Poleni Watanganyika, poleni sana

Poleni Watanganyika, poleni sana

Bendera imependeza mimi nakumbuka tarehe 9 December 1961 uwanja wa Taifa Dar saa sita usiku bendera hii ikipandishwa nilikuwepo nashuhudia nikiwa mtoto mdogo darasa la tatu tulichaguliwa kucheza halaiki na kuvaa fulana za bendera hii mimi nilipangwa rangi ya njano.....Mungu ataturudishia bendera yetu na Tanganyika yetu
Ile Bendera kumbe ilikuwa ni nzuri sana, hata mwonekano wake unavutia hata kuliko hili tambara tulilonalo sasa.
'Mugassa' saa sita za usiku, mtoto wa darasa la tatu ulikuwa bado macho! Inawezekana ilikuwa ni kwa sabau ya kula vichwa vingi vya furu wakati huo; lakini Dar, ulivipata wapi?
 
Zanzibar ipo ila Tanganyika haipo huu ndio ujinga wetu mkubwa, sijawahi kuwaelewa watetezi wa muungano kuhusu kutokuwepo kwa Tanganyika
Kwa akili hizi ,halali naibu wako apate ujauzito

Yaani ,Zanzibar IPO Tanganyika inakosekana

Yaani

Unahoji ,kwann Kuna Tanzania bara na Tanzania visiwani ,lakini ukifatilia zaidi ,Tanzania visiwani haipo ila

Ila Kuna Zanzibar
 
hebu kwanza.

Inawezekana alishaona kazi iliyokuwa tayari inaandaliwa; halafu yeye kwa pupa karopoka hadharani?

Maana historia ya huyo huyo Ndugai siyo ya kujivunia sana mbele za watu wenye akili timamu.
Maana historia ya huyo huyo Ndugai siyo ya kujivunia sana mbele za watu wenye akili timamu.[emoji419][emoji375]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuuweke unafique kando! Tunapaswa kujitathmini upya
Sisi ni wanafiki. (Kupitia bunge hilo limethibitika
Sisi ni waoga na wazito kuchukua maamuzi magumu
Sisi ni waongeaji sana kuliko watendaji (keyboard warriors)
Sisi ni makuwadi (huu ukweli mchungu)
Sisi ni wabinafsi
Sisi ni waongo sana
Sisi si wamoja na hatuna umoja
Sisi hatuna uzalendo na hatujanyooka

Leo hii kuna Tanzania na kuna Zanzibar! Nyeusi tuite nyeusi jamani.. Je Tanganyika iko wapi? Imebaki kwenye makabrasha ya kumbukumbu ghalani..!

Suala la kuuza/kugawa/kubinafsisha bandari zetu zote za Tanganyika ya makaratasi, limetuacha uchi na kuthibitisha sisi ni watu wa namna gani!
Wenzetu ndugu zetu na jirani zetu Zanzibar wametuzodoa, wametubeza, wametupasha, wametukejeli na kutucheka sana humu mitandaoni.. Wametupa majina mengi mabaya na ya kukarahisha sana! TUNASTAHILI!

Tumejawa na unyonge na unafiki wa ajabu kabisa! Hatuna mbele hatuna nyuma kama sigara kali! Nyuma ni mbele na mbele ni kama nyuma
Tukiwashwa mbele nyuma tunavutika! Tukiwashwa nyuma mbele tunavutika!

Jana kilichoitwa kikao cha viongozi wa dini kimetoa mwelekeo mpya mpya kwenye hili sakata! Kimepangua na kufisha hoja zote zilizotumiwa na bunge kukubaliana na kile kilichokuwa kimepangwa na wenye ajenda zao!

Nyeusi tuite nyeusi, kikao kile pamoja na kuitwa ni kikao cha viongozi wa dini.. Lakini kiuhalisia RC ndio ilikuwa kila kitu kwenye kile kikao, kuanzia maandalizi, mipango, hoja mpaka wayforward ya nini kifanyike baada ya hapo! Kuna taasisi bado zitabaki kuwa juu miongo mingi ijayo kutokana na elimu! Na ndio maana EL alisisitiza sana elimu
Bunge letu! a laughing stock of the century tusiwaseme vibaya marehemu kwakuwa hawapo kujitetea lakini tukumbuke nyayo zao zinaishi kila walikopita! Tusingekuwa na bunge la namna hii kama kuna watu wasingekuwa na fikra finyu maono kimo cha mbilikimo!

Watetezi wa uwekezaji kandamizi wa kinyonyaji na kitapeli, wameokotezwa huko na huko na kupewa chochote kulingana na hadhi zao (price tags) lakini zisikilize hoja zao sasa! Sio hoja ni vioja! Wanapiga tu kelele na kupayuka kama mahoka kwa sangoma! Cha kushangaza wamepata uungwaji mkono na wajinga wengi.

Viongozi na wanasiasa walioko madarakani! Hawa sijui wanawaza nini! Au ndio ule usemi shibe mwana malevya? Hakuna hata mmoja aliyejitokeza waziwazi na kusema kwa sauti thabiti HILI HALIFAI! wote wanaishia kunong'ona mafichoni tena kwa sauti ya woga! Hawatuwazii sisi, hawaliwazii taifa! Wanajiwazia wao na matumbo yao na familia zao.

Poleni Watanganyika! Poleni sana! Kuna tabaka la wapigaji walioamua kujimilikisha hii nchi[emoji24], ubinafsi na unafiki wetu na woga wetu vimetufanya tuwaache wakue na kujijenga kwa nguvu mno! Sasa hawagusiki tena! Na kamwe hawajitokezi hadharani bali huwatumia makuwadi na vibaraka wao tangu juu mpaka chini kabisa, kila mahali na kila penye mikono ya uamuzi.. NA WOTE HAO NI WATANGANYIKA WENZETU

Tusiwalaumu wezi tuwalaumu waliowaonesha wezi mlango wa kuingilia huku wakiwalinda ili waweze kuiba nyumbani kwetu bila kukamatwa!

Poleni watanganyika! Tumeziona rangi zetu halisi


Na bado mama anaupiga mwingi, sasa taasisi nyeti anawajaza waleeeeeeee.
Niishie hapo
 
Kwa kweli kati ya vitu vilivyosikitisha ni huu uamuzi wa Huyu Mama, Nimetafakari sana, Nyerere hakuwaza kubinafsisha bandari, Mwinyi pia, Mkapa aliyekuwa mwanzilishi wa uwekezaji hakubinafsisha bandari, JK Mzee wa wapigaji hakuthubutu hata kuwaza hili, JPM Mzalendo wa kweli alikuwa sambamba na huyu mama Mnafiki hakuwaza kubinafsisha hiyo Bandari, Leo hii Huyu Mama ujasiri anautoa wapi?

Inasikitisha sana, Kama unatakiwa ufanisi wa kuendesha Bandari si bora wawekeze kwenye mitambo hata kama kwa mkopo??? Kinachoenda kufanyika ni kupeleka mapato yote ya nchi DUBAI, Kwa muda usiojulikana.
R.I.P TANGANYIKA.

Ulipokosea hapo “JPM mzalendo wa kweli”

Hili bunge la ovyo lililopitisha unachopinga sasa ni zao lake

Labda nikulize, lengo la mzalendo wa kwel kutuchagulia bunge la kina waitara na babu tale ni nini?
 
Tushajiambia sana kuwa sisi ni waoga(japo binafsi sikubaliani na hilo) na tushaamini hivyo na kujiita ni keyboard warriors, sasa mimi nashauri kwamba tufanye kile tunachokiweza kwa maana tuitumie hii mitandao kujibu mapigo ambayo yataleta athari nje ya mitandao badala ya kuitumia kulalamika na kukosoa tu. Kama huko uraiani tunaogopa hata kuwabana wabunge wetu basi tutumie mitandao.
 
Tuuweke unafique kando! Tunapaswa kujitathmini upya
Sisi ni wanafiki. (Kupitia bunge hilo limethibitika
Sisi ni waoga na wazito kuchukua maamuzi magumu
Sisi ni waongeaji sana kuliko watendaji (keyboard warriors)
Sisi ni makuwadi (huu ukweli mchungu)
Sisi ni wabinafsi
Sisi ni waongo sana
Sisi si wamoja na hatuna umoja
Sisi hatuna uzalendo na hatujanyooka

Leo hii kuna Tanzania na kuna Zanzibar! Nyeusi tuite nyeusi jamani.. Je Tanganyika iko wapi? Imebaki kwenye makabrasha ya kumbukumbu ghalani.

Suala la kuuza/kugawa/kubinafsisha bandari zetu zote za Tanganyika ya makaratasi, limetuacha uchi na kuthibitisha sisi ni watu wa namna gani.

Wenzetu ndugu zetu na jirani zetu Zanzibar wametuzodoa, wametubeza, wametupasha, wametukejeli na kutucheka sana humu mitandaoni. Wametupa majina mengi mabaya na ya kukarahisha sana! TUNASTAHILI!

Tumejawa na unyonge na unafiki wa ajabu kabisa! Hatuna mbele hatuna nyuma kama sigara kali! Nyuma ni mbele na mbele ni kama nyuma. Tukiwashwa mbele nyuma tunavutika! Tukiwashwa nyuma mbele tunavutika!

Jana kilichoitwa kikao cha viongozi wa dini kimetoa mwelekeo mpya mpya kwenye hili sakata! Kimepangua na kufisha hoja zote zilizotumiwa na bunge kukubaliana na kile kilichokuwa kimepangwa na wenye ajenda zao!

Nyeusi tuite nyeusi, kikao kile pamoja na kuitwa ni kikao cha viongozi wa dini.. Lakini kiuhalisia RC ndio ilikuwa kila kitu kwenye kile kikao, kuanzia maandalizi, mipango, hoja mpaka wayforward ya nini kifanyike baada ya hapo! Kuna taasisi bado zitabaki kuwa juu miongo mingi ijayo kutokana na elimu! Na ndio maana EL alisisitiza sana elimu.

Bunge letu! a laughing stock of the century tusiwaseme vibaya marehemu kwakuwa hawapo kujitetea lakini tukumbuke nyayo zao zinaishi kila walikopita! Tusingekuwa na bunge la namna hii kama kuna watu wasingekuwa na fikra finyu maono kimo cha mbilikimo!

Watetezi wa uwekezaji kandamizi wa kinyonyaji na kitapeli, wameokotezwa huko na huko na kupewa chochote kulingana na hadhi zao (price tags) lakini zisikilize hoja zao sasa! Sio hoja ni vioja! Wanapiga tu kelele na kupayuka kama mahoka kwa sangoma! Cha kushangaza wamepata uungwaji mkono na wajinga wengi.

Viongozi na wanasiasa walioko madarakani! Hawa sijui wanawaza nini! Au ndio ule usemi shibe mwana malevya? Hakuna hata mmoja aliyejitokeza waziwazi na kusema kwa sauti thabiti HILI HALIFAI! wote wanaishia kunong'ona mafichoni tena kwa sauti ya woga! Hawatuwazii sisi, hawaliwazii taifa! Wanajiwazia wao na matumbo yao na familia zao.

Poleni Watanganyika! Poleni sana! Kuna tabaka la wapigaji walioamua kujimilikisha hii nchi[emoji24], ubinafsi na unafiki wetu na woga wetu vimetufanya tuwaache wakue na kujijenga kwa nguvu mno! Sasa hawagusiki tena! Na kamwe hawajitokezi hadharani bali huwatumia makuwadi na vibaraka wao tangu juu mpaka chini kabisa, kila mahali na kila penye mikono ya uamuzi.. NA WOTE HAO NI WATANGANYIKA WENZETU.

Tusiwalaumu wezi tuwalaumu waliowaonesha wezi mlango wa kuingilia huku wakiwalinda ili waweze kuiba nyumbani kwetu bila kukamatwa.

Poleni watanganyika! Tumeziona rangi zetu halisi


Asante
 
Tatizo hatufanyi critical thinking ,critical analysis ila tuko very very emotion with very low emotional intelligence na pia tumeaminishwa kwamba serikali ni lazima imiliki kila kitu kwa asilimia mia yaani kila kitu na pia serikali lazima iwabane sana wafanyabiashara ndio ustawi wa nchi na pia kwa kuwa bado wazee wetu ndio ujana wao ulikuwa ule wa enzi za mwalimu na kila kitu mali ya umma fikra hizo zitaendelea tu.
Critical ukiangalia utendaji wa mfano mzuri makampuni ya mwasiliano na huduma za mawasiliano nchini na kwa kiwango gani zimeboreka toka sekta binafsi ziliporuhusiwa kuwekeza kwenye mawasiliano utaona kabisa kuna umuhimu mkubwa wa mageuzi ya kiuendeshaji wa mashirika yetu kwa kujipunguzia mzigo wa mishahara na matumizi ya mashirika huku serikali ikijizatiti zaidi kwenye kuweka regulations na kukusanya kodi iliipate surplus bajeti ,hayo mashirika yanayokuwa na poor performance yanarudisha nyuma maendeleo ya nchi na kuwapa mzigo watanzania wa kawaida kulipa kodi kubwa ili serikali zijiendeshe yangeweza kuwa efficiently yangeleta tija pia yameshindwa kufanya biashara na kupenetrate kwenye markets ya nchi nyingine na kutuletea profit home.
Mkuu MshanaJR hii hoja inafikirisha.. embu tutanue kidogo mtazamo wa huyu mwenzetu
 
Back
Top Bottom