Police General Orders(PGO) ni nini, nitaipata wapi?

Police General Orders(PGO) ni nini, nitaipata wapi?

Limekuwa neno maarufu sana kipindi hiki japo binafsi nilianza kulisikia kwenye clip ya Siro akimchana Mamboleo kuhusu uvaaji wa sare ya polisi (kimakosa) na kuanika watuhumiwa.

Nashukuru kuna mjumbe humu kafafanua kuwa PGO ni Police General Orders. Lakini swali langu ni kutaka kujua zaidi hiyo kitu na upatikanaji wake. Nauliza hivi kwasababu.

Zamani kidogo nikiwa mdogo kitambo hicho nikiwa primary (darasa la 4-5 hivi) nakumbuka Mzee alitoa vitu vingivingi kwenye makabrasha yake akidai ni takataka anataka kuvichoma moto.

Sasa tulikuwa na tabia (na yeye mwenyewe alishatuzoesha) kuwa kila anapokuwaga anafanya safisha safisha kwenye makabrasha yake basi ni lazima avikusanye vile asivyovihitaji na kutuachia sebuleni hapo tuchague tuvipendavyo vyote then vitavyobaki tukavichome moto.

Basi siku hiyo nakumbuka katika nilivyopendezwa navvyo na kuviokoa ilikuwa ni vitabu vidogo vidogo vitatu; viwili vilikuwa ni katiba ya NCCR Mageuzi kwa miaka tofauti tofauti (Kamoja kalikuwa kana cover kama bluu fulani hivi na kengine cover yake ilikuwa ina rangi mbili upande bluu na upande nyeupe.

Maswali yalikuwa hayachezi mbali pia nilimuuliza mara kwa mara sababu ya kuvitupa vitu hivyo kila mara alipokuwa akifanya hivyo. Katika vitabu vile nakumbuka alinijibu tu kuwa havina kazi kwasababu ni vya zamani zaidi (matoleo ya zamani) na pia yeye hajihusishi na siasa tena. Alisema yeye alikuwa ni Mpinzani damu enzi hizo NCCR-Mageuzi ndo iko moto ila mwaka 1995 ndo ilikuwa mwisho wa kujihusisha na siasa na hataki tena kuisikia wala sisi tujihusishe.

Tuache huko maana siyo lengo la uzi twende kwenye kitabu cha tatu sasa. Nakumbuka kitabu kile nilikuwa nakipenda sana na nilikuwa nasoma mara kwa mara. Kiliandikwa mambo mengi sana kuhusu kazi ya polisi na kwakuwa ni zamani sana siwezi kuyakumbuka yote ila kwa ujumla nakumbuka kilielezea namna ya kukamata mtu, kupokea na kuandika maelezo ya mtu, mahabusu, mavazi na vitu vingi vingi tu.

Kitu ambacho sikuweza kujua ni jina la kile kikitabu maana hakikuwa na kava na ukurasa wake wa kwanza uliokwepo ni kuanzia kwenye yaliyomo nakumbuka. Nakumbuka mzee nilimuuliza pia kwamba kwanini ana kitabu kinachoelezea mambo ya polisi (enzi hizo polisi tunawachukulia kama nini sijui) basi mzee alinijibu tu kuwa alikipata alipokuwa mgambo.

Dah najuta kupoteza vile vitabu (mchwa walikula vingine vilichakaa) pia najilaumu kwani kama kale kakitabu ndo PGO huenda saivi ningekuwa zangu napitia pitia PGO mdogo mdogo mwenyewe kila siku[emoji23].
 
Mimi huwa najiuliza na Pia nakosa Majibu, Wenzetu ulaya wamejiongeza hadi Kuweka body Cam (kamera mwilini) Ili kuzuia police asitende nje ya sheria ya kazi Yake, ila hapa Tanzania mambo ni tofauti kabisa!!
1 :Fikiria hapa police wanafanya kazi Bila utambulisho wowote au kuwa na fake identity!?
2: Vitendea kazi vyao Magari kwa Mfano mengine hayana hata number (identification)
3: Pia Mengine yamewekwa numba fake! Huwa kwa hali hii huwa nashangaa sana, hii kwa tafsiri rahisi inahamasisha, Polisi anaweza kufanya jambo lolote baya na kuharibu taswira yote ya jeshi letu!
Pendekezo
Naomba ikiwezekana na iwe kwa udharura Magari yote ya Jeshi yawekwe numba kwa ajili ya utambulisho!! Kwani Polisi sio Malaika!! Hii itaongeza uwajibikaji WA Jeshi na kuongeza utoaji haki
 
PGO,GPO,au OPG... Maana huku mtaani ni sarakasi tupu. Hizo herufi zinachangnywa mno. Ila polisi wetu nawahurumia, wao wanfunzwa namna ya kuonea raia,hasa walio kinyume na mawazo ya serikali. Sheria za polisi ni za kikoloni...
kibatala: ieleze mahakama,PGO inayotumika ni toleo la mwaka gani
Shahidi:sijui

PGO 😛olisi general order
GPO :government polisi order
OPG 😱rder polisi to government

tunasubiri tamko la ccm
 
Mimi huwa najiuliza na Pia nakosa Majibu, Wenzetu ulaya wamejiongeza hadi Kuweka body Cam (kamera mwilini) Ili kuzuia police asitende nje ya sheria ya kazi Yake, ila hapa Tanzania mambo ni tofauti kabisa!!
1 :Fikiria hapa police wanafanya kazi Bila utambulisho wowote au kuwa na fake identity!?
2: Vitendea kazi vyao Magari kwa Mfano mengine hayana hata number (identification)
3: Pia Mengine yamewekwa numba fake! Huwa kwa hali hii huwa nashangaa sana, hii kwa tafsiri rahisi inahamasisha, Polisi anaweza kufanya jambo lolote baya na kuharibu taswira yote ya jeshi letu!
Pendekezo
Naomba ikiwezekana na iwe kwa udharura Magari yote ya Jeshi yawekwe numba kwa ajili ya utambulisho!! Kwani Polisi sio Malaika!! Hii itaongeza uwajibikaji WA Jeshi na kuongeza utoaji haki
Kweli kabisa mkuu, hata ukamataji tu haufanyiki inavyotakiwa polisi hajitambulishi, mtuhumiwa hasomewi haki zake wala kuambiwa sababu ya kukamatwa utaskia twende utajua hukohuko kituoni which is not right unaweza kubambikiwa kesi..
 
sasaa wewe endelea kusubiri uje usikie polisi anakuja kukupakapaka mafuta kaja kukukamata ni mwendo wa virungu tu magaidi kama nyie mapak mjinyee
Kuna siku watajichanganya pabaya saana na ndio itakuwa fundisho kwa wengine. Haki yangu ni mali yangu. Time will tell
 
PGO ina kanuni ambazo zinatakiwa Manjagu wetu wazimeze na kuzielewa na ndio muongozo wa kazi yao kila siku wanapokua kituo cha kazi au kuondoka na mtuhumiwa kama zilivyo sheria za kodi tatizo hiyo PGO ipo kwa kidhungu ndio maana wakina kibatala wanatamba kama Gaucho uwanjani...na hiyo PGO huwezi kusoma leo uamke kesho unaijua ukajibu maswali ya Mawakili watata..
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom