Elections 2010 Picha: Kikwete Tanga, Bumbuli, Kilindi, Kilimanjaro, Arusha

Elections 2010 Picha: Kikwete Tanga, Bumbuli, Kilindi, Kilimanjaro, Arusha

Maji Marefu for uwaziri! This guy is setting a precedent. Si ajabu 2015 walozi wenzake km akina Sheik Yahya Hussein; wale wa kule Ghamboshi, n.k. wakaunga bodi kutafuta ubunge kupitia CCM. Maana ilianza wimbi la wafanyabiashara mafisadi, sasa wachawi.
 
Mie naogopa kuchangia mawazo jamaa anaweza kukuadhibu huko huko ilipo
Hapa mi nacheza na 'electronics' hata awe profesa au docta wa kienyeji, hawezi kukatiza akanipata katika hizi 'electrons' hawaniwezi hawa! kwanza namwamini Mungu ambaye 'rafiki' yao Yahya anasema aalimzidi nguvu yule nanihii, pale nanihii alipokuwa akihutubia halafu akaanguka!!!:smile-big:
 
Maji Marefu for uwaziri! This guy is setting a precedent. Si ajabu 2015 walozi wenzake km akina Sheik Yahya Hussein; wale wa kule Ghamboshi, n.k. wakaunga bodi kutafuta ubunge kupitia CCM. Maana ilianza wimbi la wafanyabiashara mafisadi, sasa wachawi.
Nimeota kuwa atapewa na uwaziri wa usalama wa viongozi Tanzania
 
Anayejua jamani PROF.MAJI MAREFU and DR .KIKWETE where did they graduate on their PhDs?
 
kama kuna tatizo basi ni kwa wananchi waliompitisha kwenye kura za maoni.
 
Ok. Ni vizuri Wabunge wetu wakawa na akina Prof Majimarefu ndani ya mjengo kuliko kufunga safari kwenda kuwatafuta Korogwe, Bagamoyo, Kigoma, Shinyanga,....., na angalau wakionekana karibu na milango ya Ikulu yetu tunajua wako pale kwakuwa ni wawakilishi wa wananchi wetu!
 
Ok. Ni vizuri Wabunge wetu wakawa na akina Prof Majimarefu ndani ya mjengo kuliko kufunga safari kwenda kuwatafuta Korogwe, Bagamoyo, Kigoma, Shinyanga,....., na angalau wakionekana karibu na milango ya Ikulu yetu tunajua wako pale kwakuwa ni wawakilishi wa wananchi wetu!

Mambo mengine ni vigumu kusadiki lakini mhhhhh inawezekana yapo. Nakumbuka Mh Chenge aliwahi kushukiwa kuweka vitu vya ajabu mle kwenye jengo la Bunge! Nimewahi kusoma magazeti kuwa mauaji ya ndugu zetu albino yakihusishwa na viongozi wa ngazi za juu serikalini. Wakati wote sikuamini. Niliwahi kusikia viongozi huonekana mlingotini kule Bagamoyo kabla ya kwenda kwenye uchaguzi, sikuamini.

Sasa Kikwete hajakanusha madai ya uchawi kuhusiana na ulinzi alioahidiwa na Sheikh Yahya, na wala kujinasua katika fununu za yeye kuwa mshirikina. Sasa huyu tena! Sikumfahamu kabla, kwa muda wote nilifikiri ni hawa vijana wanaoijiita maprofesa katika fani ya usanii, kumbe ni ya uchawi tena.

Najiuliza sasa hivi, kweli wenye ulemavu wa ngozi(albino), wa nywele (vipara) na vitoto vidogo(vibikira) watapona kweli kwa awamu hii inayokuja! Mungu atuepushie hili janga. Kweli Kikwete na BA yako ya Economics unakwenda that low!?
 
Hivi ndo vituko vya mwaka. Waganga wa kienyeji wa CCM kupelekwa bungeni,upande wa pili kutakuwa na wachungaji akina Lwakatare. Bungeni kutakalika? Vote for DR. SLAA na wabunge wa CHADEMA na siyo hao walioona ufisadi hautoshi sasa wanaleta ulozi!
 
Kama unamuamini mungu wewe changia tu. Shibuda huyo anadunda mbona na alijitokeza kugombea urais ijapokuwa bwana sheikh yahaya alisema atakufa!!!


SHIBUDA hakujitokeza kugombea urais,alikuwa kwenye process na hata jina lake wala halikwenda nec!Mgombea alikuwa JK tu.Ikumbukwe kuwa Shibuda alimuunga mkono JK kwa kumchangia Tshs.200,000/= za kampeni na pia kumpamba kwelikweli.Leo amegeuka,Hivi Shibuda kweli anataka kuwakomboa wananchi au anataka ulaji!!?
 
kama kuna tatizo basi ni kwa wananchi waliompitisha kwenye kura za maoni.


Ni kweli,kilichofanyika ni amepita kwenye kura za maoni ambazo ni wananchi ambao walengwa zaidi,wanamfahamu na wahahisi atawasaidia.kama ni kosa, basi ni la wananchi.
 
Mie naogopa kuchangia mawazo jamaa anaweza kukuadhibu huko huko ilipo

hakuna kitu kama hicho weewe, au na wewe ni mwamini nini wa imani za kijima kama hizo?
 
Bunge lijalo ltakuwa la ajabu sana maana hata huko kigoma kuna jamaa aliyekuwa na tuhuma nyingi za kuhusika na viungo vya albino, lakini ndio amepitishwa kugombea kwa tiketi ya CCM, nasikia jamaa mtandao wake wa nguvu za giza ni wa kibembe (kutoka Congo) ambao ni wakali kweli kweli kwenye huo upuuzi.CCM wanajiimarisha kwa mbinu za giza ili waendelee kutunyonya na kutupumbaza watanzania, lakini HAWATASHINDA..
 
Maji marefu angependeza akiwa mkuu wa itifaki, Ikulu ili ulinzi kwa mkuu uwe wa kutosha.
 
ccm ni chama cha wachawi na watu wenye mawazo dhalili na wahujumu wa uchumi na raslimali za taifa.
Yuko yule wa Urambo aligombea jina lake limenitoka ni mganga, manyaunyau ni mwanaccm pia, shehe Yahya hussein na Maji marefu.

Sheikh Yahaya nae atalamba vile viti 10
 
Back
Top Bottom