PICHA: Hili jengo linalojengwa Kariakoo kwa PPP ni balaa ni zaidi ya Mlimani City unaambiwa Serikali itajizolea zaidi ya TZS 2.5bn kila mwaka

PICHA: Hili jengo linalojengwa Kariakoo kwa PPP ni balaa ni zaidi ya Mlimani City unaambiwa Serikali itajizolea zaidi ya TZS 2.5bn kila mwaka

Ulichosahau hapa ni hela ya mwekezaji, nimesahau figure ila ni around 25% serikali na 75% mwekezaji kwa miaka 30 ya mwanzo then baada ya hapo jengo linarudi Serikalini, kwa mahesabu yako ya Milioni 900 ni roughly 2.7B kwa Serikali kwa mwaka.

Na Jengo likiwa na wapangaji 900 sio wote wana frame kuna vigoli vya mpesa na biashara Ndogo ndogo pia hivyo kama 200,000 wanakodisha.
Hakuna bil 2.7 itapatilana kwa mwaka

Hizi ni hesabu zetu. Mm nimefurahi mwekezaji kupewa sababu pataendelezwa vizuri sana na sio suala la mapato kwa serikali. Rejea kilichotokea kwa mlimani city

Huyo.mwekezaji hatalipa pesa stahiki, ataweka malimbikizo na mwisho itaibuka kesi ambayo tutarudi kwenye mkataba ulivyosema(ambao kwa Sasa wewe huujui na Mimi siujui)
 
Na wewe unapenda ku copy sababu nchi X imefanya Y kutotoboa na sisi unataka tupitie humo humo, kila nchi ina changamoto zake na namna ya kuzitatua.

Mfano mzuri angalia tu Mobile money kama Mpesa na Tigo Pesa ni kitu chetu tunajivunia Africa, tumeanzisha kitu na kimefit utamaduni zetu, so far Dunia nzima ina copy mfumo wa mobile money na Africa ikiwa pioneer.

Kwa logic zako hizi miaka 20 iliopita ungetaka na sisi tuegemee kwenye mifumo kama ya Ulaya ya Benki.

Hao unaoita wachuuzi wengi wanaingiza hela nyingi kwa mwezi kuliko Waalimu na wafanyakazi wengine wa Serikali, kawaida kkoo machinga kuingiza hadi laki kwa siku, kuna ma ofisa kibao serikalini wanatembea na Gari na kuendeshwa hawapati hio hela. So hao unaowadharau ni hope ya Taifa hili.

Siku zote mheshimu mtu ambaye Unampa 1000 anaweza akaizalisha na kesho akawa na 2000.
Wapi nimetaja nchi X?
 
Naona watu wamekurupuka kuchangia uzi kwa mihemko bila kuelewa kilichoandikwa. Mmeambiwa mradi ni wa serikali na mbia. Wakati ujenzi ukiendelea serikali itakuwa ikijipatia 2b kwa mwaka na baada ya mradi kukamilika serikali itajipatia 2.5b kama kodi ya jengo (kumbuka m'bia naye ana mgao wake nje ya hizo 2.5b) na bado hapo serikali itakusanya kodi na shuru nyingine kutoka kwenye uwekezaji huo. Kwa namna wakurupukaji wanavyochangia ni kama walitaka serikali ikusanye kilakitu na mbia asipate chochote kitu ambacho hakiwezekani. Nilidhani tungempongeza kwanza Kafulila kabla ya kucomment kwa chuki na mihemko.
Kwa uwekezaji wa pale ddc, serikali haiwezi kupata 2.5bil kwa mwaka. Mlimani city tu haipatikani hiyo pesa

Hakuna mwekezaji atatoa 2.5bil kwa mwaka, kwa mradi wa rooms 400. Pia haya maneno huwa mazuri sasa baadae wataanza ku-default na kesi juu

Mimi nilichopenda ni mwekezaji kuepewa patakua tofauti sana japo najua kwenye mapato serikali itapigwa kiini macho
 

Hatimaye PPP ya David Kafulila iliyoanzishwa kwa mujibu wa sheria namba 103 ya mwaka 2010 ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2014, 2018 na 2023 yaanza kuzaa matunda kwa Watanzania hasa baada ya kuanza kutumia marekebisho mapya ya Sheria hiyo ya mwaka 2023.

PPP kwa kumtumia mbia mzawa toka kampuni ya Tosh Logistics Limited watajenga jengo kubwa zaidi ya lile la Mlimani City lenye thamani ya TZS 36.7bn wakati matumizi yatagharimu kiasi cha TZS 13.3bn litakalokuwa na wapangaji zaidi ya 900 lenye ghorofa 10 kwenda juu.

Mkurugenzi Mtendaji wa PPP-Centre Bw. David Kafulila ameiambia kamati ya Bunge ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kuwa Dar es Salaam City Council's Economic and Development Corporation (DDC) katika wakati wote wa Ujenzi wa mradi huo kila mwaka watajizolea kiasi cha TZS 2 bilioni na baada ya mradi huo kukamilika watalipwa kiasi cha TZS 2.5 bilioni kama kodi ya jengo tu bila kuhesabu kodi na shuru mbalimbali na baada ya muda wa mkataba jengo hilo litakuwa ni mali halali ya serikali ya Tanzania.

Mkurugenzi huyo ameiambia kamati hiyo ya Bunge kuwa Ujenzi wa mradi huo ni miongoni mwamiradi yenye mikataba bora zaidi ya uwekezaji kuwahi kushuhudiwa hapa kwenye ardhi ya Tanzania.

Mkurugenzi huyo ameipongeza kamati hiyo ya Bunge huku akiomba ushirikiano kati ya TAMISEMI na PPP ili kwa pamoja waweze kuvuta mitaji toka sekta binafsi ili kujenga miradi yenye tija kwa Taifa ambayo itatupatia Kodi na tozo mbalimbali na hivyo kuchochea ukuaji wa Uchumi wetu huku Serikali ikiachwa ifanye miradi ile tu ambayo haina sura ya kibiashara na hivyo kuipa nafuu zaidi Serikali katika kutafuta Mikopo na misaada mbalimbali toka kwa wahisani.
Hatua nzuri, but eneo la ddc haliwezi kuwa kama mlimani city. Ni eneo dogo sana
 
Akili za kimasikini hizi UNAFKIRI hizo Trilioni zinafikaje kama sio kudunduliza? 2.5B kwa jengo moja ni lot of money ila I doubt serikali inapata hio hela kwenye jengo moja tu, unahitaji si Chini ya frame 400 zinazolipiwa around 2M kwa mwezi kugenerate hela hio kwenye PPP ya kariakoo.

Kikawaida kkoo Ghorofa binafsi hata 1B kwa mwaka hazifiki, la sivyo Maghorofa yasingeuzwa Bilioni 5.
Binafsi mwenyewe nimeshangaa,
2.5B kwa mwaka kwenye jengo moja tena hapo mpo kwenye PPP means kuna % kibao za mwekezaji kasepa nazo, hizo hesabu ni kubwa sana, sijui mwekezaji atarudishaje
 
Kwani kuna chochote kinachowezekana bila kuwa theoretical kwanza?

Hilo jengo kenyewe si kazima ulichore kwanza, ukikichora si ndiyo theoretical yenyewe hiyo?

Mbona mimi nikichora idea unashangaa wakati jengo likichorwa hushangai?

Nyie ndiyo maana mnalialia uchumi mdogo, hamjui hata thamani ya mlichonacho.

Tanzanite ya Tanzania inauzwa Kenya na India, mmeshindwa kudhibiti Tanzanite iuzwe Kariakoo?

Imagine unaweka floor ya kuuza madini ya wachimbaji kutika Tanzania nzima hapo, unawakusanya watu kutoka dunia nzima, utashindwa kupata dola milioni moja kwa mwezi?

Mmeshindwa kufikiria tu.
Mkuu, idea yako ni nzuri ila inahitaji eneo jingine sio kkoo,
Tutengeneze soko la madini kwingine, pale kkoo ni soko la watu wa chini la vitu vya kawaida, pale watapanga wauza TV, Nguo, simu, kapeti na vitu vingine kama hivyo,

Kama tunataka international malls hebu tukaweke maeneo mengine haina haja ya kubadili kkoo nzima kisa international malls,

Mana ukifanya hivyo, mawinga wote na kina mwajuma wa mbagala wanaoenda kkoo wataacha kwenda, utakuta ushaibadilisha kkoo kabisa,
 
Dar es salaam imejaa sana kwa sababu watu wamejenga vibanda vya chinichini mji mzima. Sasa ni wakati wa kujenga juu.

Pia, kujenga kwenda juu kunapunguza safari ndefu, badala ya kwenda maduka kumi sehemu tofauti unapata kila kitu sehemu moja.
Lakini bado maeneo yapo sio lazima mjini kwani mji unatanuka kwa huduma
Kama kutakuwa na huduma zote lazima watu watakwenda tu

Hapa nilipo kuna masoko makubwa mbali na mji lakini watu wamejaa kila siku
Kuwa na soko la ghorofa 10 ina changamoto nyingi sana ila siwezi kubisha labda ndio wajenzi wameshauri hivyo
 
Back
Top Bottom