Pita hapa kama unataka kujua chochote kuhusu biashara Kampala

Kama ni kuhusu dawa (viuatilifu) achana na Uganda, Waganda wenyewe hununua upande wa Tz ili kuepuka kununua feki.

Kwa Uganda everything is do-able ni wajanja sana wanaweza kukuingiza mjini kama hujui vitu.
Kuhusu novo
 
Israel ni nchi ndogo sana na isio na rasilimali nyingi lakini wanatumia ipasavyo Fursa kiduchu walizonazo kufanya wonders, Uganda wana fursa chache ila wanazitumia vizuri mno kibiashara.

Hata hapa Bongo biashara ipo sana tu, na tuna fursa nyingi sana ila shida ni Mimi na wewe. Tuna fursa nyingi sana ila kila siku tunalialia humu JF eti tumemaliza degree hakuna kazi, tena waliosoma ualimu ndo wanajihisi wao ni Almasi kila siku malalamiko, nenda Uganda uone graduates kibao hawana kazi ila wanajaribu kujiajiri wenyewe licha ya kuwa na utawala wanaoulalamikia sana kuliko nchi yoyote East Africa isipokuwa Burundi.

NGUZO ZA UMASIKINI WETU WATZ
NI
1.Uzembe + uvivu, tumekuwa wazembe na wavivu wa kufikiria hadi kufanya kazi.
2. Kukosa umoja na Ushirikiano, Uganda ni kawaida kabisa watu watatu kupanga chumba kimoja na kila mtu akaweka biashara yake na wakashare kodi ya pango. Sisi hapa Tz vijana wangapi tunaweza kupanga Fremu pale Kariakoo??

Itaendelea......
 
Saaafi nitumie business card na mm
 
Asante mkuu naomba unisaidie nauli Mwanza Kampala na namna ya kupata passport ya kusafilia
Passport nazani nenda Uhamiaji, utapata Ile ya mwaka mmoja ambayo ni shilingi elfu kumi kama sikosei maana na mimi yangu inaisha next week trh 20 so nitaenda kurenew. Kuhusu nauli sikumbuki maana kwa kuanzia Bukoba kwa sasa kwa bus dogo la friends ni 18000 to Kampala. Tafuta Ofisi za bus la friends huko mwanza utapata more details zaidi. Kama Jana wakati nageuza nilipanda bus la Links mpaka Mutukula kwani sikuwa na mizigo mingi.
 
Asante! Ngoja nijipange
 
Edit nauli yako mkuu
 
Mkuu umegusa mkuu, ukweli mtupu.
 
Vipi kuhusu hereni bangili pete na cheni zile za dhahabu ya kupaka
Mkuu hizo zipo za kumwaga kwa bahati mbaya siku pita maeneo hayo lakini nasikia full mzigo, kuna maduka yanauza kwa jumla vitu hivi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…