Picha: Rais Samia akiwa kwenye kiwanda cha Volkswagen nchini Rwanda

Kagame anaonekana yuko vizuri kichwani kawazidi hawa jamaa wengine, hata mambo ya ndani kwetu anaweza kuwa anayafahamu vizuri tu ila anazuga kumuuliza Samia habari za alikotoka.
Kagame sio mgeni tz kama hujui.

Hawa wote wanaijua tz vyema sana,ndio sababu huwa hawaleti ujuaji.

Labda huyo jamaa yenu wa kenya.
 
Sisi ndo kwanza tunawaza kufyatua barakoa milioni 86 kwa siku..!!
 
Rwanda imepiga hatua kubwa sana ktk teknoloji kuliko Tanzania, shida ni nn wakati tunao mawaziri na watendaji wasomi wazuri, jamani shida ni nn?
Viongozi tunawaomba muwe wazalendo wa kweli, Igeni maendeleo yanayo fanywa na nchi jirani, acheni kujigungia, badikeni kuweni wabunifu.
watanzania tu gependa kuona maendeleo kama hayo tunayo yashudia kwa jirani zetu.wanyatiwanda, tumeshuhudia kiwanda cha simu n.k.
kwa nn tunashindwa wakati nchi yetu ina urafiki ina urafiki na mataifa yenye tecknolojia ya juu kama china n.k, tuingize tecknolojia,
 

..ni kwasababu tunanunua ndege cash kwa trillion 2.

..wakati bajeti yetu ya wizara ya kilimo na ushirika ni billioni 294.

..vipaumbele vyetu sio sahihi hata kidogo.

Cc zandrano
 
..ni kwasababu tunanunua ndege cash kwa trillion 2.

..wakati bajeti yetu ya wizara ya kilimo na ushirika ni billioni 294.

..vipaumbele vyetu sio sahihi hata kidogo.

Cc zandrano
Lakini hizi ndege ni juzi tu zimenunuliwa?

Huko nyuma je?

Nadnhani kuna umuhimu wa kulitazama hili swala kiundani zaidi sababu zake, maanake hapa ndipo panapoweza kuwa mwanzo/mwisho wa kukosa maendeleo ya haraka nchini mwetu!

Nafahamu CHADEMA wana jibu juu ya sera yao ya MAJIMBO. Lakini sera hiyo kwa bahati mbaya mimi hainivutii kabisa. Pengine nikipata somo la maana nitaelewa!
 

..Kikwete na Magufuli ndio waliopata uongozi nchi ikiwa stable kiuchumi na ikiwa na budgetary flexibility ya kutekeleza vipaumbele vya nchi.

..Ukiangalia miradi ya Magufuli kama ujenzi wa makao makuu Dodoma, na ununuzi wa ndege, ni miradi gharama kubwa sana kwa uchumi mzima wa Tanzania.

..Unajiuliza what if badala ya kujenga maofisi na majumba ya kifahari Dodoma, angeelekeza fedha hizo kwenye sekta za zabibu, alizeti, na mifugo, hapo Dodoma, matumizi hayo yangeinua maisha ya wananchi wangapi?

..Pamoja na trillion 2 tulizotumia kununua ndege bado kila mwaka inabidi tubebe mzigo wa hasara ambayo ni billions of shillings.

..Kwa hiyo kwa Kikwete tulipata hasara kutokana na ufisadi, kwa Magufuli tulipata hasara kwa matumizi ya fedha yasiyo na busara.
 
Kuna watu hawana adabu kabisa unawezaje kuongea matusi kwa mtu mzima kama huyo hata kama asingekuwa Rais.
Mara nyingi,watu Hawa,wanakuwa sio watanzania,watanzania hawana utamaduni,wa kutowaheshimu wakubwa wao.
 
Mara nyingi,watu Hawa,wanakuwa sio watanzania,watanzania hawana utamaduni,wa kutowaheshimu wakubwa wao.

..tabia hizo zilianza na ccm.

..hivi mmefuatilia matusi wanayotukanwa wapinzani nchi hii?

..Na Rais SSH mnayemtetea ameteua vijana wenye rekodi ya kutukana wapinzani matusi ya nguoni.

..Rais SSH anataka tumheshimu kama mama zetu, lakini anateua vijana wanaotukana mama zetu na wake zetu.

..tabia matusi haitaisha kama hatutaikemea bila kujali inafanywa na CCM au wapinzani.
 

Wao wanaamini wakubwa ni viongozi wa Serikali yao tu.

Walimtukana sana Lowassa

Sasa sijui anaongelea wakubwa gani
 
Mkuu umeeleza vizuri tu, pia hata mkapa kipindi chake kulikuwa na mambo ya hovyo sana. Watu waliuziwa viwanda vya serikali kwa bei ya nyanya
Sasa balaa lingine tunalo awamu hii ya huyu mama.
Sijui ni lini wananchi wataamka na kuwapiga mawe CCM wote
 
Akili mbovu kabisa unadhani huyo bibi yako..uwe na nidhamu
Kama hutaki asemwe, mwambie aachie ngazi akalee wajukuu alafu uone kama Kuna Mtu atakuwa na habari nae
Ila kwa kuwa ni kiongozi basi hakuna tusi ambalo hatalipata, iwe wazi au sirini
 
Walivyopendeza utafikiri girlfriend kaegemea gari la boyfriend wake

Acha matusi ww, una mdomo mchafu sana. It seems maneno yako machafu sana, huyo ni mama yako kiumri na kila kitu ukiachia mbali ni Rais wa nchi, nidhamu chafu kabisa
 
Kagame ingawa ni Dikteta sugu ila ana akili sana anawazidi kwa mbali mno hawa marais wa East Africa. Wa pili ni Kenyatta...

Wengine hawa ni mwendo wa kudra za mwenyezi Mungu.
Mimi namkubali m7 tuu kwanza ana misemo adimu
 
Hii picha kiitifaki haijakaa vizuri, inavosomeka hii picha, kama ni makabiziano ya zawadi ya gari hilo aina Volkswagen
Maza ndio hajasimama ki itifaki sijui wasaidizi wake walikuwa wapi kumwambia head of states tunasimama namna hii yeye kapiga pozi la ku relax kitaa.

Kama yule jamaa aliyelalaga kwenye mawe ikulu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…