Pita hapa kama unataka kujua chochote kuhusu biashara Kampala

Asante sana mkuu. Unapokua unachagua hizo piece by piece ku bargain kupo kama hapa bongo au ni style ya super market?
Mkuu huwezi amini kuwa Waganda bei za jumla hufanana maduka yote isipokuwa kama nguo zinatofautiana. Ila kumbuka Watanzania tunapendwa sana na kiswahili chetu wanakifukuzia sana (wanakipenda) japo wanalaumu ni kigumu kuliko eti kiswahili cha Congo [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23], sasa fikiria kama Congo kuna kiswahili huko
 
[emoji15] [emoji15] duh! Unasenaje?? Hapana chezea Uganda, aliyekwambia alikudanganya sana mm ni mziefu sana. Sema Mganda ni mwerevu sana katika biashara. Halafu usije ukathubtu kununua electronic Uganda.
 
We hukulipa kodi, ila ulitoa rushwa mzigo ukilipiwa Mutukula hulipi Kyaka.
 
Ndugu zanguni kwa uzoefu wangu biashara ya nguo za Special kutoka Uganda inalipa sana, ila kwa mitumba sio rahisi kutoboa.

Kwa upande wa viatu Nairobi ndo pazuri ila Uganda unakuwa na priority kubwa ya kudumbukia kwenye dimbwi la viatu feki, ila kama ni viatu vya akina Dada zile simple simple ni sawa.

Pia Suti Uganda ni nyingi sana na bei poa ila usipokuwa makini watakuuzia Suti iliyoshonwa Kampala wakakwambia ni Italy made.

Jambo lingine la kuzingatia ni money exchange rate na sehemu salama kuchange pesa. Kuna maeneo si salama kwa kuchange pesa wana tabia za chuma ulete.
Pia angalau kabla ya mwezi wa kusafiri anza kufuatilia consistency ya exchange rate, ukiona pesa bongo imefika 5.6 yaani Tsh100000 = Ush156000 change ni Mara chache inavuka hapo.
Usiwe unaenda kichwakichwa sometimes pesa ya bongo hushuka mpk 5.2.
 
Mule Mule ukigoma hapo wnashusha mzigo kwa kigezo umenunulia mzigo njiani baada ya kutoka Mtukula . Uliza wafanyabiashara wote waliopita hapo Kyaka kwa hayo mabasi ya Kampala.
Kaka me naelewa vizur sana maana ni mwenyeji sana. Ukilipa Tax Mutukula unapewa risit, ukiwa na risiti hapo ndo unelipa kodi halali hutadaiwa tena. Ila wengi hulizwa na wale watumishi wasio waaminfu.
 
vipi kuhusu stationary products huko kampala? @ ng'wnapagi
 
kapicha ka kitambo haka, huo mjengo ushakuwa musuri sana
 
Mi namuunga mkono mchangiaji mmoja hapo juu..Uganda kwa nguo za mitumba sio salama sana ila talking of special ni noma..wale jamaa wana nguo kali za Turkey, China , Thailand , na Italy na bei ni nzuri sana.Kikubwa ni kuangalia exchange rate tzs/ugx hapo ndio kikubwa ila pia TRA mutukula pale ni changamoto kubwa ila ukiwa mjanja biashara ya Uganda ni poa sana
 
Duuh ng'wanapagi
 
Sijawahi fika ila niko na jamaa zangu walisoma huko. Wanasimulia watoto wa kule wanapenda sana starehe alafu wanapenda sana vijana wa ki-tz!
Wakati naaza kufika Kampala nilikuwa nakoswakoswa kugongwa na bodaboda sababu ya kuchungulia makalio ya watoto wa Kinyankole baadae nikaona isiwe shida sana................
 
Wakati naaza kufika Kampala nilikuwa nakoswakoswa kugongwa na bodaboda sababu ya kuchungulia makalio ya watoto wa Kinyankole baadae nikaona isiwe shida sana................
hahahahaha... mkuu Ng'wanapagi mbona.... kwanini hukumalizia au ukaamua uvute ndani mmoja wao? Ni ushauri namna ya kupambana na changamoto za Uganda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…