residentura
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 8,146
- 11,434
Kongole dada FaizaFoxy kwa hoja mujarabu.Polisi wa tanzania tumesoma na kusikia malalamiko mengi sana juu yao, mpaka inakuwa vigumu kuanza kutafuta mema yao.
Tunaona kuwa Polisi ndiyo wamekuwa chimbuko la rushwa, imefikia mpaka kuna msemo mitaani "kuingia kwa pesa, kutoka kwa pesa"
katika mema yao machache ni pale tunapoona kwenye vyombo vya habari wakijitangaza wao wenyewe kukamata majambazi na wezi, au, wameuwa jambazi fulani.
Nakumbuka sisi tulivyokuwa utotoni, miaka ya mwanzo 60s, tulibahatika kuliona jeshi la Polisi lililosheheni Wazungu, Wahindi, Waarabu na Waafrika. Na kila mtoto alitamani akikuwa awe polisi.
Polisi kilikuwa siyo chombo cha kutishia watoto, kila mtoto akipenda na kutamani awe polisi au kama polisi. Hivi sasa polisi imekuwa chombo cha kutishia watoto, ukimwambia mtoto "polisi huyo" basi mtoto anaweza kukulilia utafikiri kamuona ziraili mtowa roho za watu.
Tumefeli wapi na jeshi letu la Polisi?
Mtazamo wangu; Jeshi la polisi lilianza kufeli zamani sana, lilianza kufeli lilipoanza kutumiwa na wanasiasa kukandamiza wananchi wafanye watakavyo wao kwa nguvu au kwa hiyari. Chanzo nnachokikumbuka mimi ni vijiji vya ujamaa, watu walipoanzwa kuhamishwa makazi yao ya asili na kupelekwa vijiji vya ujamaa, jeshi la polisi likaanza kutumika kuwahamisha watu kwa nguvu na kuwapakia kwenye "makarandinga" kuwahamisha kutoka makazi yao ya asili na kwenda kuwatupa maporini waanzishe makazi mapya yaliyoitwa "vijiji vya ujamaa".
Kuanzia kipindi hicho serikali zote, mpaka leo hii, hazijaacha kuitumia polisi kama chombo chao cha kuhakikisha walitakalo wanasiasa ndilo wanalifanya polisi.
Tatizo liko wapi? Jee ni wakati siasa zikaachanishwa na kuendesha serikali? Serikali ibaki kama serikali na siasa zibaki kama siasa?
kinachotakiwa ni tafakuri ya kina, maji yakimwagika hayazoleki, lakini tunaweza kupiga deki na kuyakausha na kuchota mengine.
Wewe unaonaje? Umefikia wakati tuwe na Polisi binafsi?
Hivi ndio vitu tunatakiwa tuvijadili (likiwemo la IGA kati ya nchi ya Tanzania na "nchi ya DP - World") kwa mustakabali mwema wa Tanzania yetu.
Kufeli kwa TanPol ni kutokana na kuchukua Watanzania ambao hawabebeki kwenye kada zingine za ajira za "staha".
Hawabebeki kwenye kada zingine kwa kuwa hawana vigezo vya ufaulu mzuri.
Kada za ajira zinazohitaji ufaulu mzuri zimetengenezewa maslahi mazuri.
TanPol ndiyo inayooneka kuwa ni "last option" kwa yule kijana aliyemaliza kidato cha nne au cha sita na kutopata ufaulu.
Serikali kudogosha na kudunisha hii kada pamoja na wanasiasa kuwatumikisha hawa TanPol kwa manufaa yao, ndio kunapopelekea changamoto za kuwa na polisi tulionao leo hii.
Tatizo la msingi ni serikali.