Polisi wabadili gia angani, Wanadai hawajui alipo Mfanyakazi wa LHRC Tito Magoti

Inawezekana wamesha katisha uhai wake, sasa wanajitoa kabisa, huenda asipatikane.
Mambosasa keshasema Tito Magoti yuko kwenye mikono salama na ‘Habeas corpus’ case imeshaanzishwa LHRC ili kuhakikisha anafinguliwa mashtaka haraka. Kwa hiyo tuamini kuwa yuko hai na kwa haraka ataachiwa au atafiishwa mahakamani. Kinyume cha hayo patachimbika tu!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Terror squad kazini. Wasiojulikana wanajulikana na kulindwa
Mimi nadhani polisi hawakumkamata Tito Magoti badala yake alikamatwa na WATU WASIOJULIKANA ambao ni kikundi kinachopewa amri na mkuu wa rogue elements za ikulu au TISS. Baada ya makelele mengi kwenye social media waliomteka Magoti wameitaka polisi kufanya kile kinachoitwa DAMAGE CONTROL. Hiyo ndo maana RPC wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni hajui lolote kuhusu kukamatwa kwa Magoti nacwenzake watatu.
Nchi hii imeanza kushindikana kutawala!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
ITAKUWA WALIMKAMATA TITAAAAA MAGOTI SIO TITOO
 
ukiona hivyo wamemjeruhi hadi wamepitiliza wameona wampoteze tu kuficha ushahidi.
 
ukimsikiliza vizuri huyo RPC wa kinondoni amesema hana taarifa na watu wake wote amewauliza hawana taarifa,sio mzembe wala mpumbavu kusema hivyo maana kwa utaraatibu wa kipolisi jambo lolote linalotokea chini ya himaya yake ni lazima awe na taarifa nalo hasa kama waliohusika ni askari polisi hata kama wametokea mkoani ripoti lazima ifike kwake.
kwahiyo kwa maelezo yake huyo amenawa kwa upande wake na askari wake anaowaongoza hawahusiki ili lolote likitokea wakuulizwa atakuwa alietoa taarifa na kwa maana hiyo inawezekana waliohusika na kukamata sio polisi.
waandishi wa habari hawakukosea kumuuliza RPC wa kinondoni juu ya tukio hilo kwasababu ndie anaepaswa kuwa na taarifa zozote za matukio yanayohusu jeshi la polisi katika eneo lake la kazi,yani hata watoke polisi mkoani kuja kukamata mhalifu kinondoni lazima yeye apewe taarifa kwa mujibu wa utaratibu wa jeshi la polisi.
 
nadhani wewe ndio hujafanya reasoning,jambo likishavuka mamlaka ya kikanda ni lazima mwenye kanda yake awe na taarifa fullstop.labda kama yanafanyika mambo kwa mazoea bila kufuata utaratibu,nilikuwa naomuona ndugu yangu mmoja wa jeshi silitaji akitoka mkoani kuja hata ikiwa ni likizo lazima aripoti makao makuu,hata kama atakaa siku nne tu.

ukimsikiliza vizuri huyo RPC wa kinondoni amesema hana taarifa na watu wake wote amewauliza hawana taarifa,sio mzembe wala mpumbavu kusema hivyo maana kwa utaraatibu wa kipolisi jambo lolote linalotokea chini ya himaya yake ni lazima awe na taarifa nalo hasa kama waliohusika ni askari polisi hata kama wametokea mkoani ripoti lazima ifike kwake.
kwahiyo kwa maelezo yake huyo amenawa kwa upande wake na askari wake anaowaongoza hawahusiki ili lolote likitokea wakuulizwa atakuwa alietoa taarifa na kwa maana hiyo inawezekana waliohusika na kukamata sio polisi.
waandishi wa habari hawakukosea kumuuliza RPC wa kinondoni juu ya tukio hilo kwasababu ndie anaepaswa kuwa na taarifa zozote za matukio yanayohusu jeshi la polisi katika eneo lake la kazi,yani hata watoke polisi mkoani kuja kukamata mhalifu kinondoni lazima yeye apewe taarifa kwa mujibu wa utaratibu wa jeshi la polisi.
 
Umeandika UTOTO,operation ya siri ni kwetu sisi wananchi ndio inakuwa siri lakini sio kwa RPC!
 
Sawa! kwani akifanywa chochote Wa-Tanzania mtafanya nini? wangapi

1)wamepotea? na kuacha wajane na familia zinateseka!

2)kutekwa? na kutia hofu!

3)kudhalilishwa hadharani kweupeee!

4)kudhurumiwa waziwazi!

5)kukejeliwa mbele ya watu wanaokuheshimu!

6)kufukuzwa bila kujali atahari zitakazo kukumba, hadi kifo duuu!

7)kuuawa kama panya!

8)kupigwa masasi kama unua nyani muharibifu!

Mtaongeaaaa yataisha usiku mtalala, mtatekwa tena na tena, ili wana siasa waishi, inabidi waue watishe, kama alivo fanya Moi kwa kina Ouko na wenzake,

Wakurya ndo wanawezana na siasa za mauaji. hawaongeagi saana! ila utaona action tu!
 
Au ukiona operation ya siri hata RPC haambiwi basi ujue haijafuata utaratibu wa kipolisi na kuna genge ambalo linatumika ndani ya polisi kufanikisha matukio kama hayo,sasa kuna watu wengine hawapendi kuunganishwa na matukio hayo ya kiuhalifui wao wakiwa viongozi maana wanajua JINAI haina EXPIRE DATE.
 
Dah!...
 
ukisoma michango ya watu humu ndugu yangu ndio utaelewa sisi WATANZANIA ni watu wa aina gani.tupo tupo tu,hatujui wajibu wala haki zetu,bado tuna safari ndefu.
Usiseme sisi Wa tanzania hatujui haki! acha maneno yako hayo! temea mate chini, inawezekana bado mdogo weye Duniani kote hakuna haki, nenda popote ndiyo utajua bora uliyo yaacha nyuma ni nafuu, fanya chochote! Neno ''haki '' itabaki kuwa siasa tu na maneno ya propaganda! kutoka kwa Tabaka tawala dhidi ya tabaka tawaliwa milele yote!

Haya yote ni Kwa sababu mwanadamu haridhiki. kama utafanya yafuatayo;

- Ukiwa mwema utaitwa wewe ni dhaifu, hujui kuongoza,

-Ukifuata haki na sheria wewe ni Dikteta, katili, kitama kwigwa, hutaki kukosolewa,

-Ukiwa mtu kati hujui kuongoza, mbumbu,

- Ukibeba yote hayo hapo juu utaitwa mripukaji, mtambo. neno mtambo ni kitu kinacho endeshwa.hasa na Mkoloni!

-Ukisiliza shida za watu bila kjali umri dini wala kabila pale lumumba ''Ooooh anatafuta kula ana njaa!

-Ukiwa mpole lakini idealistic utaambiwa unahatarisha amani! na vurugu unaleta weye!

Sasa nambie hiyo haki utaipata vipi ikiwa wanazuoni wenyewe magwiji wa haki za kimataifa wamepigwa Risasi hadhalani mchana kweupeee! wakakimbia mpaka leo hawajulikani walipo, wako kama vibaka! wezi majambazi, wakuonewa huruma, na kazi wakaachishwa kama mbwa! wana kimbiakimbia tu kama mbwa koko!

Cha msingi hapa mpimege upepo tu unavo enda! msikurupuke bila kujipanga, Shetani unamjua?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…