Picha: Raia wa kigeni azunguka na watoto Kariakoo kuomba msaada

Wasamalia wema wawanunulie yeboyebo hao madogo.
 

Kapita mtaani kwetu anasema ametokea Syria anaomba msaada

Wanae wazuri mashaallah
 
"Hakuna kitu kibaya sana humu duniani kama shida
Haichagui mtu, siku wala mwaka
Haina katu taarifa shida huingia shida bila hodi
Si mtoto wala mkubwa wote shida
Kila siku shida shida haiishi mpaka siku ya mwisho."

Shida song by late Baraka Mwinshehe
 
kaka usiombe vita vikukute nchini mwako huyo nahisi ni msyria kwao
kuna vita zaidi ya miaka 10 walitanyika hawana maisha kuna wengine walifia amana waliugua na hawana ndugu.kuwa na shida sio lazima uwe mchafu ndio uombe, uchafu ni tabia ya mtu, lakini shida haina msafi wala mchafu
 
Mwangalie vizuri asijekuwa Dejan anatafuta nauli
 
Unaweza nifanyia mpango.kuna bi mkubwa wang anataka alee kile kitoto chake cha mwisho
Kale anakokabeba shingoni?

Tatizo namna ya kuzoeana nae maana nilipo mimi ndo kituo chake kila asubuhi na sitaki mazoea nae naweza kujifanya kumsemesha mwisho akaniganda nikawa rafiki yake wa mtaani wa kuhudumia familia yake kitu nisichokitaka.

Kama mna nia kweli ukipata wasaa pita mitaa niliyoitaja hapo juu mida ya 08:00 asubuhi hukuwakuta mtaa wa Swahili basi utawakuta mtaa wa Udoe pale kwenye jengo la Discount Center,anacheza hapo hapo junction ya Swahili & Udoe na Msimbazi mpaka saa 09:00.
 
I see.okay.nimemuonesha bi mkubwa amependa sana hako ka mwisho.
Ila huu mtihan waumin kesho maswal magumu.baitul mal ndio ilikua ua kuwasiaidia hawa.leo watu wamekalia mafurushi ya dhahab na fedha bila kutoa zakat
 
Kwanini hukumuuliza shida yake muhusika mwenyewe na badala yake ukampita picha na kuja kumuanika huku? Nani amekupa mamlaka ya kumpiga picha na kuanza kumsambaza kwenye social media bila ridhaa yake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…