#COVID19 Polepole: Hatuwezi kuzuia watalii kwa sababu ya Corona, tutapambana nayo kama tunavyopambana na Upinzani. Nchi inategemea watalii

#COVID19 Polepole: Hatuwezi kuzuia watalii kwa sababu ya Corona, tutapambana nayo kama tunavyopambana na Upinzani. Nchi inategemea watalii

WATALII WAANDALIWE MAZINGIRA SALAMA KWAO NA KWETU KWANZA. WAKIINGIA HAPA BONGO WASIJICHANGANYE NA SISI MPAKA KWANZA ZIPITE SIKU 14 tuwapime tena, NDIO TUJUE WAPO SALAMA AU WANA MAAMBUKIZI.

TUKUMBUKE DUNIA NI HII HII MOJA. TUSIPO CHUKUA HATUASTAHIKI SISI, MADHARA YATAENDELEA KUUTAFUTA ULIMWENGU WOTE NA SI WANDENGEREKO PEKE YAO.

Akihojiwa clouds Humphrey polepole amesema wapinzani Ni sawa Corona.

Kauli hii ya kiongozi kijana inaweza tafsiriwa Kama kauli ya kiongozi aliyepoteza dira na ambaye kwake maisha ya watu wasio ccm si kitu bali binadamu sahihi ni mwanaccm.

Niwaomba viongoz wa chama tawala kuchukua hatua kwake na pia vyombo vya dola kumshughulikia kwani kumwacha aendelee na tabia hii kutasababisha wapinzani nao kutumia kauli Kama hizi kujibu mapigo na hivyo kusababisha mgawanyiko kwenye taifa.

Tukumbuke ishu ya MENDE kwa wenzetu...

**********
Amesema ukizuia Watalii kuingia Nchini kwa mwezi mmoja kutokana na #coronavirus italeta shida kiuchumi, hivyo ni kuomba Mungu ugonjwa huu uondoke. #COVID19 ni sawa na wapinzani Nchini

Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi wa CCM, amesema "Tuna vituo Nchi nzima ambavyo vimetengwa kwa ajili ya kuwahudumia waathirika wa ugonjwa wa virusi vya hivyo."

Kuhusu CCM kununua Wapinzani amesema "Si kweli kuwa CCM inatoa fedha kununua Wanachama wa upinzani bali inabidi wapinzani watazame jinsi wanavyoharibikiwa wenyewe ndani kwa ndani"

"Kuna mwanachama wa Mbowe anaitwa Paulina, aliondoka kwenye Chama kwasababu alikuwa anatakiwa kimahusiano na viongozi wake hivyo akaamua kuhama ili kuokoa ndoa yake lakini alivyohama wapinzani wakatafuta kisingizo kuwa amenunuliwa"

Ameongeza, "Chama cha Freeman Mbowe wanaiitana Bwana au Kamanda wao sio ndugu. Katika chama chetu huwa natumia sana neno ndugu na siyo Mheshimiwa kwa kwasababu sisi si kitu bila ya watu waliotupa dhamana"

Aidha, amesema "Hii tume ya Uchaguzi ni huru kabisa kama si huru mbona Halima Mdee na Joseph Mbilinyi walishinda? Mtu pekee anayeweza kuzungumzia kuhusu tume ya Uchaguzi ni Umma na siyo Vyama Vya Siasa."

"Tume ya utumishi wa umma ndiyo inachakata majina 5 ya Mwenyekiti wa tume ya Taifa ya uchaguzi na kumpelekea Rais ili ateue jina moja"

"Freeman Mbowe anataka tufanye maridhiano lakini sisi na wao hatufikirii pamoja kwenye kile wanachohitaji wananchi hadi sasa"

"Tangu nimekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM sijawahi kufanya mkutano wa hadhara.
Sisi kama CCM huwa hatufanyi mikutano ya hadhara kwenye majimbo yasiyoongozwa na wanachama wetu, mfano Mbeya ni Jimbo la Joseph Mbilinyi yeye huwa anafanya mikutano lakini akifanya anazungumzia jela kubaya"

"Godbless Lema hajawahi kutembelea miradi ya kimaendeleo Arusha Mjini na akifanya mikutano ya hadhara hazungumzii vitu hivyo bali yeye anazungumza kuhusu Jela tu. Kila tunachokifanya wanasema ni kibaya na sisi hatukatai kushauriwa kwasababu siyo maroboti lakini tangu tumeanza kupewa ushauri hatujawahi kupewa ushauri wa maana."
 
Katika kuonyesha jinsi viongozi wa CCM wasivyo thamini na kuheshimu Watanzania wenzetu ambao ni wanachama wa vyama vingine nje ya CCM hata kama ni kaka zetu, Dada zetu,wajomba nk. Katibu wa Itikadi mbele ya TV amewafananisha watu na ugonjwa wa Corona.
Hakika tumeuona ukweli wa chama hiki kuwa hakina heshima kwa Watanzania na kina kiburi cha ajabu sana.
Jee tufanyeje kuwaadhibu maana wameshindwa kumuadhibu Polepole? Au ni kweli Watanzania wasio wanaccm ni sawa na Corona?
Screenshot_20200320-173121.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kasema wapinzani hajasema watanzania huwezi jua labda anaongelea wapinzani wa Tanzania kwenye world cup championship
 
Akigusia suala la virusi vya corona Kupitia kipindi cha SEBULENI cha Couds Plus, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi, Humphrey Polepole amesema:

"Ukizuia watalii kuingia Nchini kwa mwezi mmoja italeta shida kiuchumi, kwahiyo tunaomba Mungu ugonjwa huu uondoke, Corona ni sawa na wapinzani Nchini"

"Wabunge kwa sasa wataanza kuchukuliwa vipimo kabla ya kuingia bungeni na kama wakikutwa na chembechembe za virusi vya Corona basi watachukuliwa hatua za awali kuepusha mlipuko huu"

"Tuna vituo Nchi nzima ambavyo vimetengwa kwa ajili ya kuwahudumia waathirika wa ugonjwa wa virusi vya Corona"

Pia soma > Serikali kutodhibiti idadi ya wageni wanaoingia nchini kwa kisingizio cha Utalii, inahatarisha Usalama wa Taifa dhidi ya virusi vya Corona

Hili la bunge sijamuelewa.

Kwani polepole alichaguliwa lini kuwa msemaji wa bunge???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika kuonyesha jinsi viongozi wa CCM wasivyo thamini na kuheshimu Watanzania wenzetu ambao ni wanachama wa vyama vingine nje ya CCM hata kama ni kaka zetu, Dada zetu,wajomba nk. Katibu wa Itikadi mbele ya TV amewafananisha watu na ugonjwa wa Corona.
Hakika tumeuona ukweli wa chama hiki kuwa hakina heshima kwa Watanzania na kina kiburi cha ajabu sana.
Jee tufanyeje kuwaadhibu maana wameshindwa kumuadhibu Polepole? Au ni kweli Watanzania wasio wanaccm ni sawa na Corona?View attachment 1394099

Sent using Jamii Forums mobile app


Kama wapinzani ni corona kwa mujibu wa Hamphrey Polepole basi CCM ni Ebola.

Huyo msigombane naye kwa maneno mengi nanyie mpigeni kwa hoja tu.
 
Ana maana ugonjwa wa Korona ukiingia CCM unakuwa mzuri. Kwa mwendelezo ugonjwa wa Korona ukiingizwa nchini na wageni unakuwa mzuri kwa nchi!!!!!!!!!

Polepole katubu haraka.
 
Yupo sawa polepole! Hatukufunga mipaka wakati wa ebora, wakati wa mafua ya ndege, wakati wa kipindupindu! Sembuse corona!!
Uko sawa mkuu.

Acha kutetea upumbaf Kama anavowaita huyu kichaa mwenzenu...!!
Kuifananisha CORONA VIRUS(Covid-19)na sijui Ebola,SARS(Mafua ya ndege) na Chorela Ni UCHIZI NA UPUMBAFU.....!!
Hivi unaweza kutushawishi kuwa magonjwa ya Ebola,SARS na kipindupindu yamewahi KUENEA DUNIA NZIMA KAMA ILIVO CORONA wakti huu?
Polepole ni CHIZI lazima akemewe na akome kupotosha Umma wa Tanzania.
 
Ni kweli,lakini si busara tukiendelea kuweka rekodi za wagonjwa wa Corona wanaotoka nje either ni watalii au Watanzania kwa kufanya hivyo tutawaletea taharuki Wananchi wetu.
Ni vema tukajizuia kusema sana maana hatujui kesho ikoje,na kamwe tusichanganye siasa na maisha ya watu maskini otherwise kama tumejiakikishia tunazo immunities za kutosha.
Na wapinzani nao wajiweke mbali na matamko kuhusu hili janga,sio lazima kila kitu kiwe in public wakutane waandae maelezo wanayoyaona yanafaa kwa maandishi na kuyawakilisha serikalini.
Janga la Corona sio mtaji wa kisiasa Bali ni suala la Usalama na afya za wananchi,ni wajibu wetu kushikamana kama Taifa na kushauriana kwa pamoja kuliko kila ka kikundi/mtu /Taasisi kutoa matamko yenye kuligawa Taifa.
 
Kipimo cha upinzani kuimarika ni kipi?
Umesahau enzi zile Dk slaa alivyokuwa anasimama jukwaani? Umesahau Dk slaa alisema nchi haitawalika mpaka mkuu wakati huo akanywea? Umesahau Dk slaa alivyoimarisha chama mpaka wabunge wakafika zaidi ya 40. Au unajifanya hujui.
 
Acha nimshukuru Mungu tu kwa kila jambo


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Back
Top Bottom