Picha: Inawezekana kujenga nyumba kwa Design hii kwa milioni 16?

Picha: Inawezekana kujenga nyumba kwa Design hii kwa milioni 16?

Mafundi wa kibongo wowote wengi wao ni full ujanja ujanja tu na maneno meengii utadhani waga sio professional

Kwani mkiwa mna design ramani waga kuna sehemu mnaigilizia? Si unauliza mtu anataka nyumba yake iweje na wewe fundi/architecture una design kulingana na mahitaji ya mteja

Sasa jamaa karahisisha kabisa Kwa kuleta picha, it's okay, hakuna anaejua dimension za vyumba,dining nk ila umeona picha ya mwonekano wa nje hiyo ndo kazi yako sasa

Hapo ndio sehemu ya kujitofautisha wewe fundi/architecture na mteja, sasa fundi unaanza ohhh unajua hapo hatujui ndani pakoje, ohhh unajua hapo chini ukiweka beam gharama itakuwa kubwa

Ohhh ohhh nyingi WTF, kaa chini toa kitu kuhusu Mambo ya gharama ashindwe mwenyewe muhusika, kama unabuni ramani kutoka kichwani sasa unashindwa nini kubuni ramani kutoka kwenye picha?
I wonder!
 
Okay, Dr anaweza kuhisi unaumwa nini kutokana na maelezo yako pasipo ata kukupima Damu

Actually sitaki kusema kuwa narahisisha bali nasema kuwa nyie mnafanya Mambo yawe mengi sana

Wewe kama ni fundi au mchora ramani huwezi kupata shida kiasi hicho unless otherwise uwe huna uzoefu kabisa

Kama ni mzoefu basi utajua kabisa vyumba katika nyumba za kisasa let's say waga vina ukubwa wa 12*16, dining 20*25,Choo cha ndani 2*3, kitchen 8*8 and so on

Sasa hapo unashindwa kumpa simple analysis kulingana na uzoefu wako na pia jicho la kiufundi baada ya kuangalia mfano wa picha na kusikiliza matakwa yake? Kwanini usimpe mtu roughly sketch ata 3 ambazo yeye atachagua?

Na ndomana mara nyingi wateja waga wanapenda kutumia mafundi wa kawaida Kwa sababu waga wako straight na sio architecture au engineers Kwa sababu always Wana complicate Mambo
Kona kona nyingi sana, inashangaza kwakweli na kusikitisha
 
Hii ramani kali sana, nimeipenda ni nyumba ya vyumba viwili, nimeitoa huko Twitter kwa mnigeria, mwenyewe anadai anaweza kukujengea nyumba kama hiyo ya kwa Naira milioni 5 tu ambapo hiyo ni sawa na milioni 15 na laki 9 kwa pesa za kibongo (15,907,496.08)

Yule jamaa kama ni kweli anaweza kujenga hiyo nyumba kwa kiasi hicho Cha pesa basi atapata wateja wengi sana maana nimeona watu wengi wamemuomba mawasiliano yake japo wapo watu walio doubt kwamba ni japo lisilowezekana.

Halafu pia kwenye Comment Section kupitia hiyo tweet yake nimeona jamaa Kasema kwao mfuko mmoja wa cement ni Naira 8,400 ambayo ni sawa na Tsh 26,700, hiyo ni gharama kubwa sana ukilinganisha na bei ya huku kwetu ambayo inachezea kwenye 16,500 hadi 18,000 je kwa fact hiyo inawezekana kushusha mjengo kama huo kwa milioni 16 pekee

Eniwei, Mimi nimeipenda hiyo ramani hata kama itanicost milioni 50 fresh tu ilimradi kitu kitoke kama kilivyochorwa hapo japokuwa jamaa kasema hiyo design ni best suitable for 2 bedroom ila Binafsi ningependa iwe 3 bedrooms hata kwa ku convert hiyo Car garage hiyo hapo chini to another room

Kuna Eng hapa Bongo anaweza modify hiyo ramani iwe 3 bedrooms instead of 2 bedrooms?View attachment 2683359
Kwa picha tu Ni vigumu sana kufanya tathimini. Scale na Vipimo Ni muhimu sana, idadi ya vyumba pia; na materials gani. Vinginevyo ni ramli tu na watakudanganya.
 
Hii ramani kali sana, nimeipenda ni nyumba ya vyumba viwili, nimeitoa huko Twitter kwa mnigeria, mwenyewe anadai anaweza kukujengea nyumba kama hiyo ya kwa Naira milioni 5 tu ambapo hiyo ni sawa na milioni 15 na laki 9 kwa pesa za kibongo (15,907,496.08)

Yule jamaa kama ni kweli anaweza kujenga hiyo nyumba kwa kiasi hicho Cha pesa basi atapata wateja wengi sana maana nimeona watu wengi wamemuomba mawasiliano yake japo wapo watu walio doubt kwamba ni japo lisilowezekana.

Halafu pia kwenye Comment Section kupitia hiyo tweet yake nimeona jamaa Kasema kwao mfuko mmoja wa cement ni Naira 8,400 ambayo ni sawa na Tsh 26,700, hiyo ni gharama kubwa sana ukilinganisha na bei ya huku kwetu ambayo inachezea kwenye 16,500 hadi 18,000 je kwa fact hiyo inawezekana kushusha mjengo kama huo kwa milioni 16 pekee

Eniwei, Mimi nimeipenda hiyo ramani hata kama itanicost milioni 50 fresh tu ilimradi kitu kitoke kama kilivyochorwa hapo japokuwa jamaa kasema hiyo design ni best suitable for 2 bedroom ila Binafsi ningependa iwe 3 bedrooms hata kwa ku convert hiyo Car garage hiyo hapo chini to another room

Kuna Eng hapa Bongo anaweza modify hiyo ramani iwe 3 bedrooms instead of 2 bedrooms?View attachment 2683359
Hiyo bei sahau mkuu.
 
Kwa picha tu Ni vigumu sana kufanya tathimini. Scale na Vipimo Ni muhimu sana, idadi ya vyumba pia; na materials gani. Vinginevyo ni ramli tu na watakudanganya.
Idadi ya vyumba si umeshaambiwa!
 
Naona watu wameshindwa kumuuliza muhusika swali la msingi kwamba hilo jengo anajengea wapi?

Ujenzi wa mji kama wa Dar huwezi kuufananisha na wa Mbeya,gharama zinazidiana mkoa kwa mkoa.
Kabla ya hayo ..kikubwa ramani ya mjengo ....
 
Hiyo ya kuwa Scammers ni wao, sisi tunachotaka kujua ni kwamba inawezekana au haiwezekani?

Kama inawezekana unadhani nitawaacha mafundi wote hapa Tz nikamtafute mnigeria wa kazi gani?
Kifupi 16m haitoshi japo hujatoa dimensions.
Ungetoa ramani ingewasaidia wataalamu kufanya makadirio.
 
Kona kona nyingi sana, inashangaza kwakweli na kusikitisha
Ndio walivo hawa wasomi wetu, yani we ukitaka kufeli Jambo lako at the beginning kabisa mshirikishe mtu mwenye professional yake

Let's say unataka kufungua biashara, Mwambie Afisa biashara aje akushauri aina ya biashara kulingana na Eneo lako,ndo basi tena we kiuno Feni hiyo biashara imefia hapo

Unataka kujenga ita engineer akupe ushauri wa kitaalamu,uchunguzi,Tathmini,majaribio nk, ujue ndo anakuja kuzika kabisaaa ndoto zako

Yani kibongo bongo the vice versa is False, professional ndio wana behave like layman na layman ndio wana behave like professional
 
Idadi ya vyumba si umeshaambiwa!
Dimensions..Idadi sio issue.. issue vipimo, upana na urefu wa ukuta pamoja na msingi, milango, madirisha ...nyumba inaweza kuwa vyumba 3 ila Kwa mwingine vyote hivyo ni kimoja...vipimo
 
Kwani hiyo picha hadi imekaa hivyo si imetokana na ramani
Mkuu Ni kweli imetokana na ramani. Kwa hiyo leta na hiyo ramani pamoja na hiyo picha yako watu waifanyie kazi.
Ramani ina migawanyo ya vyumba na vipimo.
 
Kona kona nyingi sana, inashangaza kwakweli na kusikitisha

Mkuu hapo tusiwalaumu hawa architects wetu kwa kutokujibu unavyohitaji, kwa nijuavyo mimi hapo fundi akikupa makadirio atakuwa anakudanganya maana makadirio huwa yanatokana kwa vipimo unless just unataka makadirio yasiyo ya kitaalam.

Ila kama makadirio ya huyo mnigeria ni 16M ikiwa na garage,kwa kuwa room itakuwa na mahitaji ya material zaidi ya hapo garage tegemea zaidi ya 16M.
 
Dimensions..Idadi sio issue.. issue vipimo, upana na urefu wa ukuta pamoja na msingi, milango, madirisha ...nyumba inaweza kuwa vyumba 3 ila Kwa mwingine vyote hivyo ni kimoja...vipimo
Wewe kama mtaalamu ukipiga Calculations zako kwa Design hiyo na kiasi hicho cha pesa tutatoa vyumba vya ukubwa gani? Wacha pesa ituamulie ukubwa wa nyumba lakini materials yabaki kuwa standard
 
Back
Top Bottom