Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu Mlatinoh king,naomba nipate jibu,
Hiv raw materials za hayo macoccaine na maheroine ni nini? nadhan huko ndo kwa kudeal nako ili kueradicate hii tamu ya chid benz na ray c
The bold ulivo tiririka apa ume nifanya nimkumbuke character mmoja kweny tamthilia ya Narcos jamaa walikua wana muita "CocKroach" Mkemia uyu ndo alkua ana simamia production na ndie alie mshawish pablo aingie kweny iyo business according to the series..Mkuu Mlatinoh king,
Nijibu swali lako kwa juu juu pasipo kuingia ndani sana kuepusha kufundishana uharamia..
Tahadhali: reader's discretion is advised
Cocaine inatengenezwa kutoka katika majani ya mmea wa Coca ambao unalimwa sana huko Amerika ya kusini. Kama umewahi kuona mti wa mkahawa basi unafanana kimuonekana kwa asilimia kubwa na mmea huu wa Coca.
Baada ya majani kuchumwa kutoka katika mmea wa Coca yanapelekwa maabara na kisha yanakatwa vipande vidogo vidogo sana na kunyunyuziwa chumvi ya carbonate na kiasi kidogo cha maji. Baada ya hapo mchanganyiko huu unaongezewa mafuta ya taa au dizeli.
Kisha baada ya hapo mchanganyiko huu (majani ya coca, chumvi ya carbonate na dizeli/mafuta ya taa) unakorogwa kwa siku tatu mfululizo. Watengenezaji wengi wanatumia mashine ya kufulia au mashine ya kuchanganya zege kukoroga huu mchanganyiko kwa siku tatu mfululizo pasipo kuacha.
Hii inasaidia kutenganisha Cocaine yenyewe kitoka katika majani ya Coca. (Kwa waliopitia masomo ya kemia nadhani wanakumbuka kuhusu Solvent extraction, na hicho ndicho kinachofanyika hapo)
Baada ya hatua hiyo kimiminika kinachopatikana kinachemshwa ili kuondoa nta inayotoka kwenye majani ya Coca. Watu watabora nadhani watanielewa zaidi hapa maana inakuwa ni kama vile unapochemsha asali mbichi kuondoa nta na takataka nyingine.
Baada ya mchanganyiko kuchemshwa kuondoa nta inachujwa na kisha kuchanganywa na Sulphuric acid ili kubadili vimelea/vinasaba huru vya Cocaine (Cocaine free base) vilivyopo kwenye mchanganyiko na kuvifanya kuwa kuwa Cocaine sulphate.
Baada ya hapo mchanganyiko huu unaachwa utulie na baada ya muda Cocaine sulphate inatuama chini.
Kisha Cocaine sulphate iliyotuama chini inaondolewa na kuchanganywa na chokaa pamoja na unga wa soda. Hii inafanyika ili kufifisha sulphuric acid iliyowekwa mwanzoni.
Baada ya hatua hii kufanyika kinapatikana kitu kigumu lakini kilaini laini kama bazoka chenye rangi ya kijani. Hiki kinakaushwa na kusindikwa tayari kusafirishwa kwa wauzaji wa jumla. Hii ndio Cocaine unayoionaga kwenye runinga maarufu kama 'Pipi' ambazo watu tuliozoea kuwaita 'punda' huwa wamekamatwa nayo kwenye viwanja vya ndege wakiwa wamezimeza.
Baada ya 'Pipi' kumfikia muuzaji wa jumla inambidi aibadilishe iwe katika hali inayoweza kutumiwa na 'mlaji'.
Hapa wanaichanganya na asidi hafifu (diluted sulphuric acid) na kuongezea potassium permanganate. Kemikali hii ina uwezo mkubwa wa kuunguza (oxdizing) ambapo inaunguza taka taka ndogo ndogo zote zilizopo kwenye 'pipi' na kuibadilisha kutoka rangi ya kijani kuuu kuu (yellow-brown) na kuwa kitu kisicho na rangi kabisa au weupe kwa mbali.
Baada ya hapo inachujwa tena na kuchanganywa na ammonia ili kufifisha acid iliyowekwa na kisha inaachwa ikauke.
Ikisha kaushwa unapatikana unga mweupe, wenye ladha chungu, wenye kuyeyuka ukiwekwa maji.
Hii ndio bidhaa inayouzwa mtaani na kuharibu vijana, watu wanaiita ngada, poda, unga na majina lukuki lakini kiuhalisia yenyewe katika hali hii inaitwa Cocaine Hydrochloride.
Nashukuru!Haichoshi kusoma mkuu thanks
Nashukuru sana Mkuu..Mkuu the bold nashukuru kwa usimulizi wako murua unaotumia kiswahili fasaha mwanzo hadi mwisho. Hii stori ya Pablo Escobar nimeitizama kwenye series moja inaitwa "narcos" ina season 1 & 2. Hakika umeitendea haki kalamu yako, hongera.
Bila shaka Mkuu! NitakutagShukran The bold ndio nimeimalizia leo, kama kawaida nimejifunza kitu.
Naomba ukileta nyingine usinisahau.
Pamoja sana kiongozi! ThanksYou are great brother
Nashukuru sana Mkuu! Nitakutag..Asantee sana mkuu The bold...unajitahidi kuandika vizuri makala zako, kila nikisoma ni lazima nijifunze kitu...
Ila next time ukiandika makala zako naomba unitag
[emoji23] [emoji23] [emoji23] huyu si yule jamaa aliyenusurika kuuawa?The bold ulivo tiririka apa ume nifanya nimkumbuke character mmoja kweny tamthilia ya Narcos jamaa walikua wana muita "CocKroach" Mkemia uyu ndo alkua ana simamia production na ndie alie mshawish pablo aingie kweny iyo business according to the series..
eeeeh ndo ako ako kazee baadae kakaja kum snitch Pablo baada ya kuona jamaa ana make alot of money[emoji23] [emoji23] [emoji23] huyu si yule jamaa aliyenusurika kuuawa?
Ndio akaja kukutana na Pablo...