Polepole na Musukuma tuacheni na machinga wenu nasi tupumue

Polepole na Musukuma tuacheni na machinga wenu nasi tupumue

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Kumejitokeza wanaccm wanaoamini kuwa nchi hii ya wanaccm na wao wakisema sisi watwana tufuate. Musukuma anashiriki biashara za machinga Kariakoo amekuwa akiwatetea wamachinga akimtumia Polepole kumuunga mkono na kumshambulia Mkuu wa Mkoa Makalla.

Suala la wamachinga limeanzishwa na sisi wananchi tunaobughudhiwa na wamachinga mbele ya biashara zetu na pia watumiaji barabara wengine.

Polepole na Musukuma mjue na sisi wengine tutafika mahali tupambane na wamachinga wenu waondoke mbele ya biashara zetu, sisi kuwa na fremu za maduka si kwamba ni matajiri ila tuliamua kutimiza wajibu wetu kufuata sheria za nchi.

Polepole na Musukuma mwachieni Mkuu wa Mkoa atuondolee wamachinga wenu na mjue sisi pia tunazo familia zinazokula ugali na mchicha mara moja kwa siku tofauti na nyie mnaokula mara sita kwa siku, mjue hivi sasa kukaa ndani ya fremu ya duka kunahitaji uvumilivu wa ziada kwani mauzo yameshuka sana kutokana na CCM kushindwa kuujenga uchumi kwa zaidi ya miaka 40 mkisingizia mabeberu!

Indonezya ilitawaliwa kama sisi na hao mnaowaita mabeberu lakini wametutoka wako mbali sana huku nyie mmebaki kukomba kura, hicho ndicho muhimu kwenu.

HATUWATAKI WAMACHINGA WALIOZAGAA BARABARANI.
 
Mimi naungana nao, they are very right.
P
Ni haki yako lakini nami pia ni haki yangu kufanyabiashara bila bughudha toka kwa wapigakura wenu mnaowatetea wakae mbele ya biashara zetu.
Nyie mnawaoana wamachinga kuwa wao ndio wanahitaji hela ya kula na watoto wao mkijua watoto wetu wanashushiwa na Mungu! Jinsi mnavyowatetea kwa sababu ya kura ndivyo nasi tunavyopata hasira ya kutaka kupambana nao, mnachokijenga mtakiona.
 
Kila jambo lisipokuwa na utaratibu linakuwa shaghalabaghala tu,

Machinga hawana utaratibu wa kufanya kazi zao currently, kila mahali wamezagaa tu, hamna utaratibu, siyo kwenye barabara, mirefereji, mbele ya biashara za wengine, hovyo hovyo tu,

Nchi iwe na utaratibu,, hawajanyimwa kufanya biashara, maana ni kama watu wanahisi kwamba wamenyimwa kufanya biashara, No,

Wawe kwenye utaratibu
 
Aliyewaruhusu machinga kufanya shughuli zao kiholela ni nani? tuanzie hapo kwanza......je, ni polepole na musukuma au ni siasa za kampeni za chama chakavu kulazimisha uungwaji mkono wa machinga kwa kuwatumia kama mtaji wa kisiasa......
 
Mimi naungana nao, they are very right.
P
Nilikuwa Nairobi last week, katikati ya Jiji hakuna hizi biashara holela kila mahali, manchinga wana maeneo yao mahususi. Jiji ni clean, organized na inapendeza. Hapa Tanzania tatizo ni nini? Kuna shida gani manchinga kuwa na maeneno yao mahususi mjini? Watu wanatandaza bidhaa hovyo chini, vibanda na miavuli kina kona ya barabara. Wamanchinga wapangiwe maeneo yao wafanye biashara iliyonyooka. Tuachane na uholela huu kama nchi.
 
Kumejitokeza wanaccm wanaoamini kuwa nchi hii ya wanaccm na wao wakisema sisi watwana tufuate. Musukuma anashiriki biashara za machinga Kariakoo amekuwa akiwatetea wamachinga akimtumia Polepole kumuunga mkono na kumshambulia Mkuu wa Mkoa Makalla.

Suala la wamachinga limeanzishwa na sisi wananchi tunaobughudhiwa na wamachinga mbele ya biashara zetu na pia watumiaji barabara wengine.

Polepole na Musukuma mjue na sisi wengine tutafika mahali tupambane na wamachinga wenu waondoke mbele ya biashara zetu, sisi kuwa na fremu za maduka si kwamba ni matajiri ila tuliamua kutimiza wajibu wetu kufuata sheria za nchi.

Polepole na Musukuma mwachieni Mkuu wa Mkoa atuondolee wamachinga wenu na mjue sisi pia tunazo familia zinazokula ugali na mchicha mara moja kwa siku tofauti na nyie mnaokula mara sita kwa siku, mjue hivi sasa kukaa ndani ya fremu ya duka kunahitaji uvumilivu wa ziada kwani mauzo yameshuka sana kutokana na CCM kushindwa kuujenga uchumi kwa zaidi ya miaka 40 mkisingizia mabeberu!

Indonezya ilitawaliwa kama sisi na hao mnaowaita mabeberu lakini wametutoka wako mbali sana huku nyie mmebaki kukomba kura, hicho ndicho muhimu kwenu.

HATUWATAKI WAMACHINGA WALIOZAGAA BARABARANI.
Rubbish. Endeleeni kulewa madaraka tu.
 
Nilikuwa Nairobi last week, katikati ya Jiji hakuna hizi biashara holela kila mahali, manchinga wana maeneo yao mahususi. Jiji ni clean, organized na inapendeza. Hapa Tanzania tatizo ni nini? Kuna shida gani manchinga kuwa na maeneno yao mahususi mjini? Watu wanatandaza bidhaa hovyo chini, vibanda na miavuli kina kona ya barabara. Wamanchinga wapangiwe maeneo yao wafanye biashara iliyonyooka. Tuachane na uholela huu kama nchi.
Naunga mkono hoja, Wamachingwa watengewe maeneo yao. Lakini kwa vile waliruhusiwa kufanya biashara popote na rais wa nchi wa wakati huo, then wasifukuzwe kama mbwa, kama wahalifu kama vibaka, wasivunjiwe vibanda vyao na kuporwa mali zao, maadam mwanzo waliruhusiwa kufanya kiholela sasa wapangiwe utaratibu.
P
 
Naunga mkono hoja, Wamachingwa watengewe maeneo yao. Lakini kwa vile waliruhusiwa kufanya biashara popote na rais wa nchi wa wakati huo, then wasifukuzwe kama mbwa, kama wahalifu kama vibaka, wasivunjiwe vibanda vyao na kuporwa mali zao, maadam mwanzo waliruhusiwa kufanya kiholela sasa wapangiwe utaratibu.
P
Hapa nimekuelewa Nadhani Serikali itafuata utaratibu.
 
Ni haki yako lakini nami pia ni haki yangu kufanyabiashara bila bughudha toka kwa wapigakura wenu mnaowatetea wakae mbele ya biashara zetu.
Nyie mnawaoana wamachinga kuwa wao ndio wanahitaji hela ya kula na watoto wao mkijua watoto wetu wanashushiwa na Mungu! Jinsi mnavyowatetea kwa sababu ya kura ndivyo nasi tunavyopata hasira ya kutaka kupambana nao, mnachokijenga mtakiona.
mkuu achana na huyo ziro brain ni mbinafsi anawaza uteuzi tu.
 
Back
Top Bottom