Tetesi: Pierre Liquid amelazwa Muhimbili yuko hoi kitandani

Tetesi: Pierre Liquid amelazwa Muhimbili yuko hoi kitandani

Kwa kiasi anachokunywaga pole di haba akiwa na tatizo ini, mapafu au figo kufeli
 
Hivi wagonjwa wote walioko mahospitalinj ni watumiaji wa pombe!?

Unywe pombe au usinywe pombe siku moja ni lazima utafariki Dunia!

Kama ulizaliwa na mwanamke basi jua siku moja utafariki tu na huna namna nyingine ya kuondoka hapa Duniani!

Tuache kudhihaki wenzetu wanaopitia vipindi vigumu kwa kuugua kana kwamba sisi tutapaa!!

Watakatifu woote walifariki eidha kwa maradhi au kwa ajali!!

Jitunze uwezavyo lakini kifo ndio halali yako!
 
Wakuu, kuna siku niliona mtu ameuliza hapa mahali alipo mchekeshaji maarufu aliyejipatia umaarufu wake kupitia mitandao ya kijamii, Pierre Liquid. Aisee huyu jamaa amelazwa Hospitali ya Muhimbili Mwaisela wodi namba 6 iko ghorofa ya pili.

Haijafahamika mpaka sasa mwama huyo wa kuzipiga Pombe na vichekesho anasumbuliwa na ugonjwa gani ingawa wodi aliyolazwa ni ya wagonjwa wenye matatizo ya mfumo wa upumuaji, magonjwa yanayohusu moyo na kifua kiujumla. Muda mwingi msanii huyo ameonekana akiwa amelala.

Madhara ya kuumwagilia moyo
 
Mtu mstaarabu na muungwana yyt hawezi kusingizia MTU mwingine Kwa sababu yoyote iwe Pombe na kadhalika. Kufa tutakufa na wengine mtakufa na Figo,mapafu na maini yenu mazimaa!

Pombe ni mlango wa maovu? kwani Malaya nyinyi mnakunywa bia? Madhambi yenu hamyaoni.

Mnajua kosa ni kunywa TU,mengine mnayofanya si makosa Kwa Mungu?

Wanaomlaumu wangeonesha utu kumpa pierre pole na wagonjwa wote. Huo ndio utu
 
Mmiliki wa liquid asimamie show yote apo gharama za matibabu kwa jamaa kama fadhila... kaipa umaarufu sana
 
Bado hajatoka? Nipo Dar nataka nikamwone hapo Muhimbili.
 
Back
Top Bottom