PICHA: Je Unaikumbuka Jambo Forums? Ulikuwa Wapi enzi hizo?

Nyani Ngabu na yeye alikuwaga na I'd kibao, na kuna chizi mmoja anaitwa Yo Yo walikuwa wanamtukanana sana aiseee.

Niliamua kuwa halisi tu 😀😀😀
Mimi alternative IDs zangu zote zilikuwa zinajulikana na sikuwahi kujificha hata kidogo.

Matter of fact, nilikuwa natangaza kabisa kuwa ID flani ni mimi.

Nilikuwa nazitumia pale tu ninapopigwa ban.
 
Nilikuwa nipo Darhotwire.com ingawa pia nilikuwepo hapa kwa ile ID yangu nyingine😎
 
Mimi alternative IDs zangu zote zilikuwa zinajulikana na sikuwahi kujificha hata kidogo.

Matter of fact, nilikuwa natangaza kabisa kuwa ID flani ni mimi.

Nilikuwa nazitumia pale tu ninapopigwa ban.
Kuna Baba Mchungaji Masanilo naye alikuwaga na i'ds zaidi ya 3. Hivi Mkuu Mshikaji wako Yo Yo yuko wapi?
 
Taratibu basi wasije wakasikia🤒😂

ILa wewe 2013 mie niko S.t.d 6,. Wewe age mate kabisa
Age mate? Hahaha!
Email account nimefungua 2001, ilikuwa hotmail.com
Facebook account nimefungua 2008.
Nilitumia Darhotwire miaka hiyo.

Jf sikwahi kuiona kabisa, ni 2012 ndio nilioona na baadae nikajiunga.

Nimeanza kuzagamua 1999🤣, nashindwaje kuwa mzazi wako.
 
yahoo nilianza kutumia mwaka 2003
Facebook nilijiunga mwaka 2009
JF 2008 nikawa sina ukomavu wa juu nikajipa suspension nikarudi tena 2010
 
Aisee kweli ni baba😑,.

Ila nyie miaka inaenda sana aisee,.Just imagine leo uko jukwaani mnabishana kwelikweli na mtu unaweza kumzaa kabisa
 
Aisee kweli ni baba😑,.

Ila nyie miaka inaenda sana aisee,.Just imagine leo uko jukwaani mnabishana kwelikweli na mtu unaweza kumzaa kabisa
Basi tu sijui kwanini lakini humu Jamiiforums kuna watu wa maana sana yaani. Ni watu wenye hadhi na nyadhifa zao. Lakini ndio vile members wa kuanzia 2016 na kuendelea wengi wamekosa staha kabisa.
 
Aisee kweli ni baba😑,.

Ila nyie miaka inaenda sana aisee,.Just imagine leo uko jukwaani mnabishana kwelikweli na mtu unaweza kumzaa kabisa
Ndio raha ya utandawazi, tunajochanganya watu wa rika zote bila kubaguana, sasa kama mzee kama mimi naweza kukutongoza na kukuweka...🤪dunia inaenda kasi sana!
 
Sema wewe sio wa long time mkuu,. 2010 bado kijana

2006,2007,2008 muda huu mwingi nilikuwa guest, JF ilitawaliwa na mijadala ya kisiasa sana na mimi huwa naona siasa za TZ ni ujinga ujinga tu, chimbo langu lilikuwa kwa blogs za Ankal Michuzi, Mjengwa na jamaa mmoja hivi wa US alikiwa sijui DJ yule nimesahau jina lake (miaka hii blogs zilikuwa maarufu kuliko forums)...

2009 nilijiunga lakini baadaye nikasahau password, 2010 mwanzoni nikajiunga tena kuna jambo nilikuwa nataka nipush hapa kwa wadau...

Nilikuwa naingia sana kusikiliza miziki ya nyumbani, kulikuwa na embedded music player ilikuwa na collection ya zilipendwa na miziki mingine...

Wengi wa kitambo wataikumbuka hii interface...

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…