Polisi wa Tanzania nini mabaya na mazuri yao? Kuna umuhimu wa kuwa na Polisi binafsi?

Polisi ni wazuri sana. Wanafanya kazi kubwa ya kuenforce law. Bila polisi hizi sheria tulizonazo ni takataka. Na polisi wanatakiwa kuwa wakali, watu wasio na mchezomchezo.

Wabaya wapo kama ambavyo kuna wabaya kila kona kuanzia marais, wabunge, madaktari, madereva nk.
 
Dah! Inatisha, sasa hivi kuna mtu kanambia kuna matatizo makubwa mawili yamejipenyea kwenye jeshi la polisi, yasipodhibitiwa hayo, tutateseka sana.

Kamari ya betting na Ulevi. Sasa hivi ni tatizo kubwa jeshini humo.

Sasa ikiwa polisi ni walevi kupindukia na wachea kamari kupindukia, hivi maadili ya vijana wetu hawa tutayasimamia vipi?

Hawa Masheikh na Maaskofu wawe wanapitia vituo vya polisi kuwapa darsa, wasikae misikitini na makanisani tu, kungoja wateja wao wawafate huko. Wawe na malengo.
 
Weka details kamili hapa. Kwa utulivu.
 
Nipo mikononi mwa polisi maisha yangu bado ni mikosi afande - Sugu.

Wimbo huu maalamu kwa marehemu Michael Sikupya.
 
Kweli kabisa, natamani polisi wawe na nidhamu na sifa za polisi waliopo duniani.

Huko ulipopataja Polisi wanakuwa ni kimbilio la jamii na ni washauri wakuu wa jamii inapokosea. Hapa kwetu ni kinyume chake, jamii, inaiogopa polisi. Kwanini?

endelea kutamani tu.

polisi wenu wa bongo hapa hata mishahara ya maana mmeshindwa kuwalipa mnaota polisi wenye maadili!!!

polisi anastaafu baada ya maiak 30 ya kazi yenye masimango analipwa milioni 17 kiinua mgongo 2023[emoji28][emoji28][emoji28],
rais nayeye anashangaa hajui tatizo nini.
waziri wa mambo ya ndani naye hajui tatizo nini.
Igp katoa macho haelewi shida iko wapi.

unafikiri ni polisi gani atazubaa kutochukua rushwa kwa asante hii ya kifedhuli kutoka serikalini!!!???
ukizingatia rushwa yenyewe haombi anapewa kwa ushawishi.
juzi kwenye kamati ya haki jinai,mzee mmoja anasema polisi wanalipwa laki 9 na posho zao zinafika 1.6ml kwa mwezi[emoji28][emoji28],huyu katumwa na rais ampelekee majibu ya changamoto katika utoaji haki ngazi zote,hicho ndicho anachokijua kuhusu maslahi ya polisi.
 
Hayo ndiyo matatizo ya kuzungumzwa bila ushabiki.

Duniani huko kuna nchi zimeanza kuweka Polisi binafsi (Private Police), ni muhimu na Tanzania tukaanza huo mpango.

Ni kitu kinachowezekana kikipangwa vizuri.
 
Hayo ndiyo matatizo ya kuzungumzwa bila ushabiki.

Duniani huko kuna nchi zimeanza kuweka Polisi binafsi (Private Police), ni muhimu na Tanzania tukaanza huo mpango.

Ni kitu kinachowezekana kikipangwa vizuri.
Mfano Railway, inatakiwa iwe na polisi wake binafsi, wanalipwa na Railwa na wanafundishwa sheriaa na nidhamu zote za Kipolisi.

Bandari.

Vituo vya mabasi, ni sehemu nyingi sana zinaweza kuwa na Polisi binafsi. Ambao wanakuwa ni hawahawa polisi waliopitia vyuo vyote ila huku wanaongezewa mafunzo ya ufanisi na mishahara inakuwa ya binagfsi siyo ya serikali, mafao yanakuwa ya binafsi siyo ya sereikali.


Kuna njia nzuri zinazweza kufanyika, kuupunguzia mzigo serikali, na wale waserikalini wakajikuta wanalipwa vizuri pia.

mfano mwingine ni askari jela, jela zinatakiwa zizalishe, zinawezza kuajiri polisi binafsi wenye nidhamu na wataheshimu kazi kwa kuwa watalipwa vizuri.


Ni wakati tuanze kuwa positive.
 
Hayo ndiyo matatizo ya kuzungumzwa bila ushabiki.

Duniani huko kuna nchi zimeanza kuweka Polisi binafsi (Private Police), ni muhimu na Tanzania tukaanza huo mpango.

Ni kitu kinachowezekana kikipangwa vizuri.

kama walinzi mnao na kampuni tayari,fanyeni mchakato mpate taasisi binafsi za upelelezi sio polisi kamili.
 
Pamoja na changamoto wanazozipitia Wapiganaji wetu ila bado ni chombo makini sana tunawashukuru sana POLISI WETU.

Bila wao amani mitaani isingekuwepo.

Hongera kwao General Duty/Field Force Unit/CID's/Intelijensia kwa kazi nzuri.
 
Weka details kamili hapa. Kwa utulivu.
hili suala askari mmoja hivii Kule kitaa ,alisema hvi ndugu tu Hata nikisema niripoti ntajikuta nahamishwa kituo au wakubwa wanachukua wao hizoo nyumba au wasilifanyie Kazi,ila sana sana ni kua watachukua wao wakubwa baasi hvyo Bora kuacha tu
Hii bongo askari 99%are corrupt
 
Tueleze walikufanya nini?
Kuna diwani fulani wa kata fulani iliyopo KOROGWE ndugu yake alikamazwa na Mali ya wizi ya zahanati iliyopo kata hiyo (viatilifu) robota 2 na jamaa akafikishwa kituo cha polisi wilaya,huwezi amini alichokifanya diwani yule akishirikiana na polisi........
 
Police Wajinga wapo na police wenye akili ya kujua majukumu yao pia wapo, kazi kwako kuwatafuta police wenye maadili mema kwenye kazi zao humo humo ndani ya Jesho la Police! Mfano mdogo,Mimi kuna mpelelezi aluzingua kwenye kesi yangu,lakini baada ya kulalamika,kuna police wengine walikuja rekebisha Jambo langi hadi Mahakama ikanipa haki yangu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…