Polisi wabadili gia angani, Wanadai hawajui alipo Mfanyakazi wa LHRC Tito Magoti

Polisi wabadili gia angani, Wanadai hawajui alipo Mfanyakazi wa LHRC Tito Magoti

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni asema hana taarifa za kukamatwa na kushikiliwa kwa mwanaharakati,Tito Magoti

Mussa Taibu amesema kuwa mpaka sasa hana taarifa ya kukamatwa kwa Ofisa wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu [LHRC] Tito Magoti, katika eneo la himaya yake na hata amejaribu kuwauliza wenzake lakini nao hawana taarifa hizo.

Awali Kamanda Lazaro Mambosasa aliuthibitisha Umma kwamba Magoti alikamatwa Mwenge wilayani Kinondoni

Taarifa za awali kuhusu kutekwa kwa Tito Magoti ni kuwa alikuwa katika bodaboda akielekea Mwenge kununua simu, alipofika katika kituo cha mafuta cha Puma watu 5 waliokuwa na gari aina ya Harrier walimchukua kwa mabavu kisha kuondoka kwa uelekeo wa Posta, Dar es Salaam.

Jana Kamanda wa Polisi wa Kanda ya Dar, Lazaro Mambosasa amekaririwa akisema Polisi inamshikiliwa Magoti na wenzake watatu kwa uchunguzi wa tuhuma za makosa ya jinai inayowakabilia.

Hata hivyo, Mambosasa hajawahi kubainisha ni kituo gani ambacho Magoti anashikiliwa.

Zaidi, soma:

View attachment 1301209
View attachment 1301208

Inawezekana ACP Mambosasa ni polisi wa Rwanda na ACP Mussa ndiyo polisi wa Tanzania....

Kwanini polisi wa nchi moja tena wakiwa wanaongoza mkoa mmoja wawe na kauli za kutofautiana juu ya tukio moja la uhalifu lililotokea ndani ya eneo lao la kiutawala???

Tuseme nini sasa? Kwamba, serikali ina kikundi cha askari cha utekaji wa watu wakosiaji wa utawala huu huku baadhi ya viongozi wakuu wa polisi wakiwa hawajui??

For sure, kauli hizi mbili zinazokinzana za viongozi wakubwa wawili wa polisi ndani ya mkoa mmoja, nchi moja zinathibitisha kuwa utekaji wote wa critics wa serikali, kushambuliwa kwa risasi kwa watu kama Tundu Lissu na uhalifu wote unaofanana na huu, unatekelezwa na dola chini ya uratibu wa ikulu....!!
 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni asema hana taarifa za kukamatwa na kushikiliwa kwa mwanaharakati,Tito Magoti

Mussa Taibu amesema kuwa mpaka sasa hana taarifa ya kukamatwa kwa Ofisa wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu [LHRC] Tito Magoti, katika eneo la himaya yake na hata amejaribu kuwauliza wenzake lakini nao hawana taarifa hizo.

Awali Kamanda Lazaro Mambosasa aliuthibitisha Umma kwamba Magoti alikamatwa Mwenge wilayani Kinondoni

Taarifa za awali kuhusu kutekwa kwa Tito Magoti ni kuwa alikuwa katika bodaboda akielekea Mwenge kununua simu, alipofika katika kituo cha mafuta cha Puma watu 5 waliokuwa na gari aina ya Harrier walimchukua kwa mabavu kisha kuondoka kwa uelekeo wa Posta, Dar es Salaam.

Jana Kamanda wa Polisi wa Kanda ya Dar, Lazaro Mambosasa amekaririwa akisema Polisi inamshikiliwa Magoti na wenzake watatu kwa uchunguzi wa tuhuma za makosa ya jinai inayowakabilia.

Hata hivyo, Mambosasa hajawahi kubainisha ni kituo gani ambacho Magoti anashikiliwa.

Zaidi, soma:

View attachment 1301209
View attachment 1301208
Guys you know what?? Once the IGP tries to get his hands on Mambosasa and gets hold of him, this will be the end of his tenure in the office. With all my due respect for the IGP, I suppose you execute what is lingering in your mind and have it done once and for all.
 
Sina hakika kama huwa tunafanya reasoning kabla ya kufikia conclusion. Aliyekiri kwamba huyo Tito kakamatwa na polisi ni Kamanda wa kanda maalum ya Dar es salaam. Sasa mtu unaenda kumuuliza RPC wa Kinondoni halafu anakumbia hana taarifa hizo kisha mbio mbio unakuja kubandika bandiko hapa kuwa polisi imekanusha. Hivi RPC wa Kinondoni anajua yanayofanyika na vikosi vya kanda maalum? Hivi RPC wa kinondoni anajua yanayofanyika Central Police? Hivi RPC wa Kinondoni anajua yanayofanyika Temeke? Hivi RPC wa Kinondoni anajua yanayofanyika Ilala? Kwa nini hatupendi kwenda extra mile kuwa kwa sababu wa Kinondoni hajui basi tumuulize wa Temeke, wa Ilala na tukishindwa basi turudi kwa Mambosasa ambaye ndiye mwenye utawala katika mikoa yote mitatu ya kipolisi. Mtu kukamatwa Mwenge siyo lazima awe amepelekwa kwenye vituo vya polisi Kinondoni tena hasa kama waliohusika na kumkamata ni polisi wanaofanya kazi katika mikoa yote mitatu, yaani kanda maalumu.
Tukio kubwa la kipolisi lililotokea siku nne zilizopita lililotikisa dunia nzima polisi mkoa mzima wa Dar wasijue ikiwa ni pamoja na IGP? Lingetokea Katavi ingechukua miaka mingapi lifike Makao Makuu ya polisi? Kama hali ndo hiyo, madai ya polisi kuwa uhalifu nchini umepungua si kweli bali ni taarifa tu za uhalifu toka mikoani hazijamfikia msemaji mkuu wa polisi.
 
Tukio kubwa la kipolisi lililotokea siku nne zilizopita lililotikisa dunia nzima polisi mkoa mzima wa Dar wasijue ikiwa ni pamoja na IGP? Lingetokea Katavi ingechukua miaka mingapi lifike Makao Makuu ya polisi? Kama hali ndo hiyo, madai ya polisi kuwa uhalifu nchini umepungua si kweli bali ni taarifa tu za uhalifu toka mikoani hazijamfikia msemaji mkuu wa polisi.
Hakuna cha tukio kubwa hapo acheni kukuza mambo. Huyo Tito kakamatwa kama watu wengine wanavyokamatwa. Hana ukubwa wowote hadi eti useme tukio kubwa. Kitu kingine lazima ufahamu kuwa polisi wana taratibu zao za kutoa taarifa. Hawaropoki ropoki tu kama nyie mnavyotaka iwe. Na kitu kingine hakuna anayejua upande wa pili wa maisha ya Tito, msimfanye aonekane msafi wakati mmejulia tu kwenye twitter na kwenye maisha yake ya sheria.
 
Hakuna cha tukio kubwa hapo acheni kukuza mambo. Huyo Tito kakamatwa kama watu wengine wanavyokamatwa. Hana ukubwa wowote hadi eti useme tukio kubwa. Kitu kingine lazima ufahamu kuwa polisi wana taratibu zao za kutoa taarifa. Hawaropoki ropoki tu kama nyie mnavyotaka iwe. Na kitu kingine hakuna anayejua upande wa pili wa maisha ya Tito, msimfanye aonekane msafi wakati mmejulia tu kwenye twitter na kwenye maisha yake ya sheria.

Duuuuu, kwahiyo hapo umemaliza utetezi. Basi shughuli ipo.
 
msipende kuzua taharuki za kishamba, mamboleo kasema alikamatiwa kinondoni na sio polisi wa kinondoni waliomkamata tatizo nini?
Naona unataka kupindisha ,mamboleo anasema amekamatwa na polisi na yupo ktk mikono salama.
 
Mpaka tutekwe wote ndio tutajua umuhimu wa kuungana kama Taifa kupinga huu udhalimu.

Naanza kupata mashaka kama Tito bado tunae na kama tunae,basi sijui atakuwa katika hali gani.

Ukiona hivi, ujue kuna uwezekana wa mambo mawawili:wamemtanguliza au wamemuumiza na kumjeruhi vibaya kiasi kwamba hawako tayari kuhusishwa/kutuhumiwa na hivyo tunaweza kumuokota akiwa kama Dr.Ulimboka.
Tumekuwa wapumbavu. Hawa wauaji kila siku wanadonoa mmoja baada ya mwingine. Na sisi kwa ujinga tunaona kama yanayotokea hayatuhusu.

Ningependa kusikia kipaumbele cha kwanza cha vyama vya siasa, makanisa, misikitiki, vyama vya kiraia na taasisi za kimataifa, ni kuongoza mapambano dhidi ya wasiojulikana/watekaji na wauaji.
 
Tumekuwa wapumbavu. Hawa wauaji kila siku wanadonoa mmoja baada ya mwingine. Na sisi kwa ujinga tunaona kama yanayotokea hayatuhusu.

Ningependa kusikia kipaumbele cha kwanza cha vyama vya siasa, makanisa, misikitiki, vyama vya kiraia na taasisi za kimataifa, ni kuongoza mapambano dhidi ya wasiojulikana/watekaji na wauaji.
Jiwe anaogopeka mkuu
 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni asema hana taarifa za kukamatwa na kushikiliwa kwa mwanaharakati,Tito Magoti

Mussa Taibu amesema kuwa mpaka sasa hana taarifa ya kukamatwa kwa Ofisa wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu [LHRC] Tito Magoti, katika eneo la himaya yake na hata amejaribu kuwauliza wenzake lakini nao hawana taarifa hizo.

Awali Kamanda Lazaro Mambosasa aliuthibitisha Umma kwamba Magoti alikamatwa Mwenge wilayani Kinondoni

Taarifa za awali kuhusu kutekwa kwa Tito Magoti ni kuwa alikuwa katika bodaboda akielekea Mwenge kununua simu, alipofika katika kituo cha mafuta cha Puma watu 5 waliokuwa na gari aina ya Harrier walimchukua kwa mabavu kisha kuondoka kwa uelekeo wa Posta, Dar es Salaam.

Jana Kamanda wa Polisi wa Kanda ya Dar, Lazaro Mambosasa amekaririwa akisema Polisi inamshikiliwa Magoti na wenzake watatu kwa uchunguzi wa tuhuma za makosa ya jinai inayowakabilia.

Hata hivyo, Mambosasa hajawahi kubainisha ni kituo gani ambacho Magoti anashikiliwa.

Zaidi, soma:

View attachment 1301209
View attachment 1301208
Habari ya Tito na wengine wanaotekwa na kupotea inaweza kufanana na huyu Mwandishi

Mahakama moja nchini Saudi Arabia imewahukumu watu watano kifo na kuwafunga wengine watatu baada ya kuwakuta na hatia ya mauaji ya mwanahabari Jamal Khashoggi mwaka jana

Khashoggi, alikuwa mkosoaji kinara wa serikali ya kifalme ya Saudia aliuawa ndani ya ofisi ndogo ya ubalozi wa nchi hiyo katika Jiji la Istanbul, Uturuki mwaka 2018.


Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Saudia amesema mauaji hayo yalikuwa ni sehemu ya "operesheni haramu" na kuwashtaki watu 11 ambao hata hivyo majina yao hayakuwekwa wazi.

Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa (UN) alifikia hitimisho kuwa yalikuwa "mauaji ya serikali yasiyofuata utaratibu."

Mtaalamu huyo Agnes Callamard pia alipendekeza kwenye ripoti yake kuwa Mwanamfalme Mohammed bin Salman achunguzwe kutokana na mauaji hayo.

Bin Salman hata hivyo amekanusha kuhusika kwa namna yeyote ile, lakini mwezi Oktob mwaka huu akasema kuwa "anawajibika moja kwa moja akiwa kama kiongozi wa Saudia, na hususani kwa kuwa mauaji hayo yametekelezwa na maafisa wa serikali ya Saudia."

Shirika la kimataifa la kutetea haki za binaadamu la Human Rights Watch limesema kuwa kesi hiyo haikukidhi viwango vya kimataifa na mamlaka za nchi hiyo "zilizuia njia zote stahili za uwajibikaji".

Mwandishi huyo aliyekuwa na miaka 59 alipofikwa na umauti alikuwa akiishi Marekani na kuandika maoni kwenye gazeti maarufu la Washington Post.

Mara ya mwisho kounekana akiwa hai ilikuwa Oktoba 2, 2018 akiingia kwenye ofisi ndogo za ubalozi wa Saudia ili kuchukua karatasi zake za talaka.

Alikuwa mbioni kumuoa mpezi wake wa Kituruki Hatice Cengiz.

Baada ya kusikiliza kanda za sauti zilizonaswa na maafisa wa usalama wa taifa wa Uturuki, Bi Callamard alifikia hitimisho kuwa Khashoggi "aliuawa kinyama" siku hiyo.

Naibu mwendesha mashtaka wa Saudia Shalaan Shalaan aliwaambia wanahabari Novemba 2018 kuwa mauaji yaliamriwa na mkuu wa "timu ya mapatano" iliyotumwa Istanbul na mkuu msaidizi wa idara ya usalama wa taifa ya Saudia kwa kazi ya kumrejesha Khashoggi nyumbani "kwa jia ya ushawisi" na edapo hilo lingeshindikana, "basi kwa nguvu".

Wachunguzi pia walifikia hitimisho kuwa Khashoggi alifungwa kwa lazima ma kisha kukabwa koo na kamba kabla ya kudungwa sindano lukuki za dawa ambazo zilipekea kifo chake. kwa mujibu wa bw Shalaan.

Baada ya hapo mwili wake ulikatwa katwa vipande na kukabidhiwa kwa mshirika wa kituruki nje ya ubalozi. Mabaki hayo hayajapatikana tena.

Bw Shalaan hata hivyo anasisitiza kuwa Mwanamfalme Mohammed "hakuwa na habari yeyote juu ya tukio hilo".
Siku wasiojulikana watakapojulikana nao watanyongwa tu...
 
Muhimu umefahamu ujumbe, spellings za lugha ya watu weka pembeni..

Anyway unajua kama unaweza kuandika COLOR na COLOUR na maana ikawa ndio ile ile
Unatetea makosa ya uandishi au?
 
Hii movie musa taibu atakuwa hajashirikishwa, na mamboleo kapewa taarifa juu kwa juu
 
Nilivyomuelewa kamanda wa kinondoni ni kwamba yeye kama yeye kwenye mkoa wake hajamshika Tito ila kuna Operation zinawezwa kufanywa na mkuu wa kanda nzima na yeye asipewa taarifa kwa mantiki hiyo Mambosasa na BASHITE ndio wamemkamata Tito/Bolleni ukiunganisha nukta.
 
Nilivyomuelewa kamanda wa kinondoni ni kwamba yeye kama yeye kwenye mkoa wake hajamshika Tito ila kuna Operation zinawezwa kufanywa na mkuu wa kanda nzima na yeye asipewa taarifa kwa mantiki hiyo Mambosasa na BASHITE ndio wamemkamata Tito/Bolleni ukiunganisha nukta.
Huyo Bashite Ni Nani katika jeshi la polisi? Sirro sio pilato haogopi makelele
 
Jeshi la polisi lilimkamata Tito Magoti kwa madai eti anatumia fake I'd kuitukana serikali huku wakimhusisha na Kigogo wa Twitter pamoja na I'd ya member maarufu mkosoaji wa Jf...Cha ajabu watu waliohusishwa naye bado wapo wanapost tu...Leo wanasema hawajui alipo ili baadaye wakamtelekeze sehemu kama walivyofanya kwa Mo baada ya kumsainisha nyaraka muhimu kwa nguvu.
Nyaraka gani Hizo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpaka tutekwe wote ndio tutajua umuhimu wa kuungana kama Taifa kupinga huu udhalimu.

Naanza kupata mashaka kama Tito bado tunae na kama tunae,basi sijui atakuwa katika hali gani.

Ukiona hivi, ujue kuna uwezekana wa mambo mawawili:wamemtanguliza au wamemuumiza na kumjeruhi vibaya kiasi kwamba hawako tayari kuhusishwa/kutuhumiwa na hivyo tunaweza kumuokota akiwa kama Dr.Ulimboka.
Nchi hii imedukuliwa na wasiojulikana,wanafanya kazi zao mchana ila hawafahamiki,wanatumia vyombo vya moto(magari/pikipiki) ila hawakutani na msongamano wala traffic.
Hatuna bahati wala usalama kama wananchi na hakuna MTU kuwajibika.Kila mmoja anatoka na blah blah zake halafu kimya totoro.
Tuchukue hatua.
 
Back
Top Bottom