Uchaguzi 2020 Polepole: Dkt. Magufuli ataendelea na mikutano ya kampeni katika mikoa 6. Mama Samia ataelekea Zanzibar

Uchaguzi 2020 Polepole: Dkt. Magufuli ataendelea na mikutano ya kampeni katika mikoa 6. Mama Samia ataelekea Zanzibar

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Kamarada Humphrey Polepole leo Jumamosi Oktoba 17, 2020 atazungumza na Vyombo Vya Habari.

---
Mgombea urais kupitia CCM, John Magufuli Oktoba 19, 2020 ataendelea na mikutano ya kampeni katika mikoa sita akianzia Pwani na kumalizia mkoani Dodoma Oktoba 26, 2020.

Wakati Magufuli akichanja mbuga katika mikoa hiyo, mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassan ataendelea na mikutano Zanzibar na Kassim Majaliwa ambaye ni mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM atakuwa Mtwara na Lindi.

Hayo yameelezwa leo Jumamosi Oktoba 17, 2020 na katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Humphrey Polepole katika mkutano wake na waandishi wa habari.

Amesema mbali na mkoa wa Pwani, Magufuli ataendelea na kampeni katika mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Manyara na kumalizia Dodoma.

Amesema Samia ataelekea Zanzibar na kuhitimisha mkoani Morogoro na Majaliwa mikoa ya Kusini ikiwa ni pamoja na Lindi na Mtwara.
 
Zikiwa zimebakia takribani siku 10 hivi tuingie kwenye mtanange wa uchaguzi katibu mwenezi wa Chama Tawala ndg. Humphrey Pole Pole ataongea na wanahabari leo saa nane mchana.

Makubwa yanakuja.
 
Baada ya Oktoba 28 mtaijua kuwa CCM ni NUMBERI WANI!!!
Hakika.
Ej4FXAyWoAAPxtC.jpg
 
Zikiwa zimebakia takribani siku 10 hivi tuingie kwenye mtanange wa uchaguzi katibu mwenezi wa Chama Tawala ndg. Humphrey Pole Pole ataongea na wanahabari leo saa nane mchana.
Makubwa yanakuja....
 
Wakati serikali ina hamasisha watu waende kujiandikisha kwa ajilii ya uchaguzi mkuu, Chadema walikua wakihamasisha watu wasiende kujiandikisha mbaka ipatikane katiba Mpya. Chakushangaza baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa watalalamika wameibiwa kura. Chadema kimetoka kuwa chama cha siasa mbaka kua kikundi cha wana harakati.
 
Mzee Polepole tumechoka na press zako za udaku. Ongea mambo yenye maana.
 
I hope anaenda kukazia kauli yake kua Uchuguzi ukiwa huru na haki ccm ijiandae kuondoka ikulu
 
Back
Top Bottom