KWELI Picha ya Kasumba Baker wa Uganda aliyepigiliwa misumari mikononi

KWELI Picha ya Kasumba Baker wa Uganda aliyepigiliwa misumari mikononi

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
1732091905270.jpeg
 
Tunachokijua
Kumekuwa na picha inayomuonesha kijana amegongwa misumari mikononi huku picha hiyo ikiwa inahusishwa na matukio mbalimbali likiwemo matukio ya fumanizi (Tazama hapa, hapa, hapa na hapa)

Uhalisia wa Picha ni upi?

JamiiiCheck imefuatilia picha hiyo na kubaini ni picha halisi na Si ya kutengenezwa au kuhaririwa. Ufuatiliaji wa kimtandao kupitia Google Reverse Image umebainisha tukio hilo liliwekwa mtandaoni mara ya kwanza Agosti 29, 2019. (Tazama hapa hapa hapa na hapa)

Moja ya watu waliochapisha tukio hilo siku ya Agosti 29 2019 ni mwanaharakati na kiongozi wa Chama Cha National Unity Platform (NUP), Bobi Wine alieleza kuwa kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Kasumba Baker aliyekuwa na umri wa miaka 21 alivamiwa na watu 2 wasiojulikana ambao walimpiga kichwani pamoja na kumgongelea misumari mikononi.
1732092194591-png.3156766

Aidha tukio hilo lilichapishwa na New Vision tarehe 29, Agosti 2019 ambao walieleza kuwa kijana Kasumba baker(21) alivamiwa na watu wawili ambao hawakujulikana, siku ya Agosti 25, 2019 alipokuwa anatoka kazini kwake ambao walimpiga kichwani na kumgonga misumari mikononi, wanaeleza kuwa Kasumba alikuwa mkazi wa Avis Kivvulu Nchini Uganda. Baada ya tukio hilo alilazwa Mulago Hospitali kupatiwa matibabu huku Polisi walidai kufanyia uchunguzi ili kuwabaini wahusika waliotekeleza tukio hilo.

ryyy-03-680x457.jpg

Kasumba akiwa hospitali
Kwa mujibu wa BBC ambao walichapisha taarifa hiyo tarehe 30, Agosti 2019 walieleza kuwa tukio hilo lilizua mjadala mkali kwenye mitandao ya kijamii huku wengi wakilihusisha tukio hilo na Siasa za nchini Uganda.
Back
Top Bottom