu??!!

Negative thinking imewajaa na uzandiki. Fanyeni kazi acheni majungu. Sasa KiBONDE akifungwa au kuwekwa sero wewe unafaidika vipi?

Mchawi sio lazima akuroge

Punguzeni majungu

FP

mbona hueleweki?
 
Habari JF lovers,
Hii ishu ya Kibonde ni kama ime kick sana, kwamba alijaribu kuvunja sheria huku akiwa amelewa,
The fact is Kibonde alikua anatengeneza Tangazo la Usalama Barabarani "TII SHERIA BILA SHURUTI"
Mkuu sisi tunachojua Kibonde kanyea ndoo, hay mengine utajua Wewe mwenyewe!
 
Hii issue Kama nchi za dunia ya kwanza kazi Hana, halafu mialiko Kama ikulu au kuwa mshehereshaji kwenye shughuli kubwa hapati tena, ila bongo ili litapita tu Kama ushuzi.
 
pole sana. soma hapa mchini
ELIZABETH HOMBO WATANGAZAJI maarufu wa redio nchini, Ephraim Kibonde na Gadner G. Habash, wametiwa mbaroni katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, jijini Dar es Salaam baada ya kudaiwa kusababisha ajali na kukaidi amri ya askari wa usalama barabarani.
Kibonde ambaye amejizolea umaarufu kupitia kipindi cha ‘Jahazi’ kinachorushwa na kituo cha redio cha Clouds Fm akiwa na mtangazaji mwenzake wa Radio Times, Gadner, walikutwa na mkasa huo jana saa 12 asubuhi katika eneo la Makumbusho.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, zilieleza kuwa Kibonde ambaye alikuwa dereva wa gari hilo aligonga kwa nyuma gari lililokuwa likiendeshwa na raia wa kigeni (mzungu).
Akizungumza na gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani, Kamanda Wambura alisema baada ya Kibonde kusababisha ajali hiyo, alikaidi amri ya askari wa usalama barabarani iliyomtaka asimame ili wapime na badala yake aliondoa gari kwa mwendo kasi hali iliyoashiria alikuwa amekimbia.
Alisema baada ya kukaidi amri hiyo, askari aliyekuwepo eneo la tukio naye alipanda gari jingine kwa nia ya kumfukuza na kwamba alipofika eneo la Mwenge alifanikiwa kumsimamisha na kisha kupanda katika gari lake ili warudi eneo ilikotokea ajali.
Kwa mujibu wa Wambura, baada ya askari huyo kupanda kwenye gari la Kibonde, mtangazaji huyo hakurudi kwenye eneo la tukio na badala yake aliendelea kukata mitaa mingine.
“Bahati nzuri askari wetu huyo alikuwa anawasiliana na wenzake, walipofika eneo la Ubungo Mataa wakawawekea kizuizi kilichowasaidia kuwakamata.
“…Nilipata taarifa hizo za Kibonde nikiwa kwenye kikao, ni kweli alisababisha ajali majira ya saa 12 asubuhi pale Makumbusho na alimgonga Mzungu ambaye hata hivyo sikuishika namba ya gari lake,” alisema Kamanda Wambura.
Alieleza kuwa baada ya askari wa Ubungo kufanikiwa kuwakamata, waliwafikisha katika kituo cha Polisi cha Oysterbay na walibaini kuwa watangazaji hao walikuwa wamelewa.
“Walipofikishwa kituoni na kutakiwa kupimwa ulevi waligoma… kwa sababu Kibonde alikuwa hana uwezo wa kuendesha tena gari na walikuwa wanatoa lugha chafu za matusi kwa askari wetu,” alisema.
Alipoulizwa kuwa ni sheria zipi walizozivunja, Kamanda Wambura aliyataja makosa matano, ambayo ni kusababisha ajali, kutokutii amri ya askari, kukimbia na kutoroka na askari, kutoa lugha chafu za matusi na kukataa kupimwa ulevi.
Kamanda Wambura alisema kwa sasa wanaendelea na upelelezi wa tukio hilo, na baada ya kuukamilisha watapeleka jalada kwa wakili wa serikali ili watangazaji hao washitakiwe.
Akiwazungumzia watangazaji hao, Kamanda Wambura alisema kuwa wao wanawaona kama wahalifu wa makosa ya jinai na kamwe hawatawachukulia kama watu maarufu.
“Sisi hatutajali kama watangazaji hao ni watu maarufu, na kwamba mbele ya uso wa sheria hakuna umaarufu,” alisisitiza Wambura ambaye hadi tunakwenda mitamboni jana jioni alisema watangazaji hao walikuwa bado rumande.

Haya mtoa mada wambura kathibitisha ongea sasa.
 
Habari ya nyongeza kutoka kwa ELIZABETH HOMBO iliyopatikana hapa hapa JF inasema kuwa: Watangazaji maarufu wa redio nchini, Ephraim Kibonde na Gadner G. Habash, wametiwa mbaroni katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, jijini Dar es Salaam baada ya kudaiwa kusababisha ajali na kukaidi amri ya askari wa usalama barabarani. Kibonde ambaye amejizolea umaarufu kupitia kipindi cha ‘Jahazi' kinachorushwa na kituo cha redio cha Clouds Fm akiwa na mtangazaji mwenzake wa Radio Times, Gadner, walikutwa na mkasa huo jana saa 12 asubuhi katika eneo la Makumbusho.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, zilieleza kuwa Kibonde ambaye alikuwa dereva wa gari hilo aligonga kwa nyuma gari lililokuwa likiendeshwa na raia wa kigeni (mzungu).
Akizungumza na gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani, Kamanda Wambura alisema baada ya Kibonde kusababisha ajali hiyo, alikaidi amri ya askari wa usalama barabarani iliyomtaka asimame ili wapime na badala yake aliondoa gari kwa mwendo kasi hali iliyoashiria alikuwa amekimbia. Alisema baada ya kukaidi amri hiyo, askari aliyekuwepo eneo la tukio naye alipanda gari jingine kwa nia ya kumfukuza na kwamba alipofika eneo la Mwenge alifanikiwa kumsimamisha na kisha kupanda katika gari lake ili warudi eneo ilikotokea ajali.

Kwa mujibu wa Wambura, baada ya askari huyo kupanda kwenye gari la Kibonde, mtangazaji huyo hakurudi kwenye eneo la tukio na badala yake aliendelea kukata mitaa mingine.
"Bahati nzuri askari wetu huyo alikuwa anawasiliana na wenzake, walipofika eneo la Ubungo Mataa wakawawekea kizuizi kilichowasaidia kuwakamata. "…Nilipata taarifa hizo za Kibonde nikiwa kwenye kikao, ni kweli alisababisha ajali majira ya saa 12 asubuhi pale Makumbusho na alimgonga Mzungu ambaye hata hivyo sikuishika namba ya gari lake," alisema Kamanda Wambura. Alieleza kuwa baada ya askari wa Ubungo kufanikiwa kuwakamata, waliwafikisha katika kituo cha Polisi cha Oysterbay na walibaini kuwa watangazaji hao walikuwa wamelewa. "Walipofikishwa kituoni na kutakiwa kupimwa ulevi waligoma… kwa sababu Kibonde alikuwa hana uwezo wa kuendesha tena gari na walikuwa wanatoa lugha chafu za matusi kwa askari wetu," alisema.

Alipoulizwa kuwa ni sheria zipi walizozivunja, Kamanda Wambura aliyataja makosa matano, ambayo ni kusababisha ajali, kutokutii amri ya askari, kukimbia na kutoroka na askari, kutoa lugha chafu za matusi na kukataa kupimwa ulevi.
Kamanda Wambura alisema kwa sasa wanaendelea na upelelezi wa tukio hilo, na baada ya kuukamilisha watapeleka jalada kwa wakili wa serikali ili watangazaji hao washitakiwe. Akiwazungumzia watangazaji hao, Kamanda Wambura alisema kuwa wao wanawaona kama wahalifu wa makosa ya jinai na kamwe hawatawachukulia kama watu maarufu.
"Sisi hatutajali kama watangazaji hao ni watu maarufu, na kwamba mbele ya uso wa sheria hakuna umaarufu," alisisitiza Wambura ambaye hadi tunakwenda mitamboni jana jioni alisema watangazaji hao walikuwa bado rumande.
 
Mtakubaliana na mimi hawa Jamaa wa Couds wanamapungufu sana hawajui miiko ya taaluma yao,jamii itajifunza nini toka kwao, shame on you all clouds people.
 
Back
Top Bottom