Mkuu
Mlatinoh king,
Nijibu swali lako kwa juu juu pasipo kuingia ndani sana kuepusha kufundishana uharamia..
Tahadhali: reader's discretion is advised
Cocaine inatengenezwa kutoka katika majani ya mmea wa Coca ambao unalimwa sana huko Amerika ya kusini. Kama umewahi kuona mti wa mkahawa basi unafanana kimuonekana kwa asilimia kubwa na mmea huu wa Coca.
Baada ya majani kuchumwa kutoka katika mmea wa Coca yanapelekwa maabara na kisha yanakatwa vipande vidogo vidogo sana na kunyunyuziwa chumvi ya carbonate na kiasi kidogo cha maji. Baada ya hapo mchanganyiko huu unaongezewa mafuta ya taa au dizeli.
Kisha baada ya hapo mchanganyiko huu (majani ya coca, chumvi ya carbonate na dizeli/mafuta ya taa) unakorogwa kwa siku tatu mfululizo. Watengenezaji wengi wanatumia mashine ya kufulia au mashine ya kuchanganya zege kukoroga huu mchanganyiko kwa siku tatu mfululizo pasipo kuacha.
Hii inasaidia kutenganisha Cocaine yenyewe kitoka katika majani ya Coca. (Kwa waliopitia masomo ya kemia nadhani wanakumbuka kuhusu Solvent extraction, na hicho ndicho kinachofanyika hapo)
Baada ya hatua hiyo kimiminika kinachopatikana kinachemshwa ili kuondoa nta inayotoka kwenye majani ya Coca. Watu watabora nadhani watanielewa zaidi hapa maana inakuwa ni kama vile unapochemsha asali mbichi kuondoa nta na takataka nyingine.
Baada ya mchanganyiko kuchemshwa kuondoa nta inachujwa na kisha kuchanganywa na Sulphuric acid ili kubadili vimelea/vinasaba huru vya Cocaine (Cocaine free base) vilivyopo kwenye mchanganyiko na kuvifanya kuwa kuwa Cocaine sulphate.
Baada ya hapo mchanganyiko huu unaachwa utulie na baada ya muda Cocaine sulphate inatuama chini.
Kisha Cocaine sulphate iliyotuama chini inaondolewa na kuchanganywa na chokaa pamoja na unga wa soda. Hii inafanyika ili kufifisha sulphuric acid iliyowekwa mwanzoni.
Baada ya hatua hii kufanyika kinapatikana kitu kigumu lakini kilaini laini kama bazoka chenye rangi ya kijani. Hiki kinakaushwa na kusindikwa tayari kusafirishwa kwa wauzaji wa jumla. Hii ndio Cocaine unayoionaga kwenye runinga maarufu kama 'Pipi' ambazo watu tuliozoea kuwaita 'punda' huwa wamekamatwa nayo kwenye viwanja vya ndege wakiwa wamezimeza.
Baada ya 'Pipi' kumfikia muuzaji wa jumla inambidi aibadilishe iwe katika hali inayoweza kutumiwa na 'mlaji'.
Hapa wanaichanganya na asidi hafifu (diluted sulphuric acid) na kuongezea potassium permanganate. Kemikali hii ina uwezo mkubwa wa kuunguza (oxdizing) ambapo inaunguza taka taka ndogo ndogo zote zilizopo kwenye 'pipi' na kuibadilisha kutoka rangi ya kijani kuuu kuu (yellow-brown) na kuwa kitu kisicho na rangi kabisa au weupe kwa mbali.
Baada ya hapo inachujwa tena na kuchanganywa na ammonia ili kufifisha acid iliyowekwa na kisha inaachwa ikauke.
Ikisha kaushwa unapatikana unga mweupe, wenye ladha chungu, wenye kuyeyuka ukiwekwa maji.
Hii ndio bidhaa inayouzwa mtaani na kuharibu vijana, watu wanaiita ngada, poda, unga na majina lukuki lakini kiuhalisia yenyewe katika hali hii inaitwa Cocaine Hydrochloride.